Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Mdondoaji,

Nitajibu maeneo mawili katika hoja zako;

Suala la kukataliwa kwa MoU ya sheikh Ponda linaanzia kwa mzee wetu al haj ali hassan mwinyi aliyekuwa raisi wakati hiyo proposal imepelekwa.

Lakini pili, juzi wakati kikwete anawaambia na ninyi pelekeni proposal yenu ili mpate ruzuku, hapo ndio palikuwa mahali muafaka pa kumweleza muislamu mwenzenu kwamba kuna proposal ya sheikh ponda tayari na serikali haijasema ina mapungufu gani!

Sasa ukituuliza sisi hapa sababu za kukataliwa kwa hiyo proposal ya sheikh ponda wakati ukifahamu kwamba serikali haikuwahi kutoa majibu inakuwa vigumu kukujibu.

Wandugu,

Kama kuna uwezekano wa kuweka hiyo proposal hapa jukwaani tuione .......halafu mwenye proposal ya Wakatoliki/Wakristo..........atuwekee ili tuidadavue tujue pumba ziko wapi na mchele uko wapi..........

serikali ni watu na watu ndio sisi..............kama proposal ilikataliwa naamini kabisa ilikuwa ni baada ya uchambuzi wa binadamu kama sisi hapa JF.....kwa hiyo ninaamini hiyo proposal ikiwekwa hapa tutaona kama ina mapungufu au ilikuwa "mfumokristo" kuweka ntimanyongo.....

NOTE: Kwa atakayeweka hiyo proposal hapa......tafadhali atuwekee the original version.........
 
Sheikh Mohamed,

Ni kweli utaendelea kuutaja uislamu kama ambavyo na sisi tutaendelea kukukatalia kwamba hao wazee walipokuwa wanapigana, hawakusukumwa na uislamu wao bali uafrika wao na utanganyika wao.

Kwakuwa umeamua kumpigia back pass sweke, ngoja na mie nikurudishie back pass.

Askari wa kimanyema, kinubi na kizulu (waislamu) walishirikiana na wazungu wajerumani (wakristo) kupambana na mwafrika mwenzao mkwawa (muislamu) na hatimaye kushinda vita na kupelekea mkwawa kujinyonga.

Kwahiyo hapa tuseme waislamu walikuwa wanapigana dhidi ya uislamu ama muislamu mwenzao? hapana, ni dhahiri kwamba waafrika(niwaite mamluki) walikuwa wanatumikia mabwana zao kwa ajili ya maslahi yao binafsi. Na hawakupigana kwa mgongo wa uislamu bali walitumikia utumishi wao kwa mjerumani.

Sasa ilipofika zamu ya waingereza kuitawala tanganyika, hawa wamanyema, wanubi na wazulu (waislamu) hawakuwa na previledge walizokuwa wakipata enzi za mjerumani kwahiyo waliunganisha nguvu na wenyeji wao katika kupigana na muingereza. Walipigana kama watanganyika na si waislamu! pamoja na kwamba walikuwa na imani ya uislamu lakini hawakusukumwa kwenda kupigania uhuru kwa sababu ya uislamu wao bali utanganyika wao na uafrika wao.

Askari hao hao wa kizulu, kinubi na kimanyema(waislamu) ndio hao hao walitumika na mkoloni kupambana na bushiri pangani (muislamu). Je hapo kulikuwa na agenda ya uislamu? hapana, walikuwa wanawatumikia mabwana zao wajerumani! Tukifika mahali pa kutenganisha uislamu na utanganyika tutakwenda pamoja vizuri sana, short of that itakuwa ni kuyumbishana tu.


Ogah,

Tafadhali msome Nimitz, August H, "TheRole of Sufi Order in Political Change,"Ph D Thesis Indiana University, 1973 au "
Islam and Politics in East Africa,"University of Minnesota Press, Minnapolis, 1980 huenda hii hofu yako ya Uislam katika siasa za Tangnayika ikaondoka au ikapungua. Mimi si mtafiti wa kwanza kuona nafasi ya Uislam katika maendeleo ya siasa Tangnayika.

