Hivi kikawaida sijui hapa tuchukue hatua gani dhidi ya huyu mchungaji...

Hivi kikawaida sijui hapa tuchukue hatua gani dhidi ya huyu mchungaji...

Anapita mulemule

1706047229605.png
 
Tukimfungulia kesi ya shambulio la kudhuru mwili haitamfaa? au tukamwekee madawa ya kulevya halafu tumchomeshe hicho kikanisa uchwara kifungwe
Kwakwel mawazo yangu (binafsi ambayo bado sijamshirikisha mtu) ni kwamba acha tungoje invoice halaf katika kugawana na yeye mchunga kondoo apewe part yake
 
Sio lzm kuanguka
Na SI Kila anaeanguka basi ana spirits,wakati mwingine ni nguvu za Mungu tu!
Na ni kweli kabisa,wapo wanaoanguka!
Na kuanguka sio lzm kuwekewa mikono,nguvu za Mungu zikiwepo mahali sio lzm uwekewe mikono ,utaanguka tu
Shida watu washatapeliwa sn kiasi kwamba ht wakikutana na ukweli wanaona uongo!
Sahihi
 
,pia yake maombi ya kwanza na

Maombi ya sshv 40 days fasting unahudhuria?
Ndio mambo ya walokole haya haya nayoyasema.
U letheri haukua na mambo hiz hapo before. Hiz ni upgrades mme install from somewhere ndio maana wenye kkkt yao wakiwapiga virungu hao akina Matsai na Kimaro kwamba mnatuingizia taratibu za kigeni zisizo zetu mnafikiri wanawaonea😂😂
 
Kwanini umemtaja jina dr lupondo pia uka ainisha kuwa ulimhonga ..... unalengo gani ndugu mwandishi
 
Kabila sijamalizia kusoma mkuu,rekebisha, Mimi ni mlutheri niliyetokea RC
Ni kkkt!
Nasali kkkt kimara korogwe Kwa mchungaji W.Mastai.
Mi sio wa makanisa ya kilokole!
Rekebisha mtumishi
Umewakana walokole vibaya sana akutake radhi sio[emoji1][emoji1]
 
Mchungaji hana makosa ilitakiwa aunt amweleze apatiwaje huduma isiwe ya kuanguka maana ana shida ya kiafya
 
Sheria za nchi hazisemi kuwa mtu akija kanisani apigwe kupiga mtu ni kosa la jinai iwe kanisani , msikitini au popote. Pia hii ya kumsukuma mtu na kumvunja nyonga ni kosa kama makosa mengine. Kuwa alikuwa anakemea pepo haipo kisheria maana hawezi kuithobitisha. Mvuteni kwa pilato. Sadaka zitamsaidia matibabu.
Na Tayana-wog asisali hapo atakuja kuvunjwa uti wa mgongo kabla ya ndoa. Asiseme hatukumwambia 😂😂
 
Kwanini umemtaja jina dr lupondo pia uka ainisha kuwa ulimhonga ..... unalengo gani ndugu mwandishi
No lengo.
NA labda uwe mgeni wa huduma za muhimbili, hiv ni vitu vyabkawaida kabisa. Watu wanakufa kwa ujinga wa ubinafsi wa madaktari pale mpala uwape chochote kitu
Na by the way this can just treated as allegations tu cz no proof for any conviction agaist them.

Are you the one??
 
Ni mchungaji ndio. Wa haya makanisa ya kilokole haya ya akina Tayana-wog . Kiukwel nimesikitishwa na kushikwa na hasira kwa wakati mmoja.

Ni mama yangu mkubwa kabisaa yamemtokea.
Ni kwel sikatai hakulazimishwa kwenda huko kusali lakini ndio hivyo tena mambo ya imani (magumu sana).
Jana wakiwa katika vipindi cha maombi , mchungaji anapita anapiga maombi huku waumini nao wanagonga prayers ki individual kukemea shetani.

