Hizi ndio Taasisi zenye mishahara minono Tanzania

Hizi ndio Taasisi zenye mishahara minono Tanzania

Sasa ulichoongea ni nini na nilichoongea mimi ni nini? Si ndiyo nimetoka kukuambia kuwa SIYO KILA KITU kuhusu jeshi kinawekwa hadharani kwahiyo wewe unafikiri hivyo vilivyowekwa hadharani ndiyo vyote vinavyohusu jeshi maana naona mchanganuo unaoujua wewe ndiyo ule ule tu ambao hata mtoto wa primary anaweza kufundishwa shuleni!

Mwishoni kabisa nimeainisha kwamba raia wengi huwa mnaambiwa yale ambayo mnatakiwa kujua tu yaani vile vilivyoandikiwa kwenye katiba na takataka zote unazojua wewe vile ni sehemu tu ya matumizi yao! Kwa kuwa hakuna unalojua endelea kuamini hivyo kuwa bajeti ya $1B inayochanganuliwa kwenye hivyo vitabu ndiyo inayoenda jeshini kweli!

Halafu unapohoji kama magari ya jeshi kupita sehemu isiyohusika ni sawa kwani hapa tunaongelea uhalisia au kuhusu jambo kuwa sawa? Kama tukitaka tuongelee mambo kuwa sawa ulipaswa kwanza ujitafakari tangu mwanzo ulipoanza kusifia pesa za magumashi wanazopata matraffic na TRA nje ya mishahara kwa kudhulumu watu kana kwamba wanachofanya ni sawa!
-ukisoma bajeti Mambo muhimu lazima yawepo, usiri unaotawala Sana ni kwenye baadhi ya Sehemu/vitengo mfano Ofisi ya Rais (IKULU) hapa Kuna Siri nyingi Sana na hata hesabu zake hazichapishwi, Usalama nao pia Mambo yao ni Siri Sana ndiyo manaa hesabu zao zinakaguliwa lakini hazichapishwi, hoja yangu ni kwamba Kuna maeneo yenye Siri nzito kuliko Jeshi ambayo ni IKULU na Tiss (Usalama).
-Shule gani ya msingi hapa Tanzania wanafundisha masuala ya Bajeti na utaratibu wa matumizi ya fedha za umma hebu itaje
- Kuhusu kusema raia tunaambiwa Yale yunayostahili, tunayostahili ndiyo hayo masuala ya matumizi ambayo nimekutajia hapo juu na kimsingi nimekuchambulia vizur Sana rudia kasome
--Inaonekana hujui bajeti na dhana nzima ya Bajeti yaani ww unadhani JESHI linaweza kukwapua tu pesa na lisihojiwe na kisikaguliwe kitu ambacho siyo kweli na ndiyo maana CAG anakagua na PPRA wanawakagua, ndiyo maana kwenye Post zangu za just huko nilisema kuwa hata ikatokea matumizi ya JESHI yamezidi waziri wa ulinzi itabidi apeleke bajeti ya Ziada bungeni kwa hayo matumizi ambayo yamezidi.
-Kuhusu Magari yao kupita Sehemu sio Mimi nilikupinga kutokana na ni hatari na ww ulivyoandika hapa uliandika kiushabaki kwamba hawafanywi lolote, Kuhusu pesa za magumashi Mimi hoja yangu ilikuwa ni kwamba wenye mishahara mikubwa wanaweza kuzidiwa na wenye mishahara midogo ambao wana magumashi Mengi,
 
Mkuu kwani hapa tunashindanisha taasisi zenye usiri ama nini maana sijaona mantiki ya kusema eti kuna taasisi zenye usiri zaidi ya jeshi ambazo ni ikulu usalama na takukuru kana kwamba mimi nimesema jeshi ndiyo taasisi inayoongoza kwa usiri! It's like unataka kuniambia kwamba usiri wa hizo taasisi nyingine unabadilisha ukweli kwamba jeshi nalo lina usiri!

We jamaa mi hata sijui unashindwa kuelewa wapi hakuna sehemu nimesema jeshi linajikwapulia tu pesa! Ni hivi pesa zote zinazoenda jeshini zinakaguliwa kila sehemu lakini siyo zote zinakuwa published kama sehemu ya bajeti kwa sababu nyingine ni privileges za ziada tu ambazo siyo zote raia wanapaswa kuzijua na ni nje ya zile zote mnazozijua ninyi ambazo ni mandatory!

