Wakuu,
Nimeshindwa kuelewa wanaomuona Mwenda zake Magufuli eti alikuwa Mbunifu.
Ilikuaje akashindwa Kubuni na kutengeneza Vitu vya Maana kama Royal Tour? Rafiki yake Kagema alitengeneza yeye akawa anasema Matajiri nataka waishi kama Mashetani.
Hivi kutengeneza Royal Tour kwa Manuu ya au Kujenga Uwanja wa Chato kipi bora?
Movie ya Royal Tour iligharimu Tsh Bilioni 7. Na Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Geita Kijiji cha Nyabilezi Wilayani Chato nyumbani kwako na Mwenda zake Magufuli Ulijengwa kwa gharama ya shilingi 39.151 Bilioni.
Ndo maana tunaposema Mama anaupoga mwingi eleweni.
We fala huelewi chochote kuhusu Royal Tour na waaandaji wake.
figganigga Kwanza uelewe hii ilikuwa idea ya Wamarekani.
Haikuwa idea ya watanzania na ndio maana hatimiliki imebaki kuwa yao.
Pamoja na kwamba tumepigwa zaidi ya Bilioni 12 za kitanzania.
Huu ni mpango ambao huwa mahsusi kwa kuwaingia viongozi wenye misimamo mikali dhidi ya nchi zao.
Hizi ni mojawapo ya zile Operesheni za ndani ya CIA kupitia kitengo chake SAD
(Special Activities Department).
Ndani ya hicho kitengo ndio kuna kitengo kingine cha PAG
(Political Action Group).
Hawa ni wataalamu wa kufanya Political Influence kote Duniani.
Pale ambapo Marekani kama taifa inaona maslahi yake yakiwa shakani.
Na huko ndiko anakopatikana Peter Greenberg wa Royal Tour.
Kwa Taarifa yako hiyo haikuwa mipango ya mama yenu Samia.
Yeye amefanya kuletewa mezani na wajanja waliomtumia Dk Hassan Abbas.
Ni mipango ya vitengo ndani ya CIA.maalumu kwa kazi kama hizo.
Angalia orodha ya viongozi waliowahi kufanyiwa project ya Royal Tour Duniani na nchi zao ndio utaelewa.
Na kwa taarifa yako ni kwamba huo mpango wa Royal Tour ulianza kabla hata ya Samia kuupakata urais kupitia katiba.
Ulikuwa ni mpango mahsusi kwa Wamarekani kumuingia Magufuli kupitia Royal Tour kama walivyokuwa wamefanikiwa kumuingia Paul Kagame wa Rwanda na sasa wanachota madini ya DRC kupitia Rwanda bila shida.
Na huwasikii Marekani kumkemea tena Kagame pamoja na Udikteta wake wote.
Kwa mara ya kwanza Greebarg kuingia Tanzania alipokelewa na waziri wa maliasili wa wakati huo Khamis Kigwangalla, mbunge wa Nzega.
Mchongo mzima uliandaliwa kupitia kwa Rostam Aziz ambaye ni jirani yake Pale Igunga.
Na wote walishiriki hafla ndogo ya chakula cha usiku kwenye ubalozi wa Marekani nchini.
Baada ya kifo cha ghafla cha Marehemu Magufuli,ikawa imewarahisishia kazi zaidi kama tulivyokuja kushuhudia.
Nimekuwekea na ushahidi wa picha hapo chini ili unielewe.