Hivi ni sawa hili la kuhubiri ndani ya mabasi ya umma?

Na yale mabasi yanayoweka movie za bongo Zina maudhui sio mazuri na miziki ya ajabu ajabu wengine tunasafiri na watoto inakua shida ni vema wangekua wanaweka documentary Kama za nyerere Labda wanyama wa porini
 
Sahihi kabisa,movies zenyewe za hovyo tu.
Na yale mabasi yanayoweka movie za bongo Zina maudhui sio mazuri na miziki ya ajabu ajabu wengine tunasafiri na watoto inakua shida ni vema wangekua wanaweka documentary Kama za nyerere Labda wanyama wa porini
 
Yaani wewe na akili zako zote hizo umeshindwa kweli kumkamata huyo mtu na kumpa kichapo? Hiyo ni laana na hairuhusiwi mtu uingie ndani ya dala dala na akili zako timamu kwenda kushawishi watu washupalie dini za watu (Ukristu na Uislam).
 
Tatizo asilimia kubwa ya hao wahubiru ni wasanii tu. Hata hawahubiri toka moyoni. Wako kwa ajili ya sadaka yako.
 
Kanisani hamuendi ngoja mfatwe huko huko kwenye shughuli zenu
Sasa kwani mtu analazimishwa kuabudu dini za watu? Mtu hataki kwenda kanisani kwa sababu haoni umuhimu wake, utaabudu vipi dini wakati kila mtume ni Myahudi na mzungu, tuache kujipa ujinga bila sababu.
 
Ndio maana yakajengwa makanisa.ina maana huko akuwatoshi.isitoshe kwenye gari kila mtu ana imani yake.inakua sio ustaharabu mzur.
Hawa watu inabidi wakamatwe na kunyongwa tu, utalazimisha vipi watu wakaabudu dini zisizo zao?
 
Ni Sawa
Enendeni Duniani Mkawahubirie Wanadamu Habari Njema.

Mkuu Umepata Neema Kuisikia Hiyo Habari Njema.
Mgeukie Muumba Wako.
 
Sasa kwani mtu analazimishwa kuabudu dini za watu? Mtu hataki kwenda kanisani kwa sababu haoni umuhimu wake, utaabudu vipi dini wakati kila mtume ni Myahudi na mzungu, tuache kujipa ujinga bila sababu.
Nimeandika kama jokes tu. Siamini dini yoyote mimi
 
Binafsi nakereka balaa, wengine sisi safari ni moja ya starehe, kwa nini mtu aje anibughudhi nikiwa katikati ya starehe, halafu anakutisha kisa tu uko safarini na ajali ni nje nje eti utoe sadaka ili damu ya Yesu ikulinde.

Kila kitu na mazingira yake bwana!!
 
 
Ndio maana yakajengwa makanisa.ina maana huko akuwatoshi.isitoshe kwenye gari kila mtu ana imani yake.inakua sio ustaharabu mzur.
Kanisani huwaga hamji. Hata tunapoweka mikutano ya hadhara huwa hamji, Tumeamua kuwafuata huko huko.

"Basi imani, chanzo chake ni kusikia; Na kusikia huja kwa Neno la Kristo." WARUMI 10:17. Injili ya ufalme lazima ihubiriwe kote kwa wote ili iwe ushuhuda kwa mataifa yote MATAYO 24:14, tukiwa tunaelekea mwisho wa nyakati.


hakika Yesu ni Kristo.
 
Wanaofanya ivyo wanajichosha tu,[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]vitu vingine vya ovyo.Yan mm nimejichokea zangu na safar we unakuja na mahubiri yako ni kunipigia kelele tu.
Halafu mtu mwenye utimamu wa akili awezi fanya huo ujinga,wizi mtupu
 


[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…