#COVID19 Hizi chanjo za Corona zinaenda kuondoa herd immunity tuliyoipata nchini

#COVID19 Hizi chanjo za Corona zinaenda kuondoa herd immunity tuliyoipata nchini

Una taaluma yoyote ya Afya au ndio ukishakuwa na bundle, smartphone na vidole, umeshajua kila kitu.
Hawa
Una talamu yoyote inayohusu mambo ya chanjo ?? Au unaongea tu kwa mihemko ,ni heri haya mambo wakaongea wanaosemea fani husika ,kuliko kuleta porojo kwenye mambo ya maana,kwan mzungu akitaka kukuua lazima ahangaike na chanjo zipo ,njia nyingi za kukuondoa tuache fikra za ukale hivi elimu tunazoma zinatusaidia nini???

sent from HUAWEI
Hawa ndio wale wale wenye shahada za udakitari kutoka kanisa la Uamsho. Mkufunzi wao ni lile tapeli lililokubuhu
 
Hujui kama aliyepata chanjo haimzuii kupata korona.

Hujui kuwa aliyepata chanjo akipata korona anaweza kuambukiza wengine hata waliopata tena chanjo.

Huu mnyororo wa maambukizo ndio unazaa korona kali inayoitwa VARIANTS.
Sasa kwa vipi herd immunity inapungua hapo?......How Vaccine affect infectivity & fatality of infectious disease?
 
Watu wanakufa wewe unaleta habari za kinga za makundi.

Kwanza umesoma PCB,CBG ama PCM?

Unaelewa molecular biology? Kaa utulie mzee.

Mbona husemi kama wote wakipata chanjo inakuwaje.

Kula dozi mzee tusije tukakupoteza member wetu humu jamvini.
Umeandika ''Mbona husemi kama wote wakipata chanjo inakuwaje''

Hizo chanjo za kupata wote utazitoa wapi na lini?

Dar es Salaam pekee inahitaji dozi milioni 3 na laki 6 wakati zilizoletwa ni dozi milini 1. Hatujui lini tutapata tena batch nyingine!

Acha kujipa matumaini hewa!
 
Mwandishi hajui anacho ongea vizuri. herd immunity hii ni kwa wale waliopata Corona na kupona lakini imeonyesha kukupa kinga kwa miezi miwili tu. Tumeshaona Mama Mwingira alipata Corona mara ya kwanza mwaka jana lakini kapata tena mwaka huu na kwasasa amefariki. Lakini virus wanazidi kupata nguvu kama ulipona haina maana virus akibadilika utapona tena.

Lakini swala lingine Chanjo ni njia mojawapo ya kupata immunity lakini tofauti na ile ya kuumwa mwili wako unakuwa salama. Unaweza kuumwa na kupona Corona lakini ikawa imekuachia matatizo mengine mengi kama ya moyo , figo na mapafu.
Nimesema kwenye mada unapopata herd immunity nchini unakuwa katika mazingira ambayo korona ikikupata inakuwa kama ugonjwa ma mafua tu. ndicho kilichokuwa kinawatokea watanzania wengi kwa sasa.

Herd immunity tuliyoipata watanzania wengi kwa sasa, mtu anapata korona, anajisikia kuchoka kidogo, anakosa hamu ya kula na kunusa baada ya siku kadhaa anapona na kuendelea na kazi zake.
 
AAnnataka
Ninachosikitika ni kuwa hizi chanjo ambazo baadhi ya watu watazipa nchi zitaenda kuua herd immunity ambayo watanzania wengi kama sio wote nchini tulikuwa tumeipata kwa muda wa takribani miaka miwili.

Kwa wasiojua, herd immunity kwa lugha ya kawaida huitwa Kinga Kundi, hii ni aina ya kinga isiyo ya moja kwa moja (indirect immunity) dhidi ya ugonjwa inayotokea pale ambapo asilimia kubwa ya watu wana kinga dhidi ya ugonjwa husika iwe kwa njia ya maambukizo ya awali (kuugua kisha mwili ukatengeneza kinga).

Watanzania wengi sana kwa sasa korona kwao imekuwa ni kama ugonjwa wa mafua tu au uchovu kwa sababu miili yao imeishatengeneza kinga ya asili kutokana na kinga kundi(herd immunity). Wengi wanapoipata korona kwa sasa nchini wanapoteza uwezo wa kunusa na pia wanakosa hamu ya chakula na wanaharisha kidogo halafu baada ya siku kadhaa wanapona. Hii hali naamini inaenda kubadilika baada ya chanjo kuanza kutolewa nchini.