Hayo uliyosema ya Wanubi, Wazulu na Wamanyema kuja kama mamluki yote yamo kwenye kitabu changu tena mimi nimeingia ndani zaidi hata kueleza jinsi watu hawa walivofadhiliwa na Wajerumani kiasi cha kuwapata watu kama akina Kleist waliopewa elimu ya juu kwa wakati ule kitu ambacho kilikuja kusaidia jamii yake na yeye mwenyewe kufainikiwa sana katika maisha na siasakiasi cha kubakia kama kumbukumbu katika historia ya Tanganyika.

Ila nakukumbusha kitu kimoja AA viongozi wake wengi walikuwa Waislam na hawa ndiyo vilevile walikuwa viongozi wa Al Jamitul Islamiyya fi Tanganyika.Ali Mwinyi Tambwe na Idd Faiz Mafongo walitokea Al Jamiatul Islamiyya kuingia TANU. Michango ya hawa watu katika TANU nimeieleza humu ndani kwa kirefu sana.

Hata hivyo mimi simlazimishi yeyote kuitafsiri historia kwa muono wangu lakini popote nialikwapo mimi huwa naisomesha historia ya Tangnayika kwa mtindo huu.

Mohamed
 
Ningekuwa mmiliki wa JF mijadala hii miwili humu ningeitafsiri ikawa kitabu ikatosha kujibu kitabu chako hicho. Wazungu wanadanganyika kirahisi mno lakini wakigundua uliongozwa na hisia na vionjo vya UDINI kukiandika watakubeza sana tu.

WC,

Jibu lako mbona halifanani hata kidogo na taarifa zangu nilizokuwekea kuhusu umuhimu wa maandiko yangu katika tasnia ya historia ya Tanganyika?

Umekosa chochote cha kusema?
Basi ikiwa hivyo ndivyo kaa ukijua siandiki "porojo" ila "serious academic discourse."

Walimu wa historia wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wanakikwepa kitabu changu na siwalaumu.
Kwa nini mtu ajichome mwenyewe na mwiba?

Mohamed
 
WC,

Jibu lako mbona halifanani hata kidogo na taarifa zangu nilizokuwekea kuhusu umuhimu wa maandiko yangu katika tasnia ya historia ya Tanganyika?

Umekosa chochote cha kusema?
Basi ikiwa hivyo ndivyo kaa ukijua siandiki "porojo" ila "serious academic discourse."

Walimu wa historia wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wanakikwepa kitabu changu na siwalaumu.
Kwa nini mtu ajichome mwenyewe na mwiba?

Mohamed
Hii ya wazee wako kusahaulika kwa sababu ya Mwalimu kutaka iwe hivo mbona ni sehemu ndogo sana ya historia ya NCHI hii. Tatizo lilikuja pale ulipoingiza DINI yao kuwa ndio iliyosababisha wachukiwe na Mwalimu. Mwalimu akaendelea kushirikiana kwa karibu sana na WAISLAMU wengine wa nchi hii kuongoza taifa na TANU yetu na baadae CCM. Hawa WAISLAMU walioendelea kushirikiana na Mwalimu kwako si lolote wala chochote. Hatimaye Mwalimu alipostaafu Urais na Uenyekiti wa CCM akamwachia MWISLAMU safi kabisa. Bado hili nalo dogo mno kwako. Wewe ulitaka WAMANYEMA wako wa Kariakoo wapewe NCHI kweli?
 
Hii ya wazee wako kusahaulika kwa sababu ya Mwalimu kutaka iwe hivo mbona ni sehemu ndogo sana ya historia ya NCHI hii. Tatizo lilikuja pale ulipoingiza DINI yao kuwa ndio iliyosababisha wachukiwe na Mwalimu. Mwalimu akaendelea kushirikiana kwa karibu sana na WAISLAMU wengine wa nchi hii kuongoza taifa na TANU yetu na baadae CCM. Hawa WAISLAMU walioendelea kushirikiana na Mwalimu kwako si lolote wala chochote. Hatimaye Mwalimu alipostaafu Urais na Uenyekiti wa CCM akamwachia MWISLAMU safi kabisa. Bado hili nalo dogo mno kwako. Wewe ulitaka WAMANYEMA wako wa Kariakoo wapewe NCHI kweli?

WC,

Umehamaki.
Wala hujajibu nilichokuuliza lakini nakuacha kwanza upoe kisha Insha Allah tutaendelea.

