Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

[TABLE="width: 100%, align: left"]
[TR]
[TD="class: kaziBody"]By ALVAR MWAKYUSA, 20th October 2011 DAILY NEWS

The two leaders showered praise on the varsity for producing professionals who have played significant leadership roles in their countries.

They made the remarks when addressing delegates in Dar es Salaam on Thursday at the climax of the 50th anniversary of the university.

"I acknowledge the role played by UDSM in training key personnel for other countries in the East African region. A number of experts and graduates from this university have been recognized regionally and internationally," Mr Kikwete said.

His remarks were supported by President Museveni who mentioned some high-ranking people from his country, including himself, as graduates of the renowned university 'Hill'.

Mr Museveni mentioned former East African Community (EAC) Secretary General, Mr Amanya Mushenga, Uganda's Chief Justice Mr Benjamin Odoki as well as his wife who is also the Minister for Karamoja Affairs, Ms Janet Museveni.

"On the list of great people who studied here at the Hill, is Dr John Garang, the late Vice-President of Sudan," he noted.

Mr Museveni said most veteran lawyers in his country were trained at UDSM.


The Ugandan leader also spoke highly of Father of the Nation Mwalimu Julius Nyerere, for establishing a higher learning institution at a time when the region needed educated people.

Mr Museveni, who has been collecting funds in his country for the construction of a students' centre at UDSM, pledged to hand over the contribution to the varsity's authorities.


Meanwhile, the Father of the Nation, the late Mwalimu Nyerere, was among six people who were recognized for their contribution in setting up the university.

Others are Prof Robert Pratt, who was the first Principal of the then University College Dar es Salaam, Chief George Kunambi, who played a crucial role in locating the current site of UDSM.

Others are Justice Julie Manning (Rtd), the first and lone female student at inception, Dr Wilbard Chagula, the first indigenous Principal and Prof Arthur Weston who was the Dean of Law at the inception.

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: kaziBody"]
[TABLE="width: 100%"]
[TR]
[TD] My take: Rais Kikwete na Museveni wanasema kuwa UDSM imesaidia kutoa wahaitimu katika ukanda wa Afrika mashariki. Ninahakika aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kenya bw. Kivuitu naye pia ni mhitimu wa hapo.Watu wanaposema kuna nafasi za upendeleo ili kuminya waislam, mbona 'trend' inaonekana kuvuka mipaka?

Lakini kilichonisukuma zaidi kuleta hii habari ni hiyo kauli ya kwamba aliye locate eneo la ujenzi ni George Kunambi kwa mujibu wa UDSM
Mohamed Said anasema ni (Sykes au Dossa sikumbuki vema) aliye muonyesha mwalimu eneo hilo akimpeleka Pugu. Hapa pia historia inatakiwa kurekebishwa! ili tujue ukweli

Ufafanuzi mzee Said.

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Nguruvi3
Nilipata tabu kuweka kitu nadhani hiyo mistari ilikuwa inakorofisha nikaweka hii kwa FF sasa naiweka kwako uwaone wazee wangu walivyokuwa na ari ya maendeleo. Juzi wametoa mitaa na majengo kuipa majina ya wazalendo na waliosaidia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wazee wangu wamesahauliwa tena. Iko list ya waliochangia chuo Insha Allah nikiipata nitaimwaga hapa jamvini:

