Hivi ni kweli kileleni mwa mlima Kilimanjaro kuna shimo?

Hivi ni kweli kileleni mwa mlima Kilimanjaro kuna shimo?

nashukuru kwa wote mliojaribu kujibu na kuelezea kwa uelewa wenu. anyway, hi hivi! kupitia machame mpaka top ya mlima ni 42kms, kupitia marangu ni 38kms. mlima Kilimanjaro una 5 zones, (1) cultivate,0-1000masl,(2) montana Forest Park1000-3000masl (3) moorland 3000-4000masl(4) alpine reset 4000-5000masl (5) ice cap au summit,5000-nakuendelea. kwa wale waliopanda watakua wananielewa, base ya mlima Kilimanjaro ipo kwenye 4600-4700-4800 masl. hii inakua ni camp ya mwisho kabla ya ku summit,kutoka kwenye base camp mpaka highest point kwa wanaopitia south na western side ya mlima ni 5kms umbali. mwendo wa pole pole ni 6-7hrs walking. baridi ni kali kutegemeana na majira ila normal ipo 3-7minis.juu ya mlima kabisa kuna mabarafu makubwa yanaitwa glacier, ukweli shimo lipo ila ni mbali sana kutokea highest point. kwa kutembea kwa mtu mwenye nguvu haswa wapanda milima anaweza tumia saa 1-1:30 kufika. hili shimo linajulikana kama ash pit, au ash cone. kuingia unaweza ila sio mbali sana maana limechongeka kwa kama rim. na halina kina kikubwa ukiangalia kwa nje. nimewahi kuingia kama mita 5 .ila kuna wakati linatoa harufu kali sana ya sulphur ambayo hupelekea baadhi ya watu huumwa vichwa, kutapika,tumbo kuvurugika n. k.unaweza kuniuliza chochote kuhusu mlima Kilimanjaro na nitakujibu. kwani mimeutembea wote na nimeweza kufika highest point zaidi ya 100 times. pia mlima meru, oldonyo lengai n. k asanteni sana
Bila picha umetukosea sana.. Tuoneshe ukiwa ktk shimo hilo..
 
Marangu Route hakuna steep hivyo kwenda kileleni ni zigzag mnatembea taratibu. Tulianza SAA 6 usiku tukafika 111 alfajiri hoi bin taabani. Ni kweli usipojikazi peak utaiona karibu ila hufiki!! Tulikunywa chai tuu pale Kibo ili tusitaapike njiani tukakosa nguvu. Hansmeyer Cave, Gilmans Point nazo ni sehemu ya Kilele ila wengi huishia hapo! Safari ya kupanda Mlima isikie tu it's hard and tough!!
nataka nikuelezee kidogo tu. hamkula kwasababu mlikua too high for digestion to take a place. hivyo basi inakutaka ule chakula laini ambacho ni lite food, nyama nyekundu, karanga n.k havifai kwani huchukua mda sana kumeng'enywa hivyo hupelekea (kuvimbiwa) tumbo kujaa gas. so nivizuri kunywa uji au chai na biscuits tu.
 
1fe10a17b5ed6d65a3df0927d9b42b79.jpg
hii nimeipiga nikiwa 4200masl nikiwa upande wa kusini mwa mlima
c9a782e2642f9c23617e1d415b31b2f8.jpg
hii ni 4000masl.

Hicho ndio nnachokisema sasa, muonekano wa mlima kadri unavyo usogelea uko tofauti sana na wengi wanavyouona kwenye Picha mkuu.

Ukiwa Karanga, Barafu au Baranco si unakumbuka unavyoonekana?..hahahahaa ila sitaki kuwaza kuhusu Lava Tower!
 
kweli we mchovu ndugu yangu. kutoka getini mpaka mandara ni 8kms.so unashindwaje kuendelea?
hahahah! Ishu ilikuwa ni mpangilio na mfadhili, tulifadhiliwa na shirika flan la mazingira kuishia hapo, sasa nisingeweza kuweka mipango ya binafsi wakati tulikuwa group, ila naamini Mungu akijali ntakuja kumalizia kiporo, natamani sana
 
Naam kumbe ndio kisa Yule Guide alituambia tusisogelee Crater kuna Hewa Chafu! Kwa wakati huo wa 1980s crater ilikuwa Imetanda theluji tupu huoni Rocks wala Mchanga. Routes tuliambiwa kuna: Umbwe Route, Machame Route, Marangu Route. Route hatari na mbaya kabisa tuliambiwa ni ya Umbwe, very steep, rough and cold. Machame nayo si bora sana, ila ya Marangu ndio the best. Ugumu wake ni kuanzia last water Horombo hut kuelekea Kibo hut. Kuna bonge ya jangwa au the saddle kwa mliosoma Geography. Upepo wa Kisulisuli huvuma hapo na kuharibu mwendo. Muda wa 7hrs by foot to Kibo hut lakini ni zaidi hoi mmmh! Ukifika Kibo hut unarest kujiandaa to Peak. Sijui kama Route zingine hukutana Kibo au Jangwani pale.
the saddle area ni katikati ya milima miwili na sio jangwa! hili jangwa linaitwa alpine deset.
 
Na ukienda Amboni kuna shimo wanakwambia usilisogelee wala kuchungulia, basi wale vijana waongozaji watakwambia hilo shimo limetokezea Ml. Kilimanjaro ikifuatiwa na ubuyu wa mzungu na mbwa...

Yaani acha tu, huko amboni ndio tuliambiwa hivyo.
 
