Hivi na nyie wapenzi wenu wana wivu kama huyu wangu?

Hivi na nyie wapenzi wenu wana wivu kama huyu wangu?

kwa nini uongozane na mtu wa jinsia tofauti? [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Duuuh!! Mkwe umetumia neno kali kwelizwe si ulishasema wivu na kufuatiliana fuatiliana ndio zako!!
Ila tambua tu, too much of everthing is harmfull, hivyo wivu ukizidi ni kero, tena kero kweli kweli.
Sorry kwa lugha kali, ila unajua mkwe mpaka mtu akufatilie lazma umeonesha signals kuwa sio mtu wa kuaminika. Mimi sipendi kumfatilia mtu kabisa hasa nikikuamini ila when it happens kuwa umeanza signs za infidelity basi utanichukia, nitakufatilia tu kimya kimya na siwezi tulia.

Imagine mpenzi wako anakuaga good night amechoka sana hawezi kuongea zaidi, kisha after 5 mins unampigia unakuta yupo on another call. Una evidence unajaribu kum confront then anakuwa mdogo anaapologize kwa kuwa alidanganya.


Would you continue to believe such person hata kama ataendelea kuwa mkweli mbeleni. Tayari ile imeshatia doa kwenye trust. Sio mtu wa kumuamini huyo, a liar is always gonna find a way to lie.
 
Sorry kwa lugha kali, ila unajua mkwe mpaka mtu akufatilie lazma umeonesha signals kuwa sio mtu wa kuaminika. Mimi sipendi kumfatilia mtu kabisa hasa nikikuamini ila when it happens kuwa umeanza signs za infidelity basi utanichukia, nitakufatilia tu kimya kimya na siwezi tulia.

Imagine mpenzi wako anakuaga good night amechoka sana hawezi kuongea zaidi, kisha after 5 mins unampigia unakuta yupo on another call. Una evidence unajaribu kum confront then anakuwa mdogo anaapologize kwa kuwa alidanganya.


Would you continue to believe such person hata kama ataendelea kuwa mkweli mbeleni. Tayari ile imeshatia doa kwenye trust. Sio mtu wa kumuamini huyo, a liar is always gonna find a way to lie.
Mkwe nimekuelewa sana, ktk scenario kama hiyo uko sahihi kabisa. Ila kuna wale wazee wa kujistukia yaani hata dalili hakuna ila unafuatiliwa hadi unajuta.
 
Jamani, lazima mjue "ukipenda lazima uwe na wivu", wivu ni kipimo cha mapenzi kwa mahusiano husika.
Kumbuka, wivu lazima uwe na kiasi, kama vile vilivyo vitu vyote duniani vinavyohitaji ukiasi, maana wivu ukizidi inakuwa ni kero tena inaweza hata kuhatarisha hata hayo mahusiano yenyewe.
Hata chakula ukila bila kiasi lazima utavimbiwa, dawa ukinywa bila kiasi itakuwa ni sumu hata kupelekea kukuua.
Sasa kwenye mapenzi wivu ni lazima uwepo , na uwe wa wastani , maana yake usivuke mipaka ukawa utaabishaji kwa mwenza.
Mimi mwenyewe nitakuwa na wivu kwa nitakayempenda , lakini nitajitahidi kujitambua na kuudhibiti wivu kwa nimpendaye.
Pia kama naye atakuwa na wivu kwangu ni jambo jema maana nitajua kuwa kweli naye ananipenda.
Na kama mpenzi anajifanyisha utajua tu kupitia wivu na kubaini kiwango cha penzi lake kwako kwa urahisi kabisa.
Unajidhibiti vipi na wivu kwa mpenzi wako!,
Ni kwa kuwa na mawasiliano hai muda wowote ule kwa kila mmoja atakapokuwa anamuhitaji mwenzi wake kwa wakati, jambo ambalo litawajengea uaminifu kwa kila mmoja na kupelekea kuaminiana sana , na kusababisha wivu uwe wa kiasi "automatically", kwa pande zote.
Kwa wapenzi kukiwa na mawasiliano mazuri kunajenga kuaminiana, na mapenzi bila mawasiliano mazuri hapo penzi wala upendo , happy kutakuwa na mapenzi ya kinafiki ya kuviziana na kudanganyana.