"Salum Matimbwa anaingia katika historia ya ukombozi wa Tanganyika si tu kama mwanachama wa awali waliojiunga na TANU kabla ya 1958 bali kama mmoja wa wazalendo waliochanga fedha kuanzisha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Fikrra ya kuanzisha Chuo Kikuu inasemekana ilianza na Nyerere akiwa na Dossa. Ilkuwa kawaida ya Dossa baada ya mikutano ya TANU pale Mnazi Mmoja kumchukua Nyerere na gari lake kumrudisha Pugu. Njia ya zamani kwenda Pugu ilikuwa inapita hapo kilipo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Sasa ilikuwa kiza kimeingia na walitaka kutoka nje ya gari kuangalia mandhari ya Dar es Salaam maana kutokea pale mji ulikuwa unapendeza sana kwa taa zilizokuwa zikiwaka barabarani. Nyerere alimwambia Dossa, "Dossa tukipata uhuru wetu hapa lazima tujenge Chuo Kikuu."Hili wazo lilifanyiwa kazi na wananchi wakahamasishwa kuchangia ujenzi wa Chuo hicho. Fedha zilichangwa na Chuo kikajengwa pale New Street kwenye kiwanja cha John Rupia alichokitoa kuwapa TANU. Hapo ndipo kilipoanza Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. (Chuo hiki sasa ni Chuo Cha Watu Wazima).Abdallah Salum alikuwa mmoja wa wachangiaji wa chuo hicho na mwanae Salum Matimbwa hadi leo amehifadhi stakabadhi ya malipo y ash. 50.00 stakabadhi ambayo ina saini ya Bhoke Munanka."

Mohamed
 
Sidhani kama nimesema hivyo.

Ila itoshe tu kusema nchi hii kama zilivyo nchi zingine ina historia pana na ina mengi sana yasiyo wazi kwa wengi, kwa sie tunaopenda kujifunza ni afya kwetu kupata vingi iwezekanavyo.

Butola,
Hata mimi sijasema kwamba ndivyo ulivyosema.
Kwakuwa na mimi najifunza yale yaliyokuwa yamefichika katika historia ya ukombozi wa nchi yetu ndo nikataka kujua ulichojifunza kwa martin shikuku.
 
Samahani kwa kukuchekesha tena. Lakini ungeandika "unanichekesha" kuna "i" inakosekana hapo.

Kwetu Kariakoo, kiswahili nimezaliwa nacho, mtoto wa kike kukaza mdomo ndio nini? turejee kwenye mada. Usinkasirishe!
 
Masanja said:
Hii thread is one of my best have JF in recent years. INAFUNDISHA NA INATOA CHANGAMOTO. Nimejifunza na naendelea kujifunza sana kwa Mag3, Nguruvi, na muungwana Mohamed.

Ushauri wangu, kwa wananchi wenzangu, kamwe hatuwezi kuwa na mijadala endelevu kama hatutavua imani ya dini zetu. Kinachotukwamisha ni hiki. Tujitahidi sana kuheshimiana na tutafute suluhisho la matatizo yetu kama taifa. Umeme ukikosekana anayeathirika ni Hamisi, Said, Mwajuma, Peter, Selina nk. Tujitahidi sana kuepuka hizi emotions za udini. Siku zote nilisema kuna watu walicheza karata ya udini kwa maslahi binafsi lakini kwa uhakika walifungulia pandora`s box maana hawataweza kuuzima. In anycase it is by fate that we are a nation. Kwamba iko Siku TANZANIA inaweza kuwa nchi ya kiislam wote tukavaa kanzu. Never. Forget. Kwamba iko siku wote wataimba mapambio kanisani ya kilokole. Never. Forget it. Kikubwa tujifunze kuthaminiana na ku-celebrate tofauti zetu. Tutafute suluhisho la matatizo ya taifa letu. Kwa yeyote yule anayetaka historia imkumbuke hajachelewa bado. Tanzania kama taifa bado tunachangamoto nyingi sana. Toa mchango wako. WANANCHI tutauuona na tutakuenzi.

Swali kubwa kwetu naomba lisiwe nani alipigania uhuru. Bali tujiulize, kwa nini tulipigania uhuru? na tulipoupata tuliufanyia nini huo uhuru? je huo uhuru umetuletea nini? Mjadala kama huu ni mzuri usipokuwa na sentiments za kidini na kiimani.

Naamini kabisa taifa letu liko katika critical period na ni wasomi kama sisi wenye jukumu la kutafuta majibu ya matatizo yetu kwa kutumia elimu yetu kuliko kujenga chuki na na uhasama. Its unfortunate hizi chuki wengi wetu tunazijenga kwa maslahi binafsi. Sioni logic iko wapi ukafanye PhD Cambridge au kwingineko..halafu uje kuhubiri hapa watu wasome madrasa au mambo ya dini tuu. Its really a tragic. And this goes way far to show how the lites manipulates the poor for their own ends.

