Hivi ni Taasisi yetu tu au Taasisi zote za Umma pesa imekua ngumu kwa Wafanyakazi?

Hivi ni Taasisi yetu tu au Taasisi zote za Umma pesa imekua ngumu kwa Wafanyakazi?

Haya maisha haya...au basi tu. Kuna kipindi nilipata upenyo wa kupata pesa kirahisi mno, ilikua ni maamuzi yangu tu kwamba nitengeneze kiasi gani kwa siku (Ilikua naweza kupata hadi 500k) ila nafsi ilikua inanisuta, ikabidi tu niwaambie wahusika kwamba kuna kitu hakipo sawa mahali. Ni kweli nilizikosa zile pesa lakini nna amani na furaha hadi kesho. Vinginevyo mngeshangaa tu The Monk amepotea jukwaani.

Ni vizuri sana kuwa na ndoto, jitihada, bidii, maarifa na kila aina ya ubunifu kwenye kutafuta pesa, ila hakikisha afya yako, furaha yako, amani yako na uhuru wako hauathiriki kwa namna yeyote ile, hapo sijaongelea heshima yako.
Kama zilikuwa za selikali, hadi Mungu atakushangaa
 
Wakuu, especially waajiriwa wa serikali.

Hivi Na nyie ofisini kwenu pakavu kama kwetu au ofisi yetu ndio imekua mfano? Maana kusema kweli 2023 na 2024 hii miaka imekua migumu sana.

Posho hazitoki yapo madeni tu tokea ya September 2023, safari imekua kitu hadimu, vikao vya hela hamna wala kazi za masaa za ziada hazilipwi.

Okay, sasa sijui pesa ipo wengine tunabaniwa tuliopo chini au Taasisi zote sahivi zimebaniwa hela?

Nimechoka kushinda kwenye uzi wa Mshahara wa Januari vipi mbona unachelewa?

Mliojiajiri karibuni kunitukana!
Ze situeshen is taff.
 
Kama zilikuwa za selikali, hadi Mungu atakushangaa
Hazikua za serikali Wala za mtu binafsi. Mbaya zaidi, nilioenda kuwapa taariza za hiyo hitilafu wakataka kuniletea usumbufu wazuie pesa zangu. Nikawaambia ikifika saa nane kamili akaunti yangu bado inashida, tutakutana BoT. Wakati huo ilikua saa Saba na nusu.

Jamaa akanipa business card akasema, siku yoyote ukipata usumbufu wowote popote kwenye ofisi zetu, nipigie. Huyo alikua director wa Operations.

Lile lilikua jaribu baya sana. Unajua hadi Sasa hivi ningekua Bado napata pesa nnazoamua Mimi. Kama unavyojua pesa ya Bure/ rahisi tamu na ikikunogea, kuacha sio rahisi. Nikaona mambo yasiwe mengi...ningekuja kuambiwa nimehujumu uchumi Kwa maelfu ya USD.

Of course Kuna jamaa alinitukana sana na tuligombana nae akidai Kwa vile sikua naiba Wala kufanya udanganyifu wowote, nilitakiwa niendelee kupata Neema. Akanilaumu sana, akasema kama ni yeye, umasikini angepeana nao talaka.
 
Wakuu, especially waajiriwa wa serikali.

Hivi Na nyie ofisini kwenu pakavu kama kwetu au ofisi yetu ndio imekua mfano? Maana kusema kweli 2023 na 2024 hii miaka imekua migumu sana.

Posho hazitoki yapo madeni tu tokea ya September 2023, safari imekua kitu hadimu, vikao vya hela hamna wala kazi za masaa za ziada hazilipwi.

Okay, sasa sijui pesa ipo wengine tunabaniwa tuliopo chini au Taasisi zote sahivi zimebaniwa hela?

Nimechoka kushinda kwenye uzi wa Mshahara wa Januari vipi mbona unachelewa?

Mliojiajiri karibuni kunitukana!
Hata pesa ya wizi ni ngumu kuipata. Sasa wewe unataka pesa inayopatikana kirahisi utaipata dunia gani.
 
Wakuu, especially waajiriwa wa serikali.

Hivi Na nyie ofisini kwenu pakavu kama kwetu au ofisi yetu ndio imekua mfano? Maana kusema kweli 2023 na 2024 hii miaka imekua migumu sana.

Posho hazitoki yapo madeni tu tokea ya September 2023, safari imekua kitu hadimu, vikao vya hela hamna wala kazi za masaa za ziada hazilipwi.

Okay, sasa sijui pesa ipo wengine tunabaniwa tuliopo chini au Taasisi zote sahivi zimebaniwa hela?

Nimechoka kushinda kwenye uzi wa Mshahara wa Januari vipi mbona unachelewa?

Mliojiajiri karibuni kunitukana!
Hata pesa ya wizi ni ngumu kuipata. Sasa wewe unataka pesa inayopatikana kirahisi utaipata dunia gani.
 
Unataka safari uende wapi na kufanya nini huko utakapo kwenda? Kwanini usibaki hapo hapo upige kazi kwa nguvu uonekane alafu tukupe promotion hence mshahara wako utaimarika mwisho wa siku utaepuka kuingia uzi wa kuulizia salary

Unataka vikao vyenye fedha ili iweje, kwani ofisi yenu haina "annual work plan" mpaka uanze kuulizia vikao vya fedha ambavyo kimsingi huwa mnajadili mambo yale Yale mnayopaswa kufanya na mbaya zaidi huwa mnafanya vikao kwenye maeneo yenu ya kazi wala hakuna gharama yoyote uliyotumia kufika kwenye kikao ila mnalipana

Unataka ela ya masaa ya ziada ili iweje kwani lazima kufanya kazi muda wa ziada....kwani kwenye masaa ya kawaida umefanya nini exceptional mpaka ionekane unataka kulipwa kwa kufanya kazi masaa ya ziada. Jifunzeni ku-balance kazi na other social issues na ikifika muda wa mwisho wa kazi funga ofisi kajichanganye mtaani. (Ukihitajika utaitwa)

"Mliojiajiri karibuni kunitukana" ...maoni yangu yame-base hapo mstari wa mwisho hivyo yaheshimiwe kama yataonekana nimemtukana mtu maana sie wananchi tuliojiajiri aka wakulima wa jembe la mkono tunalia sana kwa kukosa hata rambo dogo tu la kufanya umwagiliaji alafu nyie mlipane posho tu.

Fanyeni kazi haki yenu ni mshahara sio posho kwani posho zinaweza kufutwa ila mshahara hauwezi kufutwa na endapo unaenda sehemu pambana ku-negotiate mshahara mzuri unaotaka na hata usishawishiwe ushuke kidogo kisa unaambiwa hiyo kazi ina safari sana

Nimemaliza ngoja nilie kwanza kumbe huwa mnalipana posho tu
 
Back
Top Bottom