Kwa wasiojua ni kuwa kupata chanjo hakumzuii mtu aliyepata chanjo kupata korona lakini madhara yake ni kuwa, huyo aliyechanjwa halafu akapata korona, akimuambikiza mtu asiyechanjwa inakuwa ni korona hatari sana kwa aliyeambukizwa. Hii korona haikuchukui hata siku tatu unaondoka duniani kama hujawahi kupata matibabu haraka. Kibaya zaidi, hii korona inakula kidogo kidogo na inapofikia kwenye hatua za mwisho ndipo mtu unagundua pale unapokosa nguvu kwa ghafla.

Nchi nyingi za Afrika ambazo zilianza kutoa chanjo kwa wananchi wake zilijikuta ikiibuka korona nyingine kali iliyoshika kasi na watu kuanza kupoteza maisha ndio maana nchi hizo ziliamua kurudi tena kwenye lockdown.

Wachunguzi wanasema chimbuko la inayoitwa kwa kiingereza VARIANTS ni matokeo ya chanjo. Hata variants zinaibuka kutokana na aina ya chanjo zinazotolewa kwa watu wa eneo hilo. Mfano Saouth Afrika iliibuka variants inayoitwa BETA baada ya wananchi kuanza kupatiwa chanjo ya Johnson and Johnson vaccine. Mpaka leo Afrika Kusini wako katika hali tete.

Kuna watu ninajua watakuja na hoja wakisema, basi ni bora tupate chanjo wote ili variants isitokee. Watakaouliza maswali haya lazima wajue kuwa hizi chanjo zinazokuja kwa nchi zetu hizi za Afrika niza wanasiasa, maofisa waandamizi wa juu serikalini, wafanyakazi wa afya, matajiri na familia zao. Kama hauko kwenye kundi hili utasubiri kupata chanjo kwa muda mrefu sana wakati VARIANT ikifanya kazi zake nchini.

Kwa mfano, Kenya pamoja na kelele zao za kujikinga na korona toka waanze kutoa chanjo wametoa kwa asilimia 1.5 ya wananchi wake wote. Ukichunguza kundi lililopata hizo chanjo ndilo nililolitaja hapo juu!

Watanzania tuko karibia milioni 60 kwa sasa ambapo Sensa ya Watu na Makazi ilisema idadi ya watu nchini ambao wako katika kundi la kufanya kazi ni 53% na pia kundi la wazee ni 6%. Hii inatuambia kuwa watu wanaotakiwa kuchanjwa nchini ni kama 60% ya watanzania kwa sababu watoto hawachanjwi.

Kwa hesabu ya kawaida pale juu, idadi ya Watanzania wanapaswa kupata chanjo ni milioni 36. Batch ya kwanza ya Johnson and Johnson vaccine iliyoingia nchini ni dozi milioni 1 kwa watu milioni 1

Population ya Dar es Salaam pekee ni watu karibia milioni 6 ambapo asilimia 60 ya wanaohitaji chanjo ni watu milioni 3 na laki 6. Hapo hujagusa mikoa mingine!

Mtu yuko kijijini eti unamsikia anasema twende tukachanje, hiyo chanjo utaipata wapi? Mpaka ukifikie ni majaliwa zaidi zaidi kama una bahati mbaya utafikiwa na mtu aliyechanjwa na kupata tena korona ambaye anakuja kueneza korona kali zaidi.

Mungu ibariki Tanzania!
Kwanza thibitisha uwepo wa hiyo herd immunity miongini mwa wana jamii.
 
watu wanaokaa vijijin na kula vyakula vya asili mara nying huwa hawasumbuliw sana na magonjwa na ata wakisumbuliwa na magonjwa hasa kama haya jamii ya mafua huwa wanapona haraka sana ila sisi wa mjin mafua tunatafuta madawa na tunajikuta mara kwa mara tunaumwa so najaribu kurelate na hii.

- Mazao ambayo hayapigw dawa huwa yanakuwa mazur sana ila siku unapoanza tu kupiga insectcides or fungicides ndo tatizo inapoanza hapo unakuta mara kwa mara zao limevamiwa nayo najaribu tu kurelate...

#Take at your own risk.
Umeandika maelezo mafupi lakini hoja yako niya msingi sana lakini pia ndio ukweli halisi.
 
Wakati dunia imechanganyikiwa na kujifungia ndani, mtaalam JPM hakuangaika na hizo njia. Alishauri watu wapige nyungu, wale matunda, tangawizi na malimao, kisha maisha yaendelee!

Dunia na waliokuwa wanampinga walivyoona mwingiliano kama ule wa kwenye mwendokasi na viwanjani, walipiga kelele na kusema watanzania watakufa kwa mamilioni. Lakini cha ajabu na hasa baada ya kuondolewa woga, watz waliendelea na maisha kama kawaida.

Tukiacha unafiki na kishikiliwa akili na wazungu, Tz tumeshapata somo kubwa kuhusu korona. Imewezekana na maisha yameendelea kama kawaida bila kuwa “wafungwa wa korona“ . Lakini tumeshindwa kujifunza kwenye uzoefu wetu wenyewe! Tunasubiri mpaka mzungu aseme, ndiyo tutajifanya waelewa kwa ku quote alochoongea mzungu!
Nakubaliana na angalizo lako!

Haishangazi kuona watanzania wengi wakihojiwa hawataki kusikia maneno yanayosema ''korona ni hatari''!
 
Tamko la kijinga kabisa limekwepa maswali ya msingi
1. Afrika ni nchi ipi iliyofanikiwa baada ya kuchanja?

2. Ni kwa nini tupewe chanjo na wazungu waliokufa sana na corona wakati sisi hatujaarithiriwa kihivyo
Haya ni maswali muhimu sana!
 
Kaka mbona unajidili mambo ambayo huelewi???
Ulisema : "Wachunguzi wanasema chimbuko la inayoitwa kwa kiingereza VARIANTS ni matokeo ya chanjo." -
Hebu tuambie: Mchunguzi gani?? Lini?? Wapi??? Taja chanzo!!!

Mabadiliko ya virusi SI TOKEO YA CHANJO. Kila virusi inaendelea kubadilika. Mfano virusi za Korona aina ya influenza (ni aina ya Korona pia) huathiri hasa nchi za kaskazini kila majira ya baridi. Wamebuni chanjo lakini wanahitaji kbadilisha chanjo kila baada ya miaka kadhaa kwa sababu virusi inabadilika. Virusi isiyobadilika haina uwezo wa kuruka kutoka wanyama (kama COVID) kustawi kwenye watu.

Acha kupiga makelele kwa kutumia maneno ambayo huelewi. Tafadhali!
Kaka unashindwa hata kuelewa mantiki ndogo tu kwenye mada yangu!

Kama tunakubaliana mtu aliyechanjwa anaweza kupata tena korona na kuambukiza. Kama ndivyo, sijui hata unachotaka kujua zaidi ni nini wakati maelezo yako yanakubaliana na hoja yangu ya msingi!
 
Glass ya uelewa wako wa herd immunity bado haijajaa. Herd immunity inapatikana kwa moja (au combination) ya njia mbili: (1) previous infections and/or (2) through vaccination!
Unaweza kuijaza glass yangu ili iwe na uelewa unaodhani unahitajika!
 
Watu kama wewe ndio mnapaswa kuwekwa sabasaba kwenye maonyesho ya wanyama. Banda #11 linakufaa zaidi.
Hapo ulipo hujagundua hata kiberiti lakini unataka kushindana na wanasayansi
 
Mkuu kuhusu chanjo tangu uzaliwe umechanjwa chanjo ya surua, pepopunda, usubi mpaka umefika umri huo umepata madhara gani na pia usitolee majibu ya moja kwa moja taarifa ambazo umezipata mitandaoni pasipo fanya uchunguzi hayo majibu yanapatikana maabara za uchunguzi wa dawa na tiba.
Hoja ya msingi sio kupewa chanjo bali ni kupewa chanjo ya mwendokasi ambayo madhara yake ya muda mrefu hayajulikani lakini madhara ya muda mfupi ni pamoja na kuibuka kwa korona kali baada ya jamii kuanza kuchanjwa!
 
Kwa taarifa yako👇👇
Chanjo za corona ZITAONGEZA Herd immunity...The higher the level of immunity, the larger the benefit. This is why it is important to get as many people as possible vaccinated.
Yaani unategemea upewe ''misaada'' ya chanjo ya korona halafu unasema ''it's important to get as many people as possible vaccinated''. Are you kidding me?

Kumbuka Tanzania ina watu milioni 36 wanaohitaji kupata chanjo ya korona wakati ''msaada'' wa chanjo ya korona tuliopata mpaka sasa ni kwa watu milioni 1. Hatujui huo ''msaada'' mwingine utakuja lini na kiasi gani!
 
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787]Du. Kweli awamu ya tano ilitutengenezea ''wataalam''.
Dokta uchwara huna hoja, umebaki na viroja,

Sayansi zako kanjanja, zimejaa janja janja,

Watu wote kwa pamoja, wamesusa zako hoja.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom