Hizi Harrier 3rd gen zilivyojazana hapa mjini utasema haziuzwi Mil 70+

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Sahivi Harrier tako la nyani namba E za kutafuta, kuna hizi 3rd gen za kuanzia 2013 kuja juu.


Chuma naziona aisee kibao utasema zinauzwa bei za CX5 kumbe unapata CX5 mbili hapo.


Mfano cheapest unaweza ipata BF hizi hapa, mil 30 kasoro.


Sasa ukija na ushuru wa TRA ndio utajua haujui

Ila wajomba wanazo kibao namba E kila ukitoka lazima upishane nazo.
 
Magorofa yote kariakoo la bei rahisi si chini ya billioni 4,ila hata uanze kuyahesabu unaweza usiyamalize..........utajiri kama tu ulivo umasikini sio jambo la kila mtu,tukatae tukubali
 
Mimi ndoto zakuwa tajiri naona zimepotea maana umri unakimbia sana hata baskeli Sina, licha ya kipato changu kufikia 5Mil kwa mwezi lkn ndoto at least za kupata mil 30 kwa mwezi zinaniishia.

Wenzetu wanawezaje kununua gari za mil 100 au 80 cash. Mambo ya mikopo ya sitaki kuyasikia.

Tupen code wakuu.
 
Hii 3rd gen sijui wanaipendea nn, 2nd ndo ilikua nzuri ukiondoa yale matatizo ya kupinda pinda kwenye suspension systems zake, unakuta chuma imelalia upande mmoja kabisa.

Ni kama fortuner tu, latest model siikubali kabisa bora ile previous ilokua kama hilux kwenye dash na engine ila tofauti ni body tu
 
Kama una moyo wa Siri ,njoo huku kijijini kwetu nitakuambia kila kitu ,mwaka Mimi na wewe tunachekelea kikubwa ujue lazima huo utajiri unishirikishe na Mimi .

Note :sio Mambo ya uganga ila kuiba Kama Wana siasa
 
Hiyo Fortuner unaikataa kwa hoja zipi za kitaalamu mkuu yaani Fortuner ya 2023 au 2024 ufananishe na ya 2010 kweli? ushaendesha hizi za miaka ya karibuni ukaona tofauti ya comfort na usalama kwenye hizo gari na hizo za zamani au ukiwasikia tu watu wakisema ndio unakuja na majibu ya jumla..
 
Mkuu umelipia tangazo?
 
mimi sina maisha kiiivoo wala nini, lakin hizo harrier 3rd gen wala hazivutii, bora hata mdogo ake 2nd gen matak* ya nyani iko vizuri.
lakini gari bora za nyota5 kwa Africa zitabaki zile zile;- ambazo ni
*Mercede$e BENZ
*Range Rover
*BMW
*VW
*JEEP
#CHANANJA motors.
 

Wengi wao mikopo ya riba, wengine ushirikina na kupora mali za watu bila kutolea jasho. Afrika ni afrika tu.
 
Toyota weka mbali na watoto

Marekani, germany, korea, uingereza, watatoa sana magari ilaa kwa mjapan wakasome, magari ya mjapan ni high level.

Toyota
Isuzu
Nissan
Weka mbali na watoto.

Range ukinunua mpya jua kabisa utapata tabu kupata mteja au kuuza kwa khasara, hivyo hivyo kwa Mercedes benz na gari za mmarekani.

Only japan only japan, salute kwake!
 
Mama amefungua nchi
 
Upo sahihi kabisa me mwenyewe binafsi sivutiwi na hiyo 3rd gen na pia kwenye fortuner ni hivyo hivyo
 
Hiyo Fortuner hunaikataa kwa hoja zipi za kitaalamu mkuu yaani Fortuner ya 2023 au 2024 ufananishe na ya 20010 kweli?ushaendesha hizi za miaka ya karibuni ukaona tofauti ya comfort na usalama kwenye hizo gari na hizo za zamani..
Hata mimi nimeshangaa. Fortuner ya 2020 iwe sawa na 2010? Hata Hilux za 2020 sio kama za 2010.

Kama hupendi mambo mengi SUV ya kununua ni Fortuner.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…