Hizi Software 3 hazitokuja kupata mshindani wa kuzipindua kizazi hiki

Hizi Software 3 hazitokuja kupata mshindani wa kuzipindua kizazi hiki

Nakubali kabisa kuna kozi yake nliidownload aloo mambo ni mengi nilitoka kapa, ila kichwa ikitulia ntajifunza hiyo kitu inaweza kuwa msaada mbeleni kwenye ulimwengu wa kidijitali
Tatizo la Excel ili uweze kua master Ni lazima uwe unaitumia Mara kwa mara Kwny shughuli za kila Siku,lkn mtu ukiisoma Kama Noval/notes hivi ukajaribu kui-apply kidogo Baada ya muda unasahau kabisa Kama uliwahi kujifunza Excel.

 
Yaani matumizi ya Excel tunayoyajua/kuyatumia kila siku Ni labda 0.5% ya uwezo wote wa MS Excel.Lile dude Ni kubwa mno,Lina makorokocho ambayo kiukweli Ni advanced kinyama.

Nilimuona jamaa mmoja mwanajeshi wa US huko YouTube akiitumia ku-calculate hesabu zake za milipuko,nikasema tu hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
Excel ni program kubwa sana. Ina application kama million hivi sema wabongo wengi tunatumia 0.005 ya uwezo wake.
 
Hello bosses....

Kwa mizunguko mizunguko nlopitia baada ya kufanya kazi na watu kadhaa kwenye field ya software dev nmekuja gundua (in my opinion) kuna software hizi 3 hata itokee alternative gani kizazi hiki hazitokuja kuwa replaced.

Kiufupi hizo ni:-
1) BLOOMBERG TERMINAL
2)MICROSOFT EXCEL
3)SAP BUSINESS ONE (B1)



Nitazifafanua kiufupi hapa chini

---> BLOOMBERG TERMINAL
Hii kama hujihusishi na financial markets (At Instutional Level) itakua bado hujaisikia lakini ni moja kati ya software zinazorun dunia hii. Nasema zinarun dunia coz inatumiwa na asilimia kubwa ya Financial Institutions kutrade kwenye Financial markets kuanzia kununua stocks, bonds, options, currencies na financial instruments & derivatives nyngne. Wanaohusika kwenye hii field hupenda kuiita 'BLOOMIE', ilitengenezwa na kuanza kutumika kwenye miaka ya 1980 chini ya Mike Bloomberg na kinachonifurahisha kuhusu hii software ni kwamba ime-maintain 'old-school look' ambayo naweza kuiita 'hacker-like' look. Rangi zake sana sana ni black and orange na mwonekano wake unavutia kwa wanaopenda 'less-bullshit UI'.

Gharama za kutumia hii software kwa mwaka ni USD 25,000 na mabillion ya dollar hupitia kwenye hii software kila mwaka. Toka ianze kutumika 1980s hadi sasa kuna wapinzani wengi wanatengeneza software zao lkn hawajafanikiwa kuipiku BLOOMIE.


---> MICROSOFT EXCEL.
Hii siwezi ongelea sana coz wengi tunaifahamu. Ni kati ya products za Microsoft ambazo nazikubali sana. Tumeona zinakuja spreadsheet software nyingine ila hii ipo on trend miaka nenda miaka rudi. Watu wanasema wahindi wako vzr kwenye biashara lkn deep down wengi wao wanatumia excel, hao hua ni wataalam wa excel. Nilienda kwa jamaa fln kuwapa proposal ya kutumia custom made accounting software lkn wakanionyesha excel setup zao na sikuamini nlichokiona, kuanzia accounting, stock management etc... zote walikua wanafanya kwa excel tu.

---> SAP Business One (B1)
Hii nayo ni kati ya software za zamani sana ambazo hadi leo bado zinatumika. ilitengenezwa mwanzoni kabisa mwa computer Era. Hii software iko complicated na pia ina programming language yake lkn hayo hayazuii watu kuendelea kuitumia. Kazi yake kubwa ni Kufanya Enterprise Resource Planning, software za category hii hujulikana kama ERP software. Kwenye business ndg ndg huwezi kuikuta lkn ukienda kwa Giants kama Alphabet, Meta na silicon valley companies nyingine basi utaikuta. Hata hapa Tanzania nimeona inatumika kwenye baadhi ya makampuni makubwa makubwa ya uzalishaji na usafirishaji.



