Hivi kuna sehemu Tanzania bodaboda wanakimbia kama hawa wa Arusha?

Hivi kuna sehemu Tanzania bodaboda wanakimbia kama hawa wa Arusha?

Arusha sio boda boda tuu hata hao wanaoemdesha magari wengi wao hawana fair na kutukana ni jadi yao awe mzee au kijana..Arusha ndio mji nimeshangaa unakuta machalii wanatukanana bara barani watu wanaona kawaida tuu na hakuna anaeshangaa wewe ukishangaa ndio wanakuita mang'aa...

[emoji38][emoji38]umenikumbusha mbali na hili neno mang'aa[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nimekulia Moshi Kilimanjaro, yeah kuna vijana wanakimbia na pikipiki mitaa ya Kalimani, kaloleni kule na njoro.
Nimekaa Dar kidogo yes kuna vijana wanajitahidi kukimbia na pikipiki

Ila Arusha hapana vijana kama hawana Roho na nyama, yaani pikipiki unasikia imepita kama mlio wa nyuki halafu sio mmoja sasa ni wengi karibia wote.

Mibangi
 
Niliwah kuchelewa ndege nikaamua nichukue boda kutoka Arusha kwenda Kia aisee nilipofika nilipiga goti nikamshukuru Mungu yule ni mvuta bangi sio binadam wa kawaida
 
Waache wakimbie wajitwange humo barabarani tupungue kidogo hapa duniani
Upuuzi mwingi sana kwa sasa
 
Vijana waliozaliwa na kukulia Arusha, kwa wastani wanaupeo mkubwa wa mambo ukilinganisha na vijana wengi wanaotoka mikoa mingine hapa Tz.

Utagundua hili kwa urahisi tu ukifanya uchunguzi.

Lakini pia wageni/watalii wanaofika Tz na kutembelea mikoa tofauti wanawaona hii tofauti na wanauliza kwanini wakazi wa mikoa mingine Tanzania wanaonekana wapo slow sana? Mimi ni TO kwahiyo ninakutana na maswali ya namna hii. Kwa mfano mgeni akitoka Dar au Zanzibar au Mwanza akifika Arusha lazima ataona utofauti vile vijana/wakazi wa Arusha wanavyofikiri kuhusu maisha na kazi. Arusha ni pesa na biashara. Hakuna unyonge.

Mwisho niseme tu vijana wote wa Tz ni vijana wema na ninawaheshimu bila kujali wanaishi wapi, iwe Ruvuma au Kigoma au Mwanza. Sisi ni wamoja haija haja yakubaguana.
 
Umetumia kigezo gani kuwajumuisha wote kuwa hawana akili sawasawa? Saa zingine Kuliko uandike nonsense and look like a fool, it’s better to just shut up.

Allow him to look like a fool, or you will look a fool instead, unajitetea nini kwa mtu aliyeandika bangi zake?
 
Vijana waliozaliwa na kukulia Arusha, kwa wastani wanaupeo mkubwa wa mambo ukilinganisha na vijana wengi wanaotoka mikoa mingine hapa Tz.

Utagundua hili kwa urahisi tu ukifanya uchunguzi.

Lakini pia wageni/watalii wanaofika Tz na kutembelea mikoa tofauti wanawaona hii tofauti na wanauliza kwanini wakazi wa mikoa mingine Tanzania wanaonekana wapo slow sana? Mimi ni TO kwahiyo ninakutana na maswali ya namna hii. Kwa mfano mgeni akitoka Dar au Zanzibar au Mwanza akifika Arusha lazima ataona utofauti vile vijana/wakazi wa Arusha wanavyofikiri kuhusu maisha na kazi. Arusha ni pesa na biashara. Hakuna unyonge.

Mwisho niseme tu vijana wote wa Tz ni vijana wema na ninawaheshimu bila kujali wanaishi wapi, iwe Ruvuma au Kigoma au Mwanza. Sisi ni wamoja haija haja yakubaguana.
Arusha hii hii iliyojaa vijana wala gomba kutwa nzima na kusubiri kuomba hela kwa watalii
 
Arusha hii hii iliyojaa vijana wala gomba kutwa nzima na kusubiri kuomba hela kwa watalii
Huo ndiyo ukweli. Kwa wastani vijana au wakazi wa Arusha wanaupeo mkubwa zaidi kuliko vijana/wakzi wa maeneo mengine Tanzania.

Nafahamu unaweza kujisikia vibaya au ukajiona inferior lakini hii si lengo langu. Hayo pia si maoni yangu binafsi bali wageni wanaofika kutembelea Tanzania wanasema hili waziwazi tu.
 
Niliwah kuchelewa ndege nikaamua nichukue boda kutoka Arusha kwenda Kia aisee nilipofika nilipiga goti nikamshukuru Mungu yule ni mvuta bangi sio binadam wa kawaida
Sasa kama ulichelewa ndege kwanini upande boda c ungepanda tu costa au hice ili upande ndege lingine
 
Huo ndiyo ukweli. Kwa wastani vijana au wakazi wa Arusha wanaupeo mkubwa zaidi kuliko vijana/wakzi wa maeneo mengine Tanzania.

Nafahamu unaweza kujisikia vibaya au ukajiona inferior lakini hii si lengo langu. Hayo pia si maoni yangu binafsi bali wageni wanaofika kutembelea Tanzania wanasema hili waziwazi tu.
Ni ukweli mtupu hilo halina ubishi.
 
Back
Top Bottom