Hivi Simba SC mbona kama hawapo serious na usajili?

Hivi Simba SC mbona kama hawapo serious na usajili?

Nitajie timu yenye mafanikio makubwa duniani na mmiliki wake ni mhindi au anatoka India
Kwahiyo yanga inaenda kuwa na mafanikio kisa haiongozwi na mshindi!!![emoji23][emoji23]dah hii nchi had aibu
 
Acha kujijaza kama vile hujui sysytem za michezo Tz, unasema hata nila Muddy Simba Sc ingeweza kuyafanya haya iliyoyafanya ndani ya hii miaka minne(Ligi+Caf)? Leo hii muddy akae pembeni ni nani anaeweza kuwalipa hao wachezaji wa kigeni mishahara hata ya mwaka mmoja?

Hapo Yanga mlitamba enzi za Manji mkawa mnajiita wa kimataifa na team tajiri Tz, alivyojitoa hamkutembeza bakuli ili kupata hela za kulipa wachezaji? Ndege mlipanda tena??

Sasahivi kaja GSM mnajisahaulisha tena, mnaona kama yanga inaweza kukiendesha yenyewe😂, itokee leo GSM kabwaga manyanga hakuna kitu hapo.

NB:Sio Simba Sc wala Yanga inayoweza kujiendesha yenyewe kibiashara bila wawekezaji matajiri.

Kwahiyo waacheni wenye hela wafanye maamuzi, nyinyi mbuzi kaeni pembeni msubiri matokeo.
Nyie si mabingwa wa kuchangia timu yenu,mtoeni Gabachori ili muendelee kuendesha timu kwa kuchangia
 
Yaan wewe ndio kiaz balaa ,kwahiyo Simba kabla haijawa na mudy haikuwah kupata ubingwa?
Uchawa kwa magabachori utawamaliza marinda yote.
Wewe unaweza kulipa mchezaji yoyote wa kigeni hapo Simba Sc hata kwa mwezi mmoja (assume muddy hayupo)? Kabwela mkubwa wewe utaisaidia nini Simba?

Haya umeshindwa kuwalipa wakaondoka team ikabaki na wachezaji wa ndani tupu, utategemea kuchukua kombe gani mbele ya team zenye wafadhili kama GSM na Azam?😂.

Simba bila Muddy kwasasa haiwezi kuchukua kombe ikiwa Yanga itaendelea kubaki na mfadhili wake GSM, mmesahau enzi za Manji Simba iliitwa ya matopeni?? Na huko CAFCL&CAFCC mlifika wapi?

Mnapiga kelele humu na wakati mmeambiwa mchangie team na mmeshindwa kufikisha hata 100M, halafu unakuja kumkoromea MO humu kama sio ujinga ni nini?

KUBALI WEWE NI MJINGA KWASABABU UMESHINDWA KUTAMBUA KUWA MPIRA WA SASA NI FEDHA NA SIO MANENO.
 
kwani ni lini makolo wamewahi kuwa serious???
 
Jambo kubwa na la muhimu kwa Simba ni kutafuta kocha.

Baada ya kumpata Kocha ndio yeye afanye usajili na sio Viongozi wafanye usajili bila kufuata mahitaji na matakwa yake. Na ndicho kinachofanyika kwa sasa.
 
Viongozi wa Simba wameshituka uwekezaji wa Mchongo wa Dk Mudi Dewuji....

Hawana Sauti na Timu yao, fedha za Simba ndio zinazungushwa na Dewji ktk uendeshaji Club...

Hawajui mikataba ya matangazo ya bidhaa za mwekezaji Dewuji Iko vipi na club inanufaikaje na mapato!!?

Bil 20 maelezo yake hayaeleweki....hisa zao 51 nguvu yake Iko wapi...yaani 49 ndio inafanya wao waonekane kazi yao kufungua mikutano na kufunga kwa mujibu wa Ndg Rage...


Yaani wamechanganyikiwa Dewuji kawabana hawana mapato yoyote kama club...mapato ni ya Dewuji Dk...

