Hivi ni kweli kileleni mwa mlima Kilimanjaro kuna shimo?

Hivi ni kweli kileleni mwa mlima Kilimanjaro kuna shimo?

nashukuru kwa wote mliojaribu kujibu na kuelezea kwa uelewa wenu. anyway, hi hivi! kupitia machame mpaka top ya mlima ni 42kms, kupitia marangu ni 38kms. mlima Kilimanjaro una 5 zones, (1) cultivate,0-1000masl,(2) montana Forest Park1000-3000masl (3) moorland 3000-4000masl(4) alpine reset 4000-5000masl (5) ice cap au summit,5000-nakuendelea. kwa wale waliopanda watakua wananielewa, base ya mlima Kilimanjaro ipo kwenye 4600-4700-4800 masl. hii inakua ni camp ya mwisho kabla ya ku summit,kutoka kwenye base camp mpaka highest point kwa wanaopitia south na western side ya mlima ni 5kms umbali. mwendo wa pole pole ni 6-7hrs walking. baridi ni kali kutegemeana na majira ila normal ipo 3-7minis.juu ya mlima kabisa kuna mabarafu makubwa yanaitwa glacier, ukweli shimo lipo ila ni mbali sana kutokea highest point. kwa kutembea kwa mtu mwenye nguvu haswa wapanda milima anaweza tumia saa 1-1:30 kufika. hili shimo linajulikana kama ash pit, au ash cone. kuingia unaweza ila sio mbali sana maana limechongeka kwa kama rim. na halina kina kikubwa ukiangalia kwa nje. nimewahi kuingia kama mita 5 .ila kuna wakati linatoa harufu kali sana ya sulphur ambayo hupelekea baadhi ya watu huumwa vichwa, kutapika,tumbo kuvurugika n. k.unaweza kuniuliza chochote kuhusu mlima Kilimanjaro na nitakujibu. kwani mimeutembea wote na nimeweza kufika highest point zaidi ya 100 times. pia mlima meru, oldonyo lengai n. k asanteni sana
Asante sana Mkuu...tujuze kuhusu gharama zake
 
Duh!!!kutokaana na kani ya mvutano na imagine kama Ikipita ndege tu inavutana kama mvutano unaotokea pale rufiji yanapokutana maji chumvi na maji yasiyo na chumvi,au Kama ukanda wa nungwi. Kuna mtu ashawahi ingia huko kwenye hiyo crater kweli jamani??
mm ndie niliefika na sio mm pekee bali wapo watu wengi sana. tatizo mnakua mnaishi kwa hisia na sio uhalisia ndio maana mnabisha kila kitu. kama una nafasi naomba uje moshi tarehe 09/7/2017nina safari tarehe 10/07/2017 ya siku tano. yakupanda na nitakupeleka for free, ukajionee kwa macho na urudi ukawaadithie ukweli wa hilo. utakakacho lipia ni kiingilio tu ili mwisho wa safari upate cheti chako.nitakupa vifaa vyote bure kabisa. kuanzia sleeping bag,sleeping mat, hiking boots, warm clothes, day parking,yani vyote kabisa bure bure. nitakupa mawasiliano yangu kama unataka.
 
kuhusu mvutano wa ndege na hilo shimo hauna ukweli sana, tunachojua au kwa kitaalamu ni kua kwenye milima hakutabiriki sana! na kunakua na ukungu sana, pia ndege zina njia zake hizi nisababu ya kutopita ktkat ya hilo shimo. ila kwa watu walio wahi kutumia ndege za klm watakua mashahidi kua moja ya kivutio kikubwa kwa hizi ndege haswa Nairobi, Kilimanjaro na dsm hua wanapita karibu sana ili abiria waweze kuuona.
 
mm ndie niliefika na sio mm pekee bali wapo watu wengi sana. tatizo mnakua mnaishi kwa hisia na sio uhalisia ndio maana mnabisha kila kitu. kama una nafasi naomba uje moshi tarehe 09/7/2017nina safari tarehe 10/07/2017 ya siku tano. yakupanda na nitakupeleka for free, ukajionee kwa macho na urudi ukawaadithie ukweli wa hilo. utakakacho lipia ni kiingilio tu ili mwisho wa safari upate cheti chako.nitakupa vifaa vyote bure kabisa. kuanzia sleeping bag,sleeping mat, hiking boots, warm clothes, day parking,yani vyote kabisa bure bure. nitakupa mawasiliano yangu kama unataka. ili ukirudi ufute hilo tusi (((genye)) sio kila kitu niuzushi ndugu yangu.
Tusi liko wapi Hapo nilipo andika mie??we li highlight tu,nijue nimetukana. Umeanza vizuri umemaliza vibaya...
 
