Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

hawezi kukuelewa hapa mkuu akili zao zimejaa mashindano wanataka kila kitu tufanye sawa
Wewe unaweza kutafuta pesa na huku unamsaidia mkeo kazi za nyumbani? Kama wewe hauwezi kwanini unataka yeye aweze?
 
Ndio as long as anafanya majukumu yake ya nyumban na ananieshimu kama mume sio alete propaganda zake za usawa kisa na yeye ana earn


Halafu nilichogundua wanawake nyie ni selfish kwahyo mkuu Siku mume akikwama kwa sababu imezoeleka sisi ndo watoaji kama hana huwez msaidia?
Wewe mke wako hata kama anatafuta pesa bado utamhudumia kama kawaida?
 
Nahisi nipo nje ya mada kidogo lakini sometimes wanawake tunajichanganya

Tunataka haki sawa kwa wote wakati huo huo tuna ile kauli mbiu yetu eti wanawake tukiwezeshwa tunaweza...SMH!😔😔

Kwanini tuhitaji kuwezeshwa wakati tuko na mikono na miguu miwili mixer ubongo kama wanaume
Watakutenga wenzio hizo akili za kiume 🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️
 
Kwa mwanamke kufanya kazi si lazima. Naweza kukustopisha na maswali sitaki.
Ila hali za sasa ndio kwa kiasi kikubwa huchangia haya yote.
Wote mna degree, pesa wote mnazo. Yaani automatically kuna ile akili huwaijia kuwa hanibabaishi(mwanamke ni chombo dhaifu). Hata kama haikuwa dhamira yako. Hapo ndipo kiburi huzaliwa na kujikuta unataka umpande.
Atakupanda kichwani kama hautimizi jukumu lako kwake mwanaume unatakiwa umhudumie mkeo hata kama ana pesa zake mnapoacha kuwahudumia wake zenu kwa kisingizio cha kuwa kila mtu ana pesa zake hapo ndipo mnapotengeneza usawa wenyewe ni lazima muonyeshe utofauti
 
So ulitakaje ss ikiwa Mungu alishawaumba Wanawake hivyo na kuwathibitishia watazaa kwa uchungu na watatawaliwa na Me daima na tamaa za Ke zitakuwa juu ya Me ilihali sisi Me tuliambiwa tule kwa jasho [emoji848]
Mbona kuna wanaume siku hizi hawali kwa jasho lao wanakula kwa jasho la wake zao hao nao unawaongeleaje?
 
But Edelyn, me sidhani kama hao wanaume wa kuachia mwanamke majukumu wapo wengi kiasi hicho. Na asilimia kubwa wanawake wanaopitia scenario za kulipia gharama za maisha bila msaada wa mwanamke huwa ni wale wanaochagua wanaume wa kuishi nao.

Ni mara chache sana mwanaume atakaye kufuata na kukutaka na kukuomba uwe wake atakutegemea wengi wanakuwa wapo tayari kukuhudumia na hata kama alikuwa hajiwezi ni rahisi sana kwake kuniongeza ili akufurahishe.

Golden rule ni mwanaume akuchague uwe wake, ila naona wadada wengi leo mnachagua wanaume wa kuwa nao az if mnachagua magari na mind you ukichagua mwanaume nakupa guarantee ni mara chache sana atakupambania maana wewe si chaguo lake ila ulikuwa available kwake na wanaume huwa hatuchagui chakula tunakula chochote kinachokatiza na kuzagaa mbele ya macho.
Sawa mkuu nimekuelewa.
 
Africa hatuna huo upumbavu bali yote hayo yameratibiwa na shetani kupitia Mawakala wake ughaibuni, ndiyomaana ss hv pamebakiwa na mvunjiko wa ndoa kwa kila mwaka ni zaidi ya 45%-67% hadi kuunda upya ndoa za mikataba.
Hapo nimeongelea mengi sasa ni upumbavu upi huo unaousemea kati ya hayo niliyoyaongelea? Au unasemea yote?
 
Me huwa nashangaa sana. Sababu hizi kelele zote huwa zinakuja kama watu wanaendekeza mashindano ya kitoto. Katika maisha ya ndoa kuna mambo mengi sana ya muhimu ya kufanya. Ukiona mwanamke unapata muda wa kurumbana na mume wako, na kufanya vituko, hebu jiulize ni nani anasimamia majukumu ya familia yaani household operations.... Na hilo ni jukumu kuu la mama.....

Ni sawa leo waziri mkuu atake kuwa sawa na raisi.... Haiwezekani in practicing ingawa ukiweka kinadharia inakuwa kama kweli.
Yes waziri mkuu hawezi kuwa sawa na rais kinafasi na kimajukumu pia na kumbuka rais ndo ana majukumu mengi kuliko waziri mkuu sasa inakuwaje ndoa za leo unakuta mwanamke ndo anafanya majukumu mengi kuliko mwanaume?
 