Ushauri wangu: tuwekeze katika elimu na mambo mengineyo yanayojenga ustawi wa binadamu. Yes, Iamni ni jambo muhimu sana, lakini tujitahidi kadri tuwezavyo kuwaachia wananchi/waumini wenyewe waamue ni jinsi gani ya kuabudu. Hii ya kujifanya kwamba we know what is good for entire 'we' si jambo la busara. Na ndo maana muungwana mmoja kasema hapo juu..nenda huko ulaya na America..watoto wa hao hao masultani na wafalme wanaolinda msikiti wa Mecca wanasoma top schools za ulimwengu wa leo..Harvard, Oxford, Yale, Princeton, Imperial, LSE, nk...na ndo kesho wanaenda kuwatawala wananchi wao....jamani imani ni muhimu lakini we shouldnt collectivise it. Kila mtu apewe uhuru wa kuwa yeye.

Watanzania tuamke, matatizo tuliyonayo ni mengi mno, dini inabidi liwe swala la mwisho kutufarakanisha.

Masanja,

..asante.

..uliyosema ni kweli. LIGI za udini hazina maslahi kwa taifa.​

 
Sasa hapo umeelewa nini? ni wazi kabisa hayo maneno "kaandika kuhusu TANU lakini hakuandika kuhusu walioianzisha" au na hilo ni tatizo kwako kulielewa?

"He/she wrote about TANU but he/she did not write about those who founded it..." maana naona kiswahili kinakupa taabu kuelewa.
Kweli, Bibie, Kiswahili kinanipa taabu. Mimi ni wakuja.
 
Mohammed,
Nisahihishe kama nimekosea. Katika toleo la kwanza la kitabu chako cha "Life and times of Abdulwahid Sykes" version ya Kiingereza, uliandika kuwa kura tatu zilikuwa zinalenga kuwabagua Waislamu. Baadaye nikashtuka umeandika kitabu au makala nyingine na kuita kura tatu "uamuzi wa busara." Je, unaweza kukiri hapa kwamba ulikosea kuita uamuzi wa kura tatu kuwa ulikuwa ni kuwabagua Waislamu, na ni lini ulipogundua kuwa kumbe uamuzi wa kura tatu Tabora ulikuwa ni uamuzi wa busara?
 
Butola,
Hata mimi sijasema kwamba ndivyo ulivyosema.
Kwakuwa na mimi najifunza yale yaliyokuwa yamefichika katika historia ya ukombozi wa nchi yetu ndo nikataka kujua ulichojifunza kwa martin shikuku.

Kwa ajili ya mada iliyo mbele yetu, ebu hili tuliache kwa sasa..
 
Mohammed,
Nisahihishe kama nimekosea. Katika toleo la kwanza la kitabu chako cha "Life and times of Abdulwahid Sykes" version ya Kiingereza, uliandika kuwa kura tatu zilikuwa zinalenga kuwabagua Waislamu. Baadaye nikashtuka umeandika kitabu au makala nyingine na kuita kura tatu "uamuzi wa busara." Je, unaweza kukiri hapa kwamba ulikosea kuita uamuzi wa kura tatu kuwa ulikuwa ni kuwabagua Waislamu, na ni lini ulipogundua kuwa kumbe uamuzi wa kura tatu Tabora ulikuwa ni uamuzi wa busara?
--------------------

Jasusi,

Walichokuwa wanakitafuta Waingereza ni kutia mjiti katika ya Waislam na Wakristo ili ipatikane farka. Waislam wangelikataa kushiriki katika uchaguzi ule chama kingemeguka na Nyerere angepwelewa.

Sasa hapa kigetoka chama kingine ambacho kingeingia katika kura tatu na chama hiki kingelikuwa na Wakristo kwani Waislam wangelibaki wengi katika TANU.

Hili lingetendeka lingevuruga mstakbali wa nchi yetu kabisa.

