Hotuba ya Pieter Willem Botha aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini ya Makaburu

Hotuba ya Pieter Willem Botha aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini ya Makaburu

Mwafrika amenyanyasika, ananyanyasika na ataendelea kunyanyasika kama hataendelea kuchukua hatua endelevu za kujikomboa. Harakati za ukombozi zilizofanyika huko nyuma zimetoa mafaniko kidogo lakini ni muhimu kujua kwamba mapambano ya ubaguzi na uonevu yanatakiwa kuendelezwa muda wote.
Ubinafsi na ulevi wa madaraka wa viongozi wa Afrika umewafanya wawe vibaraka wa watu weupe kuendeleza unyonyaji na ukandamizaji dhidi ya ndugu zao weusi.
Hata hivyo, kwa kuendana na wakati, njia za mapambano lazima zibadilishwe, ziwe za kimya kimya ikiwa ni hujuma dhidi ya watesi pamoja na vibaraka wao. Ni makosa makubwa kuridhika na hali iliyopo kwani safari ya ukombozi bado ni ndefu sana.
 
Ni hotuba iliyojaa kila aina ya ubaguzi...lakini pia ndani yake kuna ukweli mchungu!!!!
 
Cheap propaganda Botha hajawahi kutoa hiyo hotuba anaebisha alete video however nakubali asilimia mia2 Botha ni mbaguzi
 
Faiza foxy alienda shule kusomea ujinga.. sasa unataka achangie ujinga ili ujinga wake uenee kwa watu wengine?

Kuna mtu kauliza huyu Botha alikuwa Muislam au Mkiristo?

Naona mnashindwa kumjibu mpaka sasa.
 
Mwafrika amenyanyasika, ananyanyasika na ataendelea kunyanyasika kama hataendelea kuchukua hatua endelevu za kujikomboa. Harakati za ukombozi zilizofanyika huko nyuma zimetoa mafaniko kidogo lakini ni muhimu kujua kwamba mapambano ya ubaguzi na uonevu yanatakiwa kuendelezwa muda wote.
Ubinafsi na ulevi wa madaraka wa viongozi wa Afrika umewafanya wawe vibaraka wa watu weupe kuendeleza unyonyaji na ukandamizaji dhidi ya ndugu zao weusi.
Hata hivyo, kwa kuendana na wakati, njia za mapambano lazima zibadilishwe, ziwe za kimya kimya ikiwa ni hujuma dhidi ya watesi pamoja na vibaraka wao. Ni makosa makubwa kuridhika na hali iliyopo kwani safari ya ukombozi bado ni ndefu sana.
Nakubaliana na wewe ndugu lebabu 11. Ndiyo maana wazungu bado wanatuona sisi bado ni masokwe, kwani wanawatumia weusi wenzetu- hasa watawala walafi wa madaraka na wabinafsi, wasio na maono yoyote ya kuwakomboa wanaowaongoza katika nyanja mbalimbali kuendelea kutukandamiza. Safari ya kufika kwenye ukombozi wa kweli bado ni ndefu.
 
image.jpeg
image.jpeg
image.jpeg

Wenyewe walimwiita "Groot Krokodil" means "Great Crocodile"...Huyu jamaa alikuwa ni kiboko sana
Licha ya kumtesa sana Mandela Gerezani,lakini eti Mandela alivyotoka akamsamehe na kukaa nae meza moja kwa upatanisho


...
 
View attachment 344250 View attachment 344245 View attachment 344246
Wenyewe walimwiita "Groot Krokodil" means "Great Crocodile"...Huyu jamaa alikuwa ni kiboko sana
Licha ya kumtesa sana Mandela Gerezani,lakini eti Mandela alivyotoka akamsamehe na kukaa nae meza moja kwa upatanisho


...
Wengi wanaamini '' Mandela was a sell-out ''..kaacha waafrika wakiwa wanamiliki asilimia 30 ya ardhi ya babu zao.
Suala la kuua weusi linafahamika na lina ushahidi mwingi.
 
