Hivi umewahi kuhisi kuna upendeleo wa baadhi ya watoto kwenye familia yenu?

Watu tumechukiwa bila sababu Hadi timefukuzwa nyumbani na tumefuta undugu.
Saa hizi ndugu yangu ni mke wangu na watoto wangu tu, full stop
Pole sana aisee, najua ni namna gani unajiona mwenye hatia pasipo hatia. Samehe na maisha yaendelee(ingawa ni ngumu kuikabili hali hiyo). Kikubwa kama kuna mabaya hakikisha hayajirudii kwa uzao wako.
Jenga familia yako, ifundishe upendo na kujipambania.
Usilipe kisasi na utabarikiwa.
 
Basii vitoto vinavyojua vinapendwa huwa vinajua kudeka, huwa huvimbi kweli Cvez.??
Hahahaha unaachaje sasa... Kila ukienda home kumcheck mama unapunguza stress za maisha unapata ile pure love.
 
Mkuu punguza jazba kidogo[emoji2957][emoji3]
 
Na haya ndiyo madhara ya kukosa upendo utotoni hata maandishi tu yanajidhihirisha jinsi ulivyo na chuki,mkali na kila kitu kibaya.
 
Lakini hata unavyo mtaja huyo mtoto wa pili inaonyesha kabisa mambo yake ya kulia lia na utundu yanakukera, unatumia hili toto...litundu...wakati wa kwanza hata kumtaja unachagua kwa umakini herufi za kutumia.
I know my tone was different. Ni katika kuonyesha utofauti mkubwa uliopo baina yao.

I love my sons with all I have.

And I love them equally.
 
Mimi nilikuwa gangwe wa familia.Lakini nilipoondoka kwenda Msumbiji wanafamilia walilia kwa huzuni.😝😝😝😝😝
 
Watu tumechukiwa bila sababu Hadi timefukuzwa nyumbani na tumefuta undugu.
Saa hizi ndugu yangu ni mke wangu na watoto wangu tu, full stop
Mm hadi kuwajengea nyumba mambo ya NHIF, kusaidia kusomesha wajomba kuna madogo zangu hadi leo wanakaa kwenye vibanda vyangu .ila wote wanasema mm nina roho mbaya mchoyo siwajaki sasa niko kama wewe... sijui mtu tena sipigi simu wala sipigiwi simu wife nimemwambia aamue mm au wale ...
 
Watu tumechukiwa bila sababu Hadi timefukuzwa nyumbani na tumefuta undugu.
Saa hizi ndugu yangu ni mke wangu na watoto wangu tu, full stop
Duu aise. We kama mimi aise. Mimi na sister tunayefatana wote tumezaa nje ya utaratibu, nimezakisha binti wa watu sister naye kazalishwa. Ila bi mkubwa mtoto wangu ameshaniambia hamtaki na asimuone kwake. Ila wa sister amemchukua na anahanhaika naye. In Short bi mkubwa ni mkoloni ila huyu sister wakati tunakua ndo alikuwa anathubutu kumtania, kumchezea muziki n.k. Hivi tunavyoongea life lake lipo ovyo ovyo.
 
I'm the first born. Walioonesha kunipendelea mimi zaidi kuliko wadogo zangu siku nilipojitambua niliamua kujiweka mbali nao hasa kimawasiliano. Sipendi upendeleo wala ubaguzi

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
My Salimeti, kumbe wewe ni lilast born, uliyedeka sana😂 miaka 7 si ni mbabu kabisa huyu aah🙌
 
Ha ha ha ha, Mimi Ni last born and wa kiume pekee yangu tumelelewa na bibi kwa angalau 90% hasa mimi.Bi mkubwa kuna kipindi alikuwa anatamka mbele yangu eti yaaan Fulani( anamtaja sister wa kike) angezaliwa mwanaume. Hapo mimi niko zangu shule nahangaika sina mbele Wala nyuma. Ilifika point akaniudhi ikabidi nimchane. Nikakwambia bi mkubwa kwenye watoto wako wote Mimi ndo mtoto wa kiume usije ukasahau hilo. Sasa sister zangu wote Mambo yao siyo poa kabisa. Mimi Sasa hivi atleast kwa sababu ndo pekee yangu nimefanimiwa kupata elimu ya juu. Bi mkubwa ananidhiria kila kitu, ni kama kauli zake na jinsi alivyokuwa ananibagua vinamtafuna, though mimi sina tatizo kabisa na the past!
 