Kwa wazee wetu kukubali TANU iwalete watu kutoka nje kuja kusimama kuingia katika Legco na Waislam wabaki nje ya chombo hicho ilikuwa busara kwa maana kuwa ile farka iliepukwa na wananchi wakabaki wamoja. Angalia chini hapa:
"Mkutano ule ulitishia kuigawa TANU katikakambi mbili hasimu. Kambi moja ni ile ya wenye siasa za wastani waliopendeleakushiriki katika uchaguzi na ile ya pili ni ile ya wenye msimamo mkaliwaliotaka uchaguzi ususiwe kabisa. TANU ilinusurika na kile ambacho kingewezakuwa mgogoro ndani ya chama ambao ungewafanya wale wenye msimamo mkali kamaSheikh Suleiman Takadir, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU katika makaomakuu, na Zuberi Mtemvu, wakati huo katibu mwenezi wa TANU, kufanya mapinduziambayo yangekigawa chama kama isingelikuwa busara ya Julius Nyerere, Rais waTANU."

Mohamed
 
Kwetu Kariakoo, kiswahili nimezaliwa nacho, mtoto wa kike kukaza mdomo ndio nini? turejee kwenye mada. Usinkasirishe!

Mmmh! Makubwa! Haya ngoja tuendelee kuwasoma wanahistoria wetu haya ya kuzaliwa kariakoo na kukaza midomo hayana tija...
 
Kitu kimoja nilicho na hakika nacho kwa asilimia 100% ni kwamba wale wote wenye mapenzi ya kweli kwa taifa letu la Tanzania wanasita sana kuchangia hii hoja inayofinyangwafinyangwa na huyu anayejiita Mohamed Said. Bila kumung'unya maneno nayaita madai ya Mohamed Said la kutoa elimu ya historia ya kweli ni porojo hatari iliyojaa uchochezi ambayo lengo lake hasa ni kuleta uhasama wa kidini miongoni mwa wananchi. Sijui anachotegemea kufaidika nacho kwa kupanda hii mbegu ya hatari ambayo nina hakika mtu kama Mohamed Said anajua fika madhara yake.

Mohamed Said ni kama kipofu ambaye baada ya kusimuliwa na wazee kwamba tembo ni mnyama mkubwa kuliko wanyama wengi anapata nafasi ya kumpapasa tembo. Kwa bahati mbaya anaupapasa mguu wa tembo na si mwili wote halafu katika imani yake anadai anao uwezo wa kutoa somo kuhusu umbo la mnyama tembo na ushuhuda wake, kuwa tembo ni kama gogo la mti mkubwa, ndio ukweli na anayesema tofauti hajui kitu. Watu wote wanaolalamikiwa na Mohamed Said kuwa walisahauliwa, wengi wao walikuwa wakazi wa Dar es Salaam eneo la Gerezani.

Kabla ya uhuru Tanganyika iligawanywa katika majimbo makuu manane na katika majimbo yote hayo, jimbo la pwani kwa ujumla lilikuwa moja ya majimbo yaliyokuwa nyuma kimaendeleo kiuchumi, kielimu na kisiasa na hiyo ni licha ya kuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni yalikuwa Dar es Salaam. TAA ilianzishwa na watumishi wa serikali (civil servants) na kwa wakati wote kazi kubwa ya TAA ilikuwa ni kulalamika ikidai haki ya wafanyakazi bila upendeleo na hasa ubaguzi wa rangi katila utumishi kubwa ukiwa uonevu dhidi ya wazawa, mtu mweusi.

Jimbo la Ziwa ni moja ya majimbo yaliyokuwa mbele kiuchumi, kielimu na kisiasa na kama kuna kitu kinaweza kudaiwa kuwa kilisahaulika katika harakati ya kupigania uhuru ni mchango wa Jimbo la Ziwa (Bukoba, Mwanza, Mara na Shinyanga) Jimbo la Ziwa ndilo lililoongoza kwa idadi ya watu, idadi ya makabila, idadi ya mali asili na idadi ya machifu ambao nafasi yao ilikuwa kubwa tu katika kuhamasisha watu. Moja wa watu ambao mchango wao nitautaja kidogo tu ingawa alifanya jitihada kubwa labda zaidi ya wazee wa Mohamed Said ni Paul "Kishamapanda" Bomani.



