Hivi kwanini ujenzi wa makanisa mengi ya KKKT huwa hauishi?

BigBro

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
3,585
Reaction score
11,601
Tangu nakua kule Keko Magulumbasi, kunapokuwa na ujenzi wa Kanisa la KKKT huwa miaka na miaka ujenzi haukamiliki.

Mifano ipo Mingi tu. Tangu mwaka 1998 Kanisa la pale Korogwe Kimara KKKT ujenzi haujaisha.

Segerea mwisho hadi kesho bado ujenzi haujaisha.

Kibamba shule njia ya Kibwegere ujenzi haujaisha.

Kumara Suka karibu na Temboni ujenzi haujaisha.

Hii ni baadhi ya mifano michache tu, hivi shida nini?
 
Shout out kwa wanakeko ya magurumbasi wambie Malebo nipo naendelea vyema

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
KKKT lina waumini wengi sana. Ila wachaga ndio wengi zaidi kwenye nafasi za juu juu kwenye kila usharika.

Sehemu yoyote mchaga akiwepo ujenzi huwa hauishii.. hata nyumba za kuishi za wachaga huwa zinarekebishwa kila mara.

Mchaga na ujenzi ni ndugu
 
KKKT za malebo hizo

Keko ya magulumbasi
unga limited.
Majengo
Mombasa

Ukitaka kufuatilia mambo ya ujenzi na hawa wachunga kondoo.. uta ishia kuacha kuamini Mungu Yupo
 
Ujenzi ukiisha wachungaji na wazee wa makanisa watakula wapi?
 
Mkuu hapa umekita Kisu kwenye mfupa. Kuna Kanisa lina Miaka 20 bado halina hata plasta ukutani.
 
KKKT lina waumini wengi sana. Ila wachaga ndio wengi zaidi kwenye nafasi za juu juu kwenye kila usharika.

Sehemu yoyote mchaga akiwepo ujenzi huwa hauishii.. hata nyumba za kuishi za wachaga huwa zinarekebishwa kila mara.

Mchanga na ujenzi ni ndugu
umewasahau na wale wachoma makanisa na wapare
 
Unataka ujenzi uishe halafu bahasha za ujenzi zigawanywe kwa waumini kwa sababu ipi. Ujenzi ni strategic plan mojawapo ya makanisa kuingiza mapato
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…