Weka picha acha maneno mengi. Hata hivyo tunapenda maendeleo, wacha watu wainvest pesa zao!!
Ajira zitapatikana kwa Watanzania wenzetu, wakulima watauza mboga zao na vyakula vingine, watalii watapata sehemu nzuri za kulala, serikali itapata kodi!! Kuna baadhi ya watanzania wenzetu watafaidika kwa namna nyingi.
Tatizo la watanzania ni wivu tu unawasumbua!!
Kwa mfano huu uzi umeandikwa kimbeya sana, SIYO kwa namna ya kupongeza ni jambo zuri limefanyika, umeandikwa kwa namna ya labda hawa waliojenga ni majizi au wala rushwa au wahujumu uchumi!! Some people are never positive!! Wamejawa na wivu mpaka wanajichukia wao wenyewe!!
Hakuna MTU mwenye wivu na Maendeleo ya MTU Wala mwekezaji. Tatizo kubwa ni watu kuiba fedha za umma Kwa kushindana. Hii Nchi Ina pesa nyingi sana na Rasilimali nyingi sana. Hakuna Waziri au mkubwa Wa Idara ambaye akipewa Hata mwaka anatoka bila kuchota mabilion ya pesa. Hapo Ndipo panapowakera watu . Na Nature ilivyo dhulma haidumu . Hata Wazungu na Waarabu walitumyonya sana lakini wanakoelekea ni kwenye uharibifu mkubwa. Wachini walinyonywa sana Lakini wanatelekea juu. Wahindi ni ubahili wao na ujanja ujanja Lakini Hawana mambo ya kukwapua ni kama Wachagga ,wachagga wakiwa maofisini Hawana mambo ya kuchota pesa za umma na mamilataba ya kuhujumu Nchi. Wanacheza na Fursa Lakini wanafanya jambo zuri na la kudumu. Kuna kundi Fulani limepita Madarakani kuanzia miaka 20 iliyopita KAZI yake imekua ni kuchota na kukwapua Mali za umma Wakati Hawana Historia Wala uwezo Wa KUFANYA Biashara. Walikwapua viwanda wakaviua watu wakakosa ajira wao wakawa mabilionea.
Hii Nchi ilikua na viwanda vingi sana kiasi kwamba ajira isingekua tatizo.Chuki za kisiasa na kampeni chafu dhidi ya watu wenye uwezo Wa kusimamia na kuongoza makampuni na Biashara zikawa zinafanywa na kundi la watu waliojaa tamaa ya fedha za kukwapua Ili tu waonekane ni mabilionea.
Haiwezekani kiwanda cha Cement kife Wakati wenye ujenzi Mkubwa sana Wa miradi na majengo Binafsi, Haiwezekani kiwanda Cha tairi kife wakati Kuna Magari mengi sana ya serikali na Binafsi kuliko wakati kinaanzishwa. Haiwezekani kiwanda cha ngozi kife Wakati Nchi nzima watu wanavaa viatu na mikanda ya ngozi kiunoni.
Haiwezekani ,dhahabu ikose soko Benki kuu,haiwekani Tanzanite ikose soko Benki kuu n.k. Haiwezekani mashamba ya mpunga ya Mbarali yafe wakati Dunia nzima inahitaji chakula,haiwezekani mashamba ya Ngano yafe n.k. .
Ilikua rahisi tu kuanzisha mradi na kumkabidhi mangi kwa mkataba Wa kifo. Hao wengine unawapa mradi kama Huo Huo lakini kwa majaribio wakishindwa unampa Mangi mkataba Wa kifo mana uwezo wanao na ubunifu Wa ushindani wanao.
Badala yake pamekua na usimamizi Wa kupeana na kupendeleana na kudhani wanawakomoa Akina Mangi kumbe wanaua uchumi Wa Nchi na kunufaisha Wageni Kwa tamaa za kutajirika haraka haraka.
Watanzania watawezeshwa Kwa kuwatumia wazawa wenye uwezo sio kuwatumia Wageni kukomoa wazawa kikabila. Ukabila umekwisha mana Hata wananyanyuku wanaoana na Wamangi hivyo Maendeleo ya Nchi yanafaidisha wotanzania wote.
Hili Neno wivu linapaswa kubaki Kwa wafanyabiashara wanaofanya Biashara Kwa ushindani Wenye tija sio Biashara zisizoeleweka kama Rushwa, magendo,wizi,madawa ya kulevya, pesa za ugaidi ambazo zinaingia Kwa Kasi na zitavuruga nchi Kwa Kasi pia. Magaidi na mabeberu wanagombania uchumi na siasa za Dunia hivyo Ufadhili wao Kwa Sasa ni mkubwa sana na wanatumia wanasiasa na wanye madaraka kufanikisha misheni zao za muda mrefu.
Wananchi wanaona ndio maana wanachukia maendeleo ya mtu yanayoua Taifa lao.