Historia ya harakati za uhuru ni zaidi ya porojo za Mohamed Said, watu walipigania uhuru kama Watanganyika na bila kubaguana kikabila, kidini wala kijinsia. Ndio maana mimi sitaki kabisa kuwa na majibizano na huyu Mohamed Said moja kwa moja ila kwa kuwa hoja ileletwa JF, akae tayari kupewa somo kuhusu umbile zima la mnyama tembo na sio mguu moja wa tembo alioupapasa. Hapa mimi nitaongea sana kuhusu mchango wa Jimbo la Ziwa na baadaye kuonyesha jinsi maadui wa nchi yetu wanavyowatumia kidini watu kama huyu Mohamed Said.



Baadaye nitaeleza jinsi Mkoa wa Mara yenye makabila karibu hamsini yalivyoweza kushirikiana bila mfarakano na kuitikia mwito wa Mwalimu Nyerere katika hizo harakati za kudai uhuru. Je mwamko wa wakazi wa jimbo la Ziwa ulikuwaje na mapokezi gani aliyapata kila wakati Mwalimu aliporudi kwenye hili jimbo ambalo idadi ya wakazi wake kwenye miaka ya 50s ilikuwa mara tatu ya majimbo mengi Tanganyika kama Pwani. Pia nitaonyesha ni wakati gani walianza kuyasikia hayo majina anayodai Mohamed Said ya wazee wa Gerezani Dar es Salaam !

Wanaukumbi,

Kuna uzi niliambiwa kuwa mimi sijui chochote kuhusu Sablak na wenzake wa huko Meru. Nikamwaga hapa jamvini habari za Abdulwahid Sykes na Sablak kama nilvyosoma katika nyaraza za marehemu Abdu na Tanzania National Archives. Ninachosikitika ndugu zangu ni ukimya wenu.

Jamani kuweni na huruma kwani mcheza kwao hutunzwa. Hivi imekushindeni hata kusema, "Mkuu Mohamed tumekosoma." Vibaya hivyo ndugu zanguni. Nipeni motisha kidogo.

Hilo kama hamliwezi basi nipeni mji au niruhusini nitoe salam.

Mohamed

PS: Kuna mwingine akaja na Nyerere kuandika katiba nikamwaga data. Katiba ya TANU wazee wamenyanyambua ya Nkrumah. Kimya! Sisikii kitu.
MS
 
Hili la "kutuma salamu" nimelipenda....Mkuu,haya salimia ndugu wa upande ule (kama wanavyopenda kusema wenyewe)
 
Mohmed said ni activist wa mkoa wa dar es-saalam
Mohamedd Said ni Mwanahistori wa mkoa wa dar-s esalaam



Niimemuuliza swali dogo tu kuhusu maoni yake juu mwalimu nyerere kuridhia ushauri wa wataalam na kuhamishia makao makuu dodoma. Akasema hana jibu wala maoni. from that u can sense kuwa hata makao Makuu yangekuwa yemshahamia dodoma basi Mohamed said labda agetafuta namna ya kuonyesha kuwa hiyo ilikuwa ni janja ya nyerere kubadilsiah historia ya Darau kuifini dar na wanadaresalaama sababu ya chuki yake kwa wazee wa dar.


Hili nalo la Dodoma ni sehemu ya mambo ya historia na issue Zilizoanza Chini ya Nyerere .Je lilikuwa jema au baya.? Ebu tupate majibu Mohamed Saidi acha kukwepa kwepa
.
 
Nguruvi3
.Abdallah Salum alikuwa mmoja wa wachangiaji wa chuo hicho na mwanae Salum Matimbwa hadi leo amehifadhi stakabadhi ya malipo ya sh. 50.00 stakabadhi ambayo ina saini ya Bhoke Munanka."

Mohamed
Tangu jana nimekuwa nafuatilia mjadala huu bila ya kuchangia chochote kile lakini huku nikitafakari ni nini hasa hoja ya MS. Jee MS anaamini kwamba wazee wake pekee wa Gerezani wengeweza kuikomboa nchi hii bila ya Watanganyika wa majimbo mengine kushiriki? Ms anataka tuamini hao wazee wake wa Gerezani wote ni wazaliwa wa Gerezani tangu kuumbwa kwa dunia na hawajatokea bara kama vile wamanyema, wanubi, na wanyamwezi ambao walikuwa ni wapagazi wa wajerumani?