Tusi liko wapi Hapo nilipo andika mie??we li highlight tu,nijue nimetukana. Umeanza vizuri umemaliza vibaya...
maserati. huo mlima ni wakawaida sana kama upo vizuri kiafya. nitakuwekea hapa picha mbali mbali kwani ninazo zaidi ya pich 3000 nilizopiga kwa mda wa miaka 6
 
maserati. huo mlima ni wakawaida sana kama upo vizuri kiafya. nitakuwekea hapa picha mbali mbali kwani ninazo zaidi ya pich 3000 nilizopiga kwa mda wa miaka 6
Mie siwezagi kumtusi mtu mkuu,ukinambia tusi naogopa sana.. Habari za matusi wakati mtu hajakukosea kitu huwa sipendagi.
By the way I will check mya schedule Ili kama nitapata wasaa basi nitadondoka moshi Hapo.
 
Tusi liko wapi Hapo nilipo andika mie??we li highlight tu,nijue nimetukana. Umeanza vizuri umemaliza vibaya...
17b28ae065b271fcb223c055fdfa438b.jpg
hii ni baada yakutembea kwenye barafu,
76ccbc68d313f497779d353155ded62d.jpg
hapa ndio crater yenyewe
f7a17ca7c3c8beac26e4110a903cb042.jpg
nikiwa nimejilaza kwenye glacier
431cf817aa2cffcceb3a3a6b118ea8f1.jpg
nikitoa huduma ya kwanza kwa jamaa alie anguka na kugonga kichwa. kama unavyoona anapumua kwa kutumia oxgen cylinder
 
Mie siwezagi kumtusi mtu mkuu,ukinambia tusi naogopa sana.. Habari za matusi wakati mtu hajakukosea kitu huwa sipendagi.
By the way I will check mya schedule Ili kama nitapata wasaa basi nitadondoka moshi Hapo.
karibu sana mkuu na jisikie huru ndugu yangu. hili ni kweli kabisa. utakwenda free
 
Umenikumbusha hiyo story eti mzungu alipotea na mbwa wake kwenye mapango ya amboni mbwa akaonekana mlm kilimanjaro!!!

Na ukienda Amboni kuna shimo wanakwambia usilisogelee wala kuchungulia, basi wale vijana waongozaji watakwambia hilo shimo limetokezea Ml. Kilimanjaro ikifuatiwa na ubuyu wa mzungu na mbwa...
 
kuhusu mvutano wa ndege na hilo shimo hauna ukweli sana, tunachojua au kwa kitaalamu ni kua kwenye milima hakutabiriki sana! na kunakua na ukungu sana, pia ndege zina njia zake hizi nisababu ya kutopita ktkat ya hilo shimo. ila kwa watu walio wahi kutumia ndege za klm watakua mashahidi kua moja ya kivutio kikubwa kwa hizi ndege haswa Nairobi, Kilimanjaro na dsm hua wanapita karibu sana ili abiria waweze kuuona.

Tena rubani au mhudumu wa ndege anawatangazia kabisa kwamba sasa mnapita Ml. Kilimanjaro na watu wa upande wa huo mlima wanaweza kuchungulia wauone, kama mawingu hayajauzonga sana.
 
Niliwahi kujaribu nikaishia njiani(mandara) kupitia marangu na kiranga chote kikaisha. Yaani sina hamu na sirudii kwakweli.

Kule inabidi usikamie sana, mkiwa na mwendo wa taratibu ndio inakua bora zaidi. Vilevile inategemea uzoefu wa guide na njia mliyopita. Hivyo basi, isikukatishe tamaa, unaweza kujaribu siku ingine ukafika kileleni bila tatizo.