Hahahaha uko sawa mkuu hatupungukiwi kitu ila kwani na wanaume nao wakitafuta pesa na bado wakasaidia wake zao kazi za nyumbani wanapungukiwa kitu gani?
Utakapoingia maeneo ya kazi utajifunza kitu my dear. Wanawake wachache sana huwa kweli wamafikia hata 75% ya utendaji wa majukumu ya kazi bila msaada huko maofisini.

Pili, wanawake wanavyanzo vingi sana vya kupata pesa sababu wanadhamana ya miili yao katika utafutaji wa pesa. Ndo maaan hata hizi interviews siku hizi ni changamoto sana kwa mtoto wa kiume kupita.

Mwanamke anaweza pata msaada wa kifedha toka kwa baba, mama, kaka, dada, mjomba, bosi, marafiki, workmates na kadhalika ila trust me mwanaume nje ya kipato chake vyanzo vya kupata pesa ni vichache sana...... Na yeye hutoa zaidi.

Kwa kusema hivyo nataka kukujuza kuwa wanaume wanatafuta kwa jasho sana na kwasasa hali ni ngumu inazidi kuwabana wao zaidi kuliko wanawake.

Sasa huyu mtu ambaye anatakiwa kukaa chini kubuni vyanzo vipya vya mapato daily unataka tena akae na kuwaza vyombo havijaoshwa, sijafua nguo, usafi wa nyumba, sijakuna nazi, sijapika.

Aaaaaaah hebu kuwa serious kidogo..... Nadhani upo kinadharia zaidi.

Kimsingi wanaume wanaoa lengo kuu likiwa ni kupata usaidizi wa 100% wa majukumu ya kazi za ndani na mtu wa kumliwaza. Hiyo ya kutafuta pesa ni kiherehere chenu tu maana sidhani mwanaume anae jitambua atakaa kukushurutisha utafute kazi eti ulipie bili zote za nyumba ili hali yeye analala na kuamka na kukunja nne akitizama egoli kwenye tv. Hapo utakuwa umetunga uhalisia na si ukweli wa maisha halisi.....

So kama vipi naomba tuzungumze mambo practical katika jamii yetu na si maigizo.
 
Binadamu tumeshawekewa sheria na amri na Mungu aliyetuumba tuzifuate rejea maandiko usitake kuanza kutolea mifano ya wanyama kwa sababu tu inawafaidisha wanaume hilo siyo lengo la Mungu binadamu na wanyama ni aina mbili tofauti ya viumbe
Kuhusu maandiko mwanaume kaumbwa kutawala , mwanamke kma msaidizi t
Pia ukisem ufuate maandiko bas vitu vingi tumeenda kinyume na maandiko
 
Wanaume wa leo mnataka mpate wanawake wenye akili ya maisha na wanaojua kutafuta pesa ili wawasaidie katika kuhudumia watoto na mahitaji ya nyumbani lakini ninyi hamko tayari kusaidia kufanya kazi za ndani na kulea watoto sasa hapo hamuoni kuwa wanawake ndo wanakuwa wanafanya majukumu mengi kuliko wanaume? Kitu ambacho hakitakiwi maana mwanamke aliumbwa kama msaidizi tu kwa mwanaume
Tangu lini Msaidizi akadai haki sawa ili alingane na Me[emoji848]
 
Mpenzi, hivi umeshawahi jiuliza sehemu kubwa ya bajeti ya mwanamke kimatumizi huwa inaenda wapi?!
Kati ya watu wote walioniuliza maswali kwenye huu uzi wewe ndo umeuliza swali la msingi kuliko yote na ndo swali nililokuwa nalingojea haya ngoja nikujibu

Asilimia kubwa ya bajeti ya mwanamke inaenda kwenye matumizi yake binafsi kwa sababu tumeshaaminishwa kuwa jukumu la kutafuta pesa na kuhudumia familia ni la mwanaume

Na jukumu la kufanya kazi za ndani na kulea familia ni la mwanamke hivyo basi hata ikitokea mwanamke akitafuta pesa hatohudumia familia hiyo pesa itakuwa ya kwake binafsi

Kwa sababu hata kazi za ndani anafanya peke yake wakati mume wake anaweza kumsaidia hivyo tunarudi pale pale kuwa chanzo cha haya yote ni mgawanyo wa majukumu
 
Hivi akatokea kaka jambazi ghafla hapo unadhani nani atacheza nae twist?!

Je, mfano nyumba ni ya kupanga, unadhani nani kodi atalipia?!

Je wadhani asilimia kubwa ya mshahara wa mwanaume huenda wapi?!
Mimi nimemaanisha kwamba wanawake wanaostahili kusaidiwa kazi za nyumbani na waume zao ni wale ambao wanatafuta pesa na pesa zao zinachangia katika maendeleo ya familia na haziishii kwenye matumizi yao binafsi tofauti na hapo basi mke hastahili kusaidiwa majukumu yake na mume wake
 
Ngoja nikalewe Kwanzaa kisha nirudi..[emoji124] [emoji124] kweny huu uzi
 
Back
Top Bottom