Kwahiyo wivu ni muhimu sana uwepo, ila uwe wa kiasi kati ya wapendanao.
Ukimwamini mpenzi wako , utajikuta hata kama hujala unanenepa unanawili hasa.
Lakini imani hiyo itajengwa na mawasiliano mazuri pekee, lugha nzuri kwa umpendae, kupatikana muda wowote utakaohitajika na mpenzi wako nk.
Pia uwazi baina ya wapendanao ndiyo jambo la pili la muhimu kufanya uwe kuudhibiti wivu kwa mpenzi wako. Uwazi unasaidia kujenga na kuinua kiwango cha imani kwa mpenzi wako na kusababisha wivu uwe wa kiasi. Maana atakuamini mno na kufanya muishi maisha ya furaha na amani, hata kama umechelewa wapi basi mpenzi wako hatakuwa na wasiwasi maana anakuwa anakuamini kwamba hutamsaliti.
Na kupelekea kuudhibiti wivu.
Nafikiri kwa sasa inatosha....
Kwa kifupi dawa ya wivu wa mapenzi ni kumuhakikishia Exclusivity mpenzi wako kwa kuwa mkweli na muwazi always. Ukiwa available muda wote its an added advantage.

Shida wengi hawaelewi kuwa wivu wa mpenzi wako unautengeneza mwenyewe kwa tabia zako za kishenzi.

Kwa men, unajua kabisa uko na mpenzi wako mnatoka out instead ya ku focus kwake unaanza kuangalia matako ya mademu wengine au unasalimia salimia mademu wengine un-neccessarily. Unaanza kuficha ficha simu kwa vile umeanza michepuko pembeni ukibanwa unakuwa mbabe.Mara unapokelea simu chooni au nje. Stay faithful bros.

KE unaanzisha mazoea ya kijinga na wanaume wengine mnachat full time hadi wakati upo na mpenzio we ni busy na simu tu. Mnachat vitu gani vya maana hivyo na co-workers wako ambao mmeshinda wote ofisini. Unaanza kuficha ficha simu, mipassword kibao mara ukapokelee nje, instead ya kuweka wazi kwamba you are taken unapotongozwa matokeo yake unastukiwa umeshaanza random dating.

Hapo ndio mtu anadevelop wivu wa ajabu mno halafu mnakuja kuanza lalamika bure kwa matatizo mnayoyatengeneza wenyewe.

My friends ni hayo tu kwa leo, INTEGRITY first!
 
Mkwe nimekuelewa sana, ktk scenario kama hiyo uko sahihi kabisa. Ila kuna wale wazee wa kujistukia yaani hata dalili hakuna ila unafuatiliwa hadi unajuta.
Huo wivu unaousemea wewe nauelewa, ule wivu usio na mashiko ntauita "wivu wa kisukuma".
 
Asipokukodolea macho utatafuta mwingne anaejua kukodoa macho. Hahahahaha haya bhna kazi kwako upige chin au ukomaeee
 
hhahaahahah mayo weeeee! mie nilishaweza kujitune nowdys ukiona naongea na simu mbele ya hubby bas 90%huwa ni za biashara zangu za strawberry !otherwise sipend kupigiwa simu maana unamuona mtu ananyanyuka anazima tv !sasa jichetue ukaongelee nje utajuta huo mnuno na gubu !ptu !pole !
Labda hubby wako alishaweka question mark kuhusu mwenendo wako. Haiwezekani mtu akawa na wivu from nowhere.
 
Mpe majukum ya kumfanya kua busy kama mnaishi nae...hutaona kama atakusumbua.Ila mijitu ya hivi ni kero sana..kuna wa design hii pia unakuta anakuuliza upo api?unafanya nini?umekula nini? Yaani wanakera mno mfyuu.

Labda tuseme tumetofautina kila mmoja anayachukulia mapenzi vile anavyoweza na vile anavyoona ifaa. Wapo wengine wasipoulizwa hayo maswali wanajiskia vibaya kweli kweli; sometimes hivo vitu vidogo mnavyoviona kero ndiyo big deal kwenye mapenzi.
 