I know my tone was different. Ni katika kuonyesha utofauti mkubwa uliopo baina yao.

I love my sons with all I have.

And I love them equally.

Karucee nakuelewa ndio maana nikadiriki kuandika nilichokiandika kwa vile najua your level of maturity...relax!

Hakuna mzazi anapenda apende mtoto mmoja zaidi ya anavyowapenda wengine.
Na mie naambiwa nampenda zaidi binti kuliko kajamaa kanakomfuatia, tena hii anasema Mama yake.

Nikajaribu kutafakari sikuona kama nna hizo chembechembe za ubaguzi au upungufu wa upendo kwa hao watoto kati ya mmoja na mwenzake. Ila kajamaa kenyewe ndio ukikagusa kila kitu ni Maam, Mamii hata mie kuna wakati kanajisahau kananiita Mamii, ndio jina liko mdomoni mwake la karibu kabisa.
 
Kweli first born wako mpole. Maananimekumbuka uziwako ukisema vidume vyako vinadundana. Watu tukafungua uzi tukijua kimewaka kati ya hasband na mchepuko kumbe watoto
 
Kiukweli hili suala la upendeleo lipo, nakumbuka home wazazi walivokua na vipenzi vyao, Baba alikua ananipenda sana mimi, na Mama alikua anampenda mno second born wetu wa kiume mno, na mimi nilikua najua kabisa mama mimi hanipendi sana, mfano nakumbuka tulikua tunakula pamoja plate moja ya ubwabwa, nakumbuka dogo alikua na speed anakula fasta anataka kumaliza, mimi kidogo hizo ligi nilikua mzembe nakula taratibu ikifika mwisho hata sijashiba, naskia mama anasema ebuu mbakizie mtoto huko wewe si mkubwa hapo anajua kabisa speed ya mwanae ila basi tu. Dah nilikua namind sana. Akiwepo dingi sasa anaangalia tunavokula anaangalia speed ya dogo wee then anasema wewe mdogo mbakizie Dada ako, nimeona speed yako kubwa.😂
 
Kwenye familia nyingi; baba anawapenda zaidi watoto wa kike, na mama anawapenda zaidi watoto wa kiume. Naturally watoto wa kike, tunajikuta tunakuwa karibu zaidi na baba zetu unless awe baba mwenye matatizo, awapush mbali mabinti zake. Na wamama nao na vijana wao; ukaribu unaendelea hadi vijana wanaoa, na huko ndiyo tunakutana na "nguvu ya mama mkwe". [emoji38][emoji38]

Ni kama tu nilivyosema, kuna watoto wanapendeka na wanakuvuta kwao zaidi kuliko wenzao. Imagine baby boy hadi anakuita mamii; obviously ana-base kwa mamii wake, na wewe utabase kwa dada yake tu automatically

 
Hii sasa sio kumpenda zaidi mtoto mmoja; huu ni ubaguzi per se. Huwezi kuwa unamjali mtoto mmoja zaidi, unamtimizia mahitaji yake yote; halafu wengine unawapotezea. Inatakiwa watoto wote wajihisi na wauone upendo; ila pia wanaona tu like eeh baba na mtoto fulani jamani. Ni kama vile mzazi upo mbali, unapiga simu, unaongea na watoto wote mmojammoja; ila yule kipenzi unajikuta unaongea naye kwa muda mrefu zaidi.
 
Amen swts [emoji120][emoji120][emoji120]
Whoooops'...!
Hat off Sweet C'ssy, you said it all, yaani umeichambua hasa, sijui nikuachie tu hii thread maana umejua kuitendea haki hatari..!
Naamini na Najua you're the Best Mom ever, I am so so proud ov you.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…