Hivi Mungu aliwaza nini mpaka akaamua kututupia Ibilisi duniani!

Hivi Mungu aliwaza nini mpaka akaamua kututupia Ibilisi duniani!

Historia fupi ya Iblis na uasi wake.

Iblis ni jini na hakuwa malaika licha ya kuwa alipata kipaumbele cha kuishi pamoja na malaika huko mbinguni. Iblis alinyanyuliwa na malaika akiwa ni kiumbe mchanga sana katika dunia hii mara baada ya malaika kutumwa kuja kuwaangamiza majini waliokuwa wakifanya uasi hapa duniani,ikumbukwe kuwa majini walipata kuishi katika dunia hii miaka mingi kabla ya uumbwaji wa mwanadamu ila walikengeuka na kufanya ufisadi mwingi sana. Iblis aliachwa na wazazi wake hivyo malaika wakaomba idhini kwa Mungu waondoke nae wakamlee huko mbinguni.Walikubaliwa na hatimaye iblis alikua katika mikono ya malaika , na alipata elimu kubwa tu na pia alikuwa ni kiumbe mchamungu sana.Mtume Muhammad (sala na amani ziwe juu yake) alinukuliwa akisema kuwa hapana sehemu yoyote katika ardhi hii yenye ukubwa wa kiganja cha mkono isipokuwa iblis aliinamisha paji lake la uso chini na kumsujudia Mungu.Alikuwa ni kiumbe aliyefanya sana ibada ila ndani yake alikuwa na kibri/majivuno ambayo malaika hawakuweza kuyajua ila Mungu alimjua kwasababu alimuumba kwa moto na sio Nuru kama ilivyokuwa kwa malaika.

Baada ya majini kufanya uasi na kufurushwa huku duniani ,Mungu akaamua kuumba kiumbe mwingine ambae atakuja kuwa mtawala katika ardhi hii, nae si mwingine bali ni ADAM. Uumbwaji wa adam ulitokana na udongo mweusi wa mfinyanzi tena uliovunda. Ndio asili ya mwanadamu.

Adam aliumbwa kwanza kama fremu tu ambalo lilikuwa halijapuliziwa roho, Iblis alikuwa akiliona fremu la kiumbe huyu mpya wa ajabu, kisha alikuwa akilizunguka na kupita ndani ya mwili wake na kisha kutoka kisha akajisemea kuwa hakika huyu ni kiumbe dhaifu sana na pindi atakapopuliziwa roho basi mimi ndio ntakuwa mwalimu wake.

Malaika mwanzo walikuwa na wasiwasi juu ya kiumbe huyu mpya kuwa pindi atakapoumbwa na kukabidhiwa utawala huku duniani basi atakuja kuyafanya yale waliyoyafanya majini (uasi na umwagaji damu) ila Mungu alikuwa against na maono yao na akawaambia kuwa hakika anayajua yale ambayo malaika hawayajui.Adam akakamilika kuumbwa kisha Mungu akampulizia roho na haraka adam akapata uhai. Kitu cha kwanza Mungu alichompa Adam ni ELIMU. Utambuzi wa kujua kila kitu mpk vile ambavyo malaika hawavijui. Kisha akawaita Malaika,iblis na Adam wote wahudhurie kwani kuna mtihani anataka kuwapa.Mungu alivileta vitu vingi kisha akawaambia malaika pamoja na iblis wavitaje vitu hivyo.Malaika na iblis pamoja wakashindwa kwani walikuwa hawana elimu navyo basi akaitwa Adam akaambiwa kuwa watajie majina ya hivyo vitu, Adam akataja kila kitu kwa usahihi kabisa na alifaulu ule mtihani ndipo Mungu akawaamrisha malaika pamoja na iblis kuwa wamsujudie Adam kumpa heshima. Malaika kutokana na kuwa waliumbwa kwa Nuru na wanafanya yale wanayoamrishwa, basi wote wakasujudu isipokuwa iblis yeye aligoma kusujudu.

Iblis alisimama pamoja na Adam wakati malaika wote wameinamisha mapaji yao ya uso chini, ndipo Mungu akamuuliza Iblis ni nini kilichokufanya uikatae amri yangu?

Iblis akajibu kuwa hakika yeye ni bora kuliko Adam kwani ameumbwa kwa Moto na adam ameumbwa kwa udongo hivyo asingeweza kumsujudia Adam.