Ila sina "Wamanyema wangu"

Mohamed
 

WC,

Umehamaki.
Wala hujajibu nilichokuuliza lakini nakuacha kwanza upoe kisha Insha Allah tutaendelea.

Ila sina "Wamanyema wangu"

Mohamed


WC,

Nataka kukusikia ukisema chochote kile kuhusu haya hapa chini kwa kuwa ulizunguza kuhusu KUBEZWA:

Namshukuru Allah sijabezwa ila nilitiwa katika jopo la Dictionary of African Biographies (DAB) kama mtafiti huu ni mradi wa Oxford University Press, New York.

Google hiyo DAB utapata habari zake kamili.

Waingereza wakanitia katika project nyingine ya kuandika kitabu cha historia kwa shule za msingi ili watoto wajifunze Kiingereza na historia ya nchi yao kwa pamoja.

Nimeandika kitabu "Torch on Kilimanjaro" kimechapwa na Oxford University Press, Nairobi.

Oxford Nairobi walifurahishwa na kazi hii wakanitia katika African Anthology kitabu kilichochangiwa na wandishi wengi kutoka Afrika.

Tanzania nasi tumo na mimi ndiye niliyewakilisha kazi mojawapo humo.

Na mambo mengi tu ya kunitia moyo kuwa kazi zangu ni za kisomi.

Nadhani tumefahamiana.

Lakini ukipenda kunipuuza hiyi ni khiyari yako ila ukiwa unataka kujua historia ya kweli, ahlan wasaalan.
Nilichonacho ni amana toka kwa Allah SW na mwenyewe ukijataka amana yako uadilifu ni mie kukukabidhi na hii ndiyo kazi niifanyayo humu JF.

Kuelimisha.

Mohamed

NB: Unapoingia mnakasha na mie basi ujue nini cha kutegemea kutoka kwangu siyo "porojo" " but serious world recognised academic discourse."

MS
 
Makao makuu ya Mtwa Mkwawa kuna wakati yalijulikana kwa jina la Unguja na upande wa pili wa makao hayo makuu kunajulikana kwa jina la Ibangamoyo ikiwa ni "Corrupt name" ya jina Bwagamoyo au Bagamoyo kama inavyojulikana sasa hivi. Wazee wote wanakubaliana kwamba Mkwawa na familia yake walikuwa wako karibu sana na waislamu kutoka pwani kutokana na kufanya nao biashara na ulinzi aliokuwa anaipa misafara yao ya kibiashara.

Mkwawa kuwa muslamu au la kumewafanya wazee wajiulize kama alisilimu mbona akupewa jina la Kiarabu kama kina Rumaliza? Mkwawa jina lake la kiarabu aliitwa nani?

Lakini wote wanasema hakuna ushahidi wowote kwamba Mkwawa mwenyewe aliwahi kwa wakati wowote kuwa ni muislamu. Wanasema kwa wakati fulani mkwawa alishawahi kukaa kwa mjomba waka maeneo ya Mpwapwa ya sasa na huko nako aliwa na mahusiano na chifu wa Wagogo. Familia ya kina Muyinga (Shina la ukoo wa Mkwawa) lina mahusiano ya karibu na kina Lusinde wa Dodoma

Mkwawa si jina lake halisi bali alipewa kutokana na kuteka teka nchi za makabila mengine, ndiyo akaitwa "Mkwavinyika" yaani Mteka nchi. Hadithi inaendelea hadi tufikie kama Mkwawa alikuwa ni muislamu au la. Barua za Mkwawa kwa Irabu za kiarabu zilikuwa zimeandikwa nini ndani yake na nani anaweza kututhibitishia kama kweli ziliandikwa na Mkwawa mwenyewe?

Hivi kuandika kwa Irabu za Kiarabu huwezi kuandika "migolole, magobore na chumvi vimeshafika?"
 
Makao makuu ya Mtwa Mkwawa kuna wakati yalijulikana kwa jina la Unguja na upande wa pili wa makao hayo makuu kunajulikana kwa jina la Ibangamoyo ikiwa ni "Corrupt name" ya jina Bwagamoyo au Bagamoyo kama inavyojulikana sasa hivi. Wazee wote wanakubaliana kwamba Mkwawa na familia yake walikuwa wako karibu sana na waislamu kutoka pwani kutokana na kufanya nao biashara na ulinzi aliokuwa anaipa misafara yao ya kibiashara.