Kule inabidi usikamie sana, mkiwa na mwendo wa taratibu ndio inakua bora zaidi. Vilevile inategemea uzoefu wa guide na njia mliyopita. Hivyo basi, isikukatishe tamaa, unaweza kujaribu siku ingine ukafika kileleni bila tatizo.

Kuhusu gharama kama wengi wanavyouliza, kwa watanzania tatizo sio kiingilio, ni zile za kujikimu, malazi, chakula na malipo kwa wasaidizi (wagumu) na muongoza msafara guide. Hawa inategemea ni wa kampuni au binafsi, hiyo inaacha mwanya wa mazungumzo kwenye bei.

Nafikiri jeez boy kaeleza vizuri sana mchanganuo wa malipo.
Mie sipandi tena, milima sitaki tena bora niende kwenye vivutio vingine tu.
 
asante maney.. kama nilivyo sema ukiwa mwenyewe garama nikubwa. utamlipa guide 18000 kwa siku 6,mpishi 120000,wapagazi 2 kwaijili ya kubeba chakula n.k 90000×2, chakula sh 120000 kila kitu. usafiri kutokea moshi to marangu 60000×2 kiingilio, rescue fee, vat 50000.ila hizi ni tofauti na kwenye makampuni makubwa kwani hua wanagarama za juu sana. pamoja na faida ya kampuni sh 100000.asante makuu
Dah ahsante ila hizi gharama asee ndyo maana wazawa wengi hata hawajisumbui kwenda .....mfano mkuu mkiwa watu wanne bajet ya laki moja elfu kila mtu ambapo jumla kuu laki nne itatosha kweli kukwea huo mlima .....kwa uzoefu wako em nisaidie kdogo
 
17b28ae065b271fcb223c055fdfa438b.jpg
hii ni baada yakutembea kwenye barafu,
76ccbc68d313f497779d353155ded62d.jpg
hapa ndio crater yenyewe
f7a17ca7c3c8beac26e4110a903cb042.jpg
nikiwa nimejilaza kwenye glacier
431cf817aa2cffcceb3a3a6b118ea8f1.jpg
nikitoa huduma ya kwanza kwa jamaa alie anguka na kugonga kichwa. kama unavyoona anapumua kwa kutumia oxgen cylinder
Stunningly amazing... So thats the very peak... !?? Kumbe hapo hapo shimoni panafikika...!!!!
 
Mi navyojua kila panapotokea "kilele" lazima pawe na "shimo"

Wewe mbona ume quote hayo maneno ma2?? unamaanisha kilele cha "MLIMA NA SHIMO la kilimanjaro" kweli?? au kilele kinachopatikana kwenye lile shimo la asili ya uumbaji😉
 
Physics at work; the higher you go the cooler it becomes.:
upo sahii mkuu. tatizo wajuaji wengi bila elimu ya kitu husika ndio maana upotoshaji ni mkubwa sana. kwenye hii 5000+hakuna vitu vinavyoweza kuishi kwa wingi. hapa wanapatikana white neckd raven,( crow) (panya) four strips mouse ,na ndege jamii ya eagle.
 
Sina hakika ndugu ila hiyo ni mojawapo ya Conspiracy theories za Kilele cha mlima Kilimanjaro.
ndege upo! ila sio kwenye kilele cha mlima. ipo umbali wa 4400masl ukitokea mawenzi turn hut. kwenye jangwa kubwa la alpine deset, ni miaka ya karibuni tu ilianguka, na ilikua na wageni kutokea Italy kupitia kenya. mabaki yapo na yanaonekana kwa waliopita hii njia watakua wanaelewa naongelea eneo gani,kwa ipo nijani kabisa.
 
the saddle area ni katikati ya milima miwili na sio jangwa! hili jangwa linaitwa alpine deset.
Asante kwa Elimu ndiyo raha ya Jf! Ila neno alpine desert sijawahi kutana nalo. Jangwa la pale mbona kubwa sana linaextend hadi wapi? Wa Route nyingine ukitoa Marangu wanalipita?
 
ndege upo! ila sio kwenye kilele cha mlima. ipo umbali wa 4400masl ukitokea mawenzi turn hut. kwenye jangwa kubwa la alpine deset, ni miaka ya karibuni tu ilianguka, na ilikua na wageni kutokea Italy kupitia kenya. mabaki yapo na yanaonekana kwa waliopita hii njia watakua wanaelewa naongelea eneo gani,kwa ipo nijani kabisa.
Mkuu naomba ukate huu ubishi... Hapo kwenye crater panafikika au hapafikiki...!?
 
ndege upo! ila sio kwenye kilele cha mlima. ipo umbali wa 4400masl ukitokea mawenzi turn hut. kwenye jangwa kubwa la alpine deset, ni miaka ya karibuni tu ilianguka, na ilikua na wageni kutokea Italy kupitia kenya. mabaki yapo na yanaonekana kwa waliopita hii njia watakua wanaelewa naongelea eneo gani,kwa ipo nijani kabisa.
Hiyo ndege ya hiyo theory ni ya zamani sana eti kusema ilikuwa na Wazungu.
 
Mkuu naomba ukate huu ubishi... Hapo kwenye crater panafikika au hapafikiki...!?
Panafikika ukiwa kileleni unapaona. Kilele ni kando kando ya hiyo crater. Uzoefu wangu wa miaka hiyo niliona kwa macho yangu. Tukaambiwa tukae mbali tusisogee sana kuna Hewa chafu na uvutano.
 
Back
Top Bottom