Hivi siku hizi hakuna majambazi?

Hivi siku hizi hakuna majambazi?

Kabla ya awamu iliyokatishia njiani na hii ya sasa ilikuwa haipiti wiki unasikia watu wamevamiwa, majambazi yameuwawa ila siku hzi hizo habari hazipo kwa kasi ile.

Cha ajabu sikuhizi vimeibuka vituo vingi (benk ndogo) mitaani vinavyofanya kazi kwa miamala ya simu na Benki. Zamani ikifika saa 12 vituo hivi kama sio kufungwa basi hawawezi kufanya miamala zaidi ya 100K. Sasa hivi hata 1M unaweza kutoa usiku na hakuna matata.

Sababu ya huu ushwari ni nini?

1: Majambazi yalitokomezwa kabisa?
2: Jeshi la Polisi liko imara?
3: Majambazi wametafuta shughuli za kufanya au wameadvance zaidi?
4: Upo ila taarifa ndio wengi hatuzipati?
5: Mama anaendelea kuupiga wa kutosha?

Ni hayo tu.
Ni tukio gani ambalo hautalisahau.
Ww lazma hukai kanda ya ziwa usinge andika bandiko hili...
 
Aisee umenikumbusha ule mtiti wa wale washenzi , ilikuwa ni balaa 2004 kama sikosei hiyo mzee , actually Mimi nilikuwa mhanga wa hao wapuuzi , nilikuwa nakaa na wazazi wangu mtaa wa Kiloleli - Mwanza , Tulivamiwa usiku mmoja wale wapuuzi walikuwa wanavunja milango kwa mawe flani yanaitwa Fatuma .
Na walikuwa wanafunga mtaa ,njemba thelathini , na wana magobole na silaha nyingine kali ,panya road wakasome .
Aisee nakumbuka siku hiyo ile nyumba niliyokuwa nakaa walipiga sana na kujeruhi watu na wengine wanawake walibakwa kabisa .
Yale majamaa sitasahau kabisa ,na sehemu au pango walilokuwa wanajificha ni hapo juu ya kilima cha wakatoliki karibia na Pàrokia ya Kiloleli na shule ya Montessori .
Yalikuwa yanajificha hapo halafu usiku yanaingia mtaani kukinukisha ,halafu wengi walikuwa wakurya ,
Siku wanaenda kufurushwa mle aisee zilipigwa risasi zaidi ya masaa sita na polisi ila walifanikiwa kuyaua mwishoni ,ila naamini kuna mengine yalitoroka .
2004 -2005 ilikuwa miaka hatari sana Mwanza kwa ujambazi wa kutumia silaha
Si 2014? Au ile ilikuwa awamu ya pili?
 
Kabla ya awamu iliyokatishia njiani na hii ya sasa ilikuwa haipiti wiki unasikia watu wamevamiwa, majambazi yameuwawa ila siku hzi hizo habari hazipo kwa kasi ile.

Cha ajabu sikuhizi vimeibuka vituo vingi (benk ndogo) mitaani vinavyofanya kazi kwa miamala ya simu na Benki. Zamani ikifika saa 12 vituo hivi kama sio kufungwa basi hawawezi kufanya miamala zaidi ya 100K. Sasa hivi hata 1M unaweza kutoa usiku na hakuna matata.

Sababu ya huu ushwari ni nini?

1: Majambazi yalitokomezwa kabisa?
2: Jeshi la Polisi liko imara?
3: Majambazi wametafuta shughuli za kufanya au wameadvance zaidi?
4: Upo ila taarifa ndio wengi hatuzipati?
5: Mama anaendelea kuupiga wa kutosha?

Ni hayo tu.
Ni tukio gani ambalo hautalisahau.
Mkuu
Usiwastue wakaanza kuzingua. Hawanaga akili hao
 
Kabla ya awamu iliyokatishia njiani na hii ya sasa ilikuwa haipiti wiki unasikia watu wamevamiwa, majambazi yameuwawa ila siku hzi hizo habari hazipo kwa kasi ile.