Nilirudi kwenye mada. Hapo kwenye nyekundu kuna swali ndugu yangu MS nataka kukuuliza. Umesema Abdalah Salum alikuwa ni "mmoja" wa wachangiaji, hiyo haimaanisha kwamba kulikuwa na wachangiaji wengi waliochangia ujenzi wa Chuo Kikuu Cha kwanza? Na swali la pili ni kama mchango wa sh. 50.00 ambao risiti yake bwana Salum Matimbwa ameihifadhi hadi leo ilikuwa ni asilimia ngapi ya gharama zote za ujenzi wa Chuo kikuu cha kwanza pale Lumumba? Kama unaweza kutuwekea sisi watu wakuja BOQ ya ujenzi wa jengo zima utatusaidia zaidi.
 
M Said wewe mwaga historia ya wazee wako,sisi tutachambua tunapoona au tunapohisi kuna a grain of truth,hili la katiba ya TANU kubanduliwa kwa Nkurumah ni news kubwa kwa wengi wetu
 
K
Wanaukumbi,

Kuna uzi niliambiwa kuwa mimi sijui chochote kuhusu Sablak na wenzake wa huko Meru. Nikamwaga hapa jamvini habari za Abdulwahid Sykes na Sablak kama nilvyosoma katika nyaraza za marehemu Abdu na Tanzania National Archives. Ninachosikitika ndugu zangu ni ukimya wenu.

Jamani kuweni na huruma kwani mcheza kwao hutunzwa. Hivi imekushindeni hata kusema, "Mkuu Mohamed tumekosoma." Vibaya hivyo ndugu zanguni. Nipeni motisha kidogo.

Hilo kama hamliwezi basi nipeni mji au niruhusini nitoe salam.

Mohamed

PS: Kuna mwingine akaja na Nyerere kuandika katiba nikamwaga data. Katiba ya TANU wazee wamenyanyambua ya Nkrumah. Kimya! Sisikii kitu.
MS

Mkuu bwana MS ukiacha swala la katiba kkuwa hakuandika mzee nyerere lakini pia ktk kumbukumbu zako zinaonyesha pia hata ile hotuba iliosomwa umoja wa mataifa na mwalimu nyerere pia hakuiandika yeye naomba utuweke sawa katika hilo.ili tuzidi kuiweka sawa historia iliosahaulika kutajwa.
 
K

Mkuu bwana MS ukiacha swala la katiba kkuwa hakuandika mzee nyerere lakini pia ktk kumbukumbu zako zinaonyesha pia hata ile hotuba iliosomwa umoja wa mataifa na mwalimu nyerere pia hakuiandika yeye naomba utuweke sawa katika hilo.ili tuzidi kuiweka sawa historia iliosahaulika kutajwa.

Shadhuly,

Hiyo nimeiweka kama saa moja iliyopita na nikaeleza kuwa document hiyo sasa haipatikani Maktaba ya CCM wala National Archives. Mimi kote nimepita huko kuitafuta.

Hebu zidurusu hizi nyuzi zangu utaikuta.

Mohamed
 
Tangu jana nimekuwa nafuatilia mjadala huu bila ya kuchangia chochote kile lakini huku nikitafakari ni nini hasa hoja ya MS. Jee MS anaamini kwamba wazee wake pekee wa Gerezani wengeweza kuikomboa nchi hii bila ya Watanganyika wa majimbo mengine kushiriki? Ms anataka tuamini hao wazee wake wa Gerezani wote ni wazaliwa wa Gerezani tangu kuumbwa kwa dunia na hawajatokea bara kama vile wamanyema, wanubi, na wanyamwezi ambao walikuwa ni wapagazi wa wajerumani?

