Hivi umewahi kuhisi kuna upendeleo wa baadhi ya watoto kwenye familia yenu?

Hivi umewahi kuhisi kuna upendeleo wa baadhi ya watoto kwenye familia yenu?

Amen, T.G.I.F, wale wenzangu na Mimi wapenda weekend tunaijua ile feeling ya Ijumaa,

Natumaini mpo salama, nimejikuta najiuliza hichi kitu maana ni situation ambayo nimekutana nayo sana kwa watu wengi, kuna ile namna unahisi kabisa kwamba kwenye familia yetu yenye watoto kadhaa, kuna kipenzi cha Baba na pia kuna kipenzi cha Mama, na kuna wale wanabaki wanajua kabisa Mimi siye miongoni mwao..!

Nilikuwa nazungumza na mtu wangu wa karibu siku moja, akanitamkia like 'I was not their best'...! yaani hapo si kwa Baba wala Mama, nilijiskia vibaya mno mno, na hakika ukitazama watoto waliokosa upendo wa hivyo kwa kushuhudia kabisa kuwa wenzie wanakirimiwa kuwaliko kuna namna hawako sawa kabisa kabisa tofauti na yule mtoto aliyepokea upendo wa kumtosha na kumjaziliza..!

Bado sijakuwa mzazi I don't even know how it feels, hivyo natamani nijue, unapenda watoto wote ni kweli lakini kuna yule ambaye anagusa kabisa mtima wako moja kwa moja (nimeongea na wazazi wengi na wamekiri hili), hivi hakuna namna unaweza ficha hili wenzie wasijue na wakajiskia vibaya.?

Ama umewahi pitia ile hali katika ukuaji wako ya kujua wewe ndiye unapendelewa zaidi ama ni kinyume na hapo kuliko wenzio, na ulijiskiaje.??

Natamani wajuzi wa malezi na wazazi waliweke hili sawa ili tujifunze, maana kuna kizazi chenye watu wenye tabia za ajabu sana kinazidi kutengenezwa hivi sasa na hakuna anayewaza kuhusu hili kabisa..! Kuna watu unaweza walaumu kwa tabia wanazokuonyesha ukaishia kuwalaumu na kuwachukia kumbe ni MALEZI yao tu maskiini ndiyo yamewafikisha walipo..!!

Anyways Karibuni..!
Ipo sana kwenye familia,ila ni jambo baya sana kwa mzazi kuonyesha mapenzi makubwa kwa mtoto mmoja kuliko wenzie,wale wanaobaguliwa au kuonyeshwa mapenzi kidogo,hii huwakaa moyoni na ukubwani watalipa kisasi kwa wazazi,watakuwa hawana mapenzi na wazazi wao kabisa,huwa ni mbegu mbaya wazazi wanakuwa wamefanya,
 
Hata kwenye familia bukiachilia baba na mama.
Ndugu kukuchukia.
Nimezoea.,sijali wala nn
 