Kuhusu kufundishwa shule ni wapi nimesema kuna shule za primary zinafundisha bajeti ya jeshi umesoma ile statement vizuri ukaielewa au umekurupuka kama kawaida yako? Hoja yako kuhusu pesa za magumashi ililenga kuwasifia mkuu ulisema kabisa "pesa za magumashi ndiyo zinafanya watu wanajenga maghorofa" kana kwamba hiyo ni sawa na siyo hatari!
-mantiki ya hoja yako ya kusema bajeti ya Jeshi haijadiliwi (hapo awali) ilikuwa inataka kuonesha kwamba JESHI lina Siri Sana, nikakupinga kwa hoja kwamba Bajeti ya Jeshi ni Bajeti tu Kama ya Tamisemi
- nilipoleta Hoja usiri wa IKULU na Tiss (Usalama) ilikuwa ni kukuonesha kwamba hizo Taasisi zina Siri nzito lakini bajeti yao inajadiliwa Bungeni, ila tofaut ni tu pale ambapo kwenye ukaguzi wa CAG taarifa zao hazichapishwi, na nilitaka kuondoa dhana ya kwamba JESHI ndiyo wenye nchi na kwamba wao hawasemeshwi kwenye masuala ya fedha
-Kuhusu kukwapua Pesa, ww kwenye bandiko lako hapo juu umesema kwamba zile trilioni 2.3 ambazo ndiyo bajeti ya Wizara ya Ulinzi ukasema kwamba siyo trilioni 2.3 Mimi nikakujibu kuwa bajeti ndiyo hiyo ikitokea matumizi ya Ziada itabidi Waziri wa Ulinzi aandae bajeti ya Ziada apeleke Bungeni, na siyo tu kwamba atakwapua tu pesa, na haiondoi ukweli kwamba trilioni 2.3 ndiyo bajeti yenu hayo mengine mnadanganyana tu huko kambini
-Privileges zote, matumizi yote yapo kwenye vitabu vya bajeti, ndiyo maana ikaitwa Bajeti (Mpango wa Mapato na matumizi)
-kuhusu shule ya msingi na bajeti, ww ndiye uliyesema kwamba hata huo mchanganuo kufundishwa shuleni (msingi), swali la msingi ni kwamba kwa mitaala ya hesabu Tanzania mtoto wa shule za msingi anaweza kufundishwa hesabu Hadi Trilioni?, Kalete huo muongozo unaosema watoto wa primary wanafundishwa Hadi Trilioni, na je mtoto wa msingi anajua Sheria za Kodi? Kwa maana Bajeti ni kutoza (kwa kuongeza au kupunguza) Kodi,tozo,ushuru nk
 
Mkuu mbona maelezo mengi halafu unarudi tena kule kule? Teh umeishiwa hoja sasa umeamua kusema wanajeshi wanadanganyana tu huko kambini, yaani unachofanya hapa sasa siyo kujenga hoja tena bali kubishia ukweli uliopo kwa sababu hata ukibisha huo ukweli haubadiliki, nimekuambia wewe endelea kusubiri matumizi yote ya jeshi yawekwe hadharani wakati ulishakubali kwamba hiko chombo kina usiri wake!
- Mkuu unasema nimeishiwa hoja wakati hakuna hata hoja yako hata moja sijaijibu, mfano tu unazungumzia primary school na hesabu za bajeti wapi na wapi? Hilo hujaliona?
  • mnadanganyana ndiyo huko kambini kuamini kwamba fedha zenu hazijadiliwi bungeni, fedha za JESHI ni fedha za umma, Bajeti inabeba kila kitu kinahohusu Jeshi including zana za kivita,
  • hesabu za Jeshi kupelekwa bungeni hakuondoi unyeti wa Taasisi ya Jeshi.
-
 
Mi nina huzunishwa na mfumuko huu wa bei za vitu sijui kama unazingatia mishahara ya wafanyakazi wote kwani bei zimepanda zaidi ya 30% na zaidi ya hapo bado najiuliza hivi Tz kuna vyama vya wafanyakazi kweli? Hata hao watu wa T.R.A wanaolipwa mamilioni bado hawaioni real value ya hela zao kwa mazingira haya ya mfumuko.
 
Mi nina huzunishwa na mfumuko huu wa bei za vitu sijui kama unazingatia mishahara ya wafanyakazi wote kwani bei zimepanda zaidi ya 30% na zaidi ya hapo bado najiuliza hivi Tz kuna vyama vya wafanyakazi kweli? Hata hao watu wa T.R.A wanaolipwa mamilioni bado hawaioni real value ya hela zao kwa mazingira haya ya mfumuko.
Poleni sana mkuu! Wenzenu Wanajeshi mahitaji yao mengi wananunua kwa nusu bei huko makambini kwao na bado wanalipwa mishahara mizuri kama TRA tu halafu mtu anakuja kulinganisha mambo kwa kutumia mihemko tu bila uhakika!
 
Hehe mkuu vipi bado tu hujapataga kazi kwenye chombo chochote cha mambo ya ndani? Tuambie basi wewe unayejua maana kwenda jkt uzalendo tu tayari unajionaga mwanajeshi na unajua kila kitu kuhusu majeshi na wengine wote hawajui kitu!
Umebishana imetosha. Nakuja pm kwako tuyajenge.
 
Duuh yaani mimi siku zote wanavyosemaga mishahara minono, huwa nadhani labda hizo taasisi zote ofisa anayeanza kazi anachezea kuanzia 2.5M-3M!

Kumbe wengi hata 2M hawafiki, kama ni hivyo basi TPDF linalipa vizuri asee maana jeshini hizo 1.8M-2M ni mishahara ya makoplo na masajenti ambao wengi wameishia la saba na form four!

Bado hujazungumzia wenye degree maofisa kuanzia maluteni, halafu kuna watu wanadharau eti jeshini hamna kitu eti pesa ziko TRA na BOT kumbe pesa zenyewe ndiyo hizo wabongo bhana!
Rudi shule
 
Pesa ya kawaida wakati mtu mwenye diploma tu anakula 2M+ we unaiita hela ya kawaida hio kwa level ya mishahara ya kibongo?
Bora TPA, TRA kuliko hapo jeiwii.

Hayo mashirika ya kiserikali, yana pesa nyingi mno mbali na mishahara. Tazama maafisa wengi wa hayo mashirika, tazama na maafisa ya jeshi kimaisha.

Achana na TANAPA, TRA, TPA n.k

Kuna watu kwa mwezi nje ya mshahara wanakunja mpaka 10m.
 
Mkuu, hii mishahara ya wanajeshi mnayoweka hapa mnaitoa wapi aisee?

Kwanza Jeshini hawalipi kwa Elimu.

Elimu Jeshini inakusaidia tu kupanda cheo baada ya kufanya kozi, hicho cheo ndio Chenye mshahara.

Mkuu sikudanganyi, Mimi ninao washkaji zangu nimemaliza na form 4 wengi sana wako Jeshini. Kuanzia Lugalo, Makongo, Kunduchi, Navy Kigamboni, Abdallah Twalipo Kurasini kote hakuna sehemu Sina jamaa niliyesoama naye. Police na magereza ndio usiseme.

Mimi sikupenda tu kuwa Askari.

Tena wengine wanna degree kabisa.

Mishahara ya Askari Ni ya kawaida kabisa. Na kibaya zaidi hawana Uhuru, wako busy mnooo.

Kitu pekee unachoweza kufaidi ukiwa Jeshini labda uende mission nje ya nchi.

Kuna ndugu yangu ( naye nimesoma naye) alienda Sudan akarudi na 30M hadi akataka kuacha kazi.

Sasa hivi imeisha anatamani kwenda tena.
Jeiwii maafisa wanalipwa hiviii

Ana mshahara wake
Cheo chake/fani yake jeshini (kuna kitu sikumbuki vyem apa)
Elimu yake inalipwa, degree n.k ila kwa diploma sijui
Ela umeme na maji (sio nyingi)
Lation kama laki mbili hivi au tatu

Ukikusanya vipengele hapo kama 6 hivi anagota kwenye 2m na usheee. Huyu ni luteni.

Ukienda TANAPA, TRA, Bandar, EWURA kwa mtu mwenye degree, hawa maafisa hawawanusi hao watu. Sema hayo mashirika watu pesa zao hawajioneshi lakini jeiwii hanusi hapo.

Unachosema ni kweli kabisa, wengi wakienda nje ya nchi ndo walau wanapata pesa na wengi wao hii kazi wanaona inawabana mno.
 
Kwahiyo mkuu vyote ambavyo waalimu wanakuambia darasani huwa vipo kwenye syllabus au umesoma shule za kayumba? Ndiyo maana tunaambiwa elimu yetu ina shida maana wanafunzi wanafundishwa vitu kwa kukaririshwa tu!

Bajeti ya jeshi inayojadiliwa bungeni na kuwekwa kwenye mchanganuo ni ya expenses za muhimu hata hizo privileges zote zilizojumuishwa humo ni zile za muhimu tu! Bado zile privileges za ziada ambazo wewe huzijui wala hutakaa uzijue!