Nilirudi kwenye mada. Hapo kwenye nyekundu kuna swali ndugu yangu MS nataka kukuuliza. Umesema Abdalah Salum alikuwa ni "mmoja" wa wachangiaji, hiyo haimaanisha kwamba kulikuwa na wachangiaji wengi waliochangia ujenzi wa Chuo Kikuu Cha kwanza? Na swali la pili ni kama mchango wa sh. 50.00 ambao risiti yake bwana Salum Matimbwa ameihifadhi hadi leo ilikuwa ni asilimia ngapi ya gharama zote za ujenzi wa Chuo kikuu cha kwanza pale Lumumba? Kama unaweza kutuwekea sisi watu wakuja BOQ ya ujenzi wa jengo zima utatusaidia zaidi.

Kigarama,

Niruhusu hili la kwanza kukujibu niandike Kingereza maneno machache.

"You are missing the point. It is not the value but the thought behind."

Hela alizotoa Mzee Saluma Matimbwa ni kiasi kidogo sana. Wala mimi
sikuandika yale kwa kufaharisha thamani. Hata kidogo.

Nia na madhumuni ilikuwa kuonysha ari ya wazee wangu katika kila
jambo lililokusudiwa kuleta maendeleo ya Mwafrika.

Safari ya Nyerere UNO Bantu Group na akina Tatu bint Mzee, Kidawa Bint
Abdallah walikuwa wakipita nyumba kwa nyumba kuchangishana thumni,
thumni. Hii ndiyo ilikuwa "spirit ya TANU."

Wazee wa Gerezani peke yao kamwe wasingeweza kufika popote bila ya
kuungwa mkono na Watanganyika wote.

Hili wazee wakilijua zamani na fika na ndiyo maana kuanzia 1950 Abdu
alikuwa akimshawishi Chifu Kidaha Makwaia aingie TAA wampe urais kwa
kuzingatia kuwa Chifu Kidaha akija TAA Wasukuma watamfuata kiongozi
wao na TAA itapata nguvu.

Hilo lingetendeka wangeliunda TANU na Chifu Kidaha angekuwa rais wa
TANU. Chifu Kidaha aliona yeye maslahi yake yapo zaidi na Waingereza.

Chief Kidaha alikuwa "diner" nyingi nyumbani kwa Abdulwahid lakini kila
Abdu alipomgusia hili hakufua dafu hadi alipokutana na Nyerere 1952.

Hebu staladhi na hiki kijembe cha Nyerere kwa Chifu Kidaha kwenye hafla
moja ya taarab Mtaa wa Mvita mwaka wa 1957:

"Katikahafla hiyo waheshimiwa, wageni waalikwa walipewa vitafunio, vinywaji baridi nachai. Nyerere katika kutoa shukrani kwa wanachama wa TANU alikamata kikombe chachai na kukionyesha juu kwa wasikilizaji wake. Aliwaambia watu kwamba wasidhanikitendo cha kumpa mtu kikombe cha chai ni kitu kidogo. Nyerere aliendeleakusema kuwa watu wameiuza nchi hii kwa kupewa kikombe cha chai na wakoloni.Nyerere alikuwa akitoa maneno hayo akiwa anawapigia vijembe watu maalum.Nyerere kwa maneno yake alikuwaakiwakusudia machifu. Baadhi yao walikuwa pale pale katika meza kuu wakinywachai na yeye. Wakati huo baadhi ya machifu walikuwa wakishirikiana na GavanaTwining na UTP katika hila za kuipiga vita TANU ishindwe kuikomboa Tanganyikakutoka makucha ya ukoloni. Ilikuwa dhahiri kuwa makombo waliyokuwa wakipatamachifu kutoka kwa Mwingereza hayakuwa hata na thamani ya kikombe cha chai.Maneno ya Nyerere hayakuwa fumbo kwa wale machifu. Yalikuwa maneno ya waziambayo waliyaelewa. Machifu walitambua kuwa wao ndiyo walikuwa wakisemwa katikahotuba ile ya shukurani. Lakini kijembe kile kwa hakika yake kilikuwakimeelekezwa kwa Chifu Kidaha. Chifu Kidaha alikuwa na bahati mbaya sana.Abdulwahid Sykes miaka michache nyuma alimbembeleza sana ajiunge na TAAwamfanye rais kisha waje kuunda TANU na yeye wamchague kuwa rais lakinialikataa."

