Hivi kuna Mtanzania aliyekula bata kama Jakaya Kikwete?

Hivi kuna Mtanzania aliyekula bata kama Jakaya Kikwete?

Watakatifu wapo,sio kila mtu anapenda makuu hata hivyo hii ni mada tu inayosaidia huko unakokuita kurelax.
Watakatifu kizazi hiki hawapo ndugu yangu dunia imejaa wahuni na wanafiki
 
Wazungu ni marafiki zake kuliko hata waafrika wenzake
Sasa uwe na marafiki wachawi na wafitini watakusaidia nini?

Hapa juzi Kati alikuwa ziarani Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini akiwa na Rais wa AGRA na yeye kama member wa Board walikuwa wanakagua miradi ya kilimo kwenye ukanda wa SAGGOT.

Mtu wa fursa 👇

Screenshot_20220220-084206.png


Screenshot_20220220-084227.png
 
Mara nyingi wanaokula bata na kufaidi raha za viongozi ama matajiri huwa ni Wanawake zao na Watoto wao ambao hawajui stress za Madaraka au za kumiliki Mali nyingi

Kama Mwanasiasa na kama kiongozi huwa anapitia nyakati ngumu za stress, hisia za kusalitiwa na hata wakati mwingine nafsi inakusuta unapowafanyizia wanasiasa maadui zako ama kwa ku revenge au kuwadhibiti dhidi ya hila zao

Mzee Mkuu alikuwa anamalizia stress za uongozi kwa kupiga mitungi ya kirusi kwa kwenda mbele

Mwingine akawa anamalizia stress kwa kuongeza Ibada

Mwingine hisia zilikuwa zikizidi anachukua pipa na washkaji wake kwa jina la wafanyabiashara kwenda kula bata

Mwingine akawa anapanga watu barabarana 'wazuie' msafara wake anachamba, anafoka anatoa ya Moyoni nafsi inatulia

Kwa mawazo yangu anaekula bata zaid ni yule ambae hana muda wa kuwa na stress bila ya kujali ana kipato kiasi gani
Bado 6 na 1. Tuwekee anavyo/alivyokuwa akimaliza stress.
 
Watakatifu wapo,sio kila mtu anapenda makuu hata hivyo hii ni mada tu inayosaidia huko unakokuita kurelax.
Ila mi siamini mtu siku hizi na imenisaidia sana.kuna watu niliwaamini ila waluniacha mdomo wazi
 
Kuna wimbo unaitwa Money,Power,Respect wa Lox
Fist yo get money
Then you get maza f....r power
Then maza f......r guys will respect you.
What you want in life
Money Power Respect
JK got it all
Jk hajui njaa ni mdudu gani
Kubali kataa CCM ni mali ya Jk ,kinana na makamba
Jk kazunguka dunia nzima with power money and respect
Na bado anaonekana atakula hizi bata mpaka afikishe miaka 100
Ukijumlisha bata alizokula Jk hata ujumlishe marais wote tangu uhuru hawamfikii
Wanasema Jk bado unaongoza nchi gani sijui
Jk kana ni kweli mwambie mama atuachie yule DJ disco limepoa.
Mbona we ulivumilia kelele za muziki.
Inakuwaje wengine muziki uwe kelele.nadhani Mungu alikubariki sababu roho yako nyeupe huna nongwa na mtu.
God bless you Jk
Dj tuwekee wimbo wa riziki uliopigwa na K bazil kusindikiza haters.
Haters niueni
Nimemsikia jana akiiomba serikali kuangalia/punguza bei ya mbolea. Nikawaza, huyu mzee hajui kama kipaumbele sasa ni kuleta VAR na kuweka katika viwanja vya soka!!??
 
Embu nipe ABC za bata alilokuwa anakula maana sijui
Kinyozi wake kila week anatoka ufaransa kuja kumyoa nywele,weekend anaenda ulaya kula lunch usiku dinner nyumbani,watoto wake wanasoma ulaya kila weekend wanarudi congo,kijijini kwake alijenga kanisa la ajabu,airport kama ya chato,choo cha dhahabu,kitanda cha digital,kiti cha dhahabu tupu,sahani na kijiko ni dhahabu
 
Kinyozi wake kila week anatoka ufaransa kuja kumyoa nywele,weekend anaenda ulaya kula lunch usiku dinner nyumbani,watoto wake wanasoma ulaya kila weekend wanarudi congo,kijijini kwake alijenga kanisa la ajabu,airport kama ya chato,choo cha dhahabu,kitanda cha digital,kiti cha dhahabu tupu,sahani na kijiko ni dhahabu
Duh hatari sana, ningependa kujua maisha ya watoto wake sasa yapoje?
 
Humu kuna watu wanastahili SHIKAMOO! Mwaka 83 tayari unawajua MAMA LISHE... Unavuta Sigara...
Unanikumbusha nilivyoishi Makorora Tanga miaka ya 83. Nilikua nasubiri Giza liingie ndio niende kwa mama ntilie kuchukua Maharage yakiyokwisha ungwa. Kisha nawasha mchina na kusonga chap. Ugali ukishaiva jiko linatolewa nje lipoe harufu Kisha navua Shati. Nikishamaliza kula nawasha sigara na kutoka kuvutia nje.
 
Back
Top Bottom