Cha ajabu sikuhizi vimeibuka vituo vingi (benk ndogo) mitaani vinavyofanya kazi kwa miamala ya simu na Benki. Zamani ikifika saa 12 vituo hivi kama sio kufungwa basi hawawezi kufanya miamala zaidi ya 100K. Sasa hivi hata 1M unaweza kutoa usiku na hakuna matata.

Sababu ya huu ushwari ni nini?

1: Majambazi yalitokomezwa kabisa?
2: Jeshi la Polisi liko imara?
3: Majambazi wametafuta shughuli za kufanya au wameadvance zaidi?
4: Upo ila taarifa ndio wengi hatuzipati?
5: Mama anaendelea kuupiga wa kutosha?

Ni hayo tu.
Ni tukio gani ambalo hautalisahau.
Mdomo koma kazi yako kula
 
Kuna wale walikuwa wahaishi mapangoni kule mwanza, siku wanapelekewa moto ilikuwa ni zaidi ya vita. Zilirindima risasi z kutosha hadi wakawa neutralized.
Kuna tukio moja ni Mungu tu alituvusha, kipindi hicho niko chalii mdogo nikiwa na wenzangu pamoja na mbwa tukaingia kwenye hayo mapango kwenda kuwinda.

Ebwana weee si tukakutana na wajomba wametulizana wanapiga vitu vyao. Na vile mbwa hawana siri wakaanza fujo za kubweka ovyo, ajabu wale wajomba walibaki na utulivu wao na kutuelekeza cha kufanya kwa urafiki kabisa. Niliwachukulia tu ni ma bro wanapiga mjani.

Baada ya miaka kupita nikapata habari kumbe ile ilikuwa ni kituo cha wazee wenyewe.
 
No. siwezi kuwa jambazi, Mungu anakataza.

ushwari huwa hausababishwi na uwepo na uimara wa mabunduki na askari (Jeshi). ushwari unaletwa na Mungu mwenyewe baada ya sisi watu wake kumuomba. Ushwari huanzia katika ulimwengu wa roho
Acha mlango wazi nyumbani kwako alaf sema mungu nilindie sifungi milango wala geti
 
Kipindi kile, ukikutwa na Bunduki ni bye bye 👋.

Ukishapewa kisago ukataja wenzako, wanakuchukua unaingizwa porini kisha unakula ya kichwa stori imeisha.

Huu mfumo ulianzia kenya, watu wLikua wanapigwa risasi waziwazi maeneo kama kkoo mbele ya kadamnasi.


View: https://youtu.be/pOjYnSAAcnQ?si=Px9Fz94638UZd7Xk

Umenikumbusha kuna kipindi nilikuwa Mombasa mtaa wa Ronald Ngala asubuhi mapema tu Nikakuta mtu kalala chini kafa kashika panga Mtaa wa Ronald Ngala, mombasa wakasema huyo ni jambazi alikuwa anakata watu na mapanga askari wa Kenya wamemuua wamemuacha sehemu ya wapita njia wengi ambayo hata majambazi hupita ili wamtambue mwenzao kuwa na wao zama yao inakuja wakithubutu

Hiyo maiti polisi waliiichukua muda wa saa nane mchana toka wamuue usiku akipora usiku akipora wapita njia na panga lake.Walimtandika risasi wakamuacha hapo

Niliporudi siku ingine miaka miwili baadaye niliambiwa hilo eneo hajaawahi porwa mtu hata ndala iliyochakaa ujambazi ulishaisha majambazi wanauogopa huo mtaa wa Ronald Ngala kama ukoma kama eneo hatarishi na nuksi kwao

Sasa Tanzania kwa sasa ni nuksi kwa majambazi na magaidi hilo wamegundua hilo
 
Majambazi bado yapo yalichobadili ni mbinu tu , ukisikia kiongozi fulani kachota pesa za umma huo ni ujambazi.


Mengine yanauza maji ,mafuta na udongo wanaoita wa upako ,majambazi yapo kila kona na yanabamiza kama kawaida.
 
Back
Top Bottom