Mohamed
 
Hili la "kutuma salamu" nimelipenda....Mkuu,haya salimia ndugu wa upande ule (kama wanavyopenda kusema wenyewe)

Kwanza salamu zangu ndugu mtangazaji napenda kuzituma kwa Sanda Matuta na wana ukumbi wote!

Mohamed
 
Nilirudi kwenye mada. Hapo kwenye nyekundu kuna swali ndugu yangu MS nataka kukuuliza. Umesema Abdalah Salum alikuwa ni "mmoja" wa wachangiaji, hiyo haimaanisha kwamba kulikuwa na wachangiaji wengi waliochangia ujenzi wa Chuo Kikuu Cha kwanza? Na swali la pili ni kama mchango wa sh. 50.00 ambao risiti yake bwana Salum Matimbwa ameihifadhi hadi leo ilikuwa ni asilimia ngapi ya gharama zote za ujenzi wa Chuo kikuu cha kwanza pale Lumumba? Kama unaweza kutuwekea sisi watu wakuja BOQ ya ujenzi wa jengo zima utatusaidia zaidi.
Kigarama, nashukuru sana maana nimeandika kitu kama hiki katika makala ya Mohamed Said ile inayoendelea thread nyingine.

Nimehoji kuwa ni vema kama Matimbwa alitoa mchango huo na tunauthamini sana, lakini kwa bahati mbaya kama ilivyo ada ya Mzee Said pesa hizo sio hoja, hoja ni kuinasibisha na jina la Salum na wala si Matimbwa, hapo unajua kinaendelea nini.
Katika makala zake Mohamed amemtaja John Rupia kama mtu aliyetoa kiwanja cha ujenzi, lakini huwezi kumsikia John akitajwa kwasababu ni John. Hapo ndipo tunapohoji sana makala za Mohamed na 'Biasness'.

Ukitaka kuona mkanganyiko zaidi, ni pale Mohamed Said anaposema hotuba ya Nyerere UNO iliandikwa na Sykes na kufanyiwa editing Mzumbe kabla hajaenda nayo UNO. Hili laweza kuwa ni kweli lakini linazaa maswali mengine. Nyerere alipofika Dar alikuwa ni msomi mzuri tu aliyehitimu Makerere na Edimburgh. Inaingia akilini zaidi kuwa ufahamu wake wa mambo ya kimataifa ulikuwa mkubwa sana kuliko wenzake wengi.

Labda ingeandikwa kuwa hotuba iliandikwa kwa ushirikiano wa abc ningeelewa zaidi. Sidhani Nyerere alikuwa mtu wa kuandikiwa hotuba aende akaisome tu bila ye yeye kuwa na ushiriki wa kujua nini anaenda kuongelea.

Na kuthibitisha kuwa hotuba iliandikwa kwa ushirikiano naomba nimnukuu mzee Said '........Sykes aliandika na kuituma kwa basi Mzumbe na kisha kurudishwa kwakwe.....' Sasa kama aliandika na ikafanyiwa edit Mzumbe ni wazi kulikuwa na ushirikiano wake na wenzake, ushirikiano ambao nadhani ulimgusa aliyetakiwa kwenda kutoa hotuba UNO.

Hii haina maana Sykes hakuandika au hakuna nakala ya hotuba! maana yake halisi na anachotaka kusema Mohamed ni kuendelea kumdhalilisha Nyerere kama alivyowahi kusema ' wazee walimjua Nyerere wakati akiwa si lolote si chochote' na pia ' ......Kiyate akampa pesa za kwenda kariakoo kununua mboga n.k.

Ukisoma makala za mzee Said sehemu inayomhusu Nyerere inanasibishwa sana na ubaya. In short, his intention is to potray the negative image about Mwalimu, despise him, above all to make Nyerere as public enemy number one. Mohamed hates Nyerere to the core.
Mzee Said strives to make his grievance as a 'public issue'.
As long as you stand to correct the history, the same will correct you.
 
Back
Top Bottom