Hivi naweza kujenga nyumba kwa mshahara wa laki 5 kwa mwezi?

Unajenga mkuu choo na bafu Tena Kwa mwaka mmoja hapo unadunduliza
 

Labda KUJENGA heshima BAR.
 
Kweli, ushauri mzuri nyumba itatokea kwenye chanzo nitakachokitengeneza.
Kabisaaa, ukipata hata kipato kidogo cha kukuwezesha kupata msosi wa uhakika....hiyo laki 5 unaweza kuwa unabana kidogo kidogo unapeleka hardware unapewa risit unatulia, ukipata tena unapeleka unatulia....mwisho wa siku risiti ikisoma m+ unaanza kuchukua material unaanza mdogo mdogo.
 
Unajiendekeza.
 
Unaweza kupiga njiwa wawili kwa jiwe moja.wewe vuta muda kamshaahara kaongezeke,fungua kibiashara kidogo halafu baadaye vuta mkopo wa kutosha fanya mambo yako.
 
Wanaume huwa hawakati Tamaa, kuna mzee Iringa alianza kwa kuuza Karanga tu, saizi ni Bilionea Mkubwa sana Iringa.

Wewe una kazi tayari, Chukua Mkopo benki, nenda CRDB wana Rate ya 13, Hakikisha unakuwa na vitenga uchumi zaidi ya Moja.

Masika hakikisha unalima, Hakikish unakuwa na ufungaji hata wa Kuku wa kienyeji. Mfungulie mkeo Biashara hata kama ya Genge huko Sokoni, Kwenye Maisha haya wonga wako do umasikini wako. Mkeo akiwa anaingiza % fulani itakusaidia zaidi.

Endelea kuthubutu katika biashara zingine usitegemee hela ya muajiri ya mwisho wa Mwezi.

Watu wanaazia bodaboda na wana make Maisha sebuse wewe unamshahara.

Kuna Jamaa mmoja alikuwaga bodaboda miaka ya nyuma saizi ana nyumbani na Subaru Forester ya mwaka 2013
 
Mimi mshahara wa milioni 1.6 baada ya makato yote na bado namiliki kiwanja tu na mkataba uko ukingoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…