- Afisa wa TRA vipi mbona Bado unalia? Kwa hiyo unataka kusema hata basics za taxation zilikupitia pembeni, Kuhusu ww kuwa Afisa wa TRA ni hoja tena hoja mujarabu kabisa, kwa sabbu ww mwenyewe umejinasibu uko TRA japo Mimi nilipinga, Sasa nakutishia na Maswali ya Taxation ukafyata mkia Afisa vipi tena? Sasa hutaki ni Conclude kwamba ww ni 'Incompetent'? Unaposema wataalam kwani wewe si mtaalam? eti Afisa wa TRA? Ukiajiriwa TRA na degree/ Diploma etc ww ni mtaalam hivyo huwezi kukosa basics za taaluma unayofanyia kazi, na ndiyo maana kwenye hoja yangu nikasema kwamba sio Lazima upate 100% hata ukipata 60% inatosha au Uliogopa nilivyokutajia Chuo cha Kodi (ITA), Sasa Kati ya Mimi na ww Nani mwenye uwezo mdogo? Kwanza ww ni muoga, ukitingishwa unatingishika.Mkuu kuhusu mimi kuwa afisa wa TRA kwani nayo ni hoja maana naona unasema nimeshindwa hiyo hoja! Kuhusu kujibu maswali nimekushangaa kwa ile conclusion yako awali uliposema kuwa mimi siwezi kuwa afisa wa TRA kwa sababu kuna maswali nimeshindwa kujibu na wakati unajua kuwa kuna maswali waajiri wengine hawawezi kujibu isipokuwa wataalam tu so haibadilishi ukweli kuwa huyo mtu kaajiriwa sehemu husika hivyo uwezo wako wa kuconclude mambo ni mdogo!
Kuhusu sheria inayogovern utolewaji wa nyota kwa form six jeshini haihusiani hapa kwa sababu mwanzo ulikazana kuwa kuna maluteni walioishia form six mimi nikakuambia miaka hii hawapo! Kwahiyo hata kama kuna sheria inayoruhusu form six kuvishwa nyota bado haibadilishi ukweli wa jibu la kwamba hakuna tena form six wanaovalishwa nyota ni lazima wakasome kwanza degree wawe na professions kulingana na uhitaji wa jeshi sababu utaratibu kwa sasa umebadilika!
Kuhusu privileges za majenerali nilikuuliza unitajie exact privileges zote wanazopata sababu kule juu kuna comment ulisema privileges zote expenses zake zimejumuishwa kwenye bajeti hiyo ambayo inachapishwa ndiyo nikakuambia unitajie zote na uniambie zimeandikwa kwenye sheria gani! Na kuhusu bajeti ya jeshi kama umeamua kukataa na kusema ni uongo basi siwezi kukulazimisha uamini kwa sababu kukujibu nilishakujibu hivyo kutokuamini kwako siyo hoja mkuu!
Hao niliowauliza niliwauliza yale niliyohitaji kuyajua mimi tu mfano hayo ya bajeti na privileges wanazopata ila hayo ya sheria inayogovern utolewaji wa nyota niliambiwa tu "ukitaka kuyajua yote hayo kiundani zaidi ingia jeshini" na nikaambiwa kuwa kwa sasa hakuna tena maluteni walioishia form six jeshini! Sasa hapo hiyo National Defence Act ingenisaidia nini hata kama kuna sheria ingekuwa inasema form six wanapewa nyota wakati kiuhalisia siku hizi haiko hivyo tena hadi wakasome!
Suala la kusema hii nchi inaongozwa na sheria kiuhalisia halina mashiko kwa sababu kuwa na sheria ni jambo moja na kuzifuata hizo sheria ni jambo jingine! Mambo kwa ground ni tofauti bob pesa za umma haziheshimiwi kama unavyofikiri na ndiyo maana matraffic wana pesa za magumashi ilihali serikali inajua na bado watu kama ninyi mnaona sawa tu ukweli unaujua ila unajitoa ufahamu eti unatumia sheria sheria zipi hizi hizi ambazo nyuma ya pazia serikali yenyewe ndiyo inaongoza kuzivunja?
- Hoja yangu na ugomvi wangu ulikuwa kwenye hayo maneno"Miaka hii" eti Afisa wa TRA? Mimi nimeomba tena kwa faida ya wanajf utaje exactly walizuia mwaka gani? haya neno miaka hii nini maana yake? Kuhusu Sheria inayo-govern utolewaji wa kamisheni inahusika 100% kwa sabbu huo Ni utaratibu ambao umeandikwa kwenye Sheria au miundo ya utumishi jeshini (hebu jaribu kumuuliza Mkuu wa Utumishi Jeshini) utajibiwa, Sheria ndiyo inaongoza utaratibu wowote pale, hiyo Sheria ndiyo itasema hivi mfano. Ili upande kutoka Private Hadi Koplo unatakiwa ufanye Nini (uende kozi gani), ili upande uwe commissioned Officer unatakiwa uwe na sifa zipi, i.e Kunakuwa na kitu Kama scheme of service ambayo nayo ni Sheria, Sheria Kama ikizuia form 6 itasema kabisa mfano hivi "Ili upate kamisheni ni lazima uwe na Shahada ya kwanza ya Taaluma yoyote kutoka chuo kikuu kinachotambulika na hiyo ni baada ya kwenda kwenye Mafunzo kwenye Chuo cha Taaluma ya kijeshi (TMA)" hivyo basi Sheria ndiyo inatoa masharti ya upandaji wa vyeo
-
-Kuhusu privilege za Majenerali Mimi hiyo hoja siku raise kabisa, any way ngoja nikujibu ukienda kwenye Fungu 57 utakuta Posho za majenerali, zipo zimetajwa kwa jumla kuwa ni kiasi gani kwa ujumla,mfano mwaka 2020 fedha za Majenerali zilizopokewa zilikuwa bilioni 4,
- Yani acha kudhalilisha wanajeshi aisee yani ofisa wa Jeshi asiijue Sheria ya 'The National Defense Act'? ni Kama Afisa wa police (nyota kwenda juu) ashindwe kujua Police and 'auxilliary police act' ni aibu kubwa, kwa hiyo unataka kuniambia hao maofisa hawajafundishwa wakiwa RTS? hoja ya kusema sijui uingie Jeshini ndiyo utayajua Haina msingi wowote ule,
- Sheria ndiyo ingekuongoza kuelewa Muundo wa Jeshi, ungepata kujua Unapandaje kwenda Koplo,sajenti,staffu sajenti (sajini taji), Warranty Officer,etc