Hivi ni kwanini wanaume mnaongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwenu?

Hivi ni kwanini wanaume mnaongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwenu?

Qur'an inasema "Wanaume ni viongozi wa wanawake"

Mtume Muhammad akasema "Laiti ingeruhusiwa kiumbe kumsujudia kiumbe mwenzie, basi mke angemsujudia mumewe. Hebu tazama daraja alilopewa mwanaume.

Wote waalimu, inawezekana mmoja ni mkubwa kuliko mwingine, mmesoma chuo kimoja ila mmoja ni mwalimu mkuu. Lazima apewe heshima yake. Yaani sisi ni waalimu wakuu. Haina maana hatukosei, laa. Tunakosea, ila mwenye dhamana, cheo, wadhifa, madaraka et al ni rahisi kujihalalishia makosa yake lakini ukikosea wewe atakusema sana na kukuonya. Mfano huo huo, mwalimu mkuu anaweza kuchelewa kurudi likizo kwa siku 3 na uaimuulize chochote. Sasa na wewe iga kuchelewa, akuandikie utoe maelezo.

Dada, we jua tu mwanaume ana mamlaka juu yako, ana wadhifa, cheo, ni kiongozi wako, ana daraja ya juu yako. Tuko sawa kimaumbile (sio 100%) lakini sisi wanaume tunajiona na ndivyo ilivyo ni watu wenye mamlaka juu yenu. Ni kawaida kwa mwenye mamlaka kujihalalishia mambo yake au akajitete na kutaka akubalike na aeleweke anavyotaka yeye.

Jiwe si unamuona sometimes anavunja katiba. Lakini nani anamhoji? Tutabaki kulalama tu sisi kama raia ndivyo wake zetu mtaendelea kulalamika lakini kimsingi sisi tuna kiburi cha asili.

Tuna ile ideology "unataka kushindana na mimi"

Hujawahi kusikia mtu akichaha mifukoni anasemaga "Leo nipo kama mwanamke kabisa" Haina maana hakuna wanawake matajiri, basi tu tunamaanisha ile hali ya wanawake kuwa ni watu wa kuamrishwa. Na mwanaume ukiwa huna hela ni kama mwanamke tu unaweza kuambiwa kufanya chochote na ukatii.

Dunia imeumbwa hivyo. Vitu viwili viwili na kimoja kinatawala kingine. Gizi na nuru, mke na mume, mtawala na matawaliwa, tajiri na masikini et al. Haina maana kimoja hakina umuhimu? No, ila kimoja kinamtawala kingine na lakini katika maisha lazima viwepo vyote otherwise hakuna maana yoyote ya huo mfumo.

Nadhani tumeelewana.
Kwa hiyo kuwa juu yetu, au kuwa mtawala ndio inawapa uhalali wa kufanya dhambi?
Au ndio mkifanya dhambi zinageuka kuwa "haki" huku zetu wanawake zinaonekana kinyaa?
 
Hivi nyie mkiacha kuuza, tutanunua wapi?
Mkigoma kutoa mbunye kabla ya ndoa sisi tutapata wapi?

Endelea kujilinganisha.

By the way usiyachukulie serious sana maisha ya JF
Kuna biashara yoyote inayofanikiwa bila kuwa na wanunuzi?
Mnavyoonekana kukerwa na wanawake wanaojiuza nilitegemea kwa pamoja muungane mpinge kununua lakini sio mnanunua baadae mnakuja kuhubiri dhambi zetu.
 