Duh aisee, huyu Shetani si ameshakufa?
I'm very much sure yupo kuzimu anasubiria hukumu
Tena afadhali ya huyo kuliko katili mmoja aliyeitwa John Voster huyo alipewa kiburi na aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza wakati ule Edward Heath kipindi hicho Mbwa alipewa thamani kubwa kuliko mtu mweusi.
 
HII NDIYO MOJA YA HOTUBA MBAYA ZA P. w. BOTHA


Ukweli kuwa weusi wanaofanana na binadamu na kutenda mambo kama binadamu hayawahalalishi kuwa wao ni watu wenye akili timamu au binadamu aliyetimia. Kanunguyeye si nungunungu na mijusi hawawezi kuwa mamba kwa sababu eti wanafanana.

Huyu alikuwa mjinga sana. Hata nyani au ng'ombe wapo weusi na weupe, lakini rangi ya nyani au ng'ombe mweusi haimfanyi yeye kutokuwa ng'ombe au nyani.

Kanunguyeye ni kanunguyeye na nungunungu ni nungunungu. Na kujua sio kitu kimoja (species moja) hata ukiwaweka pamoja hawawezi kuzaa. Sasa kama Botha alidhani mweusi na mweupe sio kitu kimoja (species) kisayansi, angemweka mkewe au binti yake na mwanaume mweusi aone kama wasingemtolea ka-cute chocolate baby kuthibitisha wao ni species moja.
 
Kuna mtu kauliza huyu Botha alikuwa Muislam au Mkiristo?

Naona mnashindwa kumjibu mpaka sasa.
Bothe alikuwa mkristo

Mandela pia alikuwa mkristo

Walikuja kupatana baadaye na Botha aka maliza maisha yake kawaida tuu
 
Hotuba ya aliyekuwa Rais wa
Afrika ya Kusini ya Makaburu, P.W. Botha
alipolihutubia Baraza lake la
Mawaziri.

Hotuba hii iliyochapishwa
katika gazeti la SUNDAY TIMES la
nchini humo toleo la Agosti 18,
1985,


“Kaka zangu na dada zangu,
Pretoria imetengenezwa na watu
weupe kwa ajili ya watu weupe na
hatuna haja ya kuuthibitishia
umma au kumthibitishia mtu
mweusi kuwa sisi ni watu bora,
tumekuwa tukiwaambia watu
weusi jambo hili kwa njia elfu.

Afrika ya Kusini ya leo
haikutengenezwa katika mawazo
ya kawaida, tumeitengeneza kwa
kutumia akili nyingi, jasho na
damu. Mnaposema kuwa
tunawabagua watu weusi sielewi,
Hivi ni Makaburu ndio waliojaribu
kusitisha kizazi cha Waaborigini
wa Australia? Je, ni Makaburu
waliowatenga na kuwanyanyasa
watu weusi Marekani kwa kuwaita
niggaz? Je, ni Makaburu ndio
waliowatenga na kuwanyanyasa
watu weusi huku Uingereza kwa
kuwatungia sheria za
kuwakandamiza? Kanada,
Ufaransa, Urusi na Japani nao
wana njia zao za kibaguzi. Hivi
kwa nini hasa kuna kelele nyingi
dhidi yetu? Huu ni uendawazimu!
Kwa nini wanatukaba koo kiasi
hiki? Hawatutendei haki hata
kidogo.

Nataka kuwaeleza kuwa hakuna
kibaya tunachokitenda hapa
ambacho hao wanaojiita wako
katika dunia ya ustaarabu
wameacha kukifanya. Sisi ni watu
wema tusio na hatia na ambao
tumeweka wazi mfumo wa maisha
tunayotaka tuishi kama watu
weupe. Sisi sio wanafiki kama
wazungu wenzetu wafanyao kama
kwamba wanawapenda watu
weusi.