Mkwawa kuwa muslamu au la kumewafanya wazee wajiulize kama alisilimu mbona akupewa jina la Kiarabu kama kina Rumaliza? Mkwawa jina lake la kiarabu aliitwa nani?

Lakini wote wanasema hakuna ushahidi wowote kwamba Mkwawa mwenyewe aliwahi kwa wakati wowote kuwa ni muislamu. Wanasema kwa wakati fulani mkwawa alishawahi kukaa kwa mjomba waka maeneo ya Mpwapwa ya sasa na huko nako aliwa na mahusiano na chifu wa Wagogo. Familia ya kina Muyinga (Shina la ukoo wa Mkwawa) lina mahusiano ya karibu na kina Lusinde wa Dodoma

Mkwawa si jina lake halisi bali alipewa kutokana na kuteka teka nchi za makabila mengine, ndiyo akaitwa "Mkwavinyika" yaani Mteka nchi. Hadithi inaendelea hadi tufikie kama Mkwawa alikuwa ni muislamu au la. Barua za Mkwawa kwa Irabu za kiarabu zilikuwa zimeandikwa nini ndani yake na nani anaweza kututhibitishia kama kweli ziliandikwa na Mkwawa mwenyewe?

Hivi kuandika kwa Irabu za Kiarabu huwezi kuandika "migolole, magobore na chumvi vimeshafika?"

Unaweza kabisa kuyaandika hayo, Jee, hicho kiarabu hufundishwa wapi na nani?

Unguja, Bwagamoyo, Ngazija (99% Muslims). "What a coincidence" na barua za kiarabu.
 
Unaweza kabisa kuyaandika hayo, Jee, hicho kiarabu hufundishwa wapi na nani?

Unguja, Bwagamoyo, Ngazija (99% Muslims). "What a coincidence" na barua za kiarabu.
London kumejazana wapemba utadhani wako Tunguu, wanaandika Kiingereza, wanaongea Kiingereza na kuimba Kwa Kiingereza. Wao ni Waanglican?
 
London si ilikuwa Iringa siku hizo? pale karibu ya Tosamaganga?
Tosamaganga na London kunahusiana vipi? Nimekutolea mfano wa kukutanabahisha kwamba dini na Lugha havihusiani. Kuna watu wanafanya kazi kwa waislamu kwa miaka nenda rudi lakini wao si waislamu, na hivyo hivyo kwa waislamu kwa wakristo. Kufanya biashara na jamii kwa muda fulani ni lazima utatohoa au kufanya usisi kwenye lugha yake, lakini hamaanishi kwamba wewe unakuwa ni dini au kabila lake.
 
Nilichojifunza kwenye mnakasha huu ni kwa nini dini ya Uislamu inapotoshwa na watu wachache!!

Utagundua ni rahisi kujadiliana na Mohamed Said (sijui jina lake la Kibantu ni nani) kuliko kujadiliana na FaizaFoxy na wenzake. Utagundua pia kwa Tanzania MS anaanza kuwa ni kiongozi wa kiitikadi (Ideology leader/mentor/ father) kwa wafuasi wake wengi. na hii ndiyo Dilema inayokumba watu wengi sana ambao wanafuatilia watu ambao siku za hivi karibuni wameanza kuitwa "Fanatic' na siyo "terrorist" kama huko nyuma tulivyozoezwa kuwaita.

Wakati Osama yeye amejificha na akiwa amezungukwa na walinzi pamoja na wake zake aliowaoa wakiwa vigoli kabisa, wafuasi wake wako Bize kujitoa mhanga ili kushindana na "Ibilisi" Marekani. Ninachotaka kusema ni kwamba hawa wanaojua kwamba ukijilipua na kuteketeza wamarekani na wewe ukafa unakuwa ni shahidi (martyr) wa dini ya mwenyezi mungu, si wao wala watoto wao ambao wanajitoa muhanga kupigania dini ya Mwenyezimungu.

FaizaFoxy anaisifia sana elimu inayotolewa Madrassa, lakini hapo hapo hatuambii inakuwaje hao wa Madrassa kama ndiyo wenye elimu yote inayotakiwa kwa elimu hiyo ya madrassa hawawi kwa mfano moja kwa moja Madaktari, wahasibu, Mainjinia mpaka hapo wanaposoma elimu inayotokana na mipango ya mfumo Kristo.

