Hivi ni Mabunge yote duniani Mbunge akisimama badala ya kutumia muda wake vizuri ni lazima aanze kumsifia Rais?

Shida imeanzia kwenye katiba yetu. Kitendo cha kumfanya raisi ni Mungu mtu (kwa mamlaka aliyopewa na katiba iliyopo) ndio mambo kama haya ya uchawa na ujinga mwingine umetamalaki.
Watz adui yetu mkubwa ni katiba mbovu tuanzie hapo.
Hakika
 
Ni bunge la ovyo tu ndio wabunge wake wako hivyo.dunia nzima hakuna bunge la hivyo.
 
  1. Watu wa hivyo akili zao ni finyu
  2. Watu wa hivyo ni chawa
  3. Watu wa hivyo hudhani Rais ndiye aliyewapa ubunge
  4. Watu wa hivyo ni wale wasiokwenda kusikiliza kero za wananchi ila huwasilisha mambo yao binafsi
  5. Watu wa hivyo majimbo yao ni tete
 
Leo Ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuangalia Bunge Live ingawa sijawahi kuwa interested na bunge la Tanzania. Nimeshangaa kuna wabunge wamepewa dakika kumi yaani dakika saba ni kusifu Rais na Serikali nilishangaa sana nikajiuliza swali hilo hilo
 
Sijawahi kuona bunge la kifala kama hili!
 
Wewe mwongoooooo Kwa hilo, wa Tanzania ndiyo wako hivyo tangu zama zileeeee. Kwani zidumu fikra za mwenyekiti zilianza lini?
Na yule mzee aliyebadiri jina kutoka John na kuwa Jumanne si ilikuwa kumaifu Rais?
 
Kila nikiwatazama hawa wabunge wakiwa wamesimama, nabaki tu nikitikisa kichwa na kujiuliza hivi Watanzania tumefikafikaje hapa! Ghafla naukumbuka mkataba wa DP!
Mimi huwa naona kama hawana hata familia. Wangekuwa na aibu basi hata mbele ya familia zao kwa aibu na upupu wanaotuletea Bungeni
 
Sijawahi kuona bunge la kifala kama hili!
Huu ni uthibitisho tosha kwamba mwaka 2020 hatukuwa na uchaguzi. Hakuna namna hawa FDD wangeweza kutia miguu bungeni kama wawakilishi wa wananchi.

Ushahidi mwingine ni jinsi bila busara walivyoshawishika kirahisi kubariki uuzwaji wa ardhi yetu kwa Waarabu. Gosh, even Tanzanians are better than that!
Mimi huwa naona kama hawana hata familia. Wangekuwa na aibu basi hata mbele ya familia zao kwa aibu na upupu wanaotuletea Bungeni
Fikiria familia yako inakuangalia unavyojidhalilisha bungeni halafu unarudi nyumbani na kuwasifia kwa mbwembwe wanao ulivyowauza Watanzania!
 
Rais ni mwenyekiti wa chama, pia huongoza kamati kuu itakayopitisha majina ya wagombea,

Kungekuwa na wagombea binafsi huu upuuzi usingeusikia, mijitu mizima kuwa wanafiki na machawa haifai,



Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
Ni Tanzania tu.
 
Wewe mwongoooooo Kwa hilo, wa Tanzania ndiyo wako hivyo tangu zama zileeeee. Kwani zidumu fikra za mwenyekiti zilianza lini?
Na yule mzee aliyebadiri jina kutoka John na kuwa Jumanne si ilikuwa kumaifu Rais?
Ulikuwa na umri gani wakati Mzindakaya anashusha makombora bungeni?
 
Kusifu, kukosoa ni haki ya mzungumzaji, we kinakuuma nini? Kafanye mambo yako, km unaona vipi kagombee ubunge halafu utaamua km ni kutukana, kukashifu, kulia ni juu yako waache wenzio wana uhuru wa kumsifu rais wao na watakuwa na sababu kwanini wanamsifia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…