Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Mayala safi sana unajitambua na unaitendea haki tasinia ya habari, ili la kukanyaga katiba juu ya kuzuia wanasiasa kufanya siara hakujibu
 
Binafsi swali la Sammy Awamu alilomuuliza rais magufuli limekuwa chachu na nimeliona la maana zaidi.

Ni mwandishi gani ameuliza swali lililokukonga moyo wako na lenye maslahi mapana kwa nchi yetu?
Tido,paskali,

baada ya hapokuna haja ya kujihoji kama kweli baadhi ya magazeti yanafaa kununuliwa Tsh 1000,kwa aina ya wahariri walionao,hasa Jamhuri ya.manyerere ambaye aliulizia pombe(whisky) ikulu na msosi
 
Mambo muhimu hayajaulizwa ama hayajajibiwa kikamilifu matharani suala la ajira kwa vijana,mikopo,kilimo n.k.ameyajibu kwa figure of budget but not in reality.pia kashindwa kabisa kuonyesha kama anania ya dhati katika kukuza demokrasia.
 
Daaah ahsante sana Pascal Mayalla kwa kuuliza swali lenye maudhui kama ya swali nililouliza humu Jf jana. Pole pia kwa sababu swali hilo halikujibiwa ipasavyo.
 
Sasa naweza nikaamini ule uzi wa jana kwamba kuna waandishi walipewa maswali ya kuuliza. Haiwezekani waandishi wote wale swali la msingi na lenye akili litoke kwa Pasco Mayalla peke yake.
Mkuu ninaham ya kuumlza Pasco swari hili... Katika ule uzi wa jana uliofutwa na mod katika maoni yangu niliandika kuwa "Magu ninaemfaham ndo yule wa kuandaliwa maswari na si Magu wa mswari ya papo kwa hapo." Kinachonifanya niwe na ham ya kumuulza ni sababu Pasco alilake komenti yangu..
 
Kamuuliza kuwa kapata wapi mamlaka ya kuzuia safari za watumishi nje wakati kuna mihimili mitatu na yote inajiongoza yenyewe? Pia kwa nini mikusanyiko ya kisiasa inatambulika na katiba lakini yeye kaizuia wakati aliapa kutumikia nchi kwa mujibu wa katiba?
Kama wangekuwepo hata watano tuu wenye mwelekeo wa Pasco hakika angependa hayo masaa mawili ya ishe aondoke, lakini kwa vile waliopo wengi ni makanjanja basi kawaambia waulize mpaka wachoke wenyewe.
Ni kweli kauliza swali zuri lakini rais kamjibu kiutu uzima.rais anayo mamlaka yote dhamira ikiwa ni nzuri hata kama sheria haimpi mamlaka hayo tuache ushabiki wa kimachinga eti sheria na vitu vingine
 
Ukuu wa wilaya au mkoa au ukurugenzi utausikia kwa waandishi wenzako walio uliza kwa kujipendekeza
 
DR Ryoba , swali lake lilikuwa unajitathimini vipi wewe mwenyewe? Tido swali lake lilikuwa watu wanasema maamuzi yako kuhusu demokrasia ni kama unataka kufanya udikteta unasemaje kuhusu hilo? Mayalla swali lake lilikuwa umepata wapi mamlaka ya kuzuia mikutano ya kisiasa ?
 
Mayala alianza hotuba,kujifagilia na kutangaza kampuni yake na kujipigia debe la kutafuta fursa ikulu .Sehemu kubwa ya aliyonngea yalikuwa hasa ya kujinadi mnadani yeye binafsi.Kwangu naona kama aligeuza Ikulu na ile press conference kama gulio la kujinadi zaidi kuliko kuuliza swali.
Ni mjinga pekee ambaye angeshindwa kutumia platform kama ile kujitangaza, hata hivyo pamoja na hilo kauliza swali lake vizuri.
 
Back
Top Bottom