Hivi Vijana wa CHADEMA Wanatumia kitu gani kinachoharibu uwezo wao wa kufikiri na kujenga hoja? Mbona hawana adabu wala hekima?

Hao wabunge wenu na makamanda wenu wa Bawacha walishapeleka kesi mahakamani , Hivyo endeleeni kupambana nao huko mahakamani na wakiwashinda msiitupie lawama CCM kwa udhaifu wenu na kushindwa kwenu
 

Acha uongo wewe. Kama ni Tumaini la watanzania kwanini hamtaki vyama vingine vifanye siasa?. Tanzania ingekuwa mbali Sana Kama tusingekuwa Chini ya CCM .
 
Hao wabunge wenu na makamanda wenu wa Bawacha walishapeleka kesi mahakamani , Hivyo endeleeni kupambana nao huko mahakamani na wakiwashinda msiitupie lawama CCM kwa udhaifu wenu na kushindwa kwenu

Wanakuwaje wabunge wa Chadema wakati wameshafukuzwa chama?. Kwanini wanalazimishwa uanachama nanTulia?. Siku mtakaporuhusu haki kwa wapinzani ndio nchi ya Tanzania itastawi.
 
Acha uongo wewe. Kama ni Tumaini la watanzania kwanini hamtaki vyama vingine vifanye siasa?. Tanzania ingekuwa mbali Sana Kama tusingekuwa Chini ya CCM .
Mfanye siasa zipi unazozitaka? Au mnataka siasa za Kuendelea kutukana tukana matusi yenu, mbona mnazurula zurula na matisheti yenu mitaani kwa Uhuru,
 
Wanakuwaje wabunge wa Chadema wakati wameshafukuzwa chama?. Kwanini wanalazimishwa uanachama nanTulia?. Siku mtakaporuhusu haki kwa wapinzani ndio nchi ya Tanzania itastawi.
Wamefukuzwa kwa utaratibu you na baada ya muda upi tangia wameingia Bungeni? Haki zao zililindwa? Katiba ya chama ilizingatiwa? Kama mlizingatia hivyo vyote na vingine vingi Basi nendeni na endeleeni kupambana nao huko mahakamani walikokwenda kutafuta haki zao, kwa hiyo juu ya hili usiibebeshe mzigo CCM kwa matatizo yenu na hao makamanda wenu wa Bawacha
 
Mfanye siasa zipi unazozitaka? Au mnataka siasa za Kuendelea kutukana tukana matusi yenu, mbona mnazurula zurula na matisheti yenu mitaani kwa Uhuru,

Wala hujaelewa ninachosema. Chama siasa kipo kwaajili ya kufanya siasa sio kutibu wagonjwa. Kama unazuia chama Cha siasa kufanya siasa Ina maana unakiua. Tanzania inafuata mfumo wa vyama vingi, inakuwaje Mwenyekiti wa CCM kuzuia chama kufanya siasa na kujieneza. Mh Mbowe alikamatwa kwenye mkutano wa ndani na juzi ACT imezuiliwa kufanya mkutano kwenye ziara ya katibu Mkuu wa chama hicho.
 
Ben saanane Azron tuambie wako wapi? Walinyooka nao au?
 
Hivi
Hivi ulishaona nchi Kama marekani baba wa demokrasia akimaliza uchaguzi walioshindwa wanaanza kuzurula zurula mitaani na majukwaani kuitukana serikali? Ulishaona wanafanya maandamano muda wote na kubugudhi watu katika shughuli zao za kiuchumi? Hata hivyo endelea kuwa na Subira wakati serikali sikivu ya CCM ikiandaa kupitia majadiliano na wadau kuweka utaratibu mzuri wa kuona namna ya kufanya siasa za kistaarabu na kuweza kuonana na wanachama katika maeneo yao, wananchi wanahitaji ugali mezani Pao na siyo blaa blaa, kikubwa lazima pia mjifunze kufanya siasa za kistaarabu na kuheshimiana na kuvumiliana pale tunapotofautiana kimtizamo, siyo matusii tuu muda wote
 
Hujaona namna akina mdude na wenzake wanavyokesha wakitukana na kudhalilisha viongozi? Kwamba nhie huwa hamuwezi kukosoa bila matusi? Huwezi mkaijenga hoja bila kutumia lugha za kumdhalilisha na kumvunjia heshima mtu?
Thibitisha
 

Point yangu ni kwamba akina Mdee wanapambania kurejeshwa uanachama wao, Sasa wanaendeleaje kuwa wabunge wakati sio wanachama wanasubiri hukumu ya mahakama kuu?.
 
Hungry man is
Angry man


Aliimba Bob Marley
 
Na chinjachinja ni wa chama gani? Sijawahi kusikia kauli hizi za ajabu kwa mlezi au chama chochote Cha upinzani. Tena kiongozi anaongea kwa kutishia. Hivi CCM mnachinjana wenyewe au ni hawa vijana wanaohangaoka ajira mnawaita chadema mnataka muwaadhibu. Wachukueni muwaajiri pale lumumba muone kama.mtalalamikiwa.

Chadema Ina vijana wenye busara sana kuliko CCM. Ni vijana ambao ni wawazi kwa jambo na wanapenda kuchunguza na kujadili jambo il kupata majibu.

Mfano Acaccia Leo hii mnasemaje? Mngewasikiiliza chadema leo hii msingepata shida kujibu. Punguzeni uwongo na chuki.
 
Mdude ana busara gani? Kauli ya Chinja chinja alimaanisha kuumaliza upinzani kihoja kwa kuhakikisha kuwa anavuna wanachama wengi toka upinzani na kujiunga na CCM,
 
Waliweka zuio mahakamani litakalolinda ubunge wao Bungeni wakati kesi ya msingi inaendelea kusikilizwa, Hii so Mara ya kwanza na wao siyo wakwanza kufanya hivyo, David kafurila amewahi kufanya hivi pia, Zitto kabwe amewahi kufanya hiki wanachofanya akina mdee kutafuta haki yao mahakamani
Point yangu ni kwamba akina Mdee wanapambania kurejeshwa uanachama wao, Sasa wanaendeleaje kuwa wabunge wakati sio wanachama wanasubiri hukumu ya mahakama kuu?.
 
Pima uzito wa hiyo kauli na ulichojibu. Mimi ni chinjachinja kwelikweli tena kwa hasira.

Chama kinachinjwa wewe mburira kweli. Kamdanganye mwanao.
 
CHADEMA ni chama makini na pekee kilicho beba matumaini, mitazamo na maoni ya waTanzania wanaonewa na mifumo kandamizi ya serikali ya CCM.....ndio chombo pekee kilichobakia chenye uthubutu, ujasiri na ushujaa kuwaongezea au kuwasemea Watanzania na hata kuwakemea watesi........wapo vijana wachache wanaoshindwa kujidhibiti dhidi ya hoja na michango kinzani.......wao wakighafirika ubongo na vinywa huwa vinakosa ushirikiano.........hao ndio wanaoipaka matope CHADEMA inaonekana kuwa ni chama Cha kihuni.....Hali ya kuwa sio hivyo.......
 
Hivi kwamba wewe huoni namna wanavyotukana viongozi wa serikali na yeyote anayetofautiana nao ?

Viongozi wanaongia madarakani kwa njia za kishenzi ni haki yako kutukanwa. Tena inatakiwa ifikie hatua ya machafuko ili kurudisha heshima ya box la kura.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…