Hivi huu upuuzi kwenye kazi za ofisini utaisha lini?

Hivi huu upuuzi kwenye kazi za ofisini utaisha lini?

"inamuuma kisa ni bosi na hana company alafu mimi surbodnate tu kampani kibao na Ina watu wenye uwezo kuniliko kwahiyo meza yetu huwa nachafukaa balaaaa mavinyaj ya gharama nikiingia viwanja Mimi ni alwatan kuliko yeye."

👆👆

Wewe mwenyewe una uswahili mwingi kuliko huyo boss wako.

Una kampani mbovu na bado unaiona nzuri kwako.
Jamaa Yuko na Mambo ya kiswahili sna khaa eti ansema boss anamfatilia na. Kwamba yey ni alwatani mtaani
 
Kbsaa yaani yey ndio tatuzo na Kama anasema anamzid uwezo na uwajibikaji kwanin Basi asingeteuliwa yeye kuwa boss wao jamaa miyeyusho sna na dharau anayo
Kama inafikia hatua mpaka anaulizia watu kwamba "jamaa Jana alikuwa anapigia wapi mitungi" inamaanisha yey ndiyo ananifatilia sana sasa nashangaa kivipi unasema mimi ndiyo tatizo? Yeye tatizo lake hulioni hapo?
 
Yani ni mswahili kichizi, dah hata usome namna gani kama umelelewa kwenye mazingira ya kishenzi utakuwa hivyo hivyo tu.
Aisee sina ufala kama wako wa kumyenyekea bosi tena nje yamuda wa kazi ilhali sijaharibu kazi yake. Wewe edelea tu kuwa chawa wa mabosi mzee utapandishwa cheo very soon, nimekaa paleee.......
 
Unatakiwa ujue haya:–

1.Hakuna mtu anayekupenda kazini hata kama kuna rafiki yako mlisoma shule moja hvyo fanya majukumu yako na mtegemee Mungu maana vita ni kubwa sana makazini watu wana rogana wana uawa na wanatiliana fitna nilishawahi kushuhudia mtu ana acha mshahara wa million 10 kisa fitna na majungu be carefully.

2.Acha kujipa umuhimu kazini wewe sio muhimu kiasi hicho wekeza nguvu kwenye mambo yako binafsi uliona IGP wa kenya kabla hajazikwa mrithi wake alishaapishwa raisi wa Iran kabla hajazikwa tayari mrithi kashapatikana aliyesema hapa kazi tu mchanga umeshamfukia jipe muda wa ku enjoy na familia yako na kundaa maisha yako ukitoka kazini.

3.Mtangulize Mungu sana kama ni mkristo soma sana bibilia kama ni muislamu soma sana Quran vinginevyo watakutanguliza akhera utese familia yako bure chochote wanachokusingizia muachie mungu huwezi ukajibu kila tuhuma maana tuhuma nyingine zinatoka kwa watu ambao wametuzidi cheo na uwezo hiyo vita ni kubwa.

4.Usiwaambie wafanyakazi kazi wenzako kila kitu kuhusu maendeleo yako either umejenga au mambo ya familia usiwashirikishe kila kitu watu pekee wanaofurahia maendeleo yetu ni wazazi wetu hvyo usiwe mtu wa kuropoka ropoka kila kitu mpaka mipango yako ya baadae hata kama ni kujiendeleza kielimu fanya kimya kimya.

5.Huwezi kupendwa na kila mtu mimi nasoma sana vitabu na kuna kitu nilisoma kwenye kitabu kinasema watu watatu ndio kila mtu anawapenda yaani MTOTO MCHANGA,CHIZI,NA MAITI ukiwa hai au ukiwa tofauti na hao huwezi kupendwa na kila mtu hvyo chuki ni lazima huwezi kupendwa na kila mtu ukiwa hai no one had ever kick a dead dog so learn to embrace criticism.

NB:unaweza kuepuka matatizo na changamoto nyingi za akili ukiwa unasoma vitabu hvyo nawashauri muanze kusoma vitabu yaani vita ambayo niko nayo mimi kazini bila kumtanguliza mungu na kusoma sana vitabu ningekuwa nishakuwa kichaa maana nimeanza kazi nikiwa na umri mdogo sana baadhi ya visa vyangu humu hivyo mkuu haupo peke yako kwenye hilo.
 
Haya mambo magumu sana Mkuu. Nipo na co-worker wangu na ni junior kwangu ila mshamba sana nafanya kazi mimi yeye anakimbilia kwa boss kuripoti na anasema kafanya yeye. Jana nimwahi zangu mapema ananiuliza vp mzee kuna shida gani mbona umewahi sana, nikamjibu kwani tunapangiana muda kuingia kazini hakujibu kitu. Kweli mchawi sio lazima aloge.
Hahah utanyooka
 
Hapo naona shida iko kwenye huo mji mnaofanyia kazi..ni mdogo..yaani ukute Bar mzuri ni moja au mbili hivyo uwezekano wa kukutana ni mkubwa.
Miji kama hiyo kukiwa na hata karembo fulani hivi wote mtamtaka na kuanza kugombana.
Miji kama hiyo mgeni ukifika tu unajulikana...
 
Aisee sina ufala kama wako wa kumyenyekea bosi tena nje yamuda wa kazi ilhali sijaharibu kazi yake. Wewe edelea tu kuwa chawa wa mabosi mzee utapandishwa cheo very soon, nimekaa paleee.......
Ahaaa haaa. Uchawa kwani kuna mtu kaenda kukushtaki kwa bosi wewe umetafuta ligi ya wazi na yeye pambana acha kulia.

Wewe si alwatani una marafiki wazito, mtu ambaye sio mwoga huwa anapambana sio maneno. Hii ni kidogo tu bosi kafanya siku akikufuta kazi utachanganyikiwa kabisa. Shaabash.
 
Back
Top Bottom