Hivi kwanini watu wapole wako hivi?

Hivi kwanini watu wapole wako hivi?

Ni kawaida kwa JF ... Members wa platform hii kila member ana gari .. Kila member hatumii tecno ..kila member ni muhitimu wa chuo kikuu and the likes
mzee usiwe mtu wa ku generalize mambo, JF ina members zaid ya laki tano, hapa kuna comments za members kama mia hamsin kasoro hv. afu ww unakuja kusema member wote wa Jf.......hawa memba wote wa JF hua mnawapata wapi?

Sku zote "Maudhui ya uzi ndo huamua aina ya wachangiaji". Mfano ukianzishwa uzi wa introvert utakuta introverts wanajisema humo. na sio members WOTE.
 
Wapole au wakimya, maana kuna watu ambao ni waongeaji lakini ni wapole.


Ngoja nikusaidie tu , watu wengi hasa wanawake wanachanganya kati ya watu wakimya na wapole.

Upole ni tabia ya ndani, ambayo inatafsiwa Kwa MTU kuwa na huruma, caring na upendo. Na kinyume cha upole ni ukatili.

Na kuna ukimya maana sio muongeaji. Kinyume cha mkimya ni muongeaji.

Kuna watu wakimya halafu wapole pia. Lakini kuna watu wakimya halafu ni makatili. Hawana huruma, upendo na sio caring.

Pia kuna watu waongeaji lakini wapole pia.


Watu wengi wanaingia chaka Kwa kushindwa kujua jambo hili wanapochagua wenza wao, Mara nyingine unaingia Kwa MTU mkimya lakini sio mpole unaishia kuchezea kichapo. Unakuta MTU huyo anakuwa mafia, mwenye tabia mbaya, asiyejali kabisa ila ndio hivyo sio muongeaji.
Mimi ni mpole na mkimya kwa pamoja

Ila nikigusa gambe nawaka kama moto naongea sana.
 
Mara nyingi huwa hatupendi usumbufu.
Hili ndio jibu sahihi,hata mimi ni mpole huwa sipendi kabisa usumbufu au purukushani za aina zozote zile na wala sipendi kupoteza muda kwa namna yoyote ile.
Kwa hiyo nikiingia kwenye mahusiano huwa natumia akili nyingi sana kumsoma huyo mwenza kimyakimya bila yeye mwenyewe kujua kuwa namsoma/namchunguza.
Nikishaona ana mawenge au ujuaji mwingi uliopitiliza au makelele mengi najiandaa kumpiga chini fasta.
 
Wengi mnaowaita wapole siyo wapole bali ni wa kimya tu!

Kuna tofauti kati ya upole na ukimya!

Upole ni mojawapo ya tunda la Roho Mtakatifu.

Ni mwenye Roho Mtakatifu tu anaweza kuwa mpole ijapokuwa inategemea.

Ukimya ni tabia kubwa ya majambazi!
Fafanua huo upole wa Roho mtakatifu
 
Wengi mnaowaita wapole siyo wapole bali ni wa kimya tu!

Kuna tofauti kati ya upole na ukimya!

Upole ni mojawapo ya tunda la Roho Mtakatifu.

Ni mwenye Roho Mtakatifu tu anaweza kuwa mpole ijapokuwa inategemea.

Ukimya ni tabia kubwa ya majambazi!
Tutake radhi , unawezaje kutufananisha sisi na Majambazi.

Mbona maccm sio mapole lakini yana yanajambaza pesa za watz
 
Mtu mpole.
Wanafikiri sana kabla ya kutenda na sio wakurupukaji, na nirahisi kuwaamini na pia wako tayari kutoa msaada.
Watu hawa ni wazuri kuwa nao kama marafiki, na wasikilizaji wazuri ambao wanazielewa hisia za wengine.
Wapole wanaweza kudumisha mahusiano yao na wengine na ni rahisi kukaa kwenye uhusiano kwa muda mrefu, na niwagunduzi wa vitu.

Kuna dhana kwamba Watu wakimya wana dharau kutokana na kwamba wakati wewe unaongea kwa mdomo, wao wanatabia ya kuongea kichwani mwao.
Pia inasadikika kwamba unapo ongea naye mara nyingi anaweza asijibu kwa maneno bali vitendo na pia anadaiwa kutosahau haraka alichoambiwa.
Dah mkuu wewe utakuwa umesomea saikolojia.
Yaani tabia zote ulizotaja ndio niko nazo mimi,huwa sipendi kumpa mtu promise kwa maneno mengi bali mtu akiniomba kitu nitaitikia tu kwa kichwa bila kuongea,lakini lazima nitimize kwa vitendo sasa mtu asiyejua anakasirika akihisi labda umedharau ombi lake.
Mke wangu pia unishangaa muda mwingi vitu vyangu huwa navimaliza kichwani kwangu bila kuongea,lakini mwisho wa siku naibuka na utekelezaji.
 
Mtu mpole.
Wanafikiri sana kabla ya kutenda na sio wakurupukaji, na nirahisi kuwaamini na pia wako tayari kutoa msaada.
Watu hawa ni wazuri kuwa nao kama marafiki, na wasikilizaji wazuri ambao wanazielewa hisia za wengine.
Wapole wanaweza kudumisha mahusiano yao na wengine na ni rahisi kukaa kwenye uhusiano kwa muda mrefu, na niwagunduzi wa vitu.

Kuna dhana kwamba Watu wakimya wana dharau kutokana na kwamba wakati wewe unaongea kwa mdomo, wao wanatabia ya kuongea kichwani mwao.
Pia inasadikika kwamba unapo ongea naye mara nyingi anaweza asijibu kwa maneno bali vitendo na pia anadaiwa kutosahau haraka alichoambiwa.
Pamoja sana mkuu.
 
Back
Top Bottom