Wao kama wanaamini kwamba elimu ya Madrassa ndiyo kila kitu kwenye elimu, mbona na wao walikwenda kwenye shule hizi hizi ambazo wao wanaamini hazifundishi elimu bora kama ile inayotolewa kwenye Madrassa?
 
Tosamaganga na London kunahusiana vipi? Nimekutolea mfano wa kukutanabahisha kwamba dini na Lugha havihusiani. Kuna watu wanafanya kazi kwa waislamu kwa miaka nenda rudi lakini wao si waislamu, na hivyo hivyo kwa waislamu kwa wakristo. Kufanya biashara na jamii kwa muda fulani ni lazima utatohoa au kufanya usisi kwenye lugha yake, lakini hamaanishi kwamba wewe unakuwa ni dini au kabila lake.

Tatizo lako ni nini? ni wewe uliesema unakuja na ushahidi kuwa Mwawa si Muislaam, lakini mpaka sasa hujajanao, na hizo "circumstantial" ulizozileta zinaelekea hukohuko kwenye Uislaam. Mimi nimezipoint out tu, wewe ukaja na mfano wa Uingereza ndio nikakuuliza si pale London, karibu ya Tosamaganga? kuna kakijiji pale kanaitwa London, uliza wakuambie.
 
Nilichojifunza kwenye mnakasha huu ni kwa nini dini ya Uislamu inapotoshwa na watu wachache!!

Utagundua ni rahisi kujadiliana na Mohamed Said (sijui jina lake la Kibantu ni nani) kuliko kujadiliana na FaizaFoxy na wenzake. Utagundua pia kwa Tanzania MS anaanza kuwa ni kiongozi wa kiitikadi (Ideology leader/mentor/ father) kwa wafuasi wake wengi. na hii ndiyo Dilema inayokumba watu wengi sana ambao wanafuatilia watu ambao siku za hivi karibuni wameanza kuitwa "Fanatic' na siyo "terrorist" kama huko nyuma tulivyozoezwa kuwaita.

Wakati Osama yeye amejificha na akiwa amezungukwa na walinzi pamoja na wake zake aliowaoa wakiwa vigoli kabisa, wafuasi wake wako Bize kujitoa mhanga ili kushindana na "Ibilisi" Marekani. Ninachotaka kusema ni kwamba hawa wanaojua kwamba ukijilipua na kuteketeza wamarekani na wewe ukafa unakuwa ni shahidi (martyr) wa dini ya mwenyezi mungu, si wao wala watoto wao ambao wanajitoa muhanga kupigania dini ya Mwenyezimungu.

FaizaFoxy anaisifia sana elimu inayotolewa Madrassa, lakini hapo hapo hatuambii inakuwaje hao wa Madrassa kama ndiyo wenye elimu yote inayotakiwa kwa elimu hiyo ya madrassa hawawi kwa mfano moja kwa moja Madaktari, wahasibu, Mainjinia mpaka hapo wanaposoma elimu inayotokana na mipango ya mfumo Kristo.

Wao kama wanaamini kwamba elimu ya Madrassa ndiyo kila kitu kwenye elimu, mbona na wao walikwenda kwenye shule hizi hizi ambazo wao wanaamini hazifundishi elimu bora kama ile inayotolewa kwenye Madrassa?

Mimi nilishasema humu wengine ni rahisi sana kutamka Madarasa kuliko madrasa, na wengine ni rahisi sana kuitamka alif be te kuliko Alphabet, ambayo msingi wake ni hiyo Alph Be T. Kama hujanielewa nakusudia nini niambie ntakuja kwa undani zaidi.
 
Hebu,

Tuambie wewe vita vya maji maji Kinjekitile alitokea wapi? Vita vya Maji Maji vilianza lini na vikaisha lini? Ila mbona umekimbia maswali yangu ya MoU ya ujambazi baina ya kanisa na serikali ya watanzania? Rudi kwanza unijibu Bilioni 91 za nini mnazopewa na serikali?

