Hivi Rais Samia angeamua kuanzisha uchunguzi wa tukio la Lissu kupigwa risasi, sukuma gang wangekuwa na hali gani? Shukurani kamsitiri

Magufuli hatutamsahau Kwa KAZI nzuri aliyolifanyia Taifa hili majizi TU ndo yanashangilia kuondoka kwake Duniani ila ni suala la muda TU kila mtu atakiri yule Mwanaume alikuwa analipenda taifa Hili Kwa dhati kabisa
 
Bahati mbaya CDF ni msukuma pia, sijui unasemaje napo!
 
Inawezekana kawaletea wahusika kwa kutumia kesi ya Mbowe 🐱
 
Kama CDF anamteua Rais kweli hapo kuna mziki ila kama Rais ndio anamteua Cdf mbona kazi ndogo tu kama kumsukuma mlevi.
Usiyoyajua ni ngumu kuyaelezea, CDF hana ubaya na Amirijeshi mkuu.
 
Kuongoza nchi ni kaz nzito sana tofaut na watu wanavyofikiri
 
Unaongeaga ujinga sana ww...
jikiteni kwenye siasa za sera acheni siasa za matukio!!
kamwe hamfiki mbali
 
Angeanzisha tu angejulikana ni nani aliyempiga risasi.. Kabula ya uchunguzi kwanza atafute what was the motive. Munasema HayatI Magufuli kampiga risasi what for? Mutu alishindwa uchaguzi, ampige risasi afaidike nini? Mtu alikuwa busy kuiweka sawa Tanzania. Amepokea nchi iliyokuwa imetafunwa na kuwachwa mifupa mitupu. Nchi isiyokuwa na nidhamu. Nchi iliyokuwa inanuka rushwa. Samia achunguze kwani yeye alikuwa wapi? Si alikuwa makamu wa Rais? Tundu Lissu asiangalie mbali, aangalie ndani ya chama chake, kuna ushindani wa madaraka, asishuku watu bure pengine aliyempiga risasi wanakula naye sahani moja. Samia ashukuru, kapokea nchi yenye misingi mizuri, yenye mapato makubwa kwa Hayati Kagufuli kuyapigania Madini yetu huku akizomewa na Tundu Lissu kuwa tutashitakiwa. Mutasema, mutamubeza, legacy yake hamutaifuta. Tulikuwepo wakati anaipokea nchi. Hali ilikuwa mbaya. Dhuluma Kwa wanyonge kila kona. Tanzania imepoteza kiongozi bora. HAMUWEZI KUWADANGANYA WATANZANIA TOFAUTI WANAONA.
 
Hii nchi siyo ya mama. Hii nchi ni ya Watanzania wote. Munazungumuza utumbo mtupu. Bila Hayati Magufuli Hii nchi ilikuwa imekwisha. Kwa sasa mama kakubali mali zetu kusobwa kwa mikataba mibovu. Wizi unarudi, uhalifu kila kona. Munaomusifu ni wapigaji, ni wakati wenu wa kula. Endeleeni, siku moja mutavitapika
 
well said
 
Matukio mangapi yalitokea ya kupigwa risasi wananchi kabla ya Magu? Kauli yako ni kitisho kwa sukumaGANG kwamba waogope kuzungumza?

Magu angeanzisha uchunguzi wa tukio la kuwekewa sumu yeye binafsi wangepona hao ndugu zako?
 
Tatizo ni kujipa majibu ya kwamba aliyemshambulia Lissu ni Magufuli tu na hakuna namna nyengine sasa nawaza hata ukifanyika huo uchunguzi na kuja na majibu ya tofauti utakubalika kweli?
 
Familia nyingi zingebakia yatima kwa sukuma gang wengi kwenda gerezani. Samia kaamua kupotezea
 
atizo ni kujipa majibu ya kwamba aliyemshambulia Lissu ni Magufuli tu na hakuna namna nyengine sasa nawaza hata ukifanyika huo uchunguzi na kuja na majibu ya tofauti utakubalika kweli?
Kumbe unajua ni yeye!
 
Salary Slip said:
Hivi Rais Samia angeamua kuanzisha uchunguzi wa tukio la Lissu kupigwa risasi, sukuma gang wangekuwa na hali gani? Shukrani kamsitiri

Mimi sikuwahi kumkubali mwendazake hata siku moja na namshukuru sana Mungu kutuondolea ibilisi moja muovu. Kutokana na kifo chake, wengi wetu tulipona.

Hata hivyo nadhani katika swali lako umekosea. Ungeuliza hivi...hivi Rais Samia angeamua kuanzisha uchunguzi wa tukio la Lissu kupigwa risasi, yeye Rais Samia angekuwa na hali gani?

Naomba usisahau wakati huo alikuwa ni makamu wa mwendazake!
 
Tatizo ni kujipa majibu ya kwamba aliyemshambulia Lissu ni Magufuli tu na hakuna namna nyengine sasa nawaza hata ukifanyika huo uchunguzi na kuja na majibu ya tofauti utakubalika kweli?
Ushahidi ukaja kuwa aliyemshambulia ni mbowe ama alijishambulia mwenyew ili kuteka attention vip mtajisikiaje??[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Kigogo2014 alifanikiwa kuwajaza chuki na propaganda za kitoto sana[emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…