Kuhusu gharama kama wengi wanavyouliza, kwa watanzania tatizo sio kiingilio, ni zile za kujikimu, malazi, chakula na malipo kwa wasaidizi (wagumu) na muongoza msafara guide. Hawa inategemea ni wa kampuni au binafsi, hiyo inaacha mwanya wa mazungumzo kwenye bei.

Nafikiri jeez boy kaeleza vizuri sana mchanganuo wa malipo.
 
Tulipita Machame, kufika Stela Point nilikua hoi siwezi hata kusogeza mguu. Mbaya zaidi ukishafika pale unapaona kabisa Uhuru Peak, tambarare hakuna mlima mkali sana, lakini ile hali yahewa kule juu inakufanya usiwe comfortable kabisa.
Nikawaza, sasa nikiishia hapa ntaenda kusema kwanini sijafika kileleni? Nikajipa moyo taratibu huku mgumu ananishikilia ila kila dakika tano nakaa nafimiri ile hali niliyokuwa najisikia ni mfano wa mjamzito....

Nilifika pale kileleni wanapiga ila hoi vibaya mno, mandhari ya kule juu inafuta uchovu wote na kukuliwaza baada ya kazi ngumu.

Pole sana kwa sababu ulipoishia ni karibu sana na mwisho wa safari. Siku ukienda, jitahidi kula vizuri ule usiku wa mwisho, ile safari ukiwa na njaa au umechoka hautoboi. Ni siku pekee mnatembea masaa mengi, usiku na mlima mkali sana. Mnaanza saa tano usiku hadi kufika kileleni asubuhi kutegemea na mwendo wenu. Tulifika saa tatu asubuhi.

Kila la kheri mkuu
Marangu Route hakuna steep hivyo kwenda kileleni ni zigzag mnatembea taratibu. Tulianza SAA 6 usiku tukafika 111 alfajiri hoi bin taabani. Ni kweli usipojikazi peak utaiona karibu ila hufiki!! Tulikunywa chai tuu pale Kibo ili tusitaapike njiani tukakosa nguvu. Hansmeyer Cave, Gilmans Point nazo ni sehemu ya Kilele ila wengi huishia hapo! Safari ya kupanda Mlima isikie tu it's hard and tough!!
 
kajitose mkuu nina imani utaandika historia na kuiacha pia ili watoto wakizazi kijacho wasome na kjua kuwa kuna mtanzania wakwanza kuingia humo na bado yupo kufanya utafiti kuwa kuna nibi huko ndani
Maiti yako haitakaa ioze labda ikutane tena na moto wa Volcano; kileleni ni barafu/theluji
 
Cha kushangaza kila unavyozidi kushuka ndo Hali inavyozidi kuwa nzuri... Yaani nilifika pale kibo mzima wa afya, nikatamani nirudi lakini haiwezekan. Kuna kitu kinaitwa height fever Kama sikosei,... Ndo inampata mpanda mlima yeyote.

Ndio maana nasisitiza kula vizuri siku ya mwisho, kwa uzoefu wangu, ni siku ngumu sana. Licha ya kutembea usiku na kufika kileleni asubuhi, ukisharudi pale barafu kituo cha mwisho, mnakula na ni lazima mshuke msilale usawa wa juu baada ya kufika kule juu, mnatakiwa mje kulala chini kabisa kupunguza watu kujisikia vibaya na hiyo height fever (wana jina la kitaalam). Inamaana hapo tena kuna kutembea sana mchana hadi kuja kulala kwenye geti la kutokea.


Ila furaha yake unapopewa cheti ni kubwa mno, unasahau maswahibu yote.

Katika ile safari, ukipita njia ya Machame, mnatumia siku tano kupanda tu, ni miongoni mwa njia ngumu kidogo kulinganisha na Marangu. Kuna sehem inaitwa Lava Tower, hapo kuna hali mbaya sana wengi wanatapika na kuumwa wakifika pale. Ni siku ya kwanza nilijisikia mwili unatakiwa upunguze uchafu mwilini..hahahaaaa

Kwa ufupi safari inachangamoto lakini ni uzoefu mzuri sana hasa mkiwa kikundi.
 
Back
Top Bottom