#COVID19 Hizi chanjo za Corona zinaenda kuondoa herd immunity tuliyoipata nchini

#COVID19 Hizi chanjo za Corona zinaenda kuondoa herd immunity tuliyoipata nchini

Waacheni wenye taaluma za afya watuvushe kwenye janga hili.
Taaluma gani? Eti taaluma!!!

Wangekuwa wana taaluma ya kweli tungeona wanatengeneza chanjo zao badala ya kushabikia machanjo ya mabeberu!

Hii nchi haina wanasayansi, kuna makasuku tu wanaosubiri kusikia wazungu wanasema nini, basi na wao wanakuja mbio mbio kutudunga masindano.

Hawa wanasayansi uchwara hatupaswi kuwasikiliza. Hawana uhalali wa kitaaluma wa kusikilizwa.

Ni makasuku yasiyojitambua.
 
Ninachosikitika ni kuwa hizi chanjo ambazo baadhi ya watu watazipa zitaenda kuua herd immunity ambayo watanzania wengi kama sio wote nchini tulikuwa tumeipata.

Kwa wasiojua, herd immunity kwa lugha ya kawaida huitwa Kinga Kundi, hii ni aina ya kinga isiyo ya moja kwa moja (indirect immunity) dhidi ya ugonjwa inayotokea pale ambapo asilimia kubwa ya watu wana kinga dhidi ya ugonjwa husika iwe kwa njia ya maambukizo ya awali (kuugua kisha mwili ukatengeneza kinga).

Watanzania wengi sana kwa sasa korona kwao imekuwa ni kama ugonjwa wa mafua tu au uchovu kwa sababu miili yao imeishatengeneza kinga ya asili kutokana na kinga kundi(herd immunity). Wengi wanapoipata korona kwa sasa nchini wanapoteza uwezo wa kunusa na pia wanakosa hamu ya chakula na wanaharisha kidogo halafu baada ya siku kadhaa wanapona. Hii hali naamini inaenda kubadilika baada ya chanjo kuanza kutolewa nchini.

Kwa wasiojua ni kuwa kupata chanjo hakumzuii mtu aliyepata chanjo kupata korona lakini madhara yake ni kuwa, huyo aliyechanjwa halafu akapata korona, akimuambikiza mtu asiyechanjwa inakuwa ni korona hatari sana kwa aliyeambukizwa. Hii korona haikuchukui hata siku tatu unaondoka duniani kama hujawahi kupata matibabu haraka. Kibaya zaidi, hii korona inakula kidogo kidogo na inapofikia kwenye hatua za mwisho ndipo mtu unagundua pale unapokosa nguvu kwa ghafla.

Nchi nyingi za Afrika ambazo zilianza kutoa chanjo kwa wananchi wake zilijikuta ikiibuka korona nyingine kali iliyoshika kasi na watu kuanza kupoteza maisha ndio maana nchi hizo ziliamua kurudi tena kwenye lockdown.

Wachunguzi wanasema chimbuko la inayoitwa kwa kiingereza VARIANTS ni matokeo ya chanjo. Hata variants zinaibuka kutokana na aina ya chanjo zinazotolewa kwa watu wa eneo hilo. Mfano Saouth Afrika iliibuka variants inayoitwa BETA baada ya wananchi kuanza kupatiwa chanjo ya Johnson and Johnson vaccine. Mpaka leo Afrika Kusini wako katika hali tete.

Kuna watu ninajua watakuja na hoja wakisema, basi ni bora tupate chanjo wote ili variants isitokee. Watakaouliza maswali haya lazima wajue kuwa hizi chanjo zinazokuja kwa nchi zetu hizi za Afrika niza wanasiasa, maofisa waandamizi wa juu serikalini, wafanyakazi wa afya, matajiri na familia zao. Kama hauko kwenye kundi hili utasubiri kupata chanjo kwa muda mrefu sana wakati VARIANT ikifanya kazi zake nchini.

Kwa mfano, Kenya pamoja na kelele zao za kujikinga na korona toka waanze kutoa chanjo wametoa kwa asilimia 1.5 ya wananchi wake wote. Ukichunguza kundi lililopata hizo chanjo ndilo nililolitaja hapo juu!

Watanzania tuko karibia milioni 60 kwa sasa ambapo Sensa ya Watu na Makazi ilisema idadi ya watu nchini ambao wako katika kundi la kufanya kazi ni 53% na pia kundi la wazee ni 6%. Hii inatuambia kuwa watu wanaotakiwa kuchanjwa nchini ni kama 60% ya watanzania kwa sababu watoto hawachanjwi.

