Hizi simu mbona bei rahisi hivyo kunani

Hizi simu mbona bei rahisi hivyo kunani

Ushauri wa buree...achana kabisa na hizo simu utajutaa hakuna mpuuzi ambaye anafanya biashara bila kulenga faidaa...simu za samsung nyingi kwa bei hiyo sio mpyaa ni refub au used ila ukiiona unaweza sema ni mpyaa hadi box wanakupa.
Mimi nimewahinunua Note 10+ 900k kuna jamaa wako pale Mcity simu ilikua mpya kwenye box ila nimetumia almost miezi miwili simu inachemka na ilikuja kuwa na mchezo wa kuzima na kuwaka non stop baada ya kuupdate, Mafundi wote iliwagomea wanasema box lina information tofauti nasimu kwaiyo nilifanyiwa uhuni mpka sasa nimeamua tuu kuifungia kabatini...ukitaka simu nzuri nenda kwa samsung official dealers, hivi vitu vya bei rahisi ni hasara tupu! USIJARIBU Ila kama unataka kuprove kanunue ujionee.
Kwanini usiwarudie kuwapa makavu

Ova
 
Unamaanisha soc?

Maana F62 haina kitu chochote cha maana kuiweka level moja na Flagship, haina ip ratings yoyote, haina OIS, kioo hakina Refresh rate kubwa wala HDR na kina peak 420nits tu etc.
. F62 ni midrange ya kawaida ambayo ina battery kubwa kwa ajili ya kuvutia watu wanaotaka simu zinazokaa na Chaji, A52S ni premium all arounder ina feature nyingi za flagship phone imekuwa positioned kama flagship killer (A52s inafanana sana na Nothing phone).
Samahani chief, hiso f62 kwa bongo bei inaendaje?

Sent from my SM-G930F using JamiiForums mobile app
 
Hizi simu refurb nashauri mtu kununua iphone pekee. Nineshanunua iphone mbili refurb kwa miaka tofauti pale China Plaza na mpaka sasa hazina shida yoyote, hii ya pili nimenunua mwaka huu.

Kwa samsung sijui kwa kweli.

Sent from my SM-G930F using JamiiForums mobile app
Hata iphone zipo ivo pia...nimeona kesi kadhaa za iphone X
 
Ipo simu inaitwa Samsung A52S ni midrange ila ni premium zaidi waterproof, 3.5mm jack, sd card, ram 6 mpaka 8GB, storage kuanzia 128, kioo Amoled 120hz, perfomance sawa na note 10 etc. Bei 720K kenya Mpya, sijajua hapa Bongo zinaendaje madukani, its worth it over refurb.
Hii simu niliona watu wengi wanailalamikia ilikua ina bugs nyingi baada ya Android 12 update sijui kama wameshasolve.
 
Unamaanisha soc?

Maana F62 haina kitu chochote cha maana kuiweka level moja na Flagship, haina ip ratings yoyote, haina OIS, kioo hakina Refresh rate kubwa wala HDR na kina peak 420nits tu etc.
. F62 ni midrange ya kawaida ambayo ina battery kubwa kwa ajili ya kuvutia watu wanaotaka simu zinazokaa na Chaji, A52S ni premium all arounder ina feature nyingi za flagship phone imekuwa positioned kama flagship killer (A52s inafanana sana na Nothing phone).
Sorry mkuu flagship ina maana gani?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Hizi simu refurb nashauri mtu kununua iphone pekee. Nineshanunua iphone mbili refurb kwa miaka tofauti pale China Plaza na mpaka sasa hazina shida yoyote, hii ya pili nimenunua mwaka huu.

Kwa samsung sijui kwa kweli.

Sent from my SM-G930F using JamiiForums mobile app

Hizi iphone zimewaelekea wanawake tu, kwa mwanaume kutumia iphone ni kujiaibisha tu.. kwa samsung jinsia zote zinaenda..

kitu samsung bwana, brand kubwa. Sema kuna wachache wanaharibu jina la samsung ionekane feki.
 
