Hivi Bashungwa "anatosha" pale TAMISEMI? Pamoja na Rais kutoridhishwa na mambo ya Mkoa wa Mara, bado hajachukua hatua

Hivi Bashungwa "anatosha" pale TAMISEMI? Pamoja na Rais kutoridhishwa na mambo ya Mkoa wa Mara, bado hajachukua hatua

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Ningekuwa Mimi ndio Bashungwa, ningepiga kambi Mkoa wa Mara na kuusafisha, nikiwa na kikosi kazi maalum.

Rais hajaridhishwa na yote yanayotokea Mkoa wa Mara, na hatusikii Waziri akitema cheche, amebaki Ally Happy tu alifanya ziara, na kwenye ziara bado anasema ataandika barua sijui TAMISEMI, sijui wapi, nilitarajia Bashungwa angekuwa pale amepiga kambi akichekecha mmoja baada ya mwingine.

Hii wizara kwa staili yake, itamuondoa mapema katika nafasi yake, ni wizara kubwa, pana, inayohitaji maamuzi ya haraka. Huko ndiko Kuna wananchi, TAMISEMI ikiboronga, basi serikali nzima inakuwa na mzigo wa kujitetea kwa umma, wapi makatibu wakuu TAMISEMI? Mmekaa tu Dodoma? Rais akipita mahali na akawa na maswali, tuma timu ikayafanyie kazi.

Bashungwa ajitathmini kama anatosha, kama hachukui hatua kwa Kasi ya mwewe, nashauri SSH aanze kumuondoa yeye, wengine watafata, hiyo ni sampo moja tu ya Mkoa wa Mara, nilitarajia Waziri asambaze moto mkali kwa halmashauri zote nchi nzima, Rais kampa sampo tu kwamba hasimamii vizuri TAMISEMI, Bashungwa, wake up! Kengele za tahadhari zimeanza kulia, maandishi yanasomeka ukutani ...mene mene tekeli na pelesi
 
Bashungwa sio kiongozi mbovu, ila jamaa anapendeza zaidi akiwa mzee wa kanisa..
Hahaha, kabisa, yaani TAMISEMI, kama ni mpira, basi ni kiungo, kiungo ikifa, timu haitembei(haichezi), fedha kwa asilimia kubwa zinaenda TAMISEMI, kwa wananchi, Sasa kama hatasimama kidete, basi, SSH akuondoe haraka, kwa Sasa wizara yenye kelele ni ya kwake, kashindwa hata kutoa barua za kiwasimamisha kazi hao wa Mkoa wa Mara, wanachungizwa wakiwa ofisini, what's wrong Bashungwa?

Hata kuomba special audit ya halmashauri za Mkoa wa Mara huwezi? Watu wakae pale mwezi wanabinua Jiwe moja baada ya jingine ? You are a Minister bwaaana!
 
SSH asione nongwa kuibomoa na kuisuka upya wizara hii na kuisimamia kwa karibu zaidi kuliko sasa
 
Wa Bariidi Mnoo Kama Zabayanga
Arudi Kayanga Karagwe Akaendeshe Premio
Kabisa, amepoa mno katika wizara ambayo alitakiwa awe wa "moto", hata madereva wa premio wa kwenda Karagwe huwa wanachapa raba kwelikweli
 
Wananchiiiiiiiiiiiiiiiiiiii hatujawahi feli kwnye uongoz........vp unataka pale awekwe babra au[emoji23][emoji23]
 
Msimvishe roho ya jini jiwe ya misifa na ukatili mtu muungwana na mwetevu kama Bashungwa.
 
Kabisa, amepoa mno katika wizara ambayo alitakiwa awe wa "moto", hata madereva wa premio wa kwenda Karagwe huwa wanachapa raba kwelikweli
Abadilike Maana Kama Hayupo Vile Bila Shaka
 
Back
Top Bottom