Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Nadhani hapo watu wako kwenye kupinga tu...na wala haito tufikisha kokote kama hamuwezi kuchagua haki na kuifata,hii inakumbusha ule msemo wa "mfa maji,haishi kutapata" mara hili mara lile kwa kigezo cha kujiita "censors" "see things in a big picture".
Gazeti la Mwananchi leo tena kwaniaba ya "muhandishi wetu" kuna interview ya Sihiyana Mandevu dereva wa tax aliye kuwa akimbeba Nyerere toka wakati wa mtaa wa pemba na New street,Kkoo na New street na wajumbe walele hadi St Joseph ambapo huku wajumbe walibadilika kuwa wengine ambao hakuwafahamu,sasa kama kweli we claim to see thing in that "big picture"....why then we don't connect the dots!!?? Hauitaji kwenda Bweni kujifunza
Isome tena makala hiyo ndugu yangu. Ulichokimbia kubandika humu sicho kilichoandikwa mle. Ningekuwa na uwezo wa kuishusha yote humu ningewashushia. Bahati nzuri Mzee huyu bado yuko hai. Au naye alisahaulika?
 
Mohamed mara nyingi haujibu ulichoulizwa. Tanganyika haikuwahi kuwa koloni la Mwingereza. Huku kupigania UHURU unakokukuza sana hapa sielewi kunatoka wapi. Najua unajua zipo Nchi zilizopigania uhuru kwelikweli. Hivi Mzee wetu Kleist alianzisha AA kwa kuwa alikuwa MUISLAMU? Mohamed, acha pia kuwasingizia marehemu wetu hawa mambo mengi kwa kuwa unajua hawapo tena duniani.

WC,

Kama kuna mahali nimesema Kleist alianzisha AA kwa kuwa alikuwa Muislam tafadhali nionyeshe. Lakini hebu msome na msikilize Kleist mwenyewe anasema nini:

"Mwaka wa 1929 Kleist na baadhi ya rafikizake wa karibu kama Mzee bin Sudi, ambaye wazazi wake walikuwa Wamanyema kutokaBelgian Congo, Ibrahim Hamis - Mnubi ambaye baba yake alitoka Daffur nchiniSudan, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima - Mzaramo, Suleiman Majisu, Raikes Kusi,Rawson Watts na Cecil Matola - Myao kutoka Masasi walianzisha AfricanAssociation, Kleist akiwa katibu muasisi. Wakati ule Gavana wa Tanganyika alikuwa Sir Donald Cameron ambaealitawala Tanganyika kuanzia mwaka wa 1925 ñ 1929. Cameron alikuwa gavanamliberali na alikuwa akifahamiana na Kleist. Cameron ndiye aliyeanzisha Barazala Kutunga Sheria la kwanza na mfumo wa Indirect Rule katika Tanganyika.Msimamo wake huu ndiyo hasa uliochangia katika kuwezesha kunzishwa kwa AfricanAssociation. Lakini juu ya haya yote, chama hiki kiliaswa kisijiingize kabisakatika siasa. Wakati chama hiki kinaanza tayari kulikuwepo na chama cha Wazunguna Waasia. Lakini katika Baraza la Kutunga Sheria Waafrika walikuwawakiwakilishwa na padri wa Kikatoliki, Father Gibbons, ambae hakuwa hataanaishi na Waafrika bali akikaa Minaki Misheni nje ya Dar es Salaam. Abdulwahidanakumbuka baba yake akimwambia sababu ya kuanzishwa kwa African Association: "Wakati ule vilikuwepo vyama viwili.Kilikuwapo European Association na Indian Association. Vyote viwilivilishugulika na watu wao wenyewe. Lakini Waafrika hawakuwa na chama kama hichokuwatetea. Katika Baraza la Kutunga Sheria Waafrika waliwakilishwa nammishionari Mzungu jina lake Father Gibbons, aliyekuwa akifanya kazi Misheni yaMinaki maili kadhaa nje ya Dar es Salaam. Lakini kwa hakika mzungu huyu hakuwana uhusiano wowote na Waafrika aliokuwaakiwawakilisha. Kwa ajili hii Waafrika walipohisi hawawakilishwi na hawanachama kama kile cha Wazungu na Waasia kutafuta haki zao, walikutana na kuamuakuunda chama chao wenyewe." [1]Kuanzishwa kwaAfrican Association nje ya utaratibu uliokuwapo wa kuwa na vyama vya kidini nakikabila kilikuwa kitu dhidi ya mfumo uliozoeleka na uliojengeka katika utawalawa kikoloni. Ingawaje chama hicho kilikuwa kinaungwa mkono na Gavana DonaldCameroon na kikasajiliwa kama chama cha ustawi wa jamii, wamishionariwaliwatahadharisha Wakristo wasijihusishe na chama: "mara kwa mara Wakristowalikuwa wakitahadharishwa wasijihusishe na harakati zozote zitakazopingana naserikali."[1]Katika kuwatadharisha Wakristo wasijihusishe na siasa, wamishionari walikuwawanayakini labda kutokana na uzoefu wao sehemu nyingine kuwa, vyama kama hivivya ustawi wa jamii hatimae huwakilisha madai ya watu, hili likitokea basi watuhuasi dhidi ya utawala."
(Kipande yaani haya niliyoandika yamo kwenye kitabu cha Abdu Sykes nimeyatoa kwenye kumbukumbu za Kleist Sykes alizoandika kwa mkono wake mwenyewe kabla hajafa mwaka 1949)
Mohamed
 
