Hivi unajisikiaje unapotumia choo cha kukalia?

Usha

Ushamba ni ujinga. Tafuta hela kijana kila kitu utaona rahisi.
 
Nakubaliana nawewe huwa nawaza huenda vile vyoo ni special kwa wazee wasio weza kuchuchumaa na kukata gogo. na kinakuwa special kwa mtu mmoja.
Umewahi kubahatika kutoka walau nje ya Tanzania? Bila shaka hujawahi ndiyo maana unaanzisha thread kama hii. Nasema hivi kwa sababu Bongo watu wanadhani choo ni lazima kiwe kichafu sana na inzi kwa wingi. Kwa taarifa yako Ulaya hakuna vyo vya kuchuchumaa. Infact ni kuanzia hapo airpot, ukishaingia kwenye ule ukumbi wa kuondokea, kwenye ndege, na unakokwenda kote ni vyoo vya kukaa. Uzuri ni kuwa majuu watu ni wastaarabu na wanajua maana ya hygyne. Na kwa Tanzania kuna watu wengi tu nyumbani wana vyoo vya kukaa. Kama umezaliwa mbugani huko mnakokata magogo vichakani hili linaweza kuwa jambo la ajabu kwako.
 
Mimi siwezi brother...... Mfn Kuna kumbi zile kubwa unakuta vipo na watu wako foleni kupata huduma,,
Mimi siwezi brother...... Mfn Kuna kumbi zile kubwa unakuta vipo na watu wako foleni kupata huduma,,
Mimi Huwa nawaza hapa kakaa mwanaume mwenzangu kaweka makalio na mapaja yake na mara zote huona kinyaa kukitumia
 

Huwa najiuliza sana hili swali, hivi kwanini Tanzania au Africa vyoo public vinakuwa vichafu kiasi kwamba huwezi kujisaidia.

Ukisafiri na mabus hivi vyoo kwenye mahoteli mabus yanasimama dah yaani ni hatari tupu, siku moja nikazidiwa nikaingi Choo cha stand pale Magufuri terminal dah haja yote ilikata aisee halafu sasa Choo cha kulipia.

Sijui tunakwama wapi aisee.
 
Mkuu umeshakuwa ni utamaduni wetu, tunadhani choo ni lazima iwe sehemu chafu. Majuu watu wanaingia na bia vyooni na unakuta ni kusafi kweli kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…