Hizi hapa Nauli Mpya za SGR: Dar - Moro Tsh. 13,000, Dar - Dodoma Tsh. 31,000

Hizi hapa Nauli Mpya za SGR: Dar - Moro Tsh. 13,000, Dar - Dodoma Tsh. 31,000

Kabisa, wawekwe watu wa kutosha kufanya usafi wa hali ya juu, na sheria ziwe kali kukomesha watakaofanya uharibifu, makelele na uchafu, security wa kutosha waliopewa training ya hali ya juu waajiriwe wa kutosha na fine ziwe zinazidi nauli kukomesha wahuni na waharibifu
👍
 
Wao Trc walipendekeza nauli iwe sh ngapi?
Ila walau wengefanya 45000 Dar-MAKUTUPORA,maana siyo Dodoma mjini ni mpaka Makutupora.
Makutupora ni mbali kutoka Dodoma,ni karibu kabisa na kupanda mlima Saranda.
 
Wao Trc walipendekeza nauli iwe sh ngapi?
Ila walau wengefanya 45000 Dar-MAKUTUPORA,maana siyo Dodoma mjini ni mpaka Makutupora.
Makutupora ni mbali kutoka Dodoma,ni karibu kabisa na kupanda mlima Saranda.
Dom had makutupora haizidi 30 km na hesabu za latra kwa km ni 69.51 hivyo hapo haizidi 2000
 
Hii Treni itafeli haraka sana
1. Bei hazikuzingatia gharama za soko. Kutoka Pugu hadi Dar ni '' senti 30 dollar'' not realistic
2. Bei zimepangwa kisiasa na si kiuchumi
3. Treni ilitakiwa isimame katika vituo ya Ruvu, Morogoro, Kilosa, Dodoma. Hivyo vingine viachwe kwa ''ya Mwakyembe''
4. Ubora wa Treni utakwisha katika miezi si zaidi ya 3 na '' maintanance '' itaanza mapema sana, hasara itafuata

Biashara inaongozwa na soko na si siasa. Hii imeshafeli

JokaKuu
 
Hongera kwa serikali kwani nauli zipo vizuri na zimepokelewa vema. Mwongozo wa kudhibiti huduma na Serikali kupata mapato ni mzuri.

Ishukubwa ni kusimamia huduma kwenye hili eneo pasiwepo na kuchekeana wala kujuana. Serekali imewekeza fedha nyingi lazima watendaji waelimishwe vya kutosha.

Pia kuwe na vipindi vya TV na redio kuwaelimisha abiria. Sio abiria kupanda na mbuzi na bata kwenye treni.

Pia mifumo ifanye kazi ya kuzuia hujuma yoyote inayoweza kujitokeza. Taratibu zinazotumika airport zitumike kwenye hizi treni.


Hongera TRC Hongera Serikali. Nasubiri safari ya kwanza.
 
Treni moja Ila mabehewa ndiyo Yana daraja mjumbe
Nazungumzia treni express na ya kawaida. Express haiwezi kusimama Pugu labda Morogoro tu then Dodoma. So far mabehewa waliyoleta yote yako sawa.
 
Waweke na nauli kwa daraja lisilo la kawaida tuone.
 
Tikiti siyo za dirishani unakata mwenyewe kupitia simu yako, jitahidi uwe unasafiri kwa mabasi hata kama hauna kwenu mikoani ujue jinsi ya kukata tikiti kupitia simu yako.
nitashangaa sana kama Trc watauza hizo ticket manual, maana hadi mabasi siku hizi ticket tunakata online.
Maana yake abiria watakuwa wengi kuliko nafasi. Nauli rafiki sana ingawa bus iko chini kidogo.
 
Zimekaa poa kwetu na kwa mujibu wa latra, ila Sidhani kama ni rafiki kwa Trc., proposal yao ya nauli ilikuwa juu mno na nina wasiwasi wakitumia hizi nauli za latra moja ya tatizo litakaliwakumba litakuwa ni huduma mbovu.
Mwendokasi walipendekeza nauli yao iwe 1,200/- wakapangiwa 650/- kilichotokea zimekuwa hovyo kuliko daladala. Hawa pia wamepangiwa nauli za chini itakuwa kama mwendokasi. Wataanza vizuri sana ila baadae itakuwa kama treni la Kigoma.
 
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) inawatangazia taarifa ya maamuzi ya Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini kuhusu nauli za abiria wa daraja la kawaida kwa Treni ya Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Makutupora.

Nauli hizi ni baada ya kufanyia kazi maombi yaliyoletwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) na taarifa zilizopokelewa kutoka TRC na wadau wengine.

Kuelekea kuanza kwa safari za SGR Dar es Salaam mpaka Makutupora, masharti ya kuzingatia kabla ya kuanza kutumika kwa nauli hizi ni kama ifuatavyo:

(i) Mtoa huduma (TRC) kuwa na leseni ya usafirishaji:
(ii) Kuwa na ithibati ya usalama wa miundombinu ya reli na mabehewa;
(iii) Kutumia mfumo wa utoaji wa tiketi za kielekroniki;
(iv) Kuunganisha mfumo wa tiketi za kieletroniki na mifumo ya LATRA;
(v) Kukokotoa malipo na utunzaji taarifa za abiria, nauli iliyolipwa, tiketi za kielektroniki zilizotolewa, kodi za Serikali na tozo za kisheria; na,
(vi) Kuwa na watumishi wa kada muhimu kwa masuala ya ufundi na uendeshaji wa treni ya SGR ikiwa ni pamoja na madereva waliothibitishwa na wahudumu waliosajiliwa na LATRA.

Aidha, nauli hizi ni kwa daraja la kawaida kwa watu wazima na watoto kuanzia umri wa miaka 4 hadi 12 ambapo nauli zitalipwa na abiria kwa kilomita. Nauli itakayolipwa na mtu mzima na mtoto mwenye umri zaidi ya miaka 12 ni TSH. 69.51 kwa kilomita, na mtoto kuanzia kuanzia miaka 4 hadi 12 atalipia TSH 34.76 kwa kilomita. Aidha mtoto mwenye umri chini ya miaka minne (4) hatalipa nauli, hata hivyo, taarifa zao na wasafiri wote zitatunzwa kwenye mfumo wa taarifa za abiria wanaosafiri kila siku.


View attachment 3014035
View attachment 3014036
View attachment 3014037
Kwa nauli hizo lazima shirika life.
 
Wote wa madaraja tofauti si mnavutwa na kichwa kimoja, kikisimama mnasimama wote?
Kuna express na ya kawaida inayosimama kila kituo. Ukiwa na tiketi ya kawaida huwezi kupanda express.
Kuhusu madaraja hili la kawaida huwa inakuwa daraja moja. Ila express kuna madaraja tofauti na nauli tofauti. Nauli ya chini kabisa inazidi ile ya treni ya kawaida.
 
Back
Top Bottom