Wanahali ngumu mno...
Kwani Yanga ina sauti gani kwa GSM?
 
Hata kabla ya Mo dewji kuja kuwekeza pale Simba washachukua ligi Mara tano mfululizo na hata kufika fainali ya Caf champions league

Mafanikio ya mpira ni kushinda vikombe au mataji makubwa kama lilivyo lengo la simba

Timu nyingi zinazofanya vzr duniani wamiliki wake ni waarabu kama alivyo Gharib Said Mohammed
Real Madrid inamilikiwa na Mwarabu?

Bayern inamilikiwa na Mwarabu ?

Chelsea inamilikiwa na mwarabu ?

PSG na Man City zina mafanikio gani duniani ?
 
Jambo kubwa na la muhimu kwa Simba ni kutafuta kocha.

Baada ya kumpata Kocha ndio yeye afanye usajili na sio Viongozi wafanye usajili bila kufuata mahitaji na matakwa yake. Na ndicho kinachofanyika kwa sasa.
Upo sahihi lakini je muda utatosha? Maana CAF wamesema mwisho ni june 30 tu

Sent from my Redmi Note 9 Pro using JamiiForums mobile app
 
Kuna vitu havipo sawa pale,msimu uliopita viongozi waliweka siri ktk usajili kumbe matokeo yakawa hivyo wachezaji waliowaleta wanajua wenyewe, msimu huu unaoisha tunahitaji quality players lakini utasikia mara mchezaji yule hatukumuhitaji,au alitaka dau kubwa sasa wachezaji wazuri unawapata vipi bila kutoa pesa?

Wataweka usiri sana ktk usajili mashabiki tukiamini wapo seriously ktk kutafuta wachezaji ila utaona matokeo yake
Hakuna haja ya kuwalaumu viongozi wetu kwenye usajili. Kama namna gani vipi tuchangishane tupate wachezaji wenye hadhi na klabu yetu.
 
Mashabiki wa Tz(kibongo) ni wajinga sana, nadhani hii inaletwa kukosekana kwa exposure miongoni mwao. Team imefanya vizuri ndani ya miaka minne na kuwapa burudani ya kutosha ila leo wanalalamika utafikiri wameikosa ubingwa kwa miaka kumi, au labda team ineshuka daraja, au pengine imeshindwa kufuzu CAFCL, DAAAAAH[emoji1].

Pale Simba Sc kuna critical problems zilizotokea msimu uliopita, sasa watu wapo busy kutafuta ufumbuzi ila mashabiki mpo busy kulalamika mnataka Simba Sc ianze kushindania wachezaji, huu sio ujinga?

Wengine utasikia MO kaishiwa hela na sababu yenyewe ni kutomsajili Aziz Ki, haya hizo team kubwa zote Africa (Ahly, Wydad, Eserence,Mamelod, Pirates,Berkane...nk) zenye mpunga wa maana mbona hazijamsajili ikiwa kigezo ni pesa? MO anaishiwaje pesa kwa kitu merely kama kuongoza Simba Sc kitimu kidogo tu?

Acheni ujinga aiseeh, huko ulaya team zinakosa makombe miaka 30 au 10 lakini mashabiki hawawezi kuwa mentality za kijinga hivi.
Uko sahihi sana mkuu. Tanzania kuna shida kubwa sana ya uelewa hasa wa mpira. Usajili wa Simba sidhani unahitaji mbwembwe hizo kiivyo. Hao wanaofanya mbwembwe wanajua wanafanya kwa maslahi gani? wana uchaguzi na usajili ndo karata yao kuu. ndio maana umeona barua inatembea mitandaoni, barua ya ovyo sana. yan hata mtoto wa darasa la tatu hawezi kuielewa ile barua. logo tofauti, font tofauti nk cha kushangaza waandishi wakubwa tu wanashindwa kung'amua hilo kuona ule ujinga zaidi wanaupa promo sijui wanalipwa nn? maana kuna hela ya sasa lakini tuna uadilifu kwenye carrier yako.
 
shabiki mwenzangu wa Simba umeshindwa kuhimili joto la fununu za usajili.kaa kwautulivu Simba aijawai kushindwa vita.Africa ina mamia ya wachezaji bora na mahili.
 