Ukweli kuwa watu weusi
wanafanana na binadamu na
kutenda mambo kama binadamu
hauhalalishi wao kuwa watu wenye
akili timamu au binadamu
waliotimia. Kanunguyeye si
nungunungu na mijusi hawawezi
kuwa mamba eti kwa sababu tu
wanafanana. Kama Mungu
angelitaka tufanane na watu weusi
angetufanya sote tuwe na rangi na
fikra sawa. Lakini alituumba
tofauti: Weupe, Weusi, Wanjano,
watawala na watawaliwa. Katika
upeo sisi ni bora kuliko watu weusi
na hilo halina ubishi kwani
limejidhihirisha kwa miaka mingi
iliyopita. Naamini kuwa Kaburu ni
mtu safi, mwenye hofu na Mungu.
Ni mtu ambaye ameonesha kwa
vitendo njia sahihi ya utu.

Hata hivyo, inafurahisha kuona kuwa
Ulaya, Marekani, Kanada, Australia
na wengine wengi wako nyuma
yetu achilia mbali maneno yao.
Kuhusu uhusiano wa kidiplomasia,
sote tunafahamu lugha
invyotakiwa kutumika. Na kwa
ushahidi ulio wazi hivi kuna mtu
hapa asiyejua kuwa nchi nyingi za
Ulaya zinatamani kuja kuwekeza
Afrika ya Kusini? Nani anayenunua
dhahabu yetu? Nani anayenunua
almasi yetu? Nani anafanya
biashara nasi? Nani anatusaidia
katika kuendesha silaha za
nyuklia? Ukweli ni kwamba sisi ni
watu wao na wao ni watu wetu.
Hii ni siri kubwa.

Nguvu ya uchumi wetu inajengwa
kwa kiasi kikubwa na Marekani,
Uingereza na Ujerumani. Ni jambo
kubwa sana hili na kwa maana
hiyo, mtu mweusi ni malighafi kwa
mtu mweupe. Hivyo basi, kaka na
dada zangu hebu tuungane
kumpiga vita huyu shetani mweusi.
Napiga mbiu kwa Makaburu wote
kujitokeza kwa hali na mali
kupigana vita hii. Hakika Mungu
hawezi kuwatupa watu wake
ambao ni sisi.

Hadi sasa imeonekana kwa vitendo
kuwa watu weusi hawawezi
kujitawala. Wape bunduki kama
hawataanza kuuana. Hawana
lolote jema isipokuwa mashujaa
wa kupiga kelele, kucheza ngoma,
kuoa wanawake wengi na kupenda
sana ngono. Hebu sasa tukubali
kuwa mtu mweusi ni alama ya
umaskini, udumavu wa akili, uvivu
na kukosa ushindani, Hivi hapo, je,
si kweli kwamba mtu mweupe
aliumbwa ili amtawale mtu
mweusi? Hivi utajisikiaje ukiamka
asubuhi ukamkuta kafiri, yaani
mtu mweusi amekalia kiti cha
utawala? Hivi unajua
kitakachotokea kwa wanawake
wetu? Hivi kuna mtu anawaza
kwamba mweusi ataitawala nchi
hii?

Kwa hiyo tuna sababu nzuri ya
kuwapeleka akina Mandela jela
waozee huko na katika hili
nadhani upo umuhimu wa kupewa
pongezi kwani tungekuwa na
uwezo wa kuwaangamiza lakini
bado wanaishi. Napenda
kuwatangazia mikakati mipya ya
kuwaangamiza hawa watu weusi.
Tutumie sumu kuwamaliza. Kamwe
tusiruhusu idadi ya watu weusi
iendelee kukua vinginevyo
tutakwisha.

Tayari nimeshawaleta wanasayansi ambao wamekuja na
sehemu kubwa ya mzigo wa sumu
na ninawasaka watafiti wengine
zaidi waangalie sehemu murua za
kuitumia sumu hiyo kwa lengo la
kuwaangamiza watu weusi.
Sehemu nzuri za kuwaangamizia
kwa sumu ni hospitalini na pia
katika usambazaji wa chakula
inaweza kutumika. Tumetengeneza
sumu inayoua taratibu na
kupunguza uwezo wa uzazi. Lakini
hofu yetu ni kwamba itakuwaje
kama sumu hiyo itaangukia
kwenye mikono yao. Hata hivyo,
tunafanya kila tuwezalo
kuhakikisha kuwa sumu hiyo
inabaki katika himaya yetu.

