Yes, wewe ulisikia vizuri sana. Hiki kitu alikiongea vizuri sana siku ya kwanza na akafafanua masharti kama hayo kwamba hatutakiwi kuongeza matumizi kwa kuajiri.
Na hapo walikuwa wanazungumzia deni lilipofikia yaani 91, japo wahusika ndio hawatuambiagi hayo masharti. Siku hii walikuwa Gerald, Mussa na Kitenge.
Sasa siku nyingine tena (nadhani ni ndani ya wiki) ndio akasema binafsi hapendi serikali inavyokopakopa, hii hali ngumu tunayopitia ni kwa ajili ya madeni.
Nadhani hiki ndicho kilichowauma wahusika ingawa pia hakuongea kitu kibaya.
Siku hii walikuwa yeye na Mussa.