Nakumbuka wakati niko mdogo, mimi nyumban ndo first born....nilipita kipindi kigumu sana katika ukuaji, hasa nilikua naona waziwazi jinsi ambavyo wadogo zangu mapacha walivyokua wanapenda. Hawa mapacha ni wakike na wakiume, bwana hwa jamaa darasani walikua wazima..hivyo niliona ambavyo mama anampenda mdogo wangu wa kiume na baba alikua anampenda mdogo wangu wa kike. Iliniumiza na kuninyima raha, kuna siku tulikaa kibarazani, sijui ilikuaje tukawa tupo watatu mimi, mama na baba. Ndipo nikawaambia wazazi wangu kiukweli nyie mi hamnipendi mnawapenda hawa wenzangu, ila mama akapinga na akasema hapana si kweli.
Mimi kutokupendwa kwangu kulitokana na sababu nyingi, kama ugomvi aseeh wiki haipiti sijaleta kesi nyumbani, hizi ngumi nimepigana sana.
Kingine darasanai sikua nafanya vizuri kama watoto wengine, hasa huyu wakiume ndo alikua anakua wakwanza mara nyingi, huyu wa kike labda watatu hivi. Ila namba zangu mi huko 20 na kitu.
Kiukweli kutokuoneshwa sipendwi kulinikomaza kiakili, na nikaanza kupambana na kuwa mtu ambaye nataka kuwaonesha ndani yangu kuna kitu.
Kwasasa nyumban mi ndo napendwa hasahasa mama yangu, ananipenda sana na hilo nalijua na nampenda sana mama kuliko maelezo.
Nawasilisha.
Ndugu yangu wa kwanza alipendwa sana,na wadogo zangu pia,mie nilikuwa nachukuliwa kama mtu bwege bwege hv,na kilichoniuma ni wazazi kuona ni kitu Cha kawaida kunitamkia kuwa mie ni mjinga mjinga,kubwa jinga huku wanacheka,wakichukulia kama utani,kitu kibaya kikifanyika,wa kwanza kushukiwa ni mie,hii kitu iliniuma sana na inauma sana mpaka leo,matokeo yake nilianza kujenga roho ya kuwa independent nikiwa mdogo sana,nikaona hapa kitu pekee Cha kuniokoa ni kitabu,nilisoma sana hakuna aliyeweza kunifikia kwa uhodari kwa ndugu zangu,nilibamiza mitiani na ndugu zangu hakuna aliyeweza kuwa na mafanikio ya kitaaluma kama Mimi.
Tumeishakuwa watu wazima,lakini kwa madhara yale ya kubaguliwa nikiwa mtoto huwa Sina uchungu na mapenzi kwa wazazi kabisa,mpaka wenzangu huwa wanashangaa,nikisikia mtu anasema anampenda mama yake kuliko kitu chochote,huwa nashangaa sana,sasa hv nimeishakuwa mzazi najitahidi sana kuonyesha mapenzi Sawa kwa kila mtoto wangu,kila mtoto Nampa nafasi ya kuwa anavyotaka yeye sio kulazimisha awe kama wenzie.
 
Watoto na wazaz wa siku mmekaa kindez ndez kijinga jinga..Et mtoto anakua hayuko sawa kisa hajaonyeshwa upendo..upumbavu huu wenu mnaojifanya wasomi..et na wewe umeambiwa tu "i was nit their best....blah blah" ukajiskia vibaya..au ni kingereza ndio kilikuchanganya?? Pumbavu sana huv nyie vitoto mngekulia kwenye family zile za kizaman tulizokulia sisi si mngekufa before age?? Na kwa mind set hii no wonder mnatengeneza kizaz cha kishenz na nyie watoto mnajiweka near poverty line... wakongwe wenzangu wanalijua hili. Kwenye family mko watoto 18 huo muda wa kuonyeshana upendo unatoka wapi?au wewe kama mtoto huo muda wa kuchunguzwa unapendwa au hupendwi unautoa wapi?? Na sometimea watoto wengine wanalelewa katika mazingira kabisa akijua hapendwi ila ndio inampa changamoto ya kujipambania na kujisimamia na kujitetea dhidi ya uonevu toka kwa wenzake....

Achen watoto kuwalea katika namna ambayo watashindwa kujisimamia hala baadae wajifiche kwenye kivuli hicho cha " nilikua sipendwi".

Endeleen tu kutengeneza kizaz cha kishoga shoga wapuuz nyie...
Mkuu umeandika kwa hasira sana na jazba, hakika psychology haidanganyi.. inawezekana kabisa ulichokikosa wewe ni up3ndo na ukaribu connection yako na wazazi/mzazi.

Upendo ni Amri kuu na ya Kwanza!
 
Ndugu yangu wa kwanza alipendwa sana,na wadogo zangu pia,mie nilikuwa nachukuliwa kama mtu bwege bwege hv,na kilichoniuma ni wazazi kuona ni kitu Cha kawaida kunitamkia kuwa mie ni mjinga mjinga,kubwa jinga huku wanacheka,wakichukulia kama utani,kitu kibaya kikifanyika,wa kwanza kushukiwa ni mie,hii kitu iliniuma sana na inauma sana mpaka leo,matokeo yake nilianza kujenga roho ya kuwa independent nikiwa mdogo sana,nikaona hapa kitu pekee Cha kuniokoa ni kitabu,nilisoma sana hakuna aliyeweza kunifikia kwa uhodari kwa ndugu zangu,nilibamiza mitiani na ndugu zangu hakuna aliyeweza kuwa na mafanikio ya kitaaluma kama Mimi.
Tumeishakuwa watu wazima,lakini kwa madhara yale ya kubaguliwa nikiwa mtoto huwa Sina uchungu na mapenzi kwa wazazi kabisa,mpaka wenzangu huwa wanashangaa,nikisikia mtu anasema anampenda mama yake kuliko kitu chochote,huwa nashangaa sana,sasa hv nimeishakuwa mzazi najitahidi sana kuonyesha mapenzi Sawa kwa kila mtoto wangu,kila mtoto Nampa nafasi ya kuwa anavyotaka yeye sio kulazimisha awe kama wenzie.
Inasikitisha sana hata wazazi huwa wanakosea sana kwenye malezi yao kwa watoto!

Kumuita mtoto mjinga, taahira over n over , au kumuonyesha kumbaguwa wazi wazi...unamjengea picha mbaya mtoto!!
 
Mimi nimezaliwa peke yangu sina experience hiyo. Ila kama mzazi mzani hauwez kua sawa kuna mahali utazidi tu. Hiyo ni hali ya kawaida kwa mzazi yeyote unawapenda watoto wako wote ila mzani utazidi tu kwa mwingine.

Mara nyingi wa kwanza anapendwa zaidi na wa mwisho ni kudeka deka kunaweza onesha anapendelewa sana ila mfungua njia upendo mwingi hua kwake.
 
Mimi ni litoto la mwisho na nilipendelewa kwa kila kitu. Kunyonya kwenyewe nilinyonya mpaka nikiwa na miaka saba yaani niko nachunga ndama na akili zangu kabisa lakini kichwani napiga akili kuwa nikifika tu home napata lishe ya uhakika kutoka kwa maza. Nakumbuka kulikuwa na mzee mmoja mkorofi sana alikuja pale home ndo akachimba mkwara eti hili litoto mtakuja kuliharibu hili (shwaini zake!). Na kuanzia siku ile ndo nikapotezea kunyonya. Mpaka mama amekuja kuzeeka mpaka kufariki tuko marafiki sana. Imagine anakata roho mi niko mbali lakini niko naye kwenye simu ananiaga.

Hali hii nadhani mwenyewe imeniathiri kiasi fulani (tender heart, huruma sana, kutokuwa na kifua; na mengine mengi tu) ila pia sikujua lakini baadhi ya ndugu zangu hasa wale wawili ninaowafuata wana reservations na mimi na hatuko karibu kivile no matter how hard I try. Wanasema everything came easy for me kwa vile nilikuwa mtoto mpendwa wa familia. Kwa wanangu najitahidi sana kuwa fair japo kuna katoto kamoja yaani nakapenda mpaka basi. Mungu na Atusaidie wazazi tusilete madhara na kupanda mbegu za uhasama; na hata kuacha makovu ya kudumu kwa malaika hawa tuliobarikiwa nao - hasa katika kizazi hiki cha mabroila [emoji1545][emoji1545][emoji1545].
Toto la mwisho Hujambo?!!!.
 
Mkuu umeandika kwa hasira sana na jazba, hakika psychology haidanganyi.. inawezekana kabisa ulichokikosa wewe ni up3ndo na ukaribu connection yako na wazazi/mzazi.

Upendo ni Amri kuu na ya Kwanza!
Sio kwel mkuu.wazazi wangu have been so lovely considering i am the only born kwa mama yangu i was one of the best kwa baba yangu ambako tuko wengi but i was the first kid to excell in almost everything compared to my bloods.mzee wangu ni moja ya vitu alipendea but haikua na maana hakuwapenda wengine
So sijawah kosa upendo hata kidogo

Ila tu i hate hiz mambo za kuendekeza sana watoto i really do hate..that is y vijana now days wanakuwa wapumbavu sana mpaka kwenye maisha ya kujitegemea na kujisimamia..even simple life manners tu ni tatizo.
 
Amen, T.G.I.F, wale wenzangu na Mimi wapenda weekend tunaijua ile feeling ya Ijumaa,

Natumaini mpo salama, nimejikuta najiuliza hichi kitu maana ni situation ambayo nimekutana nayo sana kwa watu wengi, kuna ile namna unahisi kabisa kwamba kwenye familia yetu yenye watoto kadhaa, kuna kipenzi cha Baba na pia kuna kipenzi cha Mama, na kuna wale wanabaki wanajua kabisa Mimi siye miongoni mwao..!

Nilikuwa nazungumza na mtu wangu wa karibu siku moja, akanitamkia like 'I was not their best'...! yaani hapo si kwa Baba wala Mama, nilijiskia vibaya mno mno, na hakika ukitazama watoto waliokosa upendo wa hivyo kwa kushuhudia kabisa kuwa wenzie wanakirimiwa kuwaliko kuna namna hawako sawa kabisa kabisa tofauti na yule mtoto aliyepokea upendo wa kumtosha na kumjaziliza..!

