Katika maisha ya kawaida binadam kusaidiana ni kitu cha kawaida. Haijalishi unamfahamu au humfahamu kama mtu anahitaji msaada msaidie tena bila kutegemea kitu chochote in return.
Kuna hii tabia wanaume ukiwasaidia lazima baadae warudi wakutongoze. Sijui huwa wanawaza nini! Umesaidiwa toa shukrani zako kisha nenda haina haja ya kutaka kuleta mazoea mengine.
Nakutana na hili mara nyingi sana nashindwa kuelewa inaonekana msaada ni kitu cha ajabu sana kwa wanaume hawaamini kama mwanamke anaweza kutoa msaada bila kuhitaji chochote kutoka kwao. Maana wao wamezoea hawatoi msaada hasa kwa jinsia tofauti mpaka wahakikishe kuna kitu atapata kutoka kwa mtu anayemsaidia.
Ukisaidiwa shukuru kisha ondoka usitake kuleta mazoea, wengine hatupendi mazoea na shobo zisizokua na maana.
Dada, upo dunia gani unayoishi bila kujua maisha na tamaduni halisi ya jamii?
Nilitaka nikuanzie mbali sana kukuelewesha sababu ya kutongozwa kila unapotoa msaada kwa wanaume, lakini wacha nifupishe stori.
Katika jamii yetu, mwanamke ni mtu wa kupewa na si kutoa, ndivyo ilivyojengeka katika jamii pia hana kauli ama tuseme 'haki' ya kumtongoza mwanamme hata ikitokea kavutiwa naye.
Kwa hiyo wanawake huexpress desire zao za mapenzi kwa ishara.
Na ishara hizo ni pamoja na kujichekesha chekesha kwa kila neno litamkwalo na ampendaye, kujipitisha pitisha inaitwa kujilengesha kwa mwanaume husika, kutoa lasirimali zake kwa mtu ampendaye kama msaada nk nk, zipo ishara nyingi sana zitumikazo kumuatract mwanamme aingie kwene box.
Hata mimi ikitokea mwanamke akanipatia msaada nitaona kama ni extraordinary, lazima ningetoa mrejesho wa namna hiyo, yaani ningelimtongoza tu.
Wewe ni mwanamke unayeishi katika jamii yenye mfumo huo , kwanini ushangae kutongozwa kama njia ya shukrani kwa msaada wako?
Halafu kwanini ulaani kutongozwa badala ya kushukuru, maana yake umebeba sifa za mwanamke wa kiafrika zinazopendwa na wanaume.
Wenzako wengine wasipotongozwa, hujihisi wameibiwa nyota zao na kupelekea kwenda kwa waganga wa kienyeji kuogeshwa madawa ya kuondoa mikosi!