Hivi ni kwanini tunapenda kuitana "Mkuu"?

Nashangazwa na matumizi ya neno MKUU humu Jf. Yaani kila mtu anamwita mwenzake mkuu hivi huu ni ukuu unatokana na kitu gani.

Mkuu Kweli Wewe Ni Bonge La Lofa Mkuu, Na Mkuu Acha Kuja Na Maswali Ya Kiliberali Mkuu, Sawa na Umesikia Mkuu?????
 
Mkuu Iron Lady naona umeifurahia sana hii thread.

Usiku mwema wakuu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mi hili neno halinishangazi hata kidogo. Kinachonishangaza ni hivi vitu vinavyouzwa humu JF asilimia 80% vimetumika miezi 3 tu, hapa ndo huwa nabaki hoi.
 
Basi wewe tutakuita msaidizi.
 
Nashangazwa na matumizi ya neno MKUU humu Jf. Yaani kila mtu anamwita mwenzake mkuu hivi huu ni ukuu unatokana na kitu gani.

Mkuu, unajua humu JF hatujuani kwa umri sasa kurahisisha ndo trait ana mkuu. Ni heshima Fulani hivi.
 
Haha Mkuu na Wakuu....ni JF...hii mkuu nafikiri ni rejesta tu ya mahali fulani na watu fulani kama ilivyokuwa Mdau na Wadau kama kule "Ze Utamu Kijing'ata Ulimi"
 
Mkuu...Ni njia rahisi ya kuitana hivyo kwa usiye mjua umri, jinsi,madaraka nk nafikiri ni hivyo tu mkuu
 
Kuna hii nyengine ya kuamini kila msomi ana mawazo bora kumbe hapana vitu hivi havina uhusiano hata kidogo na kama upo basi ni mdogo mno. So mtu kuwa na busara na hekima hakuna uhusiano wowote na umri au elimu yake. Unajua watu wazima walianzia huku kwenye utoto, ujana n.k sasa mtu kama kwenye ujana wake huoni kitu kichwani basi hapo usitegemee kama akiwa mzee atakua na busara. Kwa hiyo basi twaweza kuufanya uzee wetu uwe bora iwapo tutaamka kipindi cha ujana wetu na kuyafanyia marekebisho maeneo mbali mbali ambayo yana matatizo.
 
Hivi hata wadada wanaitwa 'wakuu'?

Wewewe!!!!!! Yaani dada hastshili kuitwa mkuu? Hebu jaribu kuifuta hiyo mifumo dume kwenye kichwa chako. By the way mimi binafsi uwa natumia hilo neno kumaddress member yeyote mwenye mchango wenye akili. Hata siku moja siwezi kumuita mkuu mtu kama Ifweero, Msalani, Rutashobolwa na Lumumba book 7 group wote kwa kuwa hawajitambui.

Tiba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…