Bado sijakuwa mzazi I don't even know how it feels, hivyo natamani nijue, unapenda watoto wote ni kweli lakini kuna yule ambaye anagusa kabisa mtima wako moja kwa moja (nimeongea na wazazi wengi na wamekiri hili), hivi hakuna namna unaweza ficha hili wenzie wasijue na wakajiskia vibaya.?

Ama umewahi pitia ile hali katika ukuaji wako ya kujua wewe ndiye unapendelewa zaidi ama ni kinyume na hapo kuliko wenzio, na ulijiskiaje.??

Natamani wajuzi wa malezi na wazazi waliweke hili sawa ili tujifunze, maana kuna kizazi chenye watu wenye tabia za ajabu sana kinazidi kutengenezwa hivi sasa na hakuna anayewaza kuhusu hili kabisa..! Kuna watu unaweza walaumu kwa tabia wanazokuonyesha ukaishia kuwalaumu na kuwachukia kumbe ni MALEZI yao tu maskiini ndiyo yamewafikisha walipo..!!

Anyways Karibuni..!
Ipo sana hii kitu,kuna siku nliwahi kumtolea uvivu dingi nikamwambia niliwahi kukusikia siku moja unaongea kuwa katika sisi watoto wenu mtoto flani unampenda zaidi kuliko wengine,nikaona mzee mzima anajihami kikubwa,lakini ukweli ni kuwa familia nzima hilo wote tunalijua kuwa yule ndio kipenzi chake.Sasa na mimi juzi kati yamenikuta,mtoto wangu mkubwa nimesikia analalamika kuwa nampendelea zaidi mwenzake wacha nianze kujiahami,ila nimejitafakari nikagundua kuwa yuko sahihi nilizidisha kidogo mahaba upande mmoja...
 
Nakumbuka wakati niko mdogo, mimi nyumban ndo first born....nilipita kipindi kigumu sana katika ukuaji, hasa nilikua naona waziwazi jinsi ambavyo wadogo zangu mapacha walivyokua wanapenda. Hawa mapacha ni wakike na wakiume, bwana hwa jamaa darasani walikua wazima..hivyo niliona ambavyo mama anampenda mdogo wangu wa kiume na baba alikua anampenda mdogo wangu wa kike. Iliniumiza na kuninyima raha, kuna siku tulikaa kibarazani, sijui ilikuaje tukawa tupo watatu mimi, mama na baba. Ndipo nikawaambia wazazi wangu kiukweli nyie mi hamnipendi mnawapenda hawa wenzangu, ila mama akapinga na akasema hapana si kweli.
Mimi kutokupendwa kwangu kulitokana na sababu nyingi, kama ugomvi aseeh wiki haipiti sijaleta kesi nyumbani, hizi ngumi nimepigana sana.
Kingine darasanai sikua nafanya vizuri kama watoto wengine, hasa huyu wakiume ndo alikua anakua wakwanza mara nyingi, huyu wa kike labda watatu hivi. Ila namba zangu mi huko 20 na kitu.
Kiukweli kutokuoneshwa sipendwi kulinikomaza kiakili, na nikaanza kupambana na kuwa mtu ambaye nataka kuwaonesha ndani yangu kuna kitu.
Kwasasa nyumban mi ndo napendwa hasahasa mama yangu, ananipenda sana na hilo nalijua na nampenda sana mama kuliko maelezo.
Nawasilisha.
Sawa ww me au ke
 
Sio kwel mkuu.wazazi wangu have been so lovely considering i am the only born kwa mama yangu i was one of the best kwa baba yangu ambako tuko wengi but i was the first kid to excell in almost everything compared to my bloods.mzee wangu ni moja ya vitu alipendea but haikua na maana hakuwapenda wengine
So sijawah kosa upendo hata kidogo

Ila tu i hate hiz mambo za kuendekeza sana watoto i really do hate..that is y vijana now days wanakuwa wapumbavu sana mpaka kwenye maisha ya kujitegemea na kujisimamia..even simple life manners tu ni tatizo.
Nimekupata mkuu..
Inawezekana watu wana udefine upendo kwa namna nyingine wanajikuta wanalea watoto kimayai mayai.. mwishowe wanaharibikiwa kiakili saikolojia hata kiafya..
Unakutana na mtoto mdogo darasa 2~4 ana kilo za mtu mzima, yani mama kanenepeana na mtoto kanenepean inabidi wote waanze maozeiz ya kukata kitambi road walk😂😂..
Malezi mengine hayafai kama mtoto kuwa na obesity ni kosa la mzazi kumuhatarisha afya mtoto
 