Kwa hesabu ya kawaida pale juu, idadi ya Watanzania wanapaswa kupata chanjo ni milioni 36. Batch ya kwanza ya Johnson and Johnson vaccine iliyoingia nchini ni dozi milioni 1 kwa watu milioni 1

Mungu ibariki Tanzania!
MsemajiUkweli ni nani aliyekufundisha hii sayansi ya kuwa mtu aliyechanja akipata korona na kuambukiza mtu mwingine ambaye hajachanjwa basi korona inakuwa ni ya hatari zaidi? Hakuna ukweli ukweli wowote kwenye hii ''sayansi'' yako. Inaonekana nyie ndiyo mlimwingiza chaka Magufuli (RIP) mara kabla hajafariki, mpaka akasema kuwa kuna watu walikwenda nje kuchanjwa na wameleta korona mbaya sana. Na suala la herd immunity... Magufuli binafsi alikataza hatua zozote kuchukuliwa na aka-declare kuwa Tanzania ni free from korona, lakini herd immunity ilikuwa haijafikiwa. Kufikia herd immunity inatakiwa japo asilimia 70 ya population iwe imeshaambukizwa virus! Mabadiliko ya msimamo wa serikali ya sasa yanonyesha kabisa suala la kukataa kukubali ukweli kuhusu korona ilikuwa ni msimamo binafsi wa Magufuli. Na pia inaonekana alichukuwa msimamo mbaya kabisa wa kutaka herd immunity ifikiwe kwa sababu ugonjwa wa korona ni mbaya sana na mpaka lengo la kinga-kundi ije kufikiwa, watakuwa wamefariki watu wengi. Na bahati mbaya zaidi msimamo wake potofu ukamrudia yeye na akawa victim wa jaribio la kutojali maisha ya watu ili kinga-kundi ifikiwe.
 
MsemajiUkweli ni nani aliyekufundisha hii sayansi ya kuwa mtu aliyechanja akipata korona na kuambukiza mtu mwingine ambaye hajachanjwa basi korona inakuwa ni ya hatari zaidi? Hakuna ukweli ukweli wowote kwenye hii ''sayansi'' yako. Inaonekana nyie ndiyo mlimwingiza chaka Magufuli (RIP) mara kabla hajafariki, mpaka akasema kuwa kuna watu walikwenda nje kuchanjwa na wameleta korona mbaya sana. Na suala la herd immunity... Magufuli binafsi alikataza hatua zozote kuchukuliwa na aka-declare kuwa Tanzania ni free from korona, lakini herd immunity ilikuwa haijafikiwa. Kufikia herd immunity inatakiwa japo asilimia 70 ya population iwe imeshaambukizwa virus! Mabadiliko ya msimamo wa serikali ya sasa yanonyesha kabisa suala la kukataa kukubali ukweli kuhusu korona ilikuwa ni msimamo binafsi wa Magufuli. Na pia inaonekana alichukuwa msimamo mbaya kabisa wa kutaka herd immunity ifikiwe kwa sababu ugonjwa wa korona ni mbaya sana na mpaka lengo la kinga-kundi ije kufikiwa, watakuwa wamefariki watu wengi. Na bahati mbaya zaidi lengo msimamo wake potofu ukamrudia yeye na akawa victim wa jaribio la kutojali maisha ya watu ili kinga-kundi ifikiwe.
Wewe acha ubishii. Hatutaki sayansi za kitapeli this time round.

Binadamu wote wana KINGA-ASILI za mwili. Kila kijidudu kinachovamia mwili kinashughulikiwa na kumalizwa na autoimmune system.

Kitendo cha watu kuambukizana corona kila mahali, kilifanya watanzania wote kujenga kinga ya asili ya mwili dhidi ya kijidudu huyo.

Ndio maana haukusikia vifo, kwa sababu miili yetu ilishajizatiti na kujilinda naturally.

Unapoenda kudunga watu machanjo ya hovyo hovyo unaharibu na kuvuruga kinga ya asili iliyokwisha kujitengeneza.

Matokeo yake ni kusababisha VIFO na autoimmune diseases.

Hiyo ndiyo SAYANSI YA KWELI, sio hizi habari za kitapeli za machanjo mnazotuambia.

Sayansi za kihuni tumeshazikataa hazina nafasi.
 
Wewe acha ubishii. Hatutaki sayansi za kitapeli this time round.

Binadamu wote wana KINGA-ASILI za mwili. Kila kijidudu kinachovamia mwili kinashughulikiwa na kumalizwa na autoimmune system.

Kitendo cha watu kuambukizana corona kila mahali, kilifanya watanzania wote kujenga kinga ya asili ya mwili dhidi ya kijidudu huyo.

Ndio maana haukusikia vifo, kwa sababu miili yetu ilishajizatiti na kujilinda naturally.

Unapoenda kudunga watu machanjo ya hovyo hovyo unaharibu na kuvuruga kinga ya asili iliyomwisha kujitengeneza.

Matokeo yake ni kusababisha VIFO na autoimmune disease.

Hiyo ndiyo SAYANSI YA KWELI, sio hizi habari za kitapeli za machanjo mnazotuambia.

Sayansi za kihuni tumeshazikataa hazina nafasi.
🤣 🤣 🤣 🤣Unatia huruma sana. Mbona watu hawajajenga kinga asili ya UKIMWI? Wewe kilaza usijujua hata kula balanced diet unabishana na sayansi ya wabobezi kutoka kila pande ya dunia? Nchi nyingine zote duniani ni wajinga na wabishi ndiyo maana wanakazana kuchanjwa raia wao ila wewe na watanzania wachache tu ndiyo werevu. Anyways kusikia ujinga kama huu siyo uncommon sana kwenye jamii dumavu.
 
Mbona watu hawajajenga kinga asili ya UKIMWI?

Hata maana ya UKIMWI tu hujui, ukielezwa habari za autoimmune utaelewa wewe ngumbaru?

Wewe ndio aina ya madokta uchwara ninaowatafuta mitandaoni ili nipambane nao KWERIII KWERII.

Zile habari za kuwalisha watu matango pori siku hizi hakuna. Watanzania wameelimika na wanajitambua.

Ndio maana nina uwezo wa kukukosoa wewe tapeli mshamba usiyejua hata maana ya UKIMWI lakini unashabikia watu wadungwe machanjo ya hovyo hovyo!

Huna ufahamu hata wa Basics tu za VVU Vs UKIMWI, lakini na wewe unajiita mjuzi!

Tena si ajabu kuna mahali wanakuita virologist [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hata maana ya UKIMWI tu hujui, ukielezwa habari za autoimmune utaelewa wewe ngumbaru?

Wewe ndio aina ya madokta uchwara ninaowatafuta mitandaoni ili nipambane nao KWERIII KWERII.

Zile habari za kuwalisha watu matango pori siku hizi hakuna. Watanzania wameelimika na wanajitambua.

Ndio maana nina uwezo wa kukukosoa wewe tapeli mshamba usiyejua hata maana ya UKIMWI lakini unashabikia watu wadungwe machanjo ya hovyo hovyo!

Huna ufahamu hata wa Basics tu za VVU Vs UKIMWI, lakini na wewe unajiita mjuzi!

Tena si ajabu kuna mahali wanakuita virologist [emoji23][emoji23][emoji23]
🤣 🤣 🤣 🤣Du. Kweli awamu ya tano ilitutengenezea ''wataalam''.
 
Hakuna cha ajabu. Tunachanja dhidi ya TB, na kila mwaka kuna watu wanakufa kwa TB. Tuna dawa nyingi za kutibu malaria, lakini kila mwaka maelfu hufa kwa malaria hata baada ya kupata tiba.

Kwa upande mwingine, kama mtu ana akili, ajiulize ni wangapi wangekufa kama watu wasingechanjwa dhidi ya TB, au ni wangapi wangekufa kama kusingekuwa na dawa za kutibu malaria? Hiyo herd immunity ifanye kazi kwa corona pekee lakini isifanye kazi kwenye malaria, TB, malaria, surua, dysentry, typhoid, etc. Ni ajabu!!

Mtu anaongelea herd immunity akiwa kwenye dirisha la dawa akinunua dawa yamalaria! Unafiki wa hali yajuu.
 
MsemajiUkweli ni nani aliyekufundisha hii sayansi ya kuwa mtu aliyechanja akipata korona na kuambukiza mtu mwingine ambaye hajachanjwa basi korona inakuwa ni ya hatari zaidi? Hakuna ukweli ukweli wowote kwenye hii ''sayansi'' yako. Inaonekana nyie ndiyo mlimwingiza chaka Magufuli (RIP) mara kabla hajafariki, mpaka akasema kuwa kuna watu walikwenda nje kuchanjwa na wameleta korona mbaya sana. Na suala la herd immunity... Magufuli binafsi alikataza hatua zozote kuchukuliwa na aka-declare kuwa Tanzania ni free from korona, lakini herd immunity ilikuwa haijafikiwa. Kufikia herd immunity inatakiwa japo asilimia 70 ya population iwe imeshaambukizwa virus! Mabadiliko ya msimamo wa serikali ya sasa yanonyesha kabisa suala la kukataa kukubali ukweli kuhusu korona ilikuwa ni msimamo binafsi wa Magufuli. Na pia inaonekana alichukuwa msimamo mbaya kabisa wa kutaka herd immunity ifikiwe kwa sababu ugonjwa wa korona ni mbaya sana na mpaka lengo la kinga-kundi ije kufikiwa, watakuwa wamefariki watu wengi. Na bahati mbaya zaidi msimamo wake potofu ukamrudia yeye na akawa victim wa jaribio la kutojali maisha ya watu ili kinga-kundi ifikiwe.
macho_mdiliko Nayaheshimu mawazo yako lakini nakubali kutokubaliana.

Kwa nchi kama Tanzania huhitaji kufikia asilimia 70 ya watu ili kutengeneza Kinga Kundi.

Sidhani kama katika analysis yako umeangalia kuwa nchini kuna asilimia 6 tu ya wazee lakini kundi lingine nila vijana ambao kwao korona haiwaathiri kama wazee kutokana na lifestyle ya kutafuta maisha na vyakula vya asili.

Hata hili kundi la wazee wengi immune system zao ni nzuri sana kwa sababu wanakula vyakula ambavyo nivya asili kwa sababu wengi wanakaa vijijini. Ndio maana korona haijaathiri sana nchi za Afrika kama ambavyo ilitegemewa.

Afrika Kusini wanaathirika sana na korona kwa sababu immune system yao ni ndogo kutokana na maisha yao ambayo kwa kiwango kikubwa yanategemea vyakula vya kwenye supermaket ambavyo sio asili lakini pia wananchi wake wengi wana magonjwa mbali mbali kama ukimwi na kisukali kutokana na maumbo yao ya mwili kuwa makubwa(unene).
 
Unabisha nini we ng'ombe???

Machanjo yanaenda kuharibu kinga asili ya mwili. Huo ndio ukweli.

Mungu alituumba akatuwekea kinga asili za mwili ambazo zinajitosheleza.

Kitendo cha kudunga watu machanjo ya hovyo hovyo kinaweza kuzi corrupt Kinga asili za mwili na kusababisha autoimmune disease!

BISHA, ewe dokta uchwara!
Kuna Makopo mengi sana humu JF siku hizi..
Sasa kama kuna kinga za asili kwanini watu wanapewa Vitamins za viwandani ili wanywe?! Hao nazo ni sumu za Wazungu za kuwaua nyie Makapuku!
Na huo mwili wako hauna kinga za kudungwa hospitali utotoni?!
Ebu jadili na wengine huko...
 
Watu hamna ujuzi wa jinsi ugonjwa ulivyo mnaongea kutokana na maneno ya vijiwen, niko mkoan uku watu wanakufa sabna kwa dalili hizo za Covid wengi sana af unasema itatokea kali zaid, kwetu vijana haina shida ila kwa wazee unashauri iweje labda,
Hapo nahis ata ujui chanjo zinavyofanyaga kaz
Hiyo chanjo unadhani itakufikia kesho? Chanjo kukufikia huko kijijini ni baada ya miaka zaidi ya miwili!
 
Waliosomea wakianza kuchangia waanzie na kuweka vyeti vya taaluma yao? Hivi ndivyo akili yako inamaanisha.
Kama una swali uliza kama hujaelewa acha kuuliza taaluma
Nashukuru kwa kunisaidia kumuelimisha zaidi.
 
Hayati Anne Mughwira aliugua kupitia hiyohyo Heard Immunity akaja kuugua tena na kirusi kimeshabadilika na safari hii kikamchukua forever

Watu wenye umri mkubwa na wenye magonjwa sugu hata kama walishaugua covid huko nyuma waende kwenye chanjo

Heard Immunity ilishafeli huko Sweden na wameanza kudunga Chanjo Raia wao.
Kwani watu wote wanaofariki wanafariki kwa sababu hakuna dawa za kuwatibu? Hoja yako niya kitoto/mufilisi!

Kuwa na herd immunity hakuzuii baadhi ya watu kufariki kwa korona kama ilivyo kuwa na madawa ya kutibu ugonjwa fulani haizuii baadhi ya watu kufa kwa ugonjwa huo.
 
Awamu ya 5 ilizalisha, na kuchochea kuongezeka kwa watu wasiyo na maarifa na wasiotaka kutumia taaluma zao au akili zao kutatua changamoto zao
Wewe unayetumia ''taaluma yako'' umetatua changamoto zote na kufanikiwa au ndio wale wale?
 
Back
Top Bottom