China plaza ipi hyo...mbona hakuna duka linaloitwa hvyo...alafu hyo bei ata used korea hupati
 
Hizi simu refurb nashauri mtu kununua iphone pekee. Nineshanunua iphone mbili refurb kwa miaka tofauti pale China Plaza na mpaka sasa hazina shida yoyote, hii ya pili nimenunua mwaka huu.

Kwa samsung sijui kwa kweli.

Sent from my SM-G930F using JamiiForums mobile app
Sure.

Hii model ya second hand naona kama iphone anaiweza sana. Ni rahisi sana kununua iphone nzuri kuliko samsung.

Binafsi naona inatokana na nature ya wateja. Mteja wa iphone mara nyingi utakuta anauza simu ili kwendana na wakati, lakini hizi simu nyingine sanasana inauzwa kukiwa na tatizo.
 
China plaza ipi hyo...mbona hakuna duka linaloitwa hvyo...alafu hyo bei ata used korea hupati
CHINA PLAZA kama unatoka soko la mitumba karume unaelekea kariakoo ni jengo kubwa lipo mkono wa kushoto kabla hujavuka mataa ya kituo cha daladala kongo
 
CHINA PLAZA kama unatoka soko la mitumba karume unaelekea kariakoo ni jengo kubwa lipo mkono wa kushoto kabla hujavuka mataa ya kituo cha daladala kongo
Kama ni hilo sidhani kama wapo humo...ingekuwa infinix au tecno sawa
 
Pole mkuu ilikuwa bahati mbaya tu kwako. Jamaa hawakukuweka wazi kama ni used?? Yani walikwambia ni brand new!
Hizi simu ni kama bahati nasibu tu unaweza ukapata refurb iko poa ukatumia miaka. Ninae mtu wangu wa karibu alinunua s9 ina miaka miwili na miezi kadhaa bado ipo makini kabisa. Mwingine alinunua s10 refurb ikawa na shida kwenye camera, akarudisha akapewa nyingine so far not bad sijamsikia akilalamika tena.

Kusema kweli hizi used/refurb zinatusaidia na sie walalahoi walau tuonje utamu wa flagship japo unakuta ishapitwa na wakati mpaka miaka minne lakini utapata performance na user experience nzuri kuliko mid ranges nyingi tu mpya za miaka ya karibuni.
Mimi natumia note edge ni refurbished nimenunua toka 2017 mwezi wa 12 mpka sasa naitumia ila imeanza kuleta shida kiidog saivi lakn nimetumia sana.

Sent from my SM-N9150 using JamiiForums mobile app
 
Flagahip kwenye simu inamaanisha simu nzuri zaidi ya kampuni iliozinduliwa ndani ya muda fulani. Nzuri kuanzia Camera, processor, display na vitu vyengine vinavyotengeneza simu.
Mkuu,

Binafsi sina uelewa sana na simu, lakini nataka ni-opt kati ya A33 &S21 ( Naziona siyo nzito, na shape siyo kubwa).

Kati ya hizi simu mbili kwa uelewa wako ipi inaweza kuwa na value for money ( Sina preference na magemu wala video), sanasana ni mpenzi wa kusoma vitabu na internet.
 
Sure.

Hii model ya second hand naona kama iphone anaiweza sana. Ni rahisi sana kununua iphone nzuri kuliko samsung.

Binafsi naona inatokana na nature ya wateja. Mteja wa iphone mara nyingi utakuta anauza simu ili kwendana na wakati, lakini hizi simu nyingine sanasana inauzwa kukiwa na tatizo.
Refurb ni lazima iwe na tatizo isingekua na tatizo isingeitwa refurb, sema tu sometime unaweza bahatisha refurb nzuri bila mwenyewe kujijua.

Hapo hapo China plaza niliwahi msindikiza mtu kununua iphone, imechezewa balaa haipokei updates, safari haingii internet etc. Mpaka utumie 3rd party apps.
 
Back
Top Bottom