Hizi hapa Nauli Mpya za SGR: Dar - Moro Tsh. 13,000, Dar - Dodoma Tsh. 31,000

Hizi hapa Nauli Mpya za SGR: Dar - Moro Tsh. 13,000, Dar - Dodoma Tsh. 31,000

Hiyo treni ina sehemu ya kubebea kuku na viazi?
Huko kwenye hizo bei lazima ukutane na huo ujinga.

Kwanza treni nzuri inayokupa fursa ya ku enjoy safari ni Tazara huko kwingine ni kama unataka kufika haraka tuu nothing else but itawasaidia watu maskini ingawa sijui kama watapata faida
 
Zimekaa poa kwetu na kwa mujibu wa latra, ila Sidhani kama ni rafiki kwa Trc., proposal yao ya nauli ilikuwa juu mno na nina wasiwasi wakitumia hizi nauli za latra moja ya tatizo litakaliwakumba litakuwa ni huduma mbovu.
Ndio maana nimesema kupelekea uchaguzi Serikali itabeba hasara ila baada ya uchaguzi Mkuu zikiendekea hizo nauli ,shirika litakufa fasta
 
Mwendokasi walipendekeza nauli yao iwe 1,200/- wakapangiwa 650/- kilichotokea zimekuwa hovyo kuliko daladala. Hawa pia wamepangiwa nauli za chini itakuwa kama mwendokasi. Wataanza vizuri sana ila baadae itakuwa kama treni la Kigoma.
When politics interfere technical matters, hicho unachokiongea ndio exactly kimetokea mwendokasi na kitatokea huku Trc, ni swala la muda tu.
Miradi mingi ya serikali kama ingeangaliwa kwa jicho la kiufundi ilikuwa hakuna haja ya kuianzisha, yote itakufa kibudu. Huku ikiwa imetutia hasara walipakodi.
 
Nauli nzuri mno, mimi napenda watuambie safari ngapi kwa siku! Tunataka asubuhi tuwe tunaenda Dom , mchana tunakula bata kisha usiku saa 6 tupande treni ya express kurudi Dar. Treni za kusimama kila kijiji hatupendi, wengine tumezaliwa town huwa tunaboreka sana kutuweka bush masaa kadhaa.
Pole, Dar to Dom itatumia saa 14
 
Serikali kwenye sekta ya biashara hawajawahi kufanya vizuri.

Anyway, naskia safari zinaanza mwakani 😎
 
Ksbls ys yote semina elekezi itolewe watu wataanza kuchafua kukojoa na haja kubwa hovyohovyo mabehewa yakaanza kunuka
Ustarabu huwa haufundishwi bali na makuzi anayokuwa nayo mtu toka utotoni!! Ndio maana usafiri kama wa ndege ningumu kukuta vitu vya ajabu ajabu kwani wanaoutumia wengi ni wastarabu. Nenda kwenye treni /mabasi ya kigoma ni aibu tupu.
 
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) inawatangazia taarifa ya maamuzi ya Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini kuhusu nauli za abiria wa daraja la kawaida kwa Treni ya Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Makutupora.

Nauli hizi ni baada ya kufanyia kazi maombi yaliyoletwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) na taarifa zilizopokelewa kutoka TRC na wadau wengine.

Kuelekea kuanza kwa safari za SGR Dar es Salaam mpaka Makutupora, masharti ya kuzingatia kabla ya kuanza kutumika kwa nauli hizi ni kama ifuatavyo:

(i) Mtoa huduma (TRC) kuwa na leseni ya usafirishaji:
(ii) Kuwa na ithibati ya usalama wa miundombinu ya reli na mabehewa;
(iii) Kutumia mfumo wa utoaji wa tiketi za kielekroniki;
(iv) Kuunganisha mfumo wa tiketi za kieletroniki na mifumo ya LATRA;
(v) Kukokotoa malipo na utunzaji taarifa za abiria, nauli iliyolipwa, tiketi za kielektroniki zilizotolewa, kodi za Serikali na tozo za kisheria; na,
(vi) Kuwa na watumishi wa kada muhimu kwa masuala ya ufundi na uendeshaji wa treni ya SGR ikiwa ni pamoja na madereva waliothibitishwa na wahudumu waliosajiliwa na LATRA.