Pili, watu weusi wanapenda sana
pesa kwa hiyo tunaweza kuwatega
kwa njia hiyo. Wataalamu wetu,
wanalifanyia kazi suala hilo ili mtu
mweusi amchukie mtu mweusi
mwenzake. Hawana upeo wa
kufikiri na huyo ndiye kiumbe
dhaifu kisicho na akili ya kuona
mbali. Kuna umuhimu mkubwa wa
kupanga mambo hayo yaendelee
kwa muda mrefu ili wasibaini
kinachoendelea. Kwa kawaida mtu
mweusi hapangi mikakati inayozidi
kipindi cha mwaka mmoja. Na
hapa napenda niwaombe akina
mama wote wa kikaburu wazae
kwa fujo kusudi kuongeza idadi
yetu. Litakuwa jambo la maana
pia kama kutatengwa vituo
maalumu ambako vijana wa kike
na wa kiume watakaa na serikali
kuwawezesha kuzaa kwa idadi
kubwa iwezekanavyo ili kuongeza
idadi yetu.

Wakati hilo likiendelea, lazima
tuwabane watu weusi waachane
na wake zao. Ninayo kamati
inayoratibu na kuangalia njia nzuri
ya kuwafanya watu hawa
wachukiane na wauane wenyewe
kwa wenyewe. Adhabu kwa mtu
mweusi aliyemuua mtu mweusi
mwenzie iwe ndogo ili kuwapa
hamasa ya kuendelea na mauaji.
Wanasayansi wangu wameshauri
pia kwamba kuna ulazima wa
kuwawekea sumu kwenye pombe,
sumu ambayo itakuwa inawaua
taratibu na kumaliza uwezo wa
kuzaa pia. Njia kama hii na
nyingine zinafananazo na hii
itarahisisha kuipunguza idadi yao.
Rekodi zinaonyesha pia kuwa mtu
mweusi anampenda sana
mwanamke mweupe.

Hii ni nafasi
nzuri kwetu. Wanawake wetu
warembo wanaotumika katika
mbinu za kuwaangamiza
wapinzani wetu watatumika
kuwaua hao wanaopinga ubaguzi
wa rangi. Hili ni jeshi letu la
mwituni la mapenzi huku tukiwa
na jeshi kama hilo kwa upande wa
wanaume weupe ambao
watawafuata wanawake weusi.
Pia serikali imeagiza malaya
kutoka Marekani na Ulaya kwa ajili
ya kukidhi haja hiyo. Ombi langu
la mwisho ni kwamba wajawazito
wanapozaa hospitalini, watoto
lazima wauawe pindi tu
wanapotoka tumboni. Hatuwalipi
wale wauguzi kwa ajili ya
kutuletea watoto weusi katika
dunia hii bali kuwaangamiza.
Serikali yangu imetenga fungu
maalumu la pesa kwa ajili ya
kujenga hospitali na kliniki kwa
ajili ya kufanikisha mpango huo.
Pesa inafanya lolote na kwa vile
tunazo tuzitumie ipasavyo.

Kwa muda huu, ndugu zangu
weupe, msiyaweke moyoni maneno
yanayosemwa dhidi yetu na wala
msione aibu kuitwa wabaguzi na
wala sijali kuitwa mhandisi na
mfalme wa ubaguzi. Siwezi
kugeuka nyani eti kwa sababu mtu
kaniita nyani. Nitabaki kuwa nyota
inayong’aa ... mtukufu Botha. Leo
naondoa mawingu; kesho
nitajaribu milima"

MWISHO WA NUKUU.
 
Racism ipo na itaendelea kuwepo. Racism haipingwi kwa maneno "say no to racism" na njia nyepesi nyepesi kama hizo.

Racism inapingwa kwa vitendo. Hadi weusi tujitambue, tuthamini vyetu na maisha ndipo tutachukuliwa serious. So far tumeonyesha upungufu wa kiwango kikubwa wa uwezo wa kufikiri. Weusi popote tulipo kama mshenzi Botha alivyosema tunaharibu tu yani hatuna jema from weusi wa Africa to America. Nina wasiwasi kama tutakuja kujitambua
 
Back
Top Bottom