Wanaume kila uchwao mnafungwa kwa kulawiti, kubaka na kuua watoto.
Mnawatoa mimba mlowamimba,mnawakimbia watoto wenu baada ya kumimba huko, nk nk nk nk
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]mlowamimba nini


[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]yaani wanaume kuwamimba wanawake inaonekana sawa ila wanawake kumimbwa inaonekana kosa
 
kwenye imani inabidi uamini kila kitu unachoambiwa. ukishaanza kutilia mashaka maandiko ambayo yamemtambulisha huyo Mungu unaemuabudu, lazma utilie mashaka na existence ya huyo Mungu, kwa sababu vyote vilivyoandikwa kwenye kitabu kitakatifu vinamuhusu yeye.

huwezi ukaisoma bible selectively kwa kuchagua sehemu unazozipenda na kuacha sehemu unazozichukia, inabidi uisome yote. ukishaanza kusema hiki kibaya, hiki kizuri, unakua unakosea, maana vyote hivyo tumeaminishwa vimetoka kwa Mungu.
[emoji16][emoji16][emoji16]imebidi nicheke, kwahyo mimi ambae sisomi maandiko simuamini Mungu? Yani kila kitu niamini na hayo maandiko yana edition tofauti tofauti ni Mungu au mwanadam anayoifanya hiyo Edition? Chuja linalofaa kwenye maandiko na uamini hvyo sio kwa sababu tu ni maandiko ndio uamini na kufanya kila kitu.
 
Tatiza lako haujasoma uzi wangu wote kuna sehemu nimesema naamini katika Mungu na dini ninafuata maandiko na pengine ninayajua maandiko kuliko hata wewe ila sijaona andiko linalomruhusu mwanaume kutenda dhambi labda uniletee wewe
Kwani wewe mpagani Dada??? Maswali yako yote yamejibiwa na Mungu Soma kitabu kitakatifu, ukiendelea kubishana basi endelea kubishana na Mungu....
Huwezi kuwa sawa na Mwanaume hata kama ukivaa suruali mama weeee,
Na hiyo ni nature huwezi kuibadili, kubali tuu kuwa wewe ni mwanamke na sisi ni Wanaume,ukishajua nafasi yako vzr, huwezi kupoteza muda kubishana na mambo ambayo majibu yake Yapo wazi
 
Na watu huchaganya dini na uonevu na wengi hawaelewi dini vzuri, wabatofauti gani na wale mafarisayo walioenda kumshtaki yule mwanamke aliyekuwa anaziniwa ili apigwe mawe na kumwacha mwanaume, Yesu akawaambiwa asiye na dhambi na awe wakwanza kumpiga yule mwanamke na mawe mbona wote walikimbia, au kule Nigeria yule mwanamke alibakwa akapata mimba under sheria law wakamhukumu apigwe mawe mpaka kufa vipi huyo mubakaji.

Upendo wa kweli huheshimu na kamwe huwezi muumiza partner wako Kwa kutafta excuses na justification za maandiko baada ya kukiri kosa
Umeeleza vyema kabisa tatizo wengi wanajihesabia ukamilifu wanasahau nao n binadam na wanatenda kama ilivyo kwa wengine.
 
Hapo kwenye Eva kumpindua Adam ili awe kama Mungu,, ushahidi wako nausubiri hapa
Vyovyote iwavyo. Asili inaonyesha Mwanaume ndiye mtawala.

Jamii karibu zote duniani mwanaume ndiye mtawala.

Hivyo yeye ndiye hubuni sheria kulingana na vile atakavyoona yeye.

Hata mwanamke kupewa haki ni matokeo ya baadhi ya wanaume kuona ipo haja ya kuwapa haki hao wanawake.

Wanawake hawana uwezo wa kukaa pamoja na kuamua kupigania haki zao bila msaada wa mwanaume. Hiyo ni nature mkuu.

Huyo Marianah anajaribu kufanya jaribio lililofeli pale Edeni lililofanywa na Mama yetu Hawa au Eva.

Eva alitaka kumpindua Adamu kisiri ili afanane na Mungu. Kumbuka Adamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu wakati Eva au Hawa akiumbwa kwa Mfano wa Adamu.

Kama jinsi Wanadamu wanavyohangaika kuwa sawa na Mungu lakini inashindikana ndivyo wanawake wanavyojitahidi kuwa sawa na Mwanaume na inashindikana.

mwanamke atabaki kutawaliwa siku zote mpaka aingie kaburini kwenye huo usawa.
 
