Kuna shida mahali mkuu. Labda katiba mpya italeta mabadiliko.Hii kwa Tanzania yetu si ngeni mkuu labda kama we ni mgeni nchi hii... Ni Ushubwada tu ndio umejaa hakuna kingine
Na despite ya kuwepo kwa vivid Gap la kiutendaji ajitokeze wananchi yeyote ahoji mambo ya Rushwa, Uwajibikaji mbaya wa watumishi, Dpw nk Uone atakavyoandamwa hutaamini
Hii nchi ni kama tu ina laana vile maana si bure yani😂
Hujanielewa wewe. Nimeuliza zile ni ziara au kampeni?. Halafu ni lini 255 walianza kutaja jina la Fulani kuwa watampigia kura kuingia ikulu?. Tofautisha mikutano ya CHADEMA ya kisiasa na ziara za kikazi za rais.Wewe unadhani Operesheni +255 Katiba Mpya siyo Kampeni za 2024 na 2025?
Kampeni zilishaanza kitambo jimbo la Kawe kwa mfano Askofu Gwajima kaanza kitambo tu sasa Tuko kwenye Gwajima Cup
Alichaguliwa lini na watanzania kuwa Rais?. Halafu Kama anapendwa mbona anatumia nguvu nyingi kukubalika.Rais Samia Ndio chaguo la watanzania kuendelea kuwaongoza mpaka 2030,Ndio maana Anaendelea kupokea na kupata mapokezi makubwa kutoka kwa wananchi kila mahali anapopita na kutua .wananchi wana shauku kubwa sana ya kumuona .Ndio maana unaona watu wakikanyagana wazee kwa vijana,akina mama kwa watoto kila mmoja anataka kumuona Rais samia na kumsikiliza.Hii yote ni kutokana na uchapa kazi wake uliyogusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti ambao kwa sasa sauti zao zinasikika kupitia Rais wao. Ambaye amekuwa mtetezi wao.
Hii itakuwa ngumu kutekelezeka. Nadhani wapambanie ile ya coalition hata miezi mitatu kabla ya uchaguzi Kama Kenya.Upinzani unatakiwa upiganie sheria ya kuruhusu kampeni za kisiasa muda wowote.
Mambo ya kusubiria mwezi mmoja au mitatu kabla ya uchaguzi yamepitwa na wakati.
Umeelewa swali langu?. Tofautisha ziara ya Rais na mkutano wa kampeni au chama Cha siasa. Unapochaguliwa kuwa Rais wewe ni kiongozi wa wote. Unapofanya ziara unakuwa unafanya ziara ya wananchi wote na kwaajili ya kusikiliza kero na matatizo yao, sio kwaajili ya kusifiwa na kuahidiwa kura na Wana CCM.kwan yule jamaa aliepeleka report ng'ambo kwa wafadhili wake alikua anafanya nin huko mwanza na ngorongoro hadi anagalagala barabarani?
na alikua amevaa suti, kanzu au?
na wafuasi wake waliohudhuria ile mikutano walikua wamevaa bendera na sare za mashuka au za Chama?
Tatizo huelewi hata maana ya ziara ya Rais. Ziara ya Rais utalinganisha na mikutano ya hadhara ya CHADEMA?. Mikutano ya CHADEMA hakuna kunadi Fulani atakuwa Rais zaidi ya kujadili katiba, bandari etc. Ila kwenye ziara ya Rais ni kumsifu na kumwabudu Rais mpaka mwisho na kumpigia debe basi.Wewe unakiitaje? Si umemuona tundulissu ziara ya Ngorongoro au utasema inaitwa ziara ya Ngorongoro? Saga wembe ule, endelea na pipoooooz yako.
Mungu awaponye Sana majeruhi. Tatizo CCM wanalazimisha kukubalika.Bahati mbaya sana leo huko Tandahimba kuna raia watatu wamefariki walipakiwa kwenye lori ili kwenda kuongeza idadi na wengine takribani kumi wamejeruhiwa na sasa wamelazwa hospitali.
RIP waliofariki na ugua pole majeruhi wote!
CCM wacheni kubeba watu kwenye malori mtaangamiza wengi!
Mkuu 'econonist', kidogo mimi ninakushangaa wewe, pamoja na kuwasilisha mada liyojitosheleza kabisa; kwamba wewe ndio kwanza unaiona hali hii ya Samia kuwa kwenye Kampeni.Kwa ushauri hizi ziara ziwe za kikazi, Rais aondokane na haya makampeni. Afike kwa wananchi aulize shida zao na Kama wahusika wapo wajibu tuhuma zao.
Cha kusikitisha zaidi, hawa waliofariki na waliojeruhiwa,huenda hata sababu iliyokuwa ikiwapeleka huko hawawezi kuieleza kwa ufasaha. Huenda wameahidiwa kutakuwepo na mlo (wali) kwenye hadhara hiyo, au wameahidiwa vijisenti kadhaa ambavyo wangepewa baada ya kuhudhuria hapo!Mungu awaponye Sana majeruhi. Tatizo CCM wanalazimisha kukubalika.