Aliiasi amri ya Mola wake mbele ya kundi lote la malaika na licha ya kuasi kwake bado alikataa kurejea kwa mola wake kuomba toba na msamaha. Alishaamua kama mbwai na iwe mbwai. Hapo ndipo MUNGU alipoamua kumlaani Iblis na akafukuzwa kutoka katika kundi la malaika. Iblis aliipokea laana ile ila alikuwa na ombi moja tu kwa Mungu. Mungu akamruhusu aombe anachokitaka ndio akaomba kuwa apewe uhai mrefu mpk mwisho wa dunia hii yaani awe miongoni mwa viumbe vitakavyokufa mwisho.

Mungu alimkubalia , na baada ya ombi lake kupitishwa kwa hasira akasema kwa kuwa Adam ndio amesababisha Mungu kumlaani basi atahakikisha kuwa anavikalia mbele,nyuma,kushoto na kulia vizazi vya adam ili visiielekee njia ya Mungu, ili mwisho wa siku apate watu wengi wa kuingia nao motoni.

Mungu akamjibu palepale kuwa kwa hakika Iblis hana uwezo wa kupoyosha waja wake isipokuwa kwa yule atakaeamua kumfuata.Na kwa hakika ataijaza jahannam kwa iblis na wale wote watakaomfuata.

Yote haya yanatokea huko mbinguni hakuna kiumbe chochote kilichowahi kumuona Mungu ana kwa ana. Sio Adam,sio malaika wala sio huyo Iblis .Walikuwa wakipokea tu sauti ila hakuna aliyemuona Mungu toka ulimwengu unaumbwa mpk pale utakapoisha.

Mungu atakuja kujidhihirisha kwa waja wake watakaoingia peponi tu ndio watapata kumuona. Na hakuna zawadi kubwa mwanadamu atawahi kuipata kama nafasi ya kumuona Mola wake. Mungu atujaalie tuwe miongoni mwao ameen.
Hahahahaaaaa daah dunia hii
 
Hivi mnajua hii thread Mungu anaisoma na kaka Shetani nae anaisoma

yani tunazidi jitengenezea mazingira Magumu,hivi mnafkiri kaka shetani

akiona tunamdskas diskas anajiskiaje,tuache kuwasema ma braza zetu asee,shauri lenu.
 
Mtafaruku ulianza baada ya binadamu kuumbwa na kupewa mamlaka kuliko ibilisi... jamaa aka mind kwamba wao wameumbwa kwa roho na moto inakuwaje watawaliwe na alieumbwa kwa udongo na kupuliziwa pumzi ya uhai... so jamaa akaamua kumsanua binadamu ale tunda la kutambua mema na mabaya ... so ili kuweka mstari mapema akatolewa asile tunda la uzima wa milele... ina maana Adam angesanuka akawahi mtini asingekufa na ingekuwa Mungu kaanzisha adui mwingine msumbufu uwenda kuliko ibilisi... na ili wasiwe na umoja Mungu akaweka uadui baini yao. Maana callable yao bado ingekuwa kasheshe.
[emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23] HUU UZI NI KISANGA
SENSA[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Lazima tuwe na Mipaka katika Matamshi yetu...

Naomba kwanza kuweka kumbukumbu sawa; I was born and raised in a conservative Christian family until I was 20 in my first year Chuo kikuu baada ya kukutana na Mtu ambaye baadaye amekuja kuwa the love of my life NDIPO NILIPOAMUA KUBADILI DINI ingawa am not that much practicing anyway but I hope Mungu atanisaidia:


Naomba sasa kulizungumza hili in ISLAMIC perspective kwa ajili ya kushare uzoefu...

According to the aforementioned perspective HAYAKUWA MAISHA HAYA YA DUNIA ILA NI SEHEMU YA MTIHANI kwa Mwanadamu kutoka kwa Mola wake Mlezi. Baada ya Kuumbwa, kupewa akili na miongozo ya namna ya kuishi hapa duniani MWANADAMU AMEWEKEWA MITIHANI ILI KUMPIMA NI YUPO ANA MKHOFU MOLA MLEZI NA KUFUATA MIONGOZO YAKE NA NANI ATAKENGEUKA NA KUFUATA MATAMANIO YA NAFSI YAKE....

KWA HAKIKA VITIMBA VYA SHETANI NI VITIMBI DHAIFU; hawezi shetani kukushika kukulazimisha jambo lolote bali hukushawishi na WEWE UTALITEKELEZA KWA UTASHI WAKO MWENYEWE....