Watu wengine sijui mapenzi wamejifunzia ukubwani!

Yani hivi kwa akili ya kawaida unaweza kunilinda mimi mtu mzima tena tuliyekutana ukubwani wote tukiwa na meno 32 mdomoni?

Jamani hivi na nyie wenzangu mnadate na watu yenye wivu wa kiporipori kama huyu wangu? Asione simu imepigwa atanikodolea macho mpaka nimalize kuongea halafu ndio aniulize eti nilikua naongea na nani.

Mtu ana wivu mpaka kwa ndugu zangu yaani. Asione nimeongozana njiani na mtu wa jinsia tofauti, atajinunisha mpaka basi.

Wenzangu mnawezaje kuishi na watu wa namna hii?
Pole mkuu,wengine wivu mpaka Kwa wadada Wa MUME,Kwa wadogo zake pia ni balaa,yanatukuta wengi,ila uvumilivu na kujitahidi kumzoea maana hiyo ni Tabia ya mtu mliyekutana ukubwani kuifuta sahau.Na umezidisha ujuzi kwa hiyo anaona ukichepuka utazidisha ufundi Kwa mchepuko.Hapo usijute pia
 
Wivu ni kitu chema kwenye penzi lakini ukipita kiasi hutia dosari penzi na hata kulivunja.

 
Watu wengine sijui mapenzi wamejifunzia ukubwani!

Yani hivi kwa akili ya kawaida unaweza kunilinda mimi mtu mzima tena tuliyekutana ukubwani wote tukiwa na meno 32 mdomoni?

Jamani hivi na nyie wenzangu mnadate na watu yenye wivu wa kiporipori kama huyu wangu? Asione simu imepigwa atanikodolea macho mpaka nimalize kuongea halafu ndio aniulize eti nilikua naongea na nani.

Mtu ana wivu mpaka kwa ndugu zangu yaani. Asione nimeongozana njiani na mtu wa jinsia tofauti, atajinunisha mpaka basi.

Wenzangu mnawezaje kuishi na watu wa namna hii?
Piga chini atakuua mapema huyo
 
Watu wengine sijui mapenzi wamejifunzia ukubwani!

Yani hivi kwa akili ya kawaida unaweza kunilinda mimi mtu mzima tena tuliyekutana ukubwani wote tukiwa na meno 32 mdomoni?

Jamani hivi na nyie wenzangu mnadate na watu yenye wivu wa kiporipori kama huyu wangu? Asione simu imepigwa atanikodolea macho mpaka nimalize kuongea halafu ndio aniulize eti nilikua naongea na nani.

Mtu ana wivu mpaka kwa ndugu zangu yaani. Asione nimeongozana njiani na mtu wa jinsia tofauti, atajinunisha mpaka basi.

Wenzangu mnawezaje kuishi na watu wa namna hii?
Si utafute kuolewa na mtu asiye na wivu kabisa hasa engineers hawana wivu kabisa mkatie talaka hana adabu huyo ili uwe huru na simu yako na hao wa barabarani desemba hiyo imeingia kakate talaka haraka engineer unakusubiri kwa hamu.
 
Hahahaaa!! Mbona wivu wa kisukuma!!
Mtu anahisi wivu ukiwa haupo nae tu, atakusakama mara umeanza mambo yako eh! Upo wapi kila saa, unafanya nini? Hapo hajawahi kuona chochote hatarishi ila accusations haziishi
 
Mtu anahisi wivu ukiwa haupo nae tu, atakusakama mara umeanza mambo yako eh! Upo wapi kila saa, unafanya nini? Hapo hajawahi kuona chochote hatarishi ila accusations haziishi
Kwakweli taabu tupu!!
 
Wivu ni sehemu ya Upendo sasa kma hana wivu kwako means hakuna upendo ova
 
In short humpendi

Penzi mpya tamu sana

Akupendae kweli anageuka kuwa kero

Take care

Usije tema BIG GIII kwa karanga za kuonjeshwa
 
Back
Top Bottom