Uchaguzi 2020 Hivi Tundu Lissu amepewa ulinzi na Serikali?

Uchaguzi 2020 Hivi Tundu Lissu amepewa ulinzi na Serikali?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
F33AD77E-FB5E-4BDC-9A98-C4AD9F9251A0.png


Katika kipindi hiki cha kampeni za urais, nimekuwa nikimwona huyo jamaa aliyevaa ‘Kaunda suti’ ya buluu hapo kwenye picha, akiwa pembeni ya Tundu Lissu karibu kila sehemu.

Nikiangalia mavazi yake pamoja na hako ka peni alikokachomekea kwenye mfuko wake wa shati, naona ana fit profile ya wale walinzi kutoka serikalini ambao huwalinda viongozi wa nchi.

Najua kwa nchi kama Marekani, wagombea urais wa vyama vikuu [Republican na Democrats na pengine hata wale wa kujitegemea kama Ross Perot] hupatiwa ulinzi wa Secret Service.

Sasa kwa Tanzania sijui. Kama kuna anayejua, itapendeza akitujuza wale ambao hatujui.

Manake kila nikimwangalia huyo jamaa naona kama vile anatoka kwenye hicho kitengo cha walinzi wa viongozi.

Kama anatokea huko, ni jambo ambalo ni la mwaka huu tu hususan kwa Tundu Lissu au ni ndivyo ilivyo miaka yote ya uchaguzi?
 
Sina hakika na huyu uliye msema Ila, Sheria na taratibu za uchaguzi huko US na hata hapa Tz zinasema wagombea wote wa nafasi ya urais kupewa walinzi na serikali maana yeyote Kati yao anaweza kuwa raisi mchaguliwa na hatimaye raisi kabisa baada ya kupishwa.
 
Sina hakika na huyu uliye msema Ila, Sheria na taratibu za uchaguzi huko US na hata hapa Tz zinasema wagombea wote wa nafasi ya uraisi kupewa walinzi na serikali maana yeyote Kati yao anaweza kuwa raisi mchaguliwa na hatimaye raisi kabisa baada ya kupishwa.
Oh ok. Sikujua hilo.

Basi huenda huyo jamaa ni wa kutoka serikalini...
 
Walinzi wa serikali toka lini wakatembea na majambia? Ila ulinzi wa kweli huutoa Mungu maana imeandikwa amelaaniwa yule amtegemeaye binadamu mwenzake kama kinga.

Haya mengine huwa ni protocol za kidunia tuu maana pia tuliambiwa tutii mamlaka zilizowekwa hapa Duniani ila ulinzi wa kweli na uhakika ni wa kupiga goti na kufanya maombi.

October 28th tujitokeze kwa wingi tukampe kura za ndio JPM maana ni Kiongozi aliyetukumbusha kumlilia Mungu tulipokuwa katika nyakati ngumu za Covid 19.

JPM ANATOSHA
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Walinzi wa serikali toka lini wakatembea na majambia? Ila ulinzi wa kweli huutoa Mungu maana imeandikwa amelaaniwa yule amtegemeaye binadamu mwenzake kama kinga.

Haya mengine huwa ni protocol za kidunia tuu maana pia tuliambiwa tutii mamlaka zilizowekwa hapa Duniani ila ulinzi wa kweli na uhakika ni wa kupiga goti na kufanya maombi.

October 28th tujitokeze kwa wingi tukampe kura za ndio JPM maana ni Kiongozi aliyetukumbusha kumlilia Mungu tulipokuwa katika nyakati ngumu za Covid 19.


JPM ANATOSHA
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
Nani ana jambia?
 
Back
Top Bottom