ATAKUPAMBIA juu ya NGONO, KUDHULUMU MALI NA HAKI ZA WENGINE, UBAKHILI KWA KUKUHOFISHA UTAFILISIKA, ATATUPAMBIA VILIVYOVICHAFU KUWA VIZURI NA MIFANO MINGINE MINGI...

MUNGU AMETUWEKEA KILA UPANDE WAZI ILI IWE JUU YA KILA MMOJA KUCHAGUA na siku ya malipo hakutakuwa na kusema hatukujua...

Na shetani siku ya HUKUMU ATAJIENGA NA KILA ATAKAMLAUMU YEYE...

MUNGU ni muweza wa kila jambo na hakuna wa kushindana na YEYE na Shetani ni kiumbe dhaifu ambaye MUNGU amejaaliwa awe mtihani kwa wanadamu...

Mungu wetu ni MUNGU mwenye Rehema na Huruma kwa viumbe wake.... tujiuulize Kwa maovu tunayoyafanya leo kama ZINAA, MAUAJI, HOMOSEXUALITY, ULEVI, DHULMA didi ya wanyonge na MACHAFU MENGINE YOTE, ZAKA HATUTOI Angekuwa ni MUNGU ASIYE NA HURUMA angeshatuangamiza Lakini KWA HURUMA YAKE AMEENDELEA KUTUPA MUDA HUENDA TUTATUBIA.. ambaye atabaki na nyendo zake mbaya mpaka mwisho wa MAISHA YAKE BASI ITAKUWA NI HASARA KWAKE...

Naomba kuwasilisha wanajamvi wenzangu..
Hakuna kitu Cha maana umeelezea hapa. Unampa mtihani mtu ambae mtokeo yake tayari unayajua si upuuzi huo
 
Umeeleza vizuri

Uzuri wa dini ni yetu ya kiislamu ni kwamba katika kuhoji mambo ya mungu kumewekwa mipaka, ambayo inaafikiana na akili.

Watu wanajiuliza kwanini mwenyezimungu amefanya hivi, au amesema hivi?

Sasa shida inaanzia pale mtu anapobuni majibu yake mwenyewe kutoka kichwani kwake, kuzungumzia asilolijua.

Allah subhaanahu wataa'la ameawatuma wajumbe(mitume), hao ndio waliotumbia kuhusu yeye na tukawaamini, sasa inakuwaje unapokuwa na swali kuhusu Allah, majibu yasiyoke kwa mtume ambaye ndiye aliyetukhabarisha habari zake, maana yeye ndiye anayejua zaidi.
(Hakuna tunachojua kuhusu Allah ila kile alichotukharisha mtume)

Sasa mtu anajiuliza mwenyewe na kujijibu mwenyewe!!!
Sasa mtume tuna mpata wapi tumuulize?
 
Mfia dini kuwa mzinifu ni kitendo Cha kibinadamu na ibilisi hahusiki
Pia ibilisi yupo kwenye eneo tengwa hakuna yoyote anaekutana nae,,,majini na viumbe wenzao walio takataka ni binadamu TU huwakaribisha kwenye mazingira Yao lakini hawana interaction yoyote na wanadamu,,ibilisi kutupwa chini ni kwenda chini zaidi ya binadamu na ajione yeye ni weak maana alitaka kuwa juu sana ila Mungu akamshusha chini sana ili ajione yeye sio chochote Wala lolote,,pia alichonacho alipewa sio kwamba ana chochote,,,ibilisi ni dhaifu kumshinda unavyodhani maana hayuko kwenye nafasi yake anambwela mbwela TU,,silaha kubwa alio nayo kwa Sasa ni fitna majungu na uchonganishi
 
Kama Ibilisi aliweza kupigana vita kuu mbinguni akiwa na malaika wake sasa binadamu ataweza kweli kupambana na kiumbe kama hiki?

Katika maeneo ambayo hua yananichanganya kwenye bible ni hii habari ya vita iliyopiganwa mbinguni kati ya Mungu na malaika zake, na shetani na malaika zake.

1. Shetani aliweza vipi kuwashawishi theluthi moja ya malaika wamuunge mkono?
2. Wakati shetani anafanya kampeni hiyo ya ushawishi, Mungu alikua wapi?
3. Mungu, malaika na shetani wote hawa ni roho. Roho zinapiganaje?
4. Ni silaha za aina gani zilitumika kwenye hii vita?
5. Ili ushinde vita, lazima uwaue maadui. Je, katika vita hii ushindi ulipatikana vipi wakati malaika hawafi wala hawaumii.