Zipo nyingine baadhi kama QuickBooks, Microsoft word, etc... lkn hizo zina washindani ambao tyr wanafanya vizuri na miaka michache baadae zinaweza kupotea kama MySpace. Lakin hizo nilizotaja hapo juu zina 'Strong' foundation na 'Loyal' Customer base kiasi kwamba hata kama ni ngumu kutumia au ni nzito bado zitaendelea kuongoza kwenye nyanja zao kwa hiki kizazi


Peace......
~Kali Linux
MS Excel? Kuna kitu kinaitwa LibreOffice, unakijua?
 
Kuna programmer mmoja niliona documentary alikuwa anatengeneza game, alitengeneza ile game miaka mi 3 yupo ndani ana code tu.
imagine mtu anakaa 3 yrs amefocus na kitu kimoja, kula, coding kulala ratiba inajirudia, hivi mtu wa aina hio unategemea atatengeneza kitu gani? game yake ilivunja rekodi kwenye mauzo, huyo ni mmoja hebu ongeza kama 1000 watengeneze programu moja kwa miaka mi 3. Vitu vingine si uchawi, tusi underestimate uwezo wa akili ya mwanadamu, sisi tunatumia akili zetu kwa level ya basic tu ila wenzetu wanajua kutumia akili zao kwa level ya advance tunabaki kusema uchawi.

Heshima sana kwa hao waliobuni hizo software.
 
Excel imefanyiwa development kubwa sana na ndiyo sababu inaendelea kua program kubwa zaidi.
Wanafunzi na watafiti wengi wanafanya tafiti zao kwa kutumia excel hivyo wanaendelea kuidevelop zaidi ili kurahisisha mambo
Kila anayetumia kwa matumizi yake anatafuta namna ya kurahisisha shughuli zake zaidi hivyo anadevelop zaidi
Imegusa kila nyanja
 
Kuna programmer mmoja niliona documentary alikuwa anatengeneza game, alitengeneza ile game miaka mi 3 yupo ndani ana code tu.
imagine mtu anakaa 3 yrs amefocus na kitu kimoja, kula, coding kulala ratiba inajirudia, hivi mtu wa aina hio unategemea atatengeneza kitu gani? game yake ilivunja rekodi kwenye mauzo, huyo ni mmoja hebu ongeza kama 1000 watengeneze programu moja kwa miaka mi 3. Vitu vingine si uchawi, tusi underestimate uwezo wa akili ya mwanadamu, sisi tunatumia akili zetu kwa level ya basic tu ila wenzetu wanajua kutumia akili zao kwa level ya advance tunabaki kusema uchawi.

Heshima sana kwa hao waliobuni hizo software.
I concur
 
muhindi wangu Vinod anaigonga excel sheet kwenye pc ya ram 8gb mpaka pc inachanginyikiwa inaanza kulia, kwa mimi najua kutafuta totals na average ya sums tu.. yeye anajua kufanyia funtions nyingi na kwa wakati mchache mno kwa kutumia excel shortcuts na anacross chek kwa excel tena. wahindi wengi wahasibu ni diploma level, wanaongezea kusoma tally, sap na adv. excel huwapati kwenye market ya uhasibu wa viwanda si kama sisi degrees, cpa's masters ila bado unaogopa kushika pc ukukotoe uhasibu.
 
Mnapotaja maajabu ya excel muwe mnaorodhesha kabisa maana sisi wengine miaka yote huwa tunaipita kama hatuioni. Yaani mimi hata budget nilikuwa natengenezea kwenye ms word kwa kuchora jedwali na kukaa na kikokotoo pembeni.

Juzi tu ndio nimejua kumbe ukiwa na excel inamaliza kila kitu yenyewe.
 
Process ndefu kiasi mkuu. Kuna banks na firms wanatoa hizo huduma ila hawachukui wateja kutoka nchini kwetu. Kama una uhitaji sana unaweza tumia proxy, nikimaanisha kama una connection na mtu wa Kenya, US au nchi ilio na access na hizo huduma unaweza pitia kwa huyo. I know 6 firms zinazochukua wateja kutoka Africa ila TZ ni blacklisted kwenye hizo zote huwa najiuliza sana sababu ni nn lkn nadhan ni yaleyale ya PayPal
Kama hutojali tafadhali shuka hizo firm 6 mkuu...... ili tuziingilie chimbo
 
Back
Top Bottom