Hivi siku hizi hakuna majambazi?

Hivi siku hizi hakuna majambazi?

Nchi za kiafrica na tawala zake ,hata majambazi na wachawi kuna muda wanatuonea huruma
Ni kweli aisee. Matatizo ni mengi sana. Sisi mtaani kwetu tuliliwa na shida ya barabara, happ panaposumbua kuna wajomba kama watatu hivi waliwahi kusimama na mashine mida ya saa mbili ya saa tatu usiku mimi nilipishana nao kama dkk 10. Waliteka magari ya watu wanatoka kazini, na kupelekea moto balaa. Baada ya tukio damu ilikuwa imetapakaa hapo chini japo hakuua zaidi ya kutoa meno na kuvunja viungo vya wabishi wachache waliokataa kutii amri..

Hilo tukio lilisamababishaga hofu kwa kila mkazi. Magu ndio alikuwa anakalia usukani bado hajachanganyia vizuri, sasa hivi ushwari wa kutosha ila vibqka tu wachovu wanashambulia kwa kushtukiza ukikaa kizembe.
 
Majambazi wabishi walikuwa mkoa wa Kagera
Ukipita pori la Kimisi au Kasindaga bila kukipata shukru Mungu
Kuna wale tukiwa watoto walileta barua Kwa jirani yetu kuwa wakija wakute elfu 90
Tunashukru jeshi la polisi pamoja na madhaifu Yao ila hili wameliondosha
Kule niliwahi kupanda bus nyuma kuna Polisi wanaescort wako na mashine zao. Nikashngaa nini tena hii? Jamaa wakasema bila hivyo kutokq tunzewe hqdi nyakanazi tu hutoboi. Ila siku hizi tunakatiza tu bila mabunduki.
 
Uchumi umeimarika , maadili na michongo imekuwa mingi,
Jeshi la polisi liko imara sana, mpaka wao Sasa ndio wamekuwa watekaji na wauwaji wa raia.

Ukuwaji wa technology imesaidia sana ujambazi kupungua.

Nakumbuka tukio la kkkt kimara, zilikuja defenders 3, zikiwa na njemba kama 6 ivi, wakawafungia waumini ndani ya kanisa hakuna kutoka MTU, wakaingia jengo la muasibu , wakatoa pipe wakapewa sadaka za makusanyo ya juma2 hio, ZaidI ya mil35 .
Walitokomea kusikojuliiana huku defender MOJA ikibaki kuhakikisha wale walio tangulia hawafuatiliwi, nao baadae wakatokomea kwa mwendo wa ngiri. 2012

Walikuja na difenda?
ndio hao hao, siku hizi wanaitwa watu wasiojulikana kazi yao kuteka au kuua

nakumbuka tukio moja hv, pale ubungo waliiba benk wakatokomea tena hapohapo ubungo kukawa na cruza inasafirisha pesa zikapigwa sana risasi, trafik mmoja akawa shujaa kupambana nao, ktk majeruhi wengine wakakutwa lugalo wakitibiwa
 
Kwa kawaida majambazi huwa ni watu wenye ufanisi mdogo katika kazi mbalimbali ambazo ni halali lakini siku hizi wanapata pesa kirahisi kwa mfano baadhi ya watu wanapewa pesa kisa wanawasifia wenye pesa (wamekuwa machawa). Angalia mtu kama Mwijaku, Baba levo bila kumsahau Maulidi Kitenge.
Fauka ya hayo, kuna watu wamekuwa tena wanaume wazima wamekuwa mashuhuri kwa kuuza nyuma (mtu mmoja humu ndani hupenda kuita kinye###), nasikia kwa Tanzania yetu Mr pdidy ameshatembea na watu kadhaa na kuwawezesha kiuchumi, labda Mr pdidy asingekuwepo hawa jamaa wangukuwa majambazi.
Hivyo basi tunapokemea uchawa na matendo ya watu kugawa nyuma kama njugu tujitafakari ili tujue iwapo yanahasara tu au pia yanafaida.

ONA JEMA KWENYE KWENYE BAYA!!
 
Kwa kawaida majambazi huwa ni watu wenye ufanisi mdogo katika kazi mbalimbali ambazo ni halali lakini siku hizi wanapata pesa kirahisi kwa mfano baadhi ya watu wanapewa pesa kisa wanawasifia wenye pesa (wamekuwa machawa). Angalia mtu kama Mwijaku, Baba levo bila kumsahau Maulidi Kitenge.
Fauka ya hayo, kuna watu wamekuwa tena wanaume wazima wamekuwa mashuhuri kwa kuuza nyuma (mtu mmoja humu ndani hupenda kuita kinye###), nasikia kwa Tanzania yetu Mr pdidy ameshatembea na watu kadhaa na kuwawezesha kiuchumi, labda Mr pdidy asingekuwepo hawa jamaa wangukuwa majambazi.
Hivyo basi tunapokemea uchawa na matendo ya watu kugawa nyuma kama njugu tujitafakari ili tujue iwapo yanahasara tu au pia yanafaida.

ONA JEMA KWENYE KWENYE BAYA!!
Unamaanisha uchawa umechangia kupunguza ujambaka 😆😆😆
 
Majambazi walikua wanashikwa na silaha ila mahakama zikawa zinawaachia kwa errors ndogo ndogo za ushahidi, ikafika hatua ukikamatwa na silaha unataja wenzako mnapelekwa nje ya mji alafu taarifa zinarudi wamekufa katika majibizano ya risasi
 
Kabla ya awamu iliyokatishia njiani na hii ya sasa ilikuwa haipiti wiki unasikia watu wamevamiwa, majambazi yameuwawa ila siku hzi hizo habari hazipo kwa kasi ile.

Cha ajabu sikuhizi vimeibuka vituo vingi (benk ndogo) mitaani vinavyofanya kazi kwa miamala ya simu na Benki. Zamani ikifika saa 12 vituo hivi kama sio kufungwa basi hawawezi kufanya miamala zaidi ya 100K. Sasa hivi hata 1M unaweza kutoa usiku na hakuna matata.

Sababu ya huu ushwari ni nini?

1: Majambazi yalitokomezwa kabisa?
2: Jeshi la Polisi liko imara?
3: Majambazi wametafuta shughuli za kufanya au wameadvance zaidi?
4: Upo ila taarifa ndio wengi hatuzipati?
5: Mama anaendelea kuupiga wa kutosha?

Ni hayo tu.
Ni tukio gani ambalo hautalisahau.
Jaribu kuwa jambazi na hautoonekana tena kwenye uso wa Dunia wala habari zako
 
Jeshi la polisi halichek na nyani
Ukileta ujambazi tu unapotezwa tu biashara imeisha watakuwa majambazi wameambiana vikao vyao kaa mbali na ujambazi Tanzania unataka familia yako ione maiti yako na ikuzike vinginevyo waweza potea hewani kama ndege ya malyasia iliyopotea hewani haijawahi patikana hadi leo

Hakuna sehemu hatari duniani kwa sasa kwa jambazi kama kufanya ujambazi Tanzania

Kitakachomkuta jambazi hata kama kanusurika kufa lakini cha moto atakiona hata kama kufa hakufa lakini cha mtema kuni atakiona na mwenyewe atajipeleka ku trend media baada ya kuonyeshwa cha mtema kuni na ataapa kimoyomoyo kuwa ujambazi basi

Tanzania bila ujambazi inawezekana kaa mbali na ujambazi
 
Back
Top Bottom