Ntashukuru kwa yoyote atakaeweza kunipa japo mwanga kidogo.
 
Katika maeneo ambayo hua yananichanganya kwenye bible ni hii habari ya vita iliyopiganwa mbinguni kati ya Mungu na malaika zake, na shetani na malaika zake.

1. Shetani aliweza vipi kuwashawishi theluthi moja ya malaika wamuunge mkono?
2. Wakati shetani anafanya kampeni hiyo ya ushawishi, Mungu alikua wapi?
3. Mungu, malaika na shetani wote hawa ni roho. Roho zinapiganaje?
4. Ni silaha za aina gani zilitumika kwenye hii vita?
5. Ili ushinde vita, lazima uwaue maadui. Je, katika vita hii ushindi ulipatikana vipi wakati malaika hawafi wala hawaumii.

Ntashukuru kwa yoyote atakaeweza kunipa japo mwanga kidogo.
Na kama roho haifi, je, malaika pamoja na wadhambi wengine wanaanzaje kuchomwa moto, alafu wenyewe wametulia tu, wanakuangalia unavyowachoma?,
Kama roho haiwezi kufa au kuuliwa basi hatutakiwi kusema hakuna kitu kisichomshinda Mungu. Kwasababu Mungu Hana uwezo wa kuiua au kuiangamiza roho
 
Katika maeneo ambayo hua yananichanganya kwenye bible ni hii habari ya vita iliyopiganwa mbinguni kati ya Mungu na malaika zake, na shetani na malaika zake.

1. Shetani aliweza vipi kuwashawishi theluthi moja ya malaika wamuunge mkono?
2. Wakati shetani anafanya kampeni hiyo ya ushawishi, Mungu alikua wapi?
3. Mungu, malaika na shetani wote hawa ni roho. Roho zinapiganaje?
4. Ni silaha za aina gani zilitumika kwenye hii vita?
5. Ili ushinde vita, lazima uwaue maadui. Je, katika vita hii ushindi ulipatikana vipi wakati malaika hawafi wala hawaumii.

Ntashukuru kwa yoyote atakaeweza kunipa japo mwanga kidogo.
Hiyo ni moja ya story ya uzushi ndani ya biblia!! Iblis ni Jini na ameumbwa kwa moto ,wala sio malaika. Iblis hana uwezo wowote wa kuwashawishi malaika wamuasi Mungu maana Malaika hawajaumbwa kwa ajili ya kuasi,infact hawajui kutenda dhambi.Wameumbwa kwa ajili ya kutii tu ,kuna malaika toka waumbwe wamepewa jukumu la kusujudu tu na wako hivyo hivyo mpk ulimwengu unaisha,kuna malaika wamepewa kazi ya kuandika mema na maovu ya mwanadamu, wao maisha yao wanaifanya kazi hiyo tu na pindi mwanadamu anapotamatika basi hurudi zao mbinguni. Hawajui kuasi.

Ila iblis ni muasi na katika mapambano, Majini ni dhaifu sana mbele ya Malaika, infact majini wanawaogopa malaika.

Malaika ana uwezo wa kumpiga jini na kumuumiza ila Jini hana uwezo wa kumdhuru malaika kwa chochote kile.

Kwahiyo suala kuwa kulikuwa na vita mbinguni kati ya iblis ,malaika na Mungu ni uongo kabisa na ni uzushi mkubwa.
 
Hiyo ni moja ya story ya uzushi ndani ya biblia!! Iblis ni Jini na ameumbwa kwa moto ,wala sio malaika. Iblis hana uwezo wowote wa kuwashawishi malaika wamuasi Mungu maana Malaika hawajaumbwa kwa ajili ya kuasi,infact hawajui kutenda dhambi.Wameumbwa kwa ajili ya kutii tu ,kuna malaika toka waumbwe wamepewa jukumu la kusujudu tu na wako hivyo hivyo mpk ulimwengu unaisha,kuna malaika wamepewa kazi ya kuandika mema na maovu ya mwanadamu, wao maisha yao wanaifanya kazi hiyo tu na pindi mwanadamu anapotamatika basi hurudi zao mbinguni. Hawajui kuasi.

Ila iblis ni muasi na katika mapambano, Majini ni dhaifu sana mbele ya Malaika, infact majini wanawaogopa malaika.