Biblia kwanza haijahalalisha dhambi yoyote vile watu mnatafsiri vibaya tu maandiko, mila za kiaftica zako hazitumiki zimeachwa siku mingi. Sasa hivi technology, education mambo mengi ya hovyo yameshaachwa ndo mana hata nyie mnalalamika wanawake wameharibika vile wanawake wanajitambua, na nyie wanaume wa Africa uanaume wenu ili ukamilike ni lazima mnyanyase wanawake mwanamke mjanja mnamuogopa ka homa ya ini
Ndo mana nakwambiaje, ni mfumo uliwekwa kupitia vitabu vya Mungu jinsi ya mwanamke na mwanaume wanavyotakiwa kubehave kwenye jamii.

Huo mfumo unaotaka wewe uwepo inabidi uwekewe utaratibu wake ili usije ukakinzana na mafunzo ya kwenye dini.

kwa sababu mtoto wako wa kiume akipelekwa mafundisho atafundishwa misimamo ya kibiblia kuhusu wanawake na wanaume katika jamii.

akirudi mtaani na akienda shuleni anakutana na misingi mipya ya iliyowekwa na utandawazi.

akikaribia kuoa, mama mzazi anampa lisala kuhusu wanawake. yani mama mzazi anaogopa mtoto wake wa kiume asipelekeshwe na mke wake na anataka ahakikishe mtoto wake wa kiume ana uwezo wa kumtawala mke wake.

mwanamke huyo huyo anaelilia usawa, ndo huyohuyo anaemnong'oneza mtoto wake wa kiume asipelekeshwe na mke wake. Na akijua mtoto wake anatawaliwa, atavuruga tu hio ndoa.

Cariha rafki angu haya mambo yanakinzana sana.
 
Baada ya kusoma taarifa yote, nime-observe vitu vichache.
  1. Mwandishi dada Marianah wewe ni mwandishi mzuri, matumizi ya alama - 100%, matumizi ya aya - 100%, mtiririko wa habari husika - 100%, kutochanganya lugha - 100% nk nk.
  2. Content ya ulichokiandika - sina comment.
  3. Inawezekana kabisa msukumo wa ulichokiandika umetokana na kelele za wanaume kulalamika kwenye mitandao, lakini naamini kuna msukumo mwingine nje ya huo, na kwa vile 3, 7, 8 na 10.
All in all, wewe ni moja ya wanawake wachache humu wanaoweza kuandika andishi likaenda kwa mtiririko mzuri, likasomeka hata kama content ni 0.

Nikipata muda nitakuelewa, big up.
[emoji120][emoji120]shukrani sana mkuu barikiwa
 
[emoji16][emoji16][emoji16]imebidi nicheke, kwahyo mimi ambae sisomi maandiko simuamini Mungu? Yani kila kitu niamini na hayo maandiko yana edition tofauti tofauti ni Mungu au mwanadam anayoifanya hiyo Edition? Chuja linalofaa kwenye maandiko na uamini hvyo sio kwa sababu tu ni maandiko ndio uamini na kufanya kila kitu.

aisee.. hili nalo tatizo.
 
Na siku mkifanikiwa kuyarekebisha maovu ya wanawake kwenye jamii mtatuambia
Kama kivumishi kikurupushi

Karibu Denmark tule bata nitaoa badae sanaaaa

Kwa hali hii????

Siku mkipata usawa mtaniambia
 
Na wala hakuna anayetaka usawa ila huo utofauti haupo kwenye dhambi
Hapa Denmark huo usawa mnao lilia haupo

Ni kipaombele tuu wanapewa ila Hakuna usawa kabsaa

Kuna kipindi nlikua Canada nako ni hivo hivo

November ntakua tz
 
Sikujua kama wanaume wa jamiiforum(jf) wanaijua biblia namna hii aisee wote leo mnaijua dini na historia vilivyo, ajabu ni kwamba mnashindwa kuiishi historia mpaka tunajipambanisha na nyie
 
Back
Top Bottom