Hivi ni akili , uoga au upumbavu kuhusu UTT ?

Hivi ni akili , uoga au upumbavu kuhusu UTT ?

Mtaani mtu anajenga banda la chips na mtaji kwa jumla ya laki 7 kwa mwaka ana make zaidi ya 5M .

Mwingine anaweka 20M UTT kwa mwaka ana make 2M

Hiki ni nini ? Mimi nadhani huko wanafaidika wanaoweka pesa nyingi
Sio kila mtu ana hobi ya biashara. Na wengine hawana interest ya kuingiza hela za haraka haraka. Wengine wanapenda slow, steady and sustainable income hata kama ni ndogo.

Mifuko ya uwekezaji kama UTT faida yake ni ndogo lakini kwa muda mrefu hela inakuwa sana na kuna wakati unaweza fika ukampita hata huyo wa chips kwenye capital gain.

Kuuza chipsi lazima uwepo au usimamie kwa karibu sana. Full stress na unakosa muda wa kuishi na kufanya mambo mengine ya kifamilia. UTT watu wanakufanyia kazi na uko huru kutumia muda wako utakavyo.
 
Hivi ukiwa na Pesa UTT kwenye mfuko wowote unaweza kwenda kuombea mkopo Benki bila kuzitoa??

Na nini Bank watahitaji kama uthibitisho?
 
Kafungue banda la chipsi upate 5M kila mwezi, sisi wengine tutaendelea kuwekeza UTT.

Kwa maana hela zetu zipo salama sana, na hatuhitaji kuziangaikia. Acha tule kuku kwa mrija.
 
Mtaani mtu anajenga banda la chips na mtaji kwa jumla ya laki 7 kwa mwaka ana make zaidi ya 5M .

Mwingine anaweka 20M UTT kwa mwaka ana make 2M

Hiki ni nini ? Mimi nadhani huko wanafaidika wanaoweka pesa nyingi
Hapa wamiliki wa UTT ndio wananufaika tu. Wanaweka pesa zao huko ni mbumbumbu wasiokuwa na kaziya kufanyia hizo pesa. Mungu anawaona.
 
Mtaani mtu anajenga banda la chips na mtaji kwa jumla ya laki 7 kwa mwaka ana make zaidi ya 5M .

Mwingine anaweka 20M UTT kwa mwaka ana make 2M

Hiki ni nini ? Mimi nadhani huko wanafaidika wanaoweka pesa nyingi
Watu tofauti, walio katika stage tofauti ya maisha yao, na mitaji tofauti, wanatakiwa kuwa na investment strategies tofauti.

Mtu Mzee, ambaye amefanya kazi miaka mingi na kustaaafu, ana pesa nyingi za mafao, na anachotaka kikubwa ni kuzitunza pesa zake zisipotee, anatakiwa kuwa na strategy ya low risk low return kama hiyo ya UTT.

Mtu kijana, ambaye ndiyo kwanza anaanza kazi, hana mtaji mkubwa, na ana miaka mingi ya kufanya kazi, anatakiwa kuwa na investment strategy ya higher risk, higher returns.

Kwa hivyo inabidi uelewe uko wapi ili kujua investment strategy gani itakufaa.

Katika hizo strategies mbili kwa mfano (and that is just a simplification of many options) hakuna strategy nzuri au mbaya, kuna strategy itakayokufaa wewe au la, na mwingine anaweza kuwa na strategy tofauti ikamfaa yeye pia.

Ndiyo maana wenzetu wanaajiri hata Financial Planners kuwasaidia kupanga haya mambo.
 
Huyo wa mwenye banda la chips anatumia muda kiasi gani kufanya kazi hapo kwenye banda lake? Na huyo aliyeweka UTT anatumia muda gani kufanya kazi ili hiyo hela iliyowela UTT uzae faida?

Ndugu, muda ni rasilimali. Hizo option mbili zote ni uwekezaji, swala la unawekeza wapi inategemea na muda ulionao wa kwenda kufanya kazi kwenye huo uwekezaji wako.