Uko sahihi sana mkuu. Tanzania kuna shida kubwa sana ya uelewa hasa wa mpira. Usajili wa Simba sidhani unahitaji mbwembwe hizo kiivyo. Hao wanaofanya mbwembwe wanajua wanafanya kwa maslahi gani? wana uchaguzi na usajili ndo karata yao kuu. ndio maana umeona barua inatembea mitandaoni, barua ya ovyo sana. yan hata mtoto wa darasa la tatu hawezi kuielewa ile barua. logo tofauti, font tofauti nk cha kushangaza waandishi wakubwa tu wanashindwa kung'amua hilo kuona ule ujinga zaidi wanaupa promo sijui wanalipwa nn? maana kuna hela ya sasa lakini tuna uadilifu kwenye carrier yako.
Ile barua ilisambazwa kwa ili ionekane kwamba Simba Sc alitaka kumsajili Aziz ila akapigwa bao, yani ilimradi tu ionekane wamesajili player aliyekuwa anatakiwa sana Africa ilhali hakina team yoyote kubwa iliyohusishwa nae.
 
Siku zote wachezaji wazuri wanagombewa. Ukiona mchezaji hagombaniwi na timu ujue huyo ni galasa

Niambie Luis miquison alikuwa anagombewa na nani?,inonga alikuwa anagombaniwa na nani?,chama alikuwa anagombaniwa na nani walivyokuwa wanataka kutua simba?ukiwa shabiki wa utopolo fc lazima akili zikuruke
 
Kuna vitu havipo sawa pale,msimu uliopita viongozi waliweka siri ktk usajili kumbe matokeo yakawa hivyo wachezaji waliowaleta wanajua wenyewe, msimu huu unaoisha tunahitaji quality players lakini utasikia mara mchezaji yule hatukumuhitaji,au alitaka dau kubwa sasa wachezaji wazuri unawapata vipi bila kutoa pesa?

Wataweka usiri sana ktk usajili mashabiki tukiamini wapo seriously ktk kutafuta wachezaji ila utaona matokeo yake
Kwenye pesa ya usajili wewe unatoa sh ngapi? Ikiwa tu mashabiki wote wa Simba kwenye changizo linaloendelea kwa wiki 1 na siku kadhaa ndo kwanza wapo milion 100!?
Unaweza kulazimisha Everton imsajili Mbape kisa tu zote ni timu za Ulaya?
 
Mashabiki wa Tz(kibongo) ni wajinga sana, nadhani hii inaletwa kukosekana kwa exposure miongoni mwao. Team imefanya vizuri ndani ya miaka minne na kuwapa burudani ya kutosha ila leo wanalalamika utafikiri wameikosa ubingwa kwa miaka kumi, au labda team ineshuka daraja, au pengine imeshindwa kufuzu CAFCL, DAAAAAH😄.

Pale Simba Sc kuna critical problems zilizotokea msimu uliopita, sasa watu wapo busy kutafuta ufumbuzi ila mashabiki mpo busy kulalamika mnataka Simba Sc ianze kushindania wachezaji, huu sio ujinga?

Wengine utasikia MO kaishiwa hela na sababu yenyewe ni kutomsajili Aziz Ki, haya hizo team kubwa zote Africa (Ahly, Wydad, Eserence,Mamelod, Pirates,Berkane...nk) zenye mpunga wa maana mbona hazijamsajili ikiwa kigezo ni pesa? MO anaishiwaje pesa kwa kitu merely kama kuongoza Simba Sc kitimu kidogo tu?

Acheni ujinga aiseeh, huko ulaya team zinakosa makombe miaka 30 au 10 lakini mashabiki hawawezi kuwa mentality za kijinga hivi.
😁😁Yani we acha kuna baadhi ya wachambuzi pia na viongozi wenye malengo ya matumbo yao wameeanza kupiga rhumba eti mara wamefeli mara nini !?Yani kukosa kombe msimu 1?seriously …
 
Back
Top Bottom