Mimi Nina watoto wawili huyu wa kwanza wakati nampata nilikuwa niko njema kwahiyo nikampeleka hizi shule za English medium, wa pili nikawa nimefulia kwahiyo nimempeleka shule za kayumba roho inaniuma kwa nini yule asome shule ile huyu asome shule hii kwaiyo nimeamua mwaka ujao wote kayumba ili niweke mizani Sawa. Kuwapeleka wote siwezi maana kila siku watabaki nyumbani kwasababu ya ada.
Sina upendeleo ni hali ya maisha imebadilika,asiejua atahisi hivyo hata huyu mtoto wangu wapili badae atajua nilimbagua ila kumbe sio ,jiwe ndio kasababisha.
 
Hii mada nilimchanaga Bi mkubwa kitambo sana kama miaka 10 nyuma ila mpaka leo analalamika kuwa nilimwambia hanipendi [emoji28]...
Huu upendeleo upo, na sio kwamba tunasema mzazi hakupendi La hasha! wanatupenda ila kuna upendeleo fulani sijui ndo tuseme ubaguzi.

Halafu mnaosema Last born wanapendelewa, nakataa hii hoja kwa experience! mimi mwenyewe Last born, mimi mwenyewe ndo nmepewa jina la mama ake Bi mkubwa, Halafu mimi huyo huyo ndo mtoto wa kike pekee kwetu. Ila huo upendeleo haujanidondokea kabisa kote kote..

Naamini binadamu anakupenda akiamua tu, hahitaji sababu za msingi, mana unaweza kuwa na msaada na mzazi ukafanya kila kitu ila ndo ivyo huna kura za ndio, wakati huo huo kuna bro anapita bila kupingwa[emoji1787][emoji1787] na hana sifa hata moja!

Katika kitu namuomba sana Mungu nikiwa mama, jambo la kwanza naomba nisiwe na huu utopolo maana najua fika unavyouma! ukiwa kipenzi cha mzazi hata ukikosea unawekewa defence, sasa ukute kipenzi chao halafu umefanikiwa [emoji86] wengine wote mnakua mafisi.
usipokua kipenzi cha wazazi basi Merit unazofanya zinakua za wote, ila ubaya unakua wako...Na katika kitu ambacho wazazi hawajuagi ukionyesha kumpenda sana mtoto unamtengenezea uadui na wenzie.

Na ukiwa last born halafu hujafanikiwa utajuta utatumwa wewe na mmeo na watoto wako kwenye vikao vya familia, mimi binafsi naitambua nafasi yangu kwetua ni mpanga mipango na mtekelezaji mkuu.. zile Responsibility za familia zote mimi ndo nizibebe
 
Katika TV series ya "The Crown", ya Ufalme wa Uingereza, kuna episode moja Malkia Elizabeth alikuwa anaongea na mume wake Prince Philip(ambaye amefariki hivi karibuni), Malkia Elizabeth alikuwa anaangalia TV, walikuwa wanaonesha mtoto wa Waziri Mkuu Margareth Thatcher alivyopotea jangwani.

Malkia akasema ameshangaa sana Thatcher kusema huyo aliyepotea ni mtoto wake anayempenda kuliko wote. Malkia akasema suala hilo ni "interesting". Prince Philip akas3ma mbona kawaida tu hiyo. Malkia akasema inakuwaje Mama asema anamoenda mtoto mmoja zaidi ya mwingine, hususan kwa mapacha?Prince Philip akamuuliza Queen mtoto wake anayempenda kabisa ni yupi?

Malkia akakataa katakata kwamba ana mtoto mmoja anayempenda zaidi.

Prince Philip akakataa, akamwambia mkewe lazima kuna mmoja unampenda zaidi.

Malkia akakataa, akamuuliza mumewe , yeye Philip anampenda nani zaid?

Prince Philip akasema hilo swali rahisi sana, akasema anampenda binti yake (Princess Anne) zaidi.

Nikasema haya mambo yapo mpaka kwenye falme huko.

Clip ipo Youtube hapa chini.

 
Back
Top Bottom