Hivi mtoto wa kike kama haolewi anapaswa kuendelea kuishi na wazazi mpaka umri gani?

Wanangu wakike watakaa kwangu mpaka watakapojiskia wenyewe haijalishi wana kazi au hawana kwanza jumba kubwa nibaki na yf peke yetu ili iwaje!? Natafuta maisha kwanguvu sababu ikiwa ni wao...wakichoka kukaa na sis nawapa nyumba zao wakaishi how they wish.
 
nani ataoa mtu ana miaka 32 anakaa kwao,hata mwanaume kama anakutaka ataona hamnazo?
 
hata kama mtoto anamiaka 32 bado hajui hata umeme unanunuliwa vipi,siku ukiwa haupo itakuwaje?hata maraisi wanahangaika watoto wao waanze kujitegemea
 
Mwambie aje tuishi na mimi
[mention]Kelsea [/mention] amenikataa[emoji16]
 
25 -26 ni akapange kwake aliwe vyema hadi aolewe
 
Hiyo dada lazima Kuna sababu mbali mbali zinazopelekea yeye kutoolewa,na nyingi Kati ya hizo sababu zimetengenezwa na yeye.

Labda huyo dada hayuko social na wanaume.Kila mwanaume anayemtokea na kumtongoza yeye amuona kinyaa na kumkataa.
Au Ana hulka Fulani Fulani ambazo ziwanawaepusha wanaume kwake.
 
Mmh! Mtu anakaribia miaka 40 sasa mwishoe atafikisha 60, aendelee tu kusubiri bwana?
Sasa atafanya nini au unataka atumie fedha kutafuta mume kama wazungu wanavyo fanya, Wazungu wakija Afrika wanatafuta kijana waki Afrika wanamuoa, kwakuwa wazungu wanakuja na pesa na vijana wengi wa kitanzania ni masikini kijana hawezi kukataa kuolewa na mwanamke waki Zungu mwenye miaka 45 kwasababu kijana atajengewa nyumba atapewa gari lakutembelea na Mzungu akienda kwao kijana anaachiwa ATM card .
 
Wasichana wasikuizi hawana hofu ya Mungu na hawana maadili kwa jamii, unaweza kuwa na dada zako lakini wakawa hawa kuheshimu utakuta anakakipato kidogo tu kukuzidi wewe na utakuta analeta Mwanaume kwenu au anakuja kuchukuliwa, anakujib husimfatilie maisha yake yeye ni mtu mzima siyo mtoto.
 
Wakipotea wachungwaji lawama haziwaendei wachungwaji bali wachungaji............haya mambo haya aanzii ukubwani bali ni mfumo wa maisha unaoanza tangu mnazaliwa
 
Hii ni impact ya ubepari, si mnashobokea ubepari... pesa ndio utu, ndio kila kitu. Uko mambele kwa mabepari wenyewe maisha yameanza kuwashinda hawataki hata kuzaa wanaogopa majukumu wanaishia kufuga umbwa na panya[emoji23]
[emoji1666][emoji23][emoji23]
 
Weka picha yake tuone maana usijekuwa unalaumu haolewi afu kumbe lawama Ni kwa mama alichagua baba bandidu mtoto akaishia kufanana na baba yake πŸ˜†πŸ˜†

Sasa unataka mtoto wa Nani amuoe mwanamke mbaya? πŸƒπŸƒ
 
Wanaomsema wako sahihi maana ndio nature, viumbe vyote tumeumbwa hivyo kwamba inategemewa kufikia umri fulani uwe umetimiza hatua kadhaa za kuendeleza kizazi, it's biological and natural, ila kwa maisha haya ya leo, imetulazimu twende kinyume na mambo mengi ya asili.

Anapaswa yeye asihangaike nao, apambane kujikwamua kimaisha hususan kwenye kusaka kipato, kama akiweza aongeze hata elimu apate masters na kuendelea kujichimbia, haina ulazima wa kuolewa almradi tu aoelewe, atateseka kwenye ndoa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…