Tatizo unadhani privileges zote za wanajeshi ndiyo zimeishia hapo kwenye hiyo bajeti ambayo sisi ndiyo tunayoijua! Wanajeshi wadanganyane kuhusu bajeti yao kwa faida ya nani kwamba wewe ndiye unayejua mambo ya jeshi kuliko wanajeshi wenyewe?
-Mkuu Kama ni ukayumba kati ya Mimi na ww Nani ameonyesha ukayumba? We ndiyo umeonesha ukayumba kwa sababu Kama hizi mosi ulisema kwamba Bajeti ya Jeshi haijadiliwi bungeni nikakwambia sio kweli na nikakufundisha jinsi fedha zinavyotolewa,pili ulisema Bajeti ya JESHI ni kubwa kuliko Wizara zote nikakwambia kwa takwimu kwamba Bajeti kubwa ni ya Wizara ya Ujenzi ambayo ni Trilioni 4, Bajeti ya pili Ni ya Wizara ya Elimu, tatu ukasema kwamba ukasema privilege zenu Kama Posho, duty free shops hazipo kwenye Bajeti kitu ambacho ni cha Uongo kwa sababu hayo yote sehemu ya Sheria na Bajeti, nne ukasema kwamba shule za msingi wanaweza ku-compute mahesabu ya matrilioni nikakupinga kwa hoja Sasa mpaka hapo Mimi na ww Nani Ni kayumba?
- privilege za Wanajeshi ziko kwenye Bajeti na Sheria za Kodi eg Mambo ya duty free shops etc, nilishakwambia kwamba huwezi kutumia zaidi ya matumizi ambayo umetengewa kwenye Bajeti yako, ikitokea hivyo waziri wa ulinzi anatakiwa apeleke bajeti ya Ziada bungeni kuomba Ziada ya Fedha tatizo unadhani JESHI linakwapua tu Pesa bila utaratibu wanafuata utaratibu na wakikosea wanaambiwa kwenye ukaguzi
-Kuhusu kudanganyana Mambo ya bajeti ndiyo inawezekana mkadanganyana kwa kutokuwa na ufahamu wa kutosha wa Mambo ya fedha za umma na bajeti,
- hata Jeshi likitaka Fedha wanaenda kuomba idhinini kwa CAG na hayo matumizi yanatakiwa yawe kwa mujibu wa Sheria.
 
Wanajeshi wanapaishwa sana mishahara yao sio mikubwa kama watu mnavyosema humu ndani.
Tatizo humu watu wanachanganya vitu mada imeelezea taasisi zenye mishahara mikubwa yaani ni entry level ikimaanisha kwamba huo ni mshahara wa degree ambae ndo anaanza kazi kwa mara ya kwanza kwenye hio taasisi.
Sasa watu mnaanza kusema kuna masajenti wanalipwa zaidi ya hizo amount zilizotajwa hapo na kuwa hao masajenti level yao ni form four hivi mnajua huyo mtu mpaka kuwa sajenti imemchukua miaka mingap ???
Na je tukichukulia mtu ambae yupo ega na ana elimu sawa na huyo sajenti na wote wamekaa kazini kwa muda sawa unafikiri nani atakuwa na mshahara mkubwa kumzidi mwenzake ???

Kwa tanzania wanajeshi bado hawajazidi hizo scale tajwa hapo juu
Mfano mwepesi tu kuwe na HR wawili wote wasome chuo kimoja halafu wote waajiliwe kwa pamoja mmoja jeshini mwingine eGA kwa mshahara wa kuanzia lazima huyu wa eGa utakuwa juu zaidi kuliko wa mwanajeshi kwa hiyo wanajeshi msiwatukuze sana mishshara yao ni ya kawaida.
Umemaliza mjadala.
 
Sasa Luteni wa Jeshi kama anapokea mil 2.3 anatofauti gani na afisa wa TRA anayeanza kazi na mwenye degree??
Ni kweli luteni anakunja 2.3 tena hiyo mimi niliona jamaa akiwa mwaka wa 5 jeshini.

Nina uhakika wa zaidi ya 100% ktk hili sababu niliona salary slip.
 
Hapan unajua akitoka luten usu ndo anafata luteni kamili sasa yan range ya mshahara ndo wapishane karibu 1.3 hapan sio nyie mtafanya tuonekane tunapesa huku mtaani kumbe hamna kitu
Hiyo 2.3 narudia ni mshahara wa luteni kanali pamoja na marupurupu
Luten kamil ni 1.3m

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa mshahara wake anafika hapo 1.3m au haifiki. Ile salary slip sijui niliitupia wapi. Cheo kinalipwa, degree inalipwa, kuna umeme na maji, kuna ration na takataka gani sijui hukoooo

Hapo ukijumlisha ndo anagota 2.3 mpaka 4.
 
Back
Top Bottom