Mchungaji akawa anaweka mikono kwa watu tofauti tofaut randomly.
Akafika kwa aunt anamuwekea mikono huku anakemea pepo (tulivyoambiwa na wahusika) sasa ile kuona muumini yuko stable haanguki ,inaonekana akatumia nguvu kama kumpushi (hii hata mimi naijua, nilishawahi kukutana nayo, pastor akiona huanguki anakupush backward, hata sijui logic yake huwa nini?).

Sasa kwakua aunt ni mtu mzima (sana) akakoshindwa kustahimili msukumo akaona kama anataka kuanguka. Sasa haraka haraka akawa anatafuta pozi ili akae kwenye kiti (cha plastic) kilicho nyuma yake, akakosea timing..TATIZO LIKATOKEA.

Akaanguka kwa kutulia makalio ila ndio habar ikaishia hapo , akawa hawez kuamka. Kumbe inaonekana alifikia kiupande akakalia/akaangukia nyonga. MAUMIVU SI YA KITOTO.

Aunt alishapata shida kama hii miaka mi 3 nyuma akiwa nyumba akijikwaa akavunjika nyonga barabarani. Na ni mimi ndiye nilimchukua nikiwa na mwanaye wa kike (mdogo angu) tukamkimbiza Regency Medical Centre. Pale kwakua kuna watu najuana nao, nikashauriwa baada ya vipimo kwamba mgonjwa wetu apelekwe Muhimbili kwakua pale ghatama zitakua nafuu maana kwa Regency ,operation ile ingetugharimu milion 20 kwakua ni private. Ma hata kama ana bima, ingeweza ku cover not more than 9 millions.

Na kwel, tukapewa rufaa Muhimbili, shukrani sana sana sana kwa mtaalamu wa mifupa pale Moi, dokta *****. Japo tulilazimika pia kumuhonga ila kupata huduma ila tunashukuru Mungu pale Muhimbili ilitugharimu million 10.

Hiz pesa tulikamuana wana ndugu ili kufanikisha hili zoezi kwakua aunt ana watoto wadogo bado hawana uwezo kiuchumi.
HAYA SASA MCHUNGAJI KALIZUA TENA.
Na maza amasema kabisaa anahis hali kama ile ya miaka ileee ila sasa ni mguu mwingine. Ameanza vipimo vya awali leo na kama wana ndugu tumekaa mkao wa kula matumbo joto kujua donei kias gani itahitajika na JANUARY yoote hii.

Kwakwel binafsi makosa majibu, huyu mchungaji tumfanye kitu gani?? Maana kikawaida hatuna namna ya kumtia hatian kwa mujibu wa sheria.

am sorry kwa uzi mrefu.

Nimemaliza
Nashindwa hata kusema.
Lakini nimeona niandike.

Mungu amponye mama
 
Sio lzm kuanguka
Na SI Kila anaeanguka basi ana spirits,wakati mwingine ni nguvu za Mungu tu!
Na ni kweli kabisa,wapo wanaoanguka!
Na kuanguka sio lzm kuwekewa mikono,nguvu za Mungu zikiwepo mahali sio lzm uwekewe mikono ,utaanguka tu
Shida watu washatapeliwa sn kiasi kwamba ht wakikutana na ukweli wanaona uongo!
Acha niwe mtazamaji tu!

Yaan miaka yote sijawahi ona naowajua wakipata miujiza inayoonekana mfano alikua anatembea kwa magongo baada ya maombezi akatoka nduki bila msaada wa magongo
 
Khaaa kumekucha
Nimedai wapi tena mkuu?[emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Jmn huu ulokole unachukuliwaje sijui,mimi Nina muamini Kristo,ni mfuasi wa Kristo!
Niondoleeni hizi lebo nyingine hazina issue ....
Sema su niweke hapa hadharani uthibithisho...[emoji2960]

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom