Hizi ni kona kali na milima, kwa barabara nchini, taja nyingine

Hizi ni kona kali na milima, kwa barabara nchini, taja nyingine

Jamaa yangu alikuwa hajawahi kupita Goba road. Siku katoka na Washkaji wakapita njia hii pale kwenye kilima Cha Mount Kibo Primary mpaka Kayuni gari yake Nissan March ilikosa nguvu akapanda kibishi.

Sasa akawa anasimulia amekutana na kilima Kikali Sana Dar, watu wakawa wanamcheka Sana wanamwambia kapanda Kitonga ya Dar na yeye ni Mwanadarisalama hajawahi kwenda Mkoa maisha yake yote.
Hahaha inabidi atembee akaone maajabu huko nyanda za juu kusini magharibi na nyanda za juu kaskazini mashariki, kwanza atambue maana ya neno nyanda za juu Kisha mumueleweshe kwanini wapaite nyanda za juu na so nyanda za chini kama dasilamu
 
Kona na milima ya Usambara (Mombo - Lushoto). Mara ya kwanza kabisa nilipita usiku kuelekea Lushoto, sikuona. Kimbembe ilikuwa siku narudi kuelekea Mombo, ilikuwa mchana tena nilikaa siti ya mbele kabisa kwenye Land Rover. Pale Soni tokea Lushoto huoni kabisa kona mpaka ukaribie. Basi nilijua sasa tunakwenda kutumbukia. Barabara nzima nilikuwa nafunga breki as if naendesha mimi. Kufika Mombo mguu wa kulia ilikuwa unauma hatari.
 
Mi nashangaa watu wanafananisha eti na mburu kusiko hata na maporomoko,

Burdani anapitaga na mpaka 90kmph usiku, Madereva Wageni wengine wakifika Mombo wanaomba Mwenyeji awasaidie kupandisha, No chance for mistakes juu kuna jabali, chini kuna falls kati hapatoshi.

Cha kushangaza Sijawahi sikia ajali njia ilee.
Ile barabara Mombo to Soni inahitaji umakini wa hali ya juu kabisa as if unafanya operation ya moyo. A slightly mistake, you are gone.
 
Ugweno na usangi road
FB_IMG_1619468198957.jpg
 
I have been there aiseeee, mwanzo wakati naenda nilipewa lift kwenye gari ya serikali ilikuwa usiku sikuona tabu sana japo nilikaaa mbele, wakati narudi nilipanda Burdan Bus aiseee unaweza kuomba kushuka na jamaa wanalala nazo tu wala hawajali[emoji23][emoji23][emoji23] naisi ni moja kati ya barabara hatarishi Tanzania inaweza kuwa ya kwanza au ya pili, maana ile road ni nyembambaa mno, uwezi kufananisha na kitonga, maana kitonga cha mtoto
Zile kona hazionekani vizuri na siyo kali sana kama unatoka Lushoto ila ukiwa unaenda Lushoto mtihani
 
I have been there aiseeee, mwanzo wakati naenda nilipewa lift kwenye gari ya serikali ilikuwa usiku sikuona tabu sana japo nilikaaa mbele, wakati narudi nilipanda Burdan Bus aiseee unaweza kuomba kushuka na jamaa wanalala nazo tu wala hawajali[emoji23][emoji23][emoji23] naisi ni moja kati ya barabara hatarishi Tanzania inaweza kuwa ya kwanza au ya pili, maana ile road ni nyembambaa mno, uwezi kufananisha na kitonga, maana kitonga cha mtoto
Wakati naenda huko nilikaa dirishani kuna fala moja likasema hapo gari ikidumbukia hakuna wakupona sikulijibu chochote [emoji23]
 
Duh aki sitaki kupita njia hiyo nimeskia ni kona mno, ile kitonga tu mimi naskia kulia huko sijui itakuaje, kuna siku tunatoka Mbeya kufika kitonga pale naona watu wanalia wameumia kuuliza ni ajali na gari imedumbukia kule chini ingawa si kule bondeni sanaa na hao watu wametolewa huko na kuletwa huku juu kwa ajili ya kuwaishwa hospital duh😪😪nilitetemeka maana dereva wetu alikua anaenda speed na hizo kona hajali.
Ukipanda New Force ya yule mchina mshenzi mvuta fegi lazma ushike roho mkononi🤓🤓🤓
 
Habari jamvi?, kwa wale wazurulaji nchini

Ukizunguka nchini utakutana na sehemu maarufu , kimandhari na kimuonekano.

Leo naongelea sehemu za barabara nchini ambazo Zina Kona Kali na sehemu ya milima, nataja chache nyingine ongeza
1. Kona za Iyovu - ukitoka tu mikumi kuelekea iringa utaziona Kona hizi, ni Tamu Sana
2. Kona za kitonga - hizi zinapatikana kutoka Moro kwenda iringa.

3. Kona za Kolo- hizi zinapatikana kutoka kondoa kuelekea babati

4.kona za Nyang'olo - hizi zinapatikana unapokaribia kufika iringa kutokea dodoma

5. Kona za Lukumbulu songea huko

6. Kona za msambiazi, korogwe kuelekea mombo
7. Kona za Mombo kuelekea Soni - Lushoto
8.Kona za Mbeya kwenda Chunya
9. Kona za Ugara - Babati kwenda Mbulu - hapa kitonga chamtoto Cha ngedele


Ni Kona hatari lakini Tamu Sana, na mabasi huwa wanalala na Kona hizi kwa speed ya 120 yaani shaa.

Ongeza Kona Kali nyingine
Mlima Nyoka🐍
 
Zile ni shida kona75 za kutisha ,mpaka Gari la juu utosi wa kichwa unaliona
Kabla sijapita njia ile nilikuwa nadhani kona za nyang'olo ndio nyingi na zinashtua,aisee nchi hii Kuna kona zinatisha kupindukia,njia chimala-matamba ukipita hutamani kupita tena na kama una gari halieleweki utaishia makorongoni.
 
Kabla sijapita njia ile nilikuwa nadhani kona za nyang'olo ndio nyingi na zinashtua,aisee nchi hii Kuna kona zinatisha kupindukia,njia chimala-matamba ukipita hutamani kupita tena na kama una gari halieleweki utaishia makorongoni.
Katikati ya mlima kuna sehemu panaitwa mwadangala ,hapo kuna kona kama sita hivi zipo karibu karibu na bonge la bonde kushoto na kulia kwako ,mlima una nyuzi 75. Gari likiachia huko chini watu hawakufati chini wanafanya ibada juu kama kwenye meli ya titanic
 
Aisee sijapita hii njia na wala siwish kuipita[emoji3] mambo ya kuminya breki kama mimi ndiye dereva sitaki[emoji3]
Mimi ilikuwa najiwahia siti ya dirishani nachapa zangu usingizi,hata sijali yaani [emoji23]
Yaani pale hata kula huwezi maana chakula chako chote kitakumwagikia[emoji1787]

Ukikaa siti ya pembeni yaani wewe utapambana kushikilia kiti hadi ukome maana gari inalala mno,kushoto kulia imagine saa nzima [emoji1787]

Mara ya kwanza napita kule Mtera nilitamani nilie[emoji23]ila ndio kulikuwa hakuna namna, nimesoma Dom hadi nimemaliza napita ile barabara,safari za kutosha.

Ila hizo Kona za Nyang'olo Zina balaa[emoji119]
It's funny sometimes,mimi nilikuwa naburudika sana ila naomba tu Mungu gari isitumbukie korongoni[emoji23].

Ukisema ushike breki za miguu basi utashika hadi miguu iume maana Kona haziishi zile[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hatari sana na kujishikilia kwenye kiti kwa nguvu huku ukiminya breki[emoji3][emoji3][emoji3] maisha ni matamu haya jamani ijapokua tunalalamika hamna pesa maisha magumu ila when it comes to uhai mmh full mabreki kama dereva[emoji3][emoji119]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji119]
Haka kamtindo nilikuwa nako zamani aisee..
Siku nimepata ajali nilikaachaga,maana ajali ikija hata ujishike vipi[emoji23][emoji23][emoji23],siku hizi huwa nasafiri tu bila kujali,lolote na liwe..kwanza huwa naamini nitafika salama na Mungu ni mwema.
 
Back
Top Bottom