Hawana hoja wenyewe wanaona serikali kuchota hela na kuzipeleka kanisa ni sawa (udini)

Halafu anayetetea hayo yasifanyike anaitwa mdini

Yaani mkweli anaitwa mwongo, mwongo na jambazi anaitwa mkweli tuna balaa nchi hii
 
Nilichojifunza kwenye mnakasha huu ni kwa nini dini ya Uislamu inapotoshwa na watu wachache!!

Utagundua ni rahisi kujadiliana na Mohamed Said (sijui jina lake la Kibantu ni nani) kuliko kujadiliana na FaizaFoxy na wenzake. Utagundua pia kwa Tanzania MS anaanza kuwa ni kiongozi wa kiitikadi (Ideology leader/mentor/ father) kwa wafuasi wake wengi. na hii ndiyo Dilema inayokumba watu wengi sana ambao wanafuatilia watu ambao siku za hivi karibuni wameanza kuitwa "Fanatic' na siyo "terrorist" kama huko nyuma tulivyozoezwa kuwaita.

Wakati Osama yeye amejificha na akiwa amezungukwa na walinzi pamoja na wake zake aliowaoa wakiwa vigoli kabisa, wafuasi wake wako Bize kujitoa mhanga ili kushindana na "Ibilisi" Marekani. Ninachotaka kusema ni kwamba hawa wanaojua kwamba ukijilipua na kuteketeza wamarekani na wewe ukafa unakuwa ni shahidi (martyr) wa dini ya mwenyezi mungu, si wao wala watoto wao ambao wanajitoa muhanga kupigania dini ya Mwenyezimungu.

FaizaFoxy anaisifia sana elimu inayotolewa Madrassa, lakini hapo hapo hatuambii inakuwaje hao wa Madrassa kama ndiyo wenye elimu yote inayotakiwa kwa elimu hiyo ya madrassa hawawi kwa mfano moja kwa moja Madaktari, wahasibu, Mainjinia mpaka hapo wanaposoma elimu inayotokana na mipango ya mfumo Kristo.

Wao kama wanaamini kwamba elimu ya Madrassa ndiyo kila kitu kwenye elimu, mbona na wao walikwenda kwenye shule hizi hizi ambazo wao wanaamini hazifundishi elimu bora kama ile inayotolewa kwenye Madrassa?

Kigarama,

Nimekushauri vp uje na data kamili kwanini Mkwawa sio mwislamu. Badala yake umekuja na hadithi za kusadikika. Nimejitolea mie kuwa judge kwasababu nina articles za wajerumani na waingereza walifanya research before hata Tanganyika kuwa huru. Kuna JF member moja akanishambulia nawaamini wazungu zaidi ya watanganyika. Hata hivyo, nakushauri get your facts right badala ya kumshambulia Faiza.

Huwezi kwenda kumuuliza Farao kuwa mkewe ni mwislamu wakati yeye haamini dini. Waulize wanaomfahamu mkewe kama ni mwislamu au la? Waulize wahusika wenyewe je Mkwawa ni mwislamu au la. Kama sio mwislamu watupatie evidence kwanini waseme hivyo? Vile watupatie tarehe, maeneo na wasifu wa watu husika.

Uislamu kumbuka sio jina. Kuna mtu ninasali nae msikiti wa Magomeni anaitwa John. Huyu jamaa ni mwislamu safi na mchamungu kweli kweli. Ila jina lake linaitwa John. Hivyo kusema jina la Mkwawa kwanini halikubadilishwa kama proof ya kuwa Mkwawa sio mwislamu that is a weak argument. Kuhusu barua za kiarabu nimeweka article hapa ikizungumza ni barua gani hizo. Hazikuwa barua mkuu bali zilikuwa taarifa za kuwahamasisha watu wabadili dini ili wanusurike na moto wa jehanamu. Zilikuwa barua za daawa na msambazaji alikuwa alikuwa akiitwa Mohammed bin Khalfan bin Khamis Al-Barwani almaarufu kama Rumaliza. Who happened to be rafiki na ndugu wa karibu na mshauri mkuu wa Mkwawa.

Njoo umekamilika mkuu usimshambulia Faiza kama umeishiwa hoja.
 
Wandugu,

Kama kuna uwezekano wa kuweka hiyo proposal hapa jukwaani tuione .......halafu mwenye proposal ya Wakatoliki/Wakristo..........atuwekee ili tuidadavue tujue pumba ziko wapi na mchele uko wapi..........

serikali ni watu na watu ndio sisi..............kama proposal ilikataliwa naamini kabisa ilikuwa ni baada ya uchambuzi wa binadamu kama sisi hapa JF.....kwa hiyo ninaamini hiyo proposal ikiwekwa hapa tutaona kama ina mapungufu au ilikuwa "mfumokristo" kuweka ntimanyongo.....

NOTE: Kwa atakayeweka hiyo proposal hapa......tafadhali atuwekee the original version.........

Ushauri murua sana huu naunga mkono hoja ndugu yangu Ogah. Pokea kalike hako kamanda.
 
Nilichojifunza kwenye mnakasha huu ni kwa nini dini ya Uislamu inapotoshwa na watu wachache!!

Utagundua ni rahisi kujadiliana na Mohamed Said (sijui jina lake la Kibantu ni nani) kuliko kujadiliana na FaizaFoxy na wenzake. Utagundua pia kwa Tanzania MS anaanza kuwa ni kiongozi wa kiitikadi (Ideology leader/mentor/ father) kwa wafuasi wake wengi. na hii ndiyo Dilema inayokumba watu wengi sana ambao wanafuatilia watu ambao siku za hivi karibuni wameanza kuitwa "Fanatic' na siyo "terrorist" kama huko nyuma tulivyozoezwa kuwaita.

Wakati Osama yeye amejificha na akiwa amezungukwa na walinzi pamoja na wake zake aliowaoa wakiwa vigoli kabisa, wafuasi wake wako Bize kujitoa mhanga ili kushindana na "Ibilisi" Marekani. Ninachotaka kusema ni kwamba hawa wanaojua kwamba ukijilipua na kuteketeza wamarekani na wewe ukafa unakuwa ni shahidi (martyr) wa dini ya mwenyezi mungu, si wao wala watoto wao ambao wanajitoa muhanga kupigania dini ya Mwenyezimungu.

FaizaFoxy anaisifia sana elimu inayotolewa Madrassa, lakini hapo hapo hatuambii inakuwaje hao wa Madrassa kama ndiyo wenye elimu yote inayotakiwa kwa elimu hiyo ya madrassa hawawi kwa mfano moja kwa moja Madaktari, wahasibu, Mainjinia mpaka hapo wanaposoma elimu inayotokana na mipango ya mfumo Kristo.

Wao kama wanaamini kwamba elimu ya Madrassa ndiyo kila kitu kwenye elimu, mbona na wao walikwenda kwenye shule hizi hizi ambazo wao wanaamini hazifundishi elimu bora kama ile inayotolewa kwenye Madrassa?
Haya ndio nisiyoyapenda mimi... watu kujaribu kuukashifu Uislaam wakati hawafahamu Uislaam ni kitu gani isipokuwa kwa majina ya watu na matukio.

Hivi kweli tunapozungumzia demokrasia kwa mfano, kwa nini watu wenye kupinga vita wanatetea demokrasia ya Libya ili hali walibya hao wamechukua silaha na kuua watu hata kama Ghadaafi alikuwa dikteta! maanake mafundisho mlopewa ni kwamba Uislaam unafundisha kuua, Je demokrasia pia inafundisha kuua?

Muda wote ktk mijadala ya hapa nimekuwa consistant na mtazamo wangu. Nitautoa mfano mdogo sana ambao wengi wenu hapa mtajikuta tofauti. Nyerere pamoja na ubaya wake iwe alikuwa dikteta au laa nampongeza kwa sababu alikuwa na malengo mazuri kwa wananchi wake sawa na navyompongeza Ghadaffi kwa utawala wake japokuwa alikuwa na mapungufu yake, sitazami dini zao kujenga hoja zangu.

Lakini tazama kinyume cha wengi, wapo watu hapa wanampongeza Nyerere lakini hawawezi kumpongeza Ghadaffi kwa makosa yale yale aloyafanya Nyerere wanayempongeza, pia wapo wanaompongeza Ghaddafi lakini sio Nyerere kwa makosa aloyafanya sawa na ya Ghadaffi.. Kwa hiyo mada hii imejengwa sana na Udini, ushabiki na fikra za kiza ambazo sii rahisi mtu kuziweka ktk maandishi. Imani binafsi ya mtu inatangulia hoja zake!
 
Back
Top Bottom