Haiwezekani mtu anayetumia masaa 12 kwenye banda la chips apate faida sawa na mtu aliyeweka fedha UTT na kuendelea na shughuli zake nyingine, HAIWEZEKANI!
 
Ngoja nikuulize hivi umeweka labda 10M kama ulivyosema baada ya muda Fulani kupita na unataka kutoa si unauwezo wa kutoa principal ( 10M) na faida zake au unatoa faida pekee?
Ndiyo Mkuu
 
Mtaani mtu anajenga banda la chips na mtaji kwa jumla ya laki 7 kwa mwaka ana make zaidi ya 5M .

Mwingine anaweka 20M UTT kwa mwaka ana make 2M

Hiki ni nini ? Mimi nadhani huko wanafaidika wanaoweka pesa nyingi
Unafanya biashara au biashara za mdomoni?
 
Mtaani mtu anajenga banda la chips na mtaji kwa jumla ya laki 7 kwa mwaka ana make zaidi ya 5M .

Mwingine anaweka 20M UTT kwa mwaka ana make 2M

Hiki ni nini ? Mimi nadhani huko wanafaidika wanaoweka pesa nyingi
Ishi ulivyoamua kuishi! Wewe nini kinakuuma kama akitengeneza 2 m? Hivi unajua wengi wanaoweka hela huko ni zile hazina pa kwenda? Sasa mtu anaamua badala ya kukaa nayo home anaweka huko itulie tu!
 
UTT kwa vijana ni uoga na ujinga mtupu. Hii nchi itapataje maendeleo kama vijana wanaogopa risks kiasi hiki? Kijana mwenye afya na akili timamu unashindwaje kuzungusha hela ikazaa hata mara 2 kwa mwaka? UTT inafaa wazee wenye mpunga mrefu ambao hawawezi hekaheka.
Tulia wewe acha wenge
 
Mkuu umetumia maneno makali saana na hapo imeonesha ni namna gani ulivyo na dharau au haufikirii nje ya box kwa lugha rahisi wewe unataka watu wote tuwe wafanyabiashara ukiwa mkulima ww ni mpumbavu ukiwa mtumishi wewe ni mpumbavu n.k
Unajua anayeweka pesa utt ana malengo gan? Kuna watu ambao wanamalengo ya saving tu akiwa na lengo baada ya miaka kumi ijayo atoe pesa yake na afanyie jambo na hapa ndio utawakuta wanafunzi,watumishi na wakulima.
Au ww wote waliowekeza UTT wamwkwambia kuwa wanataka faida kila mwisho wa mwezi?
Nashindwa kuendelea kutoa faida ya kuwekeza huko utt kwa sababu ushakuja na hitimisho kuwa huo ni upumbvu.
Mwisho usimpangie mtu cha kufanya.
Jamaa nimelipuuza sana! Hapo eti linaona lilianzisha uzi bomba kabisa!
 
Mtaani mtu anajenga banda la chips na mtaji kwa jumla ya laki 7 kwa mwaka ana make zaidi ya 5M .

Mwingine anaweka 20M UTT kwa mwaka ana make 2M

Hiki ni nini ? Mimi nadhani huko wanafaidika wanaoweka pesa nyingi
Security....!!
 
Fredwash Naomba nikuulize hivi labda umeweka 5M UTT kwa muda wa Miaka 10 na unataka kutoa pesa zako je unaweza kutoa principal ( ile pesa uliyoweka) pamoja na faida au unatoa faida pekee?
Utt saa yoyote unaweza kutoa pesa yako zote kama ukitaka isipokua mfuko wa Bond
 
Ukiona una save pesa bank, unaweka sijui fixed account , sijui UTT ni kipimo cha udogo wa akili zako na fikra mbovu ulizinazo, pesa inazungushwa muda wote bank ni njia ya kupitishia nazani sijawahi kuwa na milioni bank zaidi ya siku mbili ndio nikasave eti UTT, inamaana sioni kabisa sehemu ya kukuza pesa
Watu tunaa ela ambazo hazina kazi tunakimbiza UTT....ika kama vip njoo tuogee unisaidie matumizi ya hiz pesa basi kama hutojali
 
Back
Top Bottom