Akili yako inafanya kazi kipekee sana.Rais Samia Ndio chaguo la watanzania kuendelea kuwaongoza mpaka 2030,Ndio maana Anaendelea kupokea na kupata mapokezi makubwa kutoka kwa wananchi kila mahali anapopita na kutua .wananchi wana shauku kubwa sana ya kumuona .Ndio maana unaona watu wakikanyagana wazee kwa vijana,akina mama kwa watoto kila mmoja anataka kumuona Rais samia na kumsikiliza.Hii yote ni kutokana na uchapa kazi wake uliyogusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti ambao kwa sasa sauti zao zinasikika kupitia Rais wao. Ambaye amekuwa mtetezi wao.
???Alichaguliwa lini na watanzania kuwa Rais?. Halafu Kama anapendwa mbona anatumia nguvu nyingi kukubalika.
Uzuri watu hawaendi kwa hiariNimefuatilia hicho kinachoitwa ziara za rais huko mkoani mtwara. Kuanzia Jana mkutano wa Mtwara mjini na Leo Tandahimba. Nilichogundua, hizi sio ziara za kazi Bali ni kampeni za uchaguzi.
Sababu zangu ni zifuatazo:
1. Sababu ya kwanza, Kila anayesimama anampigia debe Rais kana kwamba ni mkutano wa kampeni. Mara Rais kaleta maji , umeme, kajenga barabara, mara royal tour nk. Kama Leo kwenye mkutano wa Tandahimba Kuna kiongozi mmoja kadai kuwa Rais Samiah ndio Rais wa kwanza tangu uhuru kuleta maendeleo Mkoa wa Mtwara. Nadhani haya yalitakiwa yasemwe 2025 wakati wa kampeni. Kuelezea Yale mafanikio ya Rais na kwanini achaguliwe Tena.
2. Jambo la pili, Wasemaji kugusia uchaguzi wa 2025. Nimeshangaa Viongozi waliopewa nafasi kudai 2025 kwenye uchaguzi mkuu Dr Samiah Hana mpinzani. Kwa mfano kwenye mkutano wa Leo hapo Tandahimba mbunge kadai, ya kwamba uchaguzi wa 2025 watamshindilia kura nyingi za urais Mh Samiah.
3. Jambo la tatu, Mikutano kujaa sare za CCM. Nadhani sio sahihi kufanya mkutano wa ziara ya Rais kuonekana katika mrengo wa kichama. Yani walioenda pale ni wanachama wa mapinduzi na hivyo kuujenga picha ya mkutano wa CCM. Kwa mfano alipoongea yule mbunge Tunza Malapa, wengi walidhani ni CCM, wakawa wanampigia makofi, ila alipomaliza kuongea na yule MC kumtaja Kama mbunge wa vitu maalum CHADEMA, umati karibia wote ulipigwa na butwaa maana hawakutegemea mbunge wa chama kingine awe pale. Kisaikilojia walijua ni mkutano wa CCM pekee yao.
4. Jambo la nne, wasanii wanaotumbuiza wote ni Kama wanamuimba Mh Samiah. Yani kila msanii akiimba lazima apayuke Samiah oyeeh!. Hii inaleta picha ya kampeni na kumjenga Mh Samiah kuliko kuwa ziara ya kazi.
5. Jambo la mwisho, mabango, t-shirt nk Zina picha ya Samiah na maneno ya kuashiria kampeni. Hii siyo sahihi kabisa.
Kwa ushauri hizi ziara ziwe za kikazi, Rais aondokane na haya makampeni. Afike kwa wananchi aulize shida zao na Kama wahusika wapo wajibu tuhuma zao.
Umeelewa swali langu?. Tofautisha ziara ya Rais na mkutano wa kampeni au chama Cha siasa. Unapochaguliwa kuwa Rais wewe ni kiongozi wa wote. Unapofanya ziara unakuwa unafanya ziara ya wananchi wote na kwaajili ya kusikiliza kero na matatizo yao, sio kwaajili ya kusifiwa na kuahidiwa kura na Wana CCM.
CHADEMA wanafanya mikutano ya hadhara na sio kampeni. Ndio maana huwezi kuona mabango ya mgombea wa CHADEMA, Wala husikii Mbowe au Lissu akinadiwa kuwa atapewa kura nyingi 2025.
sio kweli ila uko sahihi kulingana na upeo na matazamo wako na hiyo ni haki yako.Umeelewa swali langu?. Tofautisha ziara ya Rais na mkutano wa kampeni au chama Cha siasa. Unapochaguliwa kuwa Rais wewe ni kiongozi wa wote. Unapofanya ziara unakuwa unafanya ziara ya wananchi wote na kwaajili ya kusikiliza kero na matatizo yao, sio kwaajili ya kusifiwa na kuahidiwa kura na Wana CCM.
CHADEMA wanafanya mikutano ya hadhara na sio kampeni. Ndio maana huwezi kuona mabango ya mgombea wa CHADEMA, Wala husikii Mbowe au Lissu akinadiwa kuwa atapewa kura nyingi 2025.