Malaika ana uwezo wa kumpiga jini na kumuumiza ila Jini hana uwezo wa kumdhuru malaika kwa chochote kile.

Kwahiyo suala kuwa kulikuwa na vita mbinguni kati ya iblis ,malaika na Mungu ni uongo kabisa na ni uzushi mkubwa.
As per Quran
 
Wengine tunafurahia kusoma comments tu, inaonekana watu hawamjui Mungu wala shetani, basi kila mmoja anasema sumu tu. Ngoja tuone hitimisho lake.
 
ili kuwepo na balance kitu kisizidie upande mmoja lazima kuwe na vitu viwili vyenye uwiano sawa ili kubalance mzigo katikati , uwepo wa nguvu hizo mbili huleta maana halisi ya maisha yalio katika kiwango sawia , ili uujue uzuri lazima ubaya uwepo kila kimoja kina umuhimu kutegemeana na mwenzake.
 
Kitendo cha Mungu kumtupa Ibilisi duniani ni kitendo cha uonevu mkubwa sana kwa binadamu.

Ibilisi sio levo za binadamu ni levo ya Mungu maana yake Mungu yeye angekomaa naye Ibilisi hukohuko mbinguni mpaka kieleweke. Kutuletea Ibilisi huku duniani ni kutuonea tu maana hatuna uwezo wowote wa kupambana naye.

Kama Ibilisi aliweza kupigana vita kuu mbinguni akiwa na malaika wake sasa binadamu ataweza kweli kupambana na kiumbe kama hiki?

Kiumbe ambacho kiliweza kupambana na malaika wa Mungu na kikafanikiwa kuwashawishi baadhi ya malaika kwenye vita kuu mbinguni na wakaasi sasa wewe binadamu utaweza kweli kupambana na Ibilisi?

Kama mbinguni tu Ibilisi alisumbua sana ambako ndiyo kuna Mungu na malaika huku duniani tutamuweza kweli?

Kama Ibilisi anauwezo wa kuingilia mipango ya Mungu na kuiharibu kama ule wa bustani ya Edeni na Mungu hamfanyi chochote anaishia tu kuwapa adhabu zisizo na maana yoyote Adam na Hawa. Hiki kiumbe sisi binadamu tutakiweza kweli?

Ilifikia hatua Mungu mwenyewe aliamua kumtoa kafara mwanaye wa pekee( Yesu) ili aweze kupambana na Ibilisi ila mission ikabuma. Sisi binadamu tutaweza kweli kupambana na Ibilisi?

Hivi unajua kama Ibilisi anaongea na Mungu moja kwa moja? Maana yake Mungu na Ibilisi huwa wanaonana. Unajua mazungumzo ya Mungu na Ibilisi kuhusu Ayubu? Sasa sisi binadamu tutaweza kweli kupambana na Ibilisi anayeweza kuongea na Mungu moja kwa moja?

Hivi Mungu aliwaza nini mpaka akaamua kututupia Ibilisi duniani?
Hapa binadamu tumeonewa sana.

Jukumu la kupambana na Ibilisi ni jukumu la Mungu mwenyewe na sio la binadamu hivyo Mungu amtoe Ibilisi duniani na akaishi naye mbinguni sisi huku hatumuwezi.

Ndio maana imekuwa ni kawaida tu kumkuta mtu ni mfia dini haswa ila ni mzinifu,muongo,muuaji,mchawi,tapeli,mwizi, mnafiki n.k.

Nani kakudanganya kuna binadamu anaweza kupambana na Ibilisi?
Tusome maandiko ya Mungu muumba wetu kila kitu kiko wazi tusome iwe maandiko ya Mungu ndani ya Bibilia ndani ya quran na kwingineko kila kitu kiko wazi, Hivi Kwanza watambua ya kuwa sisi Mtu hatufi ni wamilele isipo kuwa kuendelea kuwepo milele ni masahihisho ya ufaulu wako mtihani wako kwa hapa Duniani?
 
Mambo yalianza kuharibika pale bustanini ambapo badala ya Mungu kutoa msamaha kwa adam na ev. Yeye akawamiminia laana.

Cha kwanza aliweka uadui kati ya mwanadamu na shetani

Pili akamwambia binadamu atakula kwa jasho atazaa kwa uchungu na hakika atakufa.

angesamehe kama mwanae anavyo tushauri tusamehe saba mara sabini Tusimge fika huku.
Hatukuomba msamaha. Tulilaumu!!
 
Back
Top Bottom