Zimekaa poa kwetu na kwa mujibu wa latra, ila Sidhani kama ni rafiki kwa Trc., proposal yao ya nauli ilikuwa juu mno na nina wasiwasi wakitumia hizi nauli za latra moja ya tatizo litakaliwakumba litakuwa ni huduma mbovu.Hivi zimekaa poa.
Sio ,ile walizopropose TRC.
Huduma ziwe nzuri sasa.
👍Kabisa, wawekwe watu wa kutosha kufanya usafi wa hali ya juu, na sheria ziwe kali kukomesha watakaofanya uharibifu, makelele na uchafu, security wa kutosha waliopewa training ya hali ya juu waajiriwe wa kutosha na fine ziwe zinazidi nauli kukomesha wahuni na waharibifu
Wahujumu wako camp kujinoaDar-Moro itajaza Kama behewa za mbuzi,mabasi biashara itadoda
Wote wa madaraja tofauti si mnavutwa na kichwa kimoja, kikisimama mnasimama wote?Hii daraja la kawaida itakuwa ile inasimama kila kituo kuanzia Pugu,Soga...mpaka Makutopora.
Express bei lazima itakuwa juu zaidi.
Weka gharama za uendeshaji.na idadi ya watu kwa safariSidhani kama hizi bei zitawalipa,labda kama wanapata ruzuku...
Dom had makutupora haizidi 30 km na hesabu za latra kwa km ni 69.51 hivyo hapo haizidi 2000Wao Trc walipendekeza nauli iwe sh ngapi?
Ila walau wengefanya 45000 Dar-MAKUTUPORA,maana siyo Dodoma mjini ni mpaka Makutupora.
Makutupora ni mbali kutoka Dodoma,ni karibu kabisa na kupanda mlima Saranda.
Kwani usipo panda wewe nini kinaathirikaHata bureeeeeeeeeee sipandi
Nazungumzia treni express na ya kawaida. Express haiwezi kusimama Pugu labda Morogoro tu then Dodoma. So far mabehewa waliyoleta yote yako sawa.Treni moja Ila mabehewa ndiyo Yana daraja mjumbe
Tikiti siyo za dirishani unakata mwenyewe kupitia simu yako, jitahidi uwe unasafiri kwa mabasi hata kama hauna kwenu mikoani ujue jinsi ya kukata tikiti kupitia simu yako.
Maana yake abiria watakuwa wengi kuliko nafasi. Nauli rafiki sana ingawa bus iko chini kidogo.nitashangaa sana kama Trc watauza hizo ticket manual, maana hadi mabasi siku hizi ticket tunakata online.
Wanaleta siasakwa bei hizi hii treni haitajilipa hata gharama za uendeshaji
Mwendokasi walipendekeza nauli yao iwe 1,200/- wakapangiwa 650/- kilichotokea zimekuwa hovyo kuliko daladala. Hawa pia wamepangiwa nauli za chini itakuwa kama mwendokasi. Wataanza vizuri sana ila baadae itakuwa kama treni la Kigoma.Zimekaa poa kwetu na kwa mujibu wa latra, ila Sidhani kama ni rafiki kwa Trc., proposal yao ya nauli ilikuwa juu mno na nina wasiwasi wakitumia hizi nauli za latra moja ya tatizo litakaliwakumba litakuwa ni huduma mbovu.
Kwa nauli hizo lazima shirika life.Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) inawatangazia taarifa ya maamuzi ya Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini kuhusu nauli za abiria wa daraja la kawaida kwa Treni ya Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Makutupora.
Nauli hizi ni baada ya kufanyia kazi maombi yaliyoletwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) na taarifa zilizopokelewa kutoka TRC na wadau wengine.
Kuelekea kuanza kwa safari za SGR Dar es Salaam mpaka Makutupora, masharti ya kuzingatia kabla ya kuanza kutumika kwa nauli hizi ni kama ifuatavyo:
(i) Mtoa huduma (TRC) kuwa na leseni ya usafirishaji:
(ii) Kuwa na ithibati ya usalama wa miundombinu ya reli na mabehewa;
(iii) Kutumia mfumo wa utoaji wa tiketi za kielekroniki;
(iv) Kuunganisha mfumo wa tiketi za kieletroniki na mifumo ya LATRA;
(v) Kukokotoa malipo na utunzaji taarifa za abiria, nauli iliyolipwa, tiketi za kielektroniki zilizotolewa, kodi za Serikali na tozo za kisheria; na,
(vi) Kuwa na watumishi wa kada muhimu kwa masuala ya ufundi na uendeshaji wa treni ya SGR ikiwa ni pamoja na madereva waliothibitishwa na wahudumu waliosajiliwa na LATRA.
Aidha, nauli hizi ni kwa daraja la kawaida kwa watu wazima na watoto kuanzia umri wa miaka 4 hadi 12 ambapo nauli zitalipwa na abiria kwa kilomita. Nauli itakayolipwa na mtu mzima na mtoto mwenye umri zaidi ya miaka 12 ni TSH. 69.51 kwa kilomita, na mtoto kuanzia kuanzia miaka 4 hadi 12 atalipia TSH 34.76 kwa kilomita. Aidha mtoto mwenye umri chini ya miaka minne (4) hatalipa nauli, hata hivyo, taarifa zao na wasafiri wote zitatunzwa kwenye mfumo wa taarifa za abiria wanaosafiri kila siku.
View attachment 3014035
View attachment 3014036
View attachment 3014037
Kuna express na ya kawaida inayosimama kila kituo. Ukiwa na tiketi ya kawaida huwezi kupanda express.Wote wa madaraja tofauti si mnavutwa na kichwa kimoja, kikisimama mnasimama wote?