Aidha, nauli hizi ni kwa daraja la kawaida kwa watu wazima na watoto kuanzia umri wa miaka 4 hadi 12 ambapo nauli zitalipwa na abiria kwa kilomita. Nauli itakayolipwa na mtu mzima na mtoto mwenye umri zaidi ya miaka 12 ni TSH. 69.51 kwa kilomita, na mtoto kuanzia kuanzia miaka 4 hadi 12 atalipia TSH 34.76 kwa kilomita. Aidha mtoto mwenye umri chini ya miaka minne (4) hatalipa nauli, hata hivyo, taarifa zao na wasafiri wote zitatunzwa kwenye mfumo wa taarifa za abiria wanaosafiri kila siku.


View attachment 3014035
View attachment 3014036
View attachment 3014037
Kongole..Bei ni Rafiki sana...Tunaomba hii kitu ipite nchi nzima kwa sasa tunabaguliwa watu wa mikoani !!
 
Mabasi biashara haiwezi doda labda kwa ambao hamjui ubovu wa kila biashara ya serikali. Tuombe uzima turudi hapa baada ya mwaka useme mabasi yalivyododa. Haitokaa itokee.

Watakuwa wanakula hasara, baadhi ya miundombinu itakufa mapema sana na hawatofanya matengenezo haraka, ratiba zitakuwa hazieleweki, wabongo wataleta umaskini kwenye hizo treni kisa ni za umma. Serikali ilete uswahili kwenye ndege sembuse treni
mwanzoni biashara ya serikali inakuwa nzuri ila ikitokea taa ya ndani ya behewa imeharibika au hata siti kuharibika itabaki hivyo hivyo na hapo ndio utajua kwanini serikali ni zero kwenye biashara. Check mabasi ya udart magari machafu utadhani hakuna maji Dar. Viti vimeharibika na camera zile zinaning'inia hadi unajiuliza hela za mradi ule zinaenda wapi ikiwa hawawezi hata kukarabati gari.

Serikali pamoja na wasomi wake wote wakipewa kampuni ya mabasi kama ya Shabiby hawataweza kuiendesha kwa faida na mabasi yakawa katika hali bora kama yanavyoonekana barabarani.
 
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) inawatangazia taarifa ya maamuzi ya Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini kuhusu nauli za abiria wa daraja la kawaida kwa Treni ya Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Makutupora.

Nauli hizi ni baada ya kufanyia kazi maombi yaliyoletwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) na taarifa zilizopokelewa kutoka TRC na wadau wengine.

Kuelekea kuanza kwa safari za SGR Dar es Salaam mpaka Makutupora, masharti ya kuzingatia kabla ya kuanza kutumika kwa nauli hizi ni kama ifuatavyo:

(i) Mtoa huduma (TRC) kuwa na leseni ya usafirishaji:
(ii) Kuwa na ithibati ya usalama wa miundombinu ya reli na mabehewa;
(iii) Kutumia mfumo wa utoaji wa tiketi za kielekroniki;
(iv) Kuunganisha mfumo wa tiketi za kieletroniki na mifumo ya LATRA;
(v) Kukokotoa malipo na utunzaji taarifa za abiria, nauli iliyolipwa, tiketi za kielektroniki zilizotolewa, kodi za Serikali na tozo za kisheria; na,
(vi) Kuwa na watumishi wa kada muhimu kwa masuala ya ufundi na uendeshaji wa treni ya SGR ikiwa ni pamoja na madereva waliothibitishwa na wahudumu waliosajiliwa na LATRA.

Aidha, nauli hizi ni kwa daraja la kawaida kwa watu wazima na watoto kuanzia umri wa miaka 4 hadi 12 ambapo nauli zitalipwa na abiria kwa kilomita. Nauli itakayolipwa na mtu mzima na mtoto mwenye umri zaidi ya miaka 12 ni TSH. 69.51 kwa kilomita, na mtoto kuanzia kuanzia miaka 4 hadi 12 atalipia TSH 34.76 kwa kilomita. Aidha mtoto mwenye umri chini ya miaka minne (4) hatalipa nauli, hata hivyo, taarifa zao na wasafiri wote zitatunzwa kwenye mfumo wa taarifa za abiria wanaosafiri kila siku.


View attachment 3014035
View attachment 3014036
View attachment 3014037
Angalau bei ni ridhishi.
Ila ni kama zinalingana na za basi.
 
Back
Top Bottom