Mzee Said unafikiri ni kwa kiasi gani mfumo wa ufisadi na vitendo vinavyotokea kwenye mfumo huo (wizi wa EPA, manunuzi ya ndege ya rais na rada na ubadhirifu wa mali ya umma pamoja na matumizi mabaya ya mabaraka - nikitaja vichache) umeathiri maisha ya mamilioni ya Waislamu wa Tanzania?

Duuuuu!

Mohamed
 
Isome tena makala hiyo ndugu yangu. Ulichokimbia kubandika humu sicho kilichoandikwa mle. Ningekuwa na uwezo wa kuishusha yote humu ningewashushia. Bahati nzuri Mzee huyu bado yuko hai. Au naye alisahaulika?

Mkuu WC,

Mimi nakubari kukosolewa na kukubari kurekebika pale nilipo teleza,sasa naomba nieleweshe lilo ambalo sijaling'amua kwenye ile habari?

Nimeileta hapa hiyo tu kwasababu yule Bwn. yu hai na anaweza kuwa source nzuri tu ya yale tunayo pingana hapa
 
GU
Bora umemjibu huyo bibi .... Nilishangaa sana huyu mama alivyokurupuka Udini ni kitu kibaya sana .... Yaani Nyerere katoka scotland na alikuwa ni mwalimu halafu unasema alikuwa hajui kuvaa suruali. Sasa hao wanafunzi aliokuwa anawafundisha si walikuwa hawavai nguo kabisa.. FF mama usikurupuke kumbuka kuwa hapa wapo watu makini
[h=2] This message is hidden because FaizaFoxy is on your ignore list. [/h] View Post
 
Mkitaka kujua udikteta wa nyerere chunguzeni habari za Tuntemeke Sanga aliporudi kutoka masomoni kitu nyerere alichomfanya na habari kama hizi zinafichwa na historia inapindishwa ili kumfanya nyerere abaki kuwa juu lakini siku zote haki na batili hutengana au kwa anayebisha akasome vutabu vifuatavyo:THE DARKNESS OF MWL J NYERERE AU THE PATNERSHIP CHA ABDU JUMBE
 
Nguruvu3,

Mimi nakutaka radhi kwa wewe kuumuzwa na lugha na vitendo vyangu. Lakini nakuhakikishia hiyo haikuwa nia yangu. Tusameheane na tuendelee na mjadala.

JF ni kubwa kuliko hisia zangu na zako na za yeyote yule na ndiyo maana katutandikia jamvi tumekaa kwa raha mustarehe tunajadili.

Hatuna cha kumlipa JF isipokuwa sisi tuoneshe ukomavu wa fikra.

Hisani anotufanyia JF ni kubwa kupita kiasi.

Niwie radhi ndugu yangu.

Mohamed
Maneno mazito sana haya ..na yamejaa busara ndani yake...kila la kheri MS
 
Mzee Said unafikiri ni kwa kiasi gani mfumo wa ufisadi na vitendo vinavyotokea kwenye mfumo huo (wizi wa EPA, manunuzi ya ndege ya rais na rada na ubadhirifu wa mali ya umma pamoja na matumizi mabaya ya mabaraka - nikitaja vichache) umeathiri maisha ya mamilioni ya Waislamu wa Tanzania?

Duuuuu!

Mohamed

MS mkuu wetu ...hata mimi nilikuwa nangojea sana jibu la hilo swali kutoka kwa mzee mwanakijiji..nadhani una andaaa nondo za kuja kumjibu..
ahsante!!
 
Hilo swali la mambo ya EPA, ndege ya rais nk kalielekeza sipo.

Mohamed

Sheikh Mohaed,

Bila shaka hili la EPA na ndege ya raisi ni mambo ya juzi juzi hapa kwa kikwete na mkapa!

Hapa tunazungumzia enzi za Nyerere. Lakini si kweli kwamba mfumo huo (wa ufisadi) una athari za moja kwa moja katika mnakasha huu?
 
Sheikh Mohaed,

Bila shaka hili la EPA na ndege ya raisi ni mambo ya juzi juzi hapa kwa kikwete na mkapa!

Hapa tunazungumzia enzi za Nyerere. Lakini si kweli kwamba mfumo huo (wa ufisadi) una athari za moja kwa moja katika mnakasha huu?

=Mohamed
 
Duh watu hamlali, hamli, hamfanyi kazi maana kasi hii inatisha mjadala mpaka saa nane za usiku!!! Mjadala moto kweli kweli. Sheikh Mohamed Endelea kumwaga vitu. Faiza hebu nifahamishe jinsi kuweka picha nina picha za jiji la Dar miaka 1960-1900. Nadhani zitamtoa Mag3 matongo kuhusu mtazamo hasi Dar ilikuwa vipi. Maana amezungumza kauli si nzuri na kudhalilisha kuhusu wakazi wa Dar. Nikipata muda nitazibandika.
 
Kuna mtu nimemuomba amalezo hapo juu,sijapata majibu na kama kuna mtu anaweza tusaidi kwa "lugha nyepesi " afanye hivyo ni maana ya ile makala ambayo mimi sijaelewa ila nimekimbilia "kupost huku"????

FF,wewe mjuzi wa kiswahili tafadhali embu ni juze,nifahamu kosa langu.Hiyo makala ipo kwenye kile kijarida chetu haya yote yalipoanzia katika gazeti la Mwananchi
 
Mkitaka kujua udikteta wa nyerere chunguzeni habari za Tuntemeke Sanga aliporudi kutoka masomoni kitu nyerere alichomfanya na habari kama hizi zinafichwa na historia inapindishwa ili kumfanya nyerere abaki kuwa juu lakini siku zote haki na batili hutengana au kwa anayebisha akasome vutabu vifuatavyo:THE DARKNESS OF MWL J NYERERE AU THE PATNERSHIP CHA ABDU JUMBE
Kwa hiyo kumbe huo "udikteta" anaosemekana kuwa nao Nyerere haukujali dini ya mtu?Au na Tuntemeke Sanga alikuwa muislam..!?
 
Kuna mtu nimemuomba amalezo hapo juu,sijapata majibu na kama kuna mtu anaweza tusaidi kwa "lugha nyepesi " afanye hivyo ni maana ya ile makala ambayo mimi sijaelewa ila nimekimbilia "kupost huku"????

FF,wewe mjuzi wa kiswahili tafadhali embu ni juze,nifahamu kosa langu.Hiyo makala ipo kwenye kile kijarida chetu haya yote yalipoanzia katika gazeti la Mwananchi

Hawana majibu huwa wanasema tu, hata nilipowauliza mimi huko wakaja wanatokwa povu mdomoni, nikawaambia haya, hayo tuyawache kiporo, tuendelee na mengine, wapii? Hakuna.

Sasa wewe huoni ajabu, hapa inajadiliwa mada za Historia na maandiko ya Mohamed Said anakuja mtu anauliza kuhusu EPA na ndege za Rais. Haki ya Mungu, nnacheka maana mengine hata kujizuwia siwezi. Wananchekesha.
 
Mkitaka kujua udikteta wa nyerere chunguzeni habari za Tuntemeke Sanga aliporudi kutoka masomoni kitu nyerere alichomfanya na habari kama hizi zinafichwa na historia inapindishwa ili kumfanya nyerere abaki kuwa juu lakini siku zote haki na batili hutengana au kwa anayebisha akasome vutabu vifuatavyo:THE DARKNESS OF MWL J NYERERE AU THE PATNERSHIP CHA ABDU JUMBE
Tuntemeke Sanga alikuwa Muislamu?
 
Tunawaambia tuonesheni hapo anapokosea Mohamed Said, hamtuoneshi. Mohamesd Said yupo hapa hapa hajajificha kujibu, mmekazana anapandikiza anapandikiza, mimi nawaambia nyinyi mmeshapanda, mmepalilia na sasa bado kuvuna tu. Msomeni vizuri Mohamed Said, anafanya kila jitihada mavuno yasiwepo.
Soma tena bango